Lithuanian

Swahili: New Testament

Matthew

9

1Įlipęs į valtį, Jėzus persikėlė per ežerą ir sugrįžo į savo miestą.
1Yesu alipanda mashua, akavuka ziwa na kufika katika mji wake.
2Ir štai Jam atnešė paralyžiuotą žmogų, paguldytą ant gulto. Pamatęs jų tikėjimą, Jėzus tarė paralyžiuotajam: “Būk drąsus, sūnau, tavo nuodėmės atleistos!”
2Hapo watu walimletea mtu mmoja aliyepooza mwili, amelazwa juu ya kitanda. Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza, "Jipe moyo mwanangu! Umesamehewa dhambi zako."
3Kai kurie Rašto žinovai ėmė murmėti: “Jis piktžodžiauja!”
3Baadhi ya walimu wa Sheria wakaanza kufikiri, "Mtu huyu anamkufuru Mungu!"
4Žinodamas jų mintis, Jėzus tarė: “Kam piktai mąstote savo širdyje?
4Yesu aliyajua mawazo yao, akasema, "Kwa nini mnawaza mabaya mioyoni mwenu?
5Kas gi lengviau­ar pasakyti: ‘Tavo nuodėmės atleistos!’, ar liepti: ‘Kelkis ir vaikščiok!’?
5Ni lipi lililo rahisi zaidi: kusema, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Simama, utembee?
6Ir todėl, kad žinotumėte Žmogaus Sūnų turint galią žemėje atleisti nuodėmes,­čia Jis kreipėsi į paralyžiuotąjį:­Kelkis, pasiimk savo gultą ir eik namo!”
6Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anao uwezo wa kuwasamehe watu dhambi duniani." Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza, "Inuka, chukua kitanda chako, uende nyumbani kwako."
7Šis atsikėlė ir nuėjo į savo namus.
7Huyo mtu aliyekuwa amepooza akainuka, akaenda nyumbani kwake.
8Visa tai pamačiusios, minios stebėjosi ir šlovino Dievą, suteikusį tokią galią žmonėms.
8Watu wote katika ule umati walipoona hayo, walishangaa na kuogopa; wakamtukuza Mungu aliyewapa binadamu uwezo wa namna hiyo.
9Iškeliaudamas iš ten, Jėzus pamatė muitinėje sėdintį žmogų, vardu Matą, ir tarė jam: “Sek paskui mane!” Šis atsikėlė ir nusekė paskui Jį.
9Yesu aliondoka hapo, na alipokuwa anakwenda zake, alimwona mtu mmoja aitwaye Mathayo, ameketi katika ofisi ya ushuru. Basi, Yesu akamwambia, "Nifuate." Naye Mathayo akainuka, akamfuata.
10Kai Jėzus sėdėjo namuose prie stalo, ten susirinko daug muitininkų bei nusidėjėlių, kurie susėdo šalia Jo ir Jo mokinių.
10Yesu alipokuwa nyumbani ameketi kula chakula, watoza ushuru wengi na wahalifu walikuja wakaketi pamoja naye na wanafunzi wake.
11Fariziejai, tai išvydę, sakė Jo mokiniams: “Kodėl jūsų Mokytojas valgo su muitininkais ir nusidėjėliais?”
11Mafarisayo walipoona hayo, wakawaambia wanafunzi wake, "Mbona mwalimu wenu anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?"
12Tai išgirdęs, Jėzus atsiliepė: “Ne sveikiesiems reikia gydytojo, o ligoniams.
12Yesu aliwasikia, akasema, "Watu wenye afya hawahitaji daktari; wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa. Sikuja kuwaita watu wema, ila wenye dhambi.
13Eikite ir pasimokykite, ką reiškia žodžiai: ‘Aš noriu gailestingumo, o ne aukos’. Aš atėjau šaukti ne teisiųjų, bet nusidėjėlių atgailai”.
13Basi, kajifunzeni maana ya maneno haya: Nataka huruma, wala si dhabihu. Sikuja kuwaita watu wema, bali wenye dhambi."
14Tada priėjo Jono mokiniai ir paklausė: “Kodėl mes ir fariziejai daug pasninkaujame, o Tavo mokiniai nepasninkauja?”
14Kisha wanafunzi wa Yohane mbatizaji walimwendea Yesu, wakamwuliza, "Sisi na Mafarisayo hufunga mara nyingi; mbona wanafunzi wako hawafungi?"
15Jėzus jiems atsakė: “Argi gali vestuvininkai gedėti, kol su jais yra jaunikis? Bet ateis dienos, kai jaunikis iš jų bus atimtas, ir tada jie pasninkaus.
15Yesu akawajibu, "Je, walioalikwa arusini wanaweza kuomboleza wakati bwana arusi yupo pamoja nao? La hasha! Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kati yao; wakati huo ndipo watakapofunga.
16Niekas sudėvėto drabužio nelopo naujo audinio lopu, nes toks lopinys atplėšia drabužio gabalą, ir pasidaro dar didesnė skylė.
16"Hakuna mtu atiaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kuukuu. Maana kiraka hicho kitararua hilo vazi kuukuu, na pale palipokuwa pameraruka pataongezeka.
17Taip pat niekas nepila jauno vyno į senus vynmaišius, nes antraip vynmaišiai plyštų, vynas išsilietų ir vynmaišiai niekais nueitų. Bet jaunas vynas pilamas į naujus vynmaišius, ir abeji išsilaiko”.
17Wala hakuna mtu awekaye divai mpya katika viriba vikuukuu. Akifanya hivyo, viriba hupasuka na divai ikamwagika, navyo viriba vikaharibika. Ila divai mpya hutiwa katika viriba vipya, na vyote viwili, viriba na divai, vikahifadhiwa salama."
18Jam taip bekalbant, prisiartino vienas vyresnysis, pagarbino Jį ir tarė: “Ką tik mirė mano dukrelė. Bet ateik, uždėk ant jos ranką, ir ji atgis”.
18Yesu alipokuwa akisema hayo, ofisa mmoja Myahudi alifika, akamwinamia na kusema, "Binti yangu amekufa sasa hivi. Lakini, tafadhali njoo umwekee mkono wako naye ataishi."
19Jėzus atsikėlė ir nuėjo paskui jį kartu su savo mokiniais.
19Yesu akaondoka pamoja na wanafunzi wake, akamfuata.
20Ir štai moteris, dvylika metų serganti kraujoplūdžiu, prisiartino iš paskos ir palietė Jo apsiausto apvadą.
20Mama mmoja, mgonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, alimfuata Yesu nyuma, akagusa pindo la vazi lake.
21Mat ji pati sau kalbėjo: “Jei tik palytėsiu Jo drabužį­išgysiu”.
21Alifanya hivyo kwani alifikiri moyoni: "Nikigusa tu vazi lake, nitapona."
22Jėzus, atsigręžęs ir ją pamatęs, tarė: “Pasitikėk, dukra, tavo tikėjimas išgydė tave”. Ir tą pačią akimirką moteris pagijo.
22Basi, Yesu akageuka akamwona, akamwambia, "Binti, jipe moyo! Imani yako imekuponya." Mama huyo akapona saa ileile.
23Atėjęs į vyresniojo namus ir pamatęs vamzdininkus bei šurmuliuojančią minią,
23Kisha Yesu akaingia nyumbani kwa yule ofisa. Na alipowaona wapiga filimbi na umati wa watu wanaofanya matanga,
24Jėzus paliepė: “Pasitraukite, nes mergaitė ne mirus, o miega”. Jie tik šaipėsi iš Jo.
24akasema, "Ondokeni hapa! Msichana huyu hakufa, amelala tu." Nao wakamcheka.
25Kai minia buvo išvaryta, Jis įėjo vidun, paėmė mergaitę už rankos, ir ji atsikėlė.
25Basi, umati wa watu ulipoondolewa, Yesu aliingia ndani, akamshika huyo msichana mkono, naye akasimama.
26Garsas apie tai pasklido po visą aną kraštą.
26Habari hiyo ikavuma sana katika nchi ile yote.
27Jėzui išeinant, du neregiai sekė paskui Jį ir šaukė: “Pasigailėk mūsų, Dovydo Sūnau!”
27Yesu aliondoka hapo, na alipokuwa anakwenda, vipofu wawili walimfuata wakipiga kelele, "Mwana wa Daudi, utuhurumie!"
28Kai Jis pasiekė namus, neregiai užėjo pas Jį. Jėzus paklausė: “Ar tikite, kad Aš galiu tai padaryti?” Šie atsakė: “Taip, Viešpatie!”
28Yesu alipoingia nyumbani, vipofu hao wawili wakamwendea, naye akawauliza, "Je, mnaamini kwamba naweza kuwafanyia jambo hilo?" Nao wakamjibu, "Naam, Mheshimiwa."
29Tada Jis palietė jų akis ir tarė: “Tebūna jums pagal jūsų tikėjimą”.
29Hapo Yesu akayagusa macho yao, akasema, "Na iwe kwenu kama mnavyoamini."
30Ir jų akys atsivėrė. Jėzus griežtai jiems įsakė: “Žiūrėkite, kad niekas nesužinotų!”
30Macho yao yakafunguliwa. Naye Yesu akawaonya kwa ukali: "Msimwambie mtu yeyote jambo hili."
31Tačiau tie išėję išgarsino Jį po visą tą kraštą.
31Lakini wao wakaondoka, wakaeneza habari za Yesu katika nchi ile yote.
32Jiems išėjus, štai atvedė pas Jį demono apsėstą nebylį.
32Watu walipokuwa wanakwenda zao, wengine walimletea Yesu mtu mmoja aliyekuwa bubu kwa sababu alikuwa amepagawa na pepo.
33Išvarius demoną, nebylys prakalbo. Minios stebėjosi ir sakė: “Dar niekad Izraelyje nebuvo tokių dalykų”.
33Mara tu huyo pepo alipotolewa, mtu huyo aliyekuwa bubu akaanza kuongea tena. Watu wakashangaa na kusema, "Jambo kama hili halijapata kuonekana katika Israeli!"
34O fariziejai kalbėjo: “Jis išvaro demonus jų valdovo jėga”.
34Lakini Mafarisayo wakawa wanasema, "Anawatoa pepo kwa nguvu ya mkuu wa pepo wabaya."
35Jėzus ėjo per visus miestus ir kaimus, mokydamas jų sinagogose, skelbdamas karalystės Evangeliją ir gydydamas visas žmonių ligas bei negalias.
35Yesu alitembelea miji yote na vijiji, akafundisha katika masunagogi yao akihubiri Habari Njema ya Ufalme wa Mungu, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila namna.
36Matydamas minias, Jis gailėjosi žmonių, nes jie buvo suvargę ir išsklaidyti lyg avys be piemens.
36Basi, alipowaona watu, makundi kwa makundi, aliwaonea huruma kwa sababu walikuwa hoi na wenye wasiwasi kama kondoo wasio na mchungaji.
37Tuomet Jis tarė savo mokiniams: “Pjūtis didelė, o darbininkų maža.
37Hapo akawaambia wanafunzi wake, "Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache.
38Todėl melskite pjūties Viešpatį, kad siųstų darbininkų į savo pjūtį”.
38Kwa hivyo mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake."