1Ir aš pamačiau danguje dar vieną didį ir įspūdingą ženklą: septynis angelus, turinčius septynias paskutines negandas, nes jomis išsibaigia Dievo rūstybė.
1Kisha nikaona ishara nyingine mbinguni, kubwa na ya kushangaza. Palikuwa hapo malaika saba wenye mabaa makubwa saba ya mwisho. Kwa mabaa hayo makubwa saba, ghadhabu ya Mungu imekamilishwa.
2Aš išvydau tarsi stiklo jūrą, sumaišytą su ugnimi, ir nugalėjusiuosius žvėrį, jo atvaizdą, jo ženklą ir jo vardo skaičių, stovinčius su Dievo arfomis ant stiklo jūros.
2Kisha nikaona kitu kama bahari ya kioo, imechanganywa na moto. Nikawaona pia wale watu waliomshinda yule mnyama na sanamu yake na ambaye jina lake lilitajwa kwa ile tarakimu. Watu hao walikuwa wamesimama kando ya hiyo bahari ya kioo, wakiwa na vinubi walivyopewa na Mungu.
3Jie giedojo Dievo tarno Mozės giesmę ir Avinėlio giesmę: “Didingi ir nuostabūs Tavo darbai, Viešpatie, visagali Dieve! Teisingi ir tikri Tavo keliai, šventųjų Karaliau!
3Walikuwa wakiimba wimbo wa Mose, mtumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwanakondoo: "Bwana Mungu Mwenye Uwezo, matendo yako ni makuu mno! Ewe Mfalme wa mataifa, njia zako ni za haki na za kweli!
4Kas gi nesibijotų Tavęs, Viešpatie, ir nešlovintų Tavojo vardo?! Juk Tu vienas šventas! Visos tautos ateis ir pagarbins Tave, nes apreikšti Tavo teisūs sprendimai”.
4Bwana, ni nani asiyekucha wewe? Nani asiyelitukuza jina lako? Wewe peke yako ni Mtakatifu. Mataifa yote yatakujia na kukuabudu maana matendo yako ya haki yameonekana na wote."
5Paskui aš regėjau: štai atsidarė Liudijimo palapinės šventykla danguje,
5Baada ya hayo nikaona Hekalu limefunguliwa mbinguni, na ndani yake hema ionyeshayo kuwapo kwa Mungu.
6ir išėjo iš šventyklos septyni angelai, turintys septynias negandas. Jie buvo apsivilkę tyra, spindinčia drobe ir persijuosę per krūtines aukso juostomis.
6Basi, wale malaika saba wenye mabaa saba wakatoka humo Hekaluni, wakiwa wamevaa nguo za kitani safi zenye kung'aa, na kanda za dhahabu vifuani mwao.
7Viena iš keturių būtybių padavė septyniems angelams septynis aukso dubenis, pilnus Gyvenančiojo per amžių amžius Dievo rūstybės.
7Kisha, mmojawapo wa vile viumbe vinne akawapa hao malaika saba mabakuli ya dhahabu yaliyojaa ghadhabu ya Mungu, aishiye milele na milele.
8Šventykla prisipildė dūmų nuo Dievo šlovės ir galybės, ir niekas negalėjo įeiti šventyklon, kol nesibaigs septynių angelų septynios negandos.
8Hekalu likajaa moshi uliosababishwa na utukufu na nguvu ya Mungu, na hakuna mtu aliyeweza kuingia Hekaluni mpaka mwisho wa mabaa makubwa saba ya wale malaika saba.