Lithuanian

Swahili: New Testament

Matthew

8

1Kai Jėzus leidosi nuo kalno, Jį sekė didelės minios.
1Yesu aliposhuka kutoka mlimani, makundi mengi ya watu yalimfuata.
2Ir štai priėjo raupsuotasis ir, pagarbinęs Jį, sakė: “Viešpatie, jei nori, Tu gali mane padaryti švarų”.
2Basi, akaja mtu mmoja mwenye ukoma, akamsujudia akisema, "Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa!"
3Jėzus ištiesė ranką, palietė jį ir tarė: “Noriu, būk švarus!” Ir tuojau raupsai išnyko.
3Yesu akanyosha mkono wake, akamgusa na kusema, "Nataka! Takasika." Mara huyo mtu akapona ukoma wake.
4Jėzus pasakė jam: “Žiūrėk, niekam nepasakok, bet eik pasirodyti kunigui ir paaukok Mozės įsakytą atnašą jiems paliudyti”.
4Kisha Yesu akamwambia, "Sikiliza, usimwambie mtu yeyote, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na ukatoe sadaka iliyoamriwa na Mose kuwathibitishia kwamba umepona."
5Jėzui sugrįžus į Kafarnaumą, prie Jo priėjo šimtininkas, maldaudamas:
5Yesu alipokuwa anaingia mjini Kafarnaumu, ofisa mmoja Mroma alimwendea, akamsihi
6“Viešpatie, mano tarnas guli namie paralyžiuotas ir baisiai kankinasi”.
6akisema, "Mheshimiwa, mtumishi wangu amelala nyumbani, mgonjwa wa kupooza na anaumwa sana."
7Jėzus jam tarė: “Einu ir išgydysiu jį”.
7Yesu akamwambia, "Nitakuja kumponya."
8Šimtininkas atsakė: “Viešpatie, nesu vertas, kad užeitum po mano stogu, bet tik tark žodį, ir mano tarnas pasveiks.
8Huyo ofisa akamwambia, "Mheshimiwa, sistahili uingie nyumbani mwangu. Lakini sema tu neno, na mtumishi wangu atapona.
9Juk ir aš, būdamas valdinys, turiu sau pavaldžių kareivių. Sakau vienam: ‘Eik!’, ir jis eina; sakau kitam: ‘Ateik!’, ir jis ateina; sakau tarnui: ‘Daryk tai!’, ir jis daro”.
9Maana, hata mimi niliye mtu chini ya mamlaka ya wengine, ninao askari chini yangu. Namwambia mmoja, Nenda! naye huenda; na mwingine, Njoo! naye huja; na mtumishi wangu, Fanya kitu hiki! naye hufanya."
10Tai girdėdamas, Jėzus stebėjosi ir kalbėjo einantiems iš paskos: “Iš tiesų sakau jums: net Izraelyje neradau tokio tikėjimo!
10Yesu aliposikia hayo, alistaajabu, akawaambia watu waliokuwa wanamfuata, "Kweli nawaambieni, sijapata kumwona mtu yeyote katika Israeli aliye na imani kama hii.
11Todėl sakau jums: daugelis ateis iš rytų ir vakarų ir susės dangaus karalystėje su Abraomu, Izaoku ir Jokūbu.
11Basi, nawaambieni kwamba watu wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi karamuni pamoja na Abrahamu, Isaka na Yakobo katika Ufalme wa mbinguni.
12O karalystės vaikai bus išmesti laukan į tamsybes. Ten bus verksmas ir dantų griežimas”.
12Lakini wale ambao wangalipaswa kuwa katika Ufalme huo watatupwa nje, gizani, ambako watalia na kusaga meno."
13Šimtininkui Jėzus tarė: “Eik, ir tebūnie tau, kaip tikėjai!” Ir tą pačią valandą tarnas pagijo.
13Kisha Yesu akamwambia huyo ofisa Mroma, "Nenda nyumbani; na iwe kama ulivyoamini." Na mtumishi wake akapona saa ileile.
14Atėjęs į Petro namus, Jėzus pamatė jo uošvę gulinčią ir karščiuojančią.
14Yesu alifika nyumbani kwa Petro, akamkuta mama mkwe wa Petro amelala kitandani, ana homa kali.
15Jis palietė jos ranką, ir karštis praėjo. Toji atsikėlė ir patarnavo jiems.
15Basi, Yesu akamgusa huyo mama mkono, na homa ikamwacha; akasimama, akamtumikia.
16Vakarui atėjus, žmonės sugabeno pas Jėzų daug demonų apsėstųjų. Jis išvarė dvasias žodžiu ir išgydė visus ligonius,
16Ilipokuwa jioni, walimletea watu wengi waliokuwa wamepagawa na pepo; naye, kwa kusema neno tu, akawafukuza hao pepo. Aliwaponya pia watu wote waliokuwa wagonjwa.
17kad išsipildytų, kas buvo pasakyta per pranašą Izaiją: “Jis pasiėmė mūsų negalias ir nešė mūsų ligas”.
17Alifanya hivyo ili yale aliyosema nabii Isaya yatimie: "Yeye mwenyewe ameondoa udhaifu wetu, ameyachukua magonjwa yetu."
18Matydamas aplinkui didžiulę minią, Jėzus įsakė irtis į kitą krantą.
18Yesu alipoona kundi la watu limemzunguka, aliwaamuru wanafunzi wake waende ng'ambo ya ziwa.
19Tuomet priėjo vienas Rašto žinovas ir tarė Jam: “Mokytojau, aš seksiu paskui Tave, kur tik Tu eisi!”
19Mwalimu mmoja wa Sheria akamwendea, akamwambia, "Mwalimu, mimi nitakufuata kokote uendako."
20Jėzus jam atsakė: “Lapės turi urvus, padangių paukščiai­lizdus, o Žmogaus Sūnus neturi kur galvos priglausti”.
20Yesu akamjibu, "Mbweha wana mapango, na ndege wana viota; lakini Mwana wa Mtu hana mahali pa kupumzikia."
21Kitas Jo mokinys prašė: “Viešpatie, leisk man pirmiau pareiti tėvo palaidoti”.
21Kisha mtu mwingine miongoni mwa wanafunzi wake akamwambia, "Bwana, niruhusu kwanza niende nikamzike baba yangu."
22Bet Jėzus atsakė: “Sek paskui mane ir palik mirusiems laidoti savo numirėlius”.
22Lakini Yesu akamwambia, "Nifuate! Waache wafu wazike wafu wao."
23Jėzus įlipo į valtį, ir mokiniai paskui Jį.
23Yesu alipanda mashua, na wanafunzi wake wakaenda pamoja naye.
24Ir štai ežere pakilo smarki audra, ir bangos liejo valtį. O Jis miegojo.
24Ghafla, dhoruba kali ikatokea ziwani, hata mawimbi yakaanza kuifunika mashua. Yesu alikuwa amelala usingizi.
25Mokiniai pripuolę ėmė Jį žadinti, šaukdami: “Viešpatie, gelbėk mus, žūvame!”
25Wanafunzi wakamwendea, wakamwamsha wakisema, "Bwana, tuokoe, tunaangamia!"
26Jis jiems tarė: “Kodėl jūs tokie bailūs, mažatikiai?” Paskui Jis atsikėlė, sudraudė vėjus bei ežerą, ir pasidarė visiškai ramu.
26Yesu akawaambia, "Enyi watu wenye imani haba; mbona mnaogopa?" Basi, akainuka, akazikemea pepo na mawimbi; kukawa shwari kabisa.
27Žmonės stebėjosi ir kalbėjo: “Kas Jis per vienas, kad net vėjai ir ežeras Jo klauso?”
27Watu wakashangaa, wakasema, "Ni mtu wa namna gani huyu? Hata pepo na mawimbi vinamtii!"
28Kai Jėzus priplaukė kitą krantą gergeziečių krašte, Jam priešais atbėgo du demonų apsėstieji, išlindę iš kapinių rūsių. Juodu buvo tokie pavojingi, kad niekas negalėjo praeiti anuo keliu.
28Yesu alifika katika nchi ya Wagerasi, ng'ambo ya ziwa, na huko watu wawili waliopagawa na pepo wakakutana naye wakitokea makaburini. Watu hawa walikuwa wenye kutisha mno, hata hakuna mtu aliyethubutu kupita katika njia hiyo.
29Ir štai jiedu ėmė šaukti: “Ko Tau iš mūsų reikia, Jėzau, Dievo Sūnau?! Atėjai pirma laiko mūsų kankinti?”
29Nao wakaanza kupiga kelele, "Una shauri gani nasi, wewe Mwana wa Mungu? Je, umekuja kututesa kabla ya wakati wake?"
30Toli nuo jų ganėsi didelė banda kiaulių.
30Karibu na mahali hapo kulikuwa na nguruwe wengi wakichungwa.
31Demonai prašė: “Jeigu mus išvarysi, tai leisk sueiti kiaulių bandon”.
31Basi, hao pepo wakamsihi, "Ikiwa utatutoa, basi uturuhusu tuwaingie nguruwe wale."
32Ir Jis jiems tarė: “Eikite!” Tuomet demonai išėjo ir apniko kiaules. Ir štai visa banda metėsi nuo skardžio į ežerą ir prigėrė vandenyje.
32Yesu akawaambia, "Haya, nendeni." Hapo wakawatoka watu hao, wakawaingia nguruwe. Kundi lote la nguruwe likaporomoka kwenye ule mteremko mkali, likatumbukia ziwani; nguruwe wote wakafa maji.
33Piemenys pabėgo ir, pasiekę miestą, viską išpasakojo, taip pat ir apie apsėstuosius.
33Wachungaji wa hao nguruwe walikimbia, wakaenda mjini. Huko walitoa habari zote na mambo yaliyowapata wale watu waliokuwa wamepagawa.
34Tada visas miestas išėjo pasitikti Jėzaus ir, Jį pamatę, maldavo pasišalinti iš jų krašto.
34Basi, watu wote katika mji ule walitoka, wakamwendea Yesu; na walipomwona, wakamsihi aondoke katika nchi yao.