1Aš stovėjau ant jūros kranto. Ir išvydau iš jūros išnyrant žvėrį, turintį septynias galvas ir dešimt ragų, o ant jo ragų buvo dešimt diademų ir ant jo galvų piktžodžiavimo vardas.
1(G12-18) Na likajisimamia ukingoni mwa bahari. (G13-1) Kisha nikaona mnyama mmoja akitoka baharini. Alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na kila pembe ilikuwa na taji. Jina la kashfa lilikuwa limeandikwa juu ya vichwa hivyo.
2Žvėris, kurį mačiau, buvo panašus į leopardą; jo kojos tarytum lokio kojos, o jo snukislyg liūto snukis. Slibinas davė jam savo jėgą, savo sostą ir didelę valdžią.
2Mnyama huyo niliyemwona alikuwa kama chui; miguu yake ilikuwa kama ya dubu, na kinywa chake kama cha simba. Lile joka likampa huyo mnyama nguvu yake, kiti chake cha enzi na uwezo mkuu.
3Ir aš mačiau vieną iš jo galvų mirtinai sužeistą, tačiau jos mirštamoji žaizda užgijo. Ir visa žemė stebėdamasi nusekė paskui žvėrį.
3Kichwa kimojawapo cha huyo mnyama kilionekana kama kilikwisha jeruhiwa vibaya sana, lakini jeraha hilo lilikuwa limepona. Dunia nzima ilishangazwa na huyo mnyama na kumfuata.
4Žmonės garbino slibiną, kuris atidavė valdžią žvėriui. Jie garbino žvėrį, sakydami: “Kas galėtų lygintis su žvėrimi, ir kas galėtų kovoti su juo!”
4Watu wote wakaliabudu lile joka kwa sababu lilimpa huyo mnyama uwezo wake. Wakamwabudu pia huyo mnyama wakisema, "Nani aliye kama huyu mnyama? Ni nani awezaye kupigana naye?"
5Jam buvo duotas snukis kalbėti išdidžiai ir piktžodžiauti, ir duota valdžia taip daryti per keturiasdešimt du mėnesius.
5Kisha huyo mnyama akaruhusiwa kusema maneno ya kujigamba na kumkufuru Mungu; akaruhusiwa kuwa na mamlaka kwa muda wa miezi arobaini na miwili.
6Ir jis atvėrė nasrus piktžodžiauti Dievui, piktžodžiauti Jo vardui, Jo buveinei ir dangaus gyventojams.
6Basi, akaanza kumtukana Mungu, kulitukana jina lake, makao yake, na wote wakaao mbinguni.
7Jam buvo duota kovoti su šventaisiais ir juos nugalėti. Jam buvo suteikta valdžia visoms gentims, kalboms ir tautoms.
7Aliruhusiwa kuwapiga vita na kuwashinda watu wa Mungu. Alipewa mamlaka juu ya watu wa kila kabila, ukoo, lugha na taifa.
8Ir jį garbins visi tie žemės gyventojai, kurių vardai neįrašyti nuo pasaulio sutvėrimo nužudytojo Avinėlio gyvenimo knygoje.
8Wote waishio duniani watamwabudu isipokuwa tu wale ambao majina yao yameandikwa tangu mwanzo wa ulimwengu katika kitabu cha uzima cha Mwanakondoo aliyechinjwa.
9Kas turi ausis, teklauso.
9"Aliye na masikio, na asikie!
10Jei kas veda į nelaisvę, pats į nelaisvę eis. O kas žudo kalaviju, turės nuo kalavijo žūti. Čia šventųjų ištvermė ir tikėjimas!
10Waliokusudiwa kuchukuliwa mateka lazima watatekwa; waliokusudiwa kuuawa kwa upanga lazima watauawa kwa upanga. Kutokana na hayo ni lazima watu wa Mungu wawe na uvumilivu na imani."
11Ir aš pamačiau kitą žvėrį, ateinantį iš žemės. Jis turėjo du ragus, panašius į Avinėlio, ir kalbėjo kaip slibinas.
11Kisha nikamwona mnyama mwingine anatoka ardhini. Alikuwa na pembe mbili kama pembe za kondoo, na aliongea kama joka.
12Jis naudojasi visa pirmojo žvėries valdžia jo akivaizdoje ir verčia žemę bei jos gyventojus garbinti pirmąjį žvėrį, kurio mirštama žaizda užgijo.
12Alikuwa na mamlaka kamili kutoka kwa yule mnyama wa kwanza, na akautumia uwezo huo mbele ya huyo mnyama. Akailazimisha dunia yote na wote waliomo humo kumwabudu huyo mnyama wa kwanza ambaye alikuwa na jeraha la kifo lililokuwa limepona.
13Jis daro didžius ženklus, netgi, žmonėms matant, nuleidžia ugnį iš dangaus į žemę.
13Basi, huyu mnyama wa pili akafanya miujiza mikubwa hata akasababisha moto kutoka mbinguni ushuke duniani mbele ya watu.
14Jis suvedžioja žemės gyventojus tais ženklais, kuriuos jam buvo duota daryti žvėries akyse, sakydamas žemės gyventojams padaryti žvėries atvaizdą, kuris gavo žaizdą nuo kalavijo ir išgijo.
14Aliwapotosha wakazi wa dunia kwa miujiza hiyo aliyojaliwa kutenda mbele ya mnyama wa kwanza. Aliwaambia wakazi wa dunia watengeneze sanamu kwa heshima ya yule mnyama aliyekuwa amejeruhiwa kwa upanga lakini akaishi tena.
15Jam buvo duota suteikti žvėries atvaizdui dvasią, kad žvėries atvaizdas imtų kalbėti, ir padaryti taip, kad visi, kurie atsisakys garbinti žvėries atvaizdą, būtų nužudyti.
15Kisha alijaliwa kuipulizia uhai hiyo sanamu ya yule mnyama wa kwanza, hata ikaweza kuongea na kuwaua watu wote ambao hawakuiabudu.
16Jis vertė visus, mažus ir didelius, turtuolius ir vargšus, laisvuosius ir vergus, pasidaryti ženklą ant dešinės rankos arba ant kaktos,
16Aliwalazimisha wote, wadogo na wakubwa, matajiri na maskini, watu huru na watumwa, watiwe alama juu ya mikono yao ya kulia au juu ya paji za nyuso zao.
17kad nė vienas negalėtų nei pirkti, nei parduoti, jei neturės to ženklo ar žvėries vardo, ar jo vardo skaičiaus.
17Akapiga marufuku mtu yeyote kununua au kuuza kitu isipokuwa tu mtu aliyetiwa alama hiyo, yaani jina la yule mnyama au tarakimu ya jina hilo.
18Čia slypi išmintis! Kas turi išmanymą, teapskaičiuoja žvėries skaičių, nes tai žmogaus skaičius; jo skaičius yra šeši šimtai šešiasdešimt šeši.
18Hapa ni lazima kutumia ujasiri! Mwenye akili anaweza kufafanua maana ya tarakimu ya mnyama huyo, maana ni tarakimu yenye maana ya mtu fulani. Tarakimu hiyo ni mia sita sitini na sita.