1Pasišaukęs dvylika savo mokinių, Jis suteikė jiems valdžią netyrosioms dvasioms, kad išvarinėtų jas ir gydytų visas ligas bei negalias.
1Yesu aliwaita wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa uwezo wa kutoa pepo wachafu na kuponya magonjwa na maradhi yote.
2Dvylikos apaštalų vardai: pirmasis Simonas, vadinamas Petru, ir jo brolis Andriejus; Zebediejaus sūnus Jokūbas ir jo brolis Jonas;
2Majina ya hao mitume kumi na wawili ni haya: wa kwanza ni Simoni aitwae Petro, na Andrea ndugu yake; Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohane ndugu yake;
3Pilypas ir Baltramiejus; Tomas ir muitininkas Matas; Alfiejaus sūnus Jokūbas ir Lebėjus, vadinamas Tadu;
3Filipo na Bartholomayo, Thoma na Mathayo aliyekuwa mtoza ushuru; Yakobo mwana wa Alfayo, na Thadayo;
4Simonas Kananietis ir Judas Iskarijotas, kuris išdavė Jėzų.
4Simoni Mkanaani, na Yuda Iskarioti ambaye alimsaliti Yesu.
5Šiuos dvylika Jėzus išsiuntė, įsakydamas jiems: “Nepasukite keliu pas pagonis ir neužeikite į samariečių miestą,
5Yesu aliwatuma hao kumi na wawili na kuwapa maagizo haya: "Msiende kwa watu wa mataifa mengine, wala msiingie katika mji wa Wasamaria.
6bet verčiau eikite pas pražuvusias Izraelio namų avis.
6Ila nendeni kwa watu wa Israeli waliopotea kama kondoo.
7Keliaudami skelbkite: ‘Prisiartino dangaus karalystė!’
7Mnapokwenda hubirini hivi: Ufalme wa mbinguni umekaribia.
8Gydykite ligonius, apvalykite raupsuotuosius, prikelkite mirusius, išvarinėkite demonus. Dovanai gavote, dovanai ir duokite!
8Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo. Mmepewa bure, toeni bure.
9Neimkite nei aukso, nei sidabro, nei variokų į savo juostas;
9Msichukue mifukoni mwenu dhahabu, wala fedha, wala sarafu za shaba.
10nei kelionmaišio, nei dviejų tunikų, nei sandalų, nei lazdos, nes darbininkas vertas savo valgio.
10Msichukue mkoba wa kuombea njiani, wala koti la ziada, wala viatu, wala fimbo. Maana mfanyakazi anastahili riziki yake.
11Atėję į kokį nors miestą ar kaimą, susiieškokite vertą žmogų ir apsistokite pas jį, kol išvyksite.
11"Mkiingia katika mji wowote au kijiji, tafuteni humo mtu yeyote aliye tayari kuwakaribisheni, na kaeni naye mpaka mtakapoondoka mahali hapo.
12Įeidami į namus, pasveikinkite juos.
12Mnapoingia nyumbani wasalimuni wenyeji wake.
13Ir jeigu namai bus verti, teateinie jiems jūsų ramybė. O jeigu nebus vertijūsų ramybė tesugrįžta jums.
13Kama wenyeji wa nyumba hiyo wakiipokea salamu hiyo, basi, amani yenu itakaa pamoja nao. Lakini ikiwa hawaipokei, basi amani yenu itawarudia ninyi.
14Jei kas jūsų nepriimtų ir neklausytų jūsų žodžių, tai, išėję iš tokių namų ar tokio miesto, nusikratykite ir dulkes nuo kojų.
14Kama mtu yeyote atakataa kuwakaribisheni au kuwasikilizeni, basi mtokapo katika nyumba hiyo au mji huo, yakung'uteni mavumbi miguuni mwenu kama onyo kwao.
15Iš tiesų sakau jums: Sodomos ir Gomoros žemei bus lengviau teismo dieną negu tokiam miestui”.
15Kweli nawaambieni, Siku ya hukumu mji huo utapata adhabu kubwa kuliko ile iliyoipata miji ya Sodoma na Gomora.
16“Štai Aš siunčiu jus kaip avis tarp vilkų. Todėl būkite gudrūs kaip žalčiai ir neklastingi kaip balandžiai.
16"Sasa, mimi nawatuma ninyi kama kondoo kati ya mbwa mwitu. Muwe na busara kama nyoka, na wapole kama njiwa.
17Saugokitės žmonių, nes jie įskųs jus teismams ir plaks savo sinagogose.
17Jihadharini na watu, maana watawapeleka ninyi mahakamani na kuwapiga viboko katika masunagogi yao.
18Jūs būsite dėl manęs vedžiojami pas valdytojus ir karalius liudyti jiems ir pagonims.
18Mtapelekwa mbele ya watawala na wafalme kwa sababu yangu, mpate kutangaza Habari Njema kwao na kwa mataifa.
19Kai jie jus įskųs, nesirūpinkite, kaip arba ką kalbėsite, nes tą valandą jums bus duota, ką jūs turite sakyti.
19Basi, watakapowapeleka ninyi mahakamani, msiwe na wasiwasi mtasema nini au namna gani; wakati utakapofika, mtapewa la kusema.
20Nes ne jūs kalbėsite, o jūsų Tėvo Dvasia kalbės jumyse.
20Maana si ninyi mtakaosema, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu.
21Brolis išduos mirti brolį ir tėvassūnų, o vaikai sukils prieš gimdytojus ir žudys juos.
21"Ndugu atamsaliti ndugu yake auawe, na baba atamsaliti mwanawe, nao watoto watawashambulia wazazi wao na kuwaua.
22Jūs būsite visų nekenčiami dėl mano vardo. Bet kas ištvers iki galo, bus išgelbėtas.
22Watu wote watawachukieni kwa sababu ya jina langu. Lakini atakayevumilia mpaka mwisho, ataokolewa.
23Kai jus persekios viename mieste, bėkite į kitą. Iš tiesų sakau jums: dar nebūsite išvaikščioję Izraelio miestų, kai ateis Žmogaus Sūnus.
23"Watu wakiwadhulumu katika mji mmoja, kimbilieni mji mwingine. Kweli nawaambieni, hamtamaliza ziara yenu katika miji yote ya Israeli kabla Mwana wa Mtu hajafika.
24Mokinys nėra aukštesnis už savo mokytoją nei tarnas už šeimininką.
24"Mwanafunzi si mkuu kuliko mwalimu wake, wala mtumishi si mkuu kuliko bwana wake.
25Pakanka, jei mokinys prilygsta mokytojui ir tarnas šeimininkui. Jei namų šeimininką jie praminė Belzebulu, tai ką bekalbėti apie namiškius!”
25Yatosha mwanafunzi kuwa kama mwalimu wake, na mtumishi kuwa kama bwana wake. Ikiwa wamemwita mkubwa wa jamaa Beelzebuli, je hawatawaita watu wengine wa jamaa hiyo majina mabaya zaidi?
26“Taigi nebijokite jų. Nes nieko nėra uždengta, kas nebus atidengta, ir nieko paslėpta, kas nepasidarys žinoma.
26"Basi, msiwaogope watu hao. Kila kilichofunikwa kitafunuliwa, na kila kilichofichwa kitafichuliwa.
27Ką jums kalbu tamsoje, sakykite šviesoje, ir ką šnibždu į ausį, skelbkite nuo stogų.
27Ninalowaambieni ninyi katika giza, lisemeni katika mwanga; na jambo mlilosikia likinong'onezwa, litangazeni hadharani.
28Nebijokite tų, kurie žudo kūną, bet negali užmušti sielos. Verčiau bijokite to, kuris gali pražudyti ir sielą, ir kūną pragare.
28Msiwaogope wale wauao mwili, lakini hawawezi kuiua roho. Afadhali zaidi kumwogopa yule awezaye kuuangamiza mwili pamoja na roho katika moto wa Jehanamu.
29Argi ne du žvirbliai parduodami už skatiką? Ir nė vienas iš jų nekrinta žemėn be jūsų Tėvo valios.
29Shomoro wawili huuzwa kwa senti tano. Lakini hata mmoja wao haanguki chini bila kibali cha Baba yenu.
30O jūsų net visi galvos plaukai suskaičiuoti.
30Lakini kwa upande wenu, hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote.
31Tad nebijokite! Jūs vertesni už daugybę žvirblių.
31Kwa hiyo msiogope; ninyi mu wa thamani kuliko shomoro wengi.
32Kas išpažins mane žmonių akivaizdoje, ir Aš jį išpažinsiu savo dangiškojo Tėvo akivaizdoje.
32"Kila mtu anayekiri hadharani kwamba yeye ni wangu, mimi pia nitamkiri mbele ya Baba yangu aliye mbinguni.
33O kas išsižadės manęs žmonių akivaizdoje, ir Aš jo išsižadėsiu savo dangiškojo Tėvo akivaizdoje”.
33Lakini yeyote atakayenikana hadharani, nami nitamkana mbele ya Baba yangu aliye mbinguni.
34“Nemanykite, jog Aš atėjau atnešti žemėn ramybės. Atėjau atnešti ne ramybės, o kalavijo.
34"Msidhani kwamba nimekuja kuleta amani duniani. Sikuja kuleta amani bali upanga.
35Atėjau sukiršinti ‘sūnaus prieš tėvą, dukters prieš motiną ir marčios prieš anytą.
35Maana nimekuja kuleta mafarakano kati ya mtu na baba yake, kati ya binti na mama yake, kati ya mkwe na mkwe wake.
36Žmogaus namiškiai taps jam priešais’.
36Na maadui wa mtu ni watu wa nyumbani mwake.
37Kas myli tėvą ar motiną labiau negu manenevertas manęs. Kas myli sūnų ar dukterį labiau negu manenevertas manęs.
37"Ampendaye baba au mama yake kuliko anipendavyo mimi, hanistahili. Ampendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.
38Kas neima savo kryžiaus ir neseka paskui mane, tas nevertas manęs.
38Mtu asiyechukua msalaba wake na kunifuata, hanistahili.
39Kas išsaugo savo gyvybę, praras ją, o kas praranda savo gyvybę dėl manęsatras ją.
39Anayeyashikilia maisha yake, atayapoteza; lakini anayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu, atayapata.
40Kas jus priima, tas mane priima. O kas priima mane, priima Tą, kuris mane siuntė.
40"Anayewakaribisha ninyi, ananikaribisha mimi; na anayenikaribisha mimi, anamkaribisha yule aliyenituma.
41Kas priima pranašą dėl to, kad jis pranašas, gaus pranašo atlygį. Kas priima teisųjį dėl to, kad jis teisusis, gaus teisiojo atlygį.
41Anayemkaribisha nabii kwa sababu ni nabii, atapokea tuzo la nabii. Anayemkaribisha mtu mwema kwa sababu ni mtu mwema, atapokea tuzo la mtu mwema.
42Ir kas paduos bent taurę šalto vandens vienam iš šitų mažųjų dėl to, kad jis yra mokinys,iš tiesų sakau jums,tas nepraras savo atlygio”.
42Kweli nawaambieni, yeyote atakayempa mmojawapo wa wadogo hawa kikombe cha maji baridi kwa sababu ni mfuasi wangu, hatakosa kamwe kupata tuzo lake."