1Ir pasirodė danguje didingas ženklas: moteris, apsisiautusi saule, po jos kojų mėnulis, o ant galvos dvylikos žvaigždžių vainikas.
1Kisha ishara kubwa ikaonekana mbinguni. Palikuwa hapo mwanamke aliyevikwa jua, na mwezi chini ya miguu yake, na taji ya nyota kumi na mbili juu ya kichwa chake!
2Ji buvo nėščia ir šaukė, kentėdama sąrėmius bei gimdymo skausmus.
2Alikuwa mja mzito, na akapaaza sauti kwa maumivu na uchungu wa kujifungua mtoto.
3Pasirodė ir kitas ženklas danguje: štai milžiniškas ugniaspalvis slibinas su septyniomis galvomis, su dešimčia ragų ir su septyniomis diademomis ant galvų.
3Ishara nyingine ikatokea mbinguni: joka kubwa jekundu na lenye pembe kumi na vichwa saba; na kila kichwa kilikuwa na taji.
4Jo uodega nušlavė trečdalį dangaus žvaigždžių ir nužėrė jas žemėn. Slibinas stojo priešais moterį, kad, jai pagimdžius, prarytų jos kūdikį.
4Joka hilo liliburuta kwa mkia wake theluthi moja ya nyota za anga na kuzitupa duniani. Nalo lilisimama mbele ya huyo mama aliyekuwa karibu kujifungua mtoto, tayari kabisa kummeza mtoto, mara tu atakapozaliwa.
5Ji pagimdė Sūnų, berniuką, kuriam skirta ganyti visas tautas geležine lazda. Ir jos kūdikis buvo paimtas pas Dievą, prie Jo sosto.
5Kisha mama huyo akajifungua mtoto wa kiume, ambaye atayatawala mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Lakini mtoto akanyakuliwa na kupelekwa kwa Mungu na kwenye kiti chake cha enzi.
6O moteris pabėgo į dykumą, kur buvo jai Dievo paruošta vieta, kad tenai ji būtų maitinama tūkstantį du šimtus šešiasdešimt dienų.
6Huyo mama akakimbilia jangwani, ambako Mungu alikuwa amemtayarishia mahali pa usalama ambapo angehifadhiwa kwa muda wa siku elfu moja mia mbili na sitini.
7Ir kilo danguje kova. Mykolas ir jo angelai kovojo su slibinu. Ir kovėsi slibinas ir jo angelai,
7Kisha kukazuka vita mbinguni: Mikaeli na malaika wake walipigana na hilo joka, nalo likawashambulia pamoja na malaika wake.
8bet jie nenugalėjo, ir nebeliko daugiau jiems vietos danguje.
8Lakini joka hilo halikuweza kuwashinda, na hatimaye hapakuwa tena na nafasi mbinguni kwa ajili yake na malaika wake.
9Taip buvo išmestas didysis slibinas, senoji gyvatė, vadinamas Velniu ir Šėtonu, kuris suvedžioja visą pasaulį. Jis buvo išmestas žemėn, ir kartu su juo buvo išmesti jo angelai.
9Basi, joka hilo kuu likatupwa nje. Joka hilo ndiye yule nyoka wa kale ambaye huitwa pia Ibilisi au Shetani. Ndiye anayeudanganya ulimwengu wote. Naam, alitupwa duniani, na malaika wake wote pamoja naye.
10Aš girdėjau danguje galingą balsą, sakantį: “Dabar atėjo mūsų Dievo išgelbėjimas, galybė, karalystė ir Jo Kristaus valdžia, nes išmestas mūsų brolių kaltintojas, skundęs juos mūsų Dievui dieną ir naktį.
10Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka mbinguni ikisema: "Sasa ukombozi utokao kwa Mungu umefika! Nguvu na Utawala wa Mungu wetu umedhihirika. Na Kristo wake ameonyesha mamlaka yake! Maana yule mdhalimu wa ndugu zetu, aliyesimama mbele ya Mungu akiwashtaki usiku na mchana, sasa ametupwa nje.
11Ir jie nugalėjo jį Avinėlio krauju ir savo liudijimo žodžiu. Jie nebrangino savo gyvybės, net iki mirties.
11Ndugu zetu wameshinda kwa damu ya Mwanakondoo na kwa nguvu ya ukweli walioutangaza; maana hawakuyathamini maisha yao kuwa kitu sana, wakawa tayari kufa.
12Todėl džiūgaukite, dangūs ir jų gyventojai! Bet vargas gyvenantiems žemėje ir jūrai, nes pas jus numestas velnias, kupinas didelio įniršio, žinodamas mažai beturįs laiko”.
12Kwa sababu hiyo, furahini enyi mbingu na vyote vilivyomo ndani yenu. Lakini, ole wenu nchi na bahari, maana Ibilisi amewajieni akiwa na ghadhabu kuu, kwa sababu anajua kwamba siku zake zilizobakia ni chache."
13Slibinas, pamatęs, kad yra nutrenktas žemėn, ėmė persekioti moterį, kuri buvo pagimdžiusi berniuką.
13Joka lilipotambua kwamba limetupwa chini duniani, likaanza kumwinda yule mama aliyekuwa amejifungua mtoto wa kiume.
14Bet moteriai buvo duoti du didžiojo erelio sparnai skristi nuo gyvatės į dykumą, į savo vietą, kur bus maitinama per laiką, laikus ir pusę laiko.
14Lakini mama huyo akapewa mabawa mawili ya tai apate kuruka mbali sana na hilo joka, mpaka mahali, pake jangwani ambapo angehifadhiwa salama kwa muda wa miaka mitatu na nusu.
15Gyvatė išliejo iš savo nasrų paskui moterį vandenį lyg upę, kad nuplukdytų ją bangomis.
15Basi, joka likatapika maji mengi kama mto, yakamfuata huyo mama nyuma ili yamchukue.
16Bet žemė pagelbėjo moteriai: žemė atvėrė savo žiotis ir sugėrė upę, kurią slibinas buvo paliejęs iš savo nasrų.
16Lakini nchi ikamsaidia huyo mama: ikajifunua kama mdomo na kuyameza maji hayo yaliyotoka kinywani mwa hilo joka.
17Ir slibinas įnirto prieš moterį, ir metėsi kautis su kitais jos palikuonimis, kurie laikosi Dievo įsakymų ir turi Jėzaus Kristaus liudijimą.
17Basi, joka hilo likamkasirikia huyo mama, likajiondokea, likaenda kupigana na wazawa wengine wa huyo mama, yaani wote wanaotii amri za Mungu na kuuzingatia ukweli wa Yesu.