1Tuomet atėjo vienas iš septynių angelų, turėjusių septynis dubenis, ir prakalbino mane, sakydamas: “Eikš, aš parodysiu tau teismą didžiosios paleistuvės, sėdinčios ant daugybės vandenų.
1Mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na bakuli akaja, akaniambia, "Njoo, mimi nitakuonyesha adhabu aliyopewa yule mzinzi mkuu, mji ule uliojengwa juu ya maji mengi.
2Su ja ištvirkavo žemės karaliai, ir jos ištvirkavimo vynu pasigėrė žemės gyventojai”.
2Wafalme wa dunia wamefanya uzinzi pamoja naye; na wakazi wa dunia wamelewa divai ya uzinzi wake."
3Ir jis Dvasia nunešė mane į dykumą. Ir aš išvydau moterį, sėdinčią ant skaisčiai raudono žvėries, pilno piktžodžiavimo vardų, turinčio septynias galvas ir dešimt ragų.
3Kisha, Roho akanikumba, akaniongoza mpaka jangwani. Huko nikamwona mwanamke ameketi juu ya mnyama mwekundu. Mnyama huyo alikuwa ameandikwa kila mahali majina ya makufuru; alikuwa na vichwa saba na pembe kumi.
4Moteris buvo apsivilkusi purpuru ir škarlatu, išsipuošusi auksu, brangakmeniais ir perlais. Ji laikė rankoje aukso taurę, pilną savo ištvirkavimo šlykštybių ir nešvarumų.
4Mwanamke huyo alikuwa amevaa vazi la rangi ya zambarau na nyekundu; alikuwa amejipamba kwa dhahabu, mawe ya thamani na lulu. Mkononi mwake alishika kikombe cha dhahabu ambacho kilikuwa kimejaa machukizo na mambo machafu yanayoonyesha uzinzi wake.
5Ant jos kaktos buvo užrašytas vardas: “Paslaptis, didžioji Babelė, ištvirkėlių ir žemės šlykštybių motina”.
5Alikuwa ameandikwa juu ya paji la uso wake jina la fumbo "Babuloni mkuu, mama wa wazinzi na wa mambo yote ya kuchukiza sana duniani."
6Mačiau tą moterį, girtą nuo šventųjų kraujo ir nuo Jėzaus liudytojų kraujo. Ją matydamas, aš stebėte stebėjausi.
6Nikamwona huyo mwanamke amelewa damu ya watu wa Mungu, na damu ya watu waliouawa kwa sababu ya kumtangaza Yesu. Nilipomwona nilishangaa mno.
7O angelas man tarė: “Ko stebiesi? Aš tau pasakysiu paslaptį moters ir ją nešančio žvėries, kuris turi septynias galvas ir dešimt ragų”.
7Lakini malaika akaniambia, "Kwa nini unashangaa? Mimi nitakuambia maana iliyofichika ya mwanamke huyu na mnyama huyo amchukuaye ambaye ana vichwa saba na pembe kumi.
8“Žvėris, kurį regėjai, buvo, bet jo nebėra; jis ruošiasi išlipti iš bedugnės, tačiau eina į pražūtį. Žemės gyventojai, kurių vardai nėra įrašyti gyvenimo knygoje nuo pasaulio sutvėrimo, stebėsis, žiūrėdami į žvėrį, kad jis buvo ir jo nebėra, ir jis vėl pasirodys.
8Huyo mnyama uliyemwona alikuwa hai hapo awali, lakini sasa amekufa. Hata hivyo, karibu sana atapanda kutoka shimoni kuzimu, lakini ataangamizwa. Wanaoishi duniani watashangaa; naam, watu wote ambao majina yao hayakupata kuandikwa katika kitabu cha uzima tangu mwanzo wa ulimwengu, watashangaa kumwona huyo mnyama ambaye hapo awali, aliishi, kisha akafa na sasa anatokea tena!
9Čia reikia proto, turinčio išmintį! Septynios galvos reiškia septynis kalnus, ant kurių sėdi moteris.
9"Hapa panahitaji akili na hekima! Hivyo vichwa saba ni vilima saba, na huyo mwanamke anaketi juu yake. Vichwa hivyo pia ni wafalme saba.
10Taip pat yra septyni karaliai; penki žlugo, vienas tebėra, o vienas dar neatėjo; kai jis ateis, turės trumpam pasilikti.
10Kati ya hao wafalme saba, watano wamekwisha angamia, mmoja anatawala bado, na yule mwingine bado hajafika; na atakapofika atabaki kwa muda mfupi.
11O žvėris, kuris buvo ir kurio nebėra,tai aštuntasis, bet vienas iš septynių, ir jis eina į pražūtį.
11Huyo mnyama ambaye alikuwa anaishi hapo awali lakini sasa haishi tena ni mfalme wa nane, naye pia ni miongoni mwa hao saba, na anakwenda zake kuharibiwa.
12Tie dešimt ragų, kuriuos matei, yra dešimt karalių, kurie dar negavo karalystės, bet jie gaus valdžią kaip karaliai vienai valandai kartu su žvėrimi.
12"Zile pembe kumi ulizoziona ni wafalme ambao bado hawajaanza kutawala. Lakini watapewa mamlaka ya kutawala kwa muda wa saa moja pamoja na yule mnyama.
13Jie turi vieną tikslą ir savo jėgą bei valdžią atiduos žvėriui.
13Shabaha ya hawa kumi ni moja, na watampa yule mnyama nguvu na mamlaka yao yote.
14Jie kovos su Avinėliu, bet Avinėlis juos nugalės, nes Jis yra viešpačių Viešpats ir karalių Karalius, ir su juo visi pašauktieji, išrinktieji ir ištikimieji”.
14Watapigana na Mwanakondoo, lakini Mwanakondoo pamoja na wale aliowaita na kuwachagua, ambao ni waaminifu, atawashinda kwa sababu yeye ni Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme."
15Angelas toliau man sako: “Vandenys, kuriuos regėjai, kur sėdi paleistuvė, yra žmonės, minios, tautos ir kalbos.
15Malaika akaniambia pia, "Yale maji uliyoyaona pale alipokaa yule mzinzi, ni mataifa, watu wa kila rangi na lugha.
16Tie dešimt ragų, kuriuos matei ant žvėriesjie ims nekęsti paleistuvės, apiplėš ją ir paliks ją nuogą, ės jos kūną ir ją pačią sudegins ugnyje.
16Pembe zile kumi ulizoziona na yule mnyama watamchukia huyo mzinzi. Watachukua kila kitu alicho nacho na kumwacha uchi; watakula nyama yake na kumteketeza kwa moto.
17Nes Dievas įkvėpė jų širdis vykdyti Jo tikslą, vykdyti vieną tikslą,kad jie atiduotų savo karalystę žvėriui, kol išsipildys Dievo žodžiai.
17Maana Mungu ametia mioyoni mwao nia ya kutekeleza shabaha yake, yaani kwa kukubaliana wao kwa wao na kumpa huyo mnyama mamlaka yao ya kutawala, mpaka hapo neno la Mungu litakapotimia.
18Ta moteris, kurią regėjai, yra didysis miestas, valdantis žemės karalius”.
18"Na yule mwanamke uliyemwona ndio ule mji mkuu unaowatawala wafalme wa dunia."