1Aš išvydau dar vieną galingą angelą, nužengiantį iš dangaus, apsisiautusį debesimi. Jo galvą supo vaivorykštė, veidas švytėjo kaip saulė ir kojostarsi ugnies stulpai.
1Kisha nikamwona malaika mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni. Alikuwa amevikwa wingu, na upinde wa mvua kichwani mwake. Uso wake ulikuwa kama jua, na miguu yake ilikuwa kama moto.
2Jis laikė rankoje išvyniotą knygelę. Ir Jis atsistojo dešiniąja koja ant jūros, o kairiąja ant sausumos,
2Mikononi mwake alishika kitabu kidogo kimefunguliwa. Aliweka mguu wake wa kulia juu ya bahari, na wa kushoto juu ya nchi kavu,
3ir ėmė šaukti galingu balsu tartum riaumojantis liūtas. Kai jis sušuko, atsiliepė septyni griaustiniai savais balsais.
3na kuita kwa sauti kubwa kama ya mngurumo wa simba. Alipopaaza sauti, ngurumo saba ziliitikia kwa kishindo.
4Septyniems griaustiniams prabilus savais balsais, puoliausi rašyti, bet išgirdau iš dangaus balsą, sakantį man: “Užantspauduok, ką pasakė septyni griaustiniai, ir to nerašyk!”
4Na hizo ngurumo saba ziliposema, mimi nikataka kuandika. Lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni: "Maneno ya ngurumo hizo saba ni siri; usiyaandike!"
5O angelas, kurį mačiau stovint ant jūros ir ant sausumos, pakėlė savo ranką į dangų
5Kisha yule malaika niliyemwona akisimama juu ya bahari na juu ya nchi kavu akainua mkono wake wa kulia juu mbinguni,
6ir prisiekė Gyvenančiuoju per amžių amžius, kuris sutvėrė dangų ir visa, kas jame, žemę ir visa, kas joje, bei jūrą ir visa, kas joje,kad laiko daugiau nebebus,
6akaapa kwa jina la Mungu aishiye milele na milele, Mungu aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, bahari na vyote vilivyomo, dunia na vyote vilivyomo. Akasema, "Wakati wa kusubiri zaidi umekwisha!
7bet septintojo angelo trimitavimo dienomis bus baigta Dievo paslaptis, kaip Jis yra paskelbęs Gerąją naujieną savo tarnams pranašams.
7Lakini wakati ule malaika wa saba atakapotoa sauti yake, wakati atakapopiga tarumbeta yake, Mungu atakamilisha mpango wake wa siri kama alivyowatangazia watumishi wake manabii."
8Tuomet balsas, kurį girdėjau iš dangaus, vėl ėmė kalbėti man ir tarė: “Eik, paimk atvyniotą knygelę iš angelo rankos, stovinčio ant jūros ir sausumos”.
8Kisha ile sauti niliyokuwa nimeisikia kutoka mbinguni pale awali ikasema nami tena: "Nenda ukakichukue kile kitabu kilichofunguliwa, kilicho mkononi mwa malaika asimamaye juu ya bahari na juu ya nchi kavu."
9Aš nuėjau pas angelą ir paprašiau, kad duotų man knygelę. O jis man tarė: “Imk ir suvalgyk ją! Ji bus karti viduriuose, bet burnoje ji bus saldi kaip medus”.
9Basi, nikamwendea huyo malaika, nikamwambia anipe hicho kitabu kidogo. Naye akaniambia, "Kichukue, ukile; kinywani mwako kitakuwa kitamu kama asali, lakini tumboni kitakuwa kichungu!"
10Ir aš paėmiau knygelę iš angelo rankos ir ją suvalgiau. Ji buvo mano burnoje saldi tarytum medus, bet kai prarijau, mano viduriuose ji apkarto.
10Basi, nikakichukua kitabu hicho kidogo kutoka mkononi mwa huyo malaika, nikakila; nacho kilikuwa kitamu kinywani mwangu kama asali, lakini nilipokimeza kikawa kichungu tumboni mwangu.
11Ir jis pasakė man: “Tu turi vėl pranašauti apie daugelį žmonių, tautų, kalbų ir karalių”.
11Kisha nikaambiwa, "Inakubidi tena kutangaza ujumbe wa Mungu kuhusu watu wengi, mataifa, watu wa lugha nyingi na wafalme!"