1Paskui aš išvydau kitą angelą, nužengiantį iš dangaus ir turintį didžią valdžią. Žemė nušvito nuo jo šlovės.
1Baada ya hayo, nilimwona malaika mwingine akishuka kutoka mbinguni. Alikuwa na uwezo mkuu, na dunia ikamulikwa na mng'ao wake.
2O jis šaukė galingai, stipriu balsu: “Krito, krito didžioji Babelė! Ji pavirto demonų buveine, visų netyrųjų dvasių pastoge, visų nešvarių ir nekenčiamų paukščių narvu.
2Basi, akapaaza sauti kwa nguvu akisema, "Umeanguka; Babuloni mkuu umeanguka! Sasa umekuwa makao ya mashetani na pepo wachafu; umekuwa makao ya ndege wachafu na wa kuchukiza mno.
3Nuo jos ištvirkimo įniršio vyno buvo girtos visos tautos; žemės karaliai su ja ištvirkavo, o žemės pirkliai pralobo iš jos nežabotos prabangos”.
3Maana mataifa yote yalileweshwa kwa divai kali ya uzinzi wake, nao wafalme wa dunia wamefanya uzinzi naye. Nao wafanyabiashara wa dunia wametajirika kutokana na anasa zake zisizo na kipimo."
4Ir aš išgirdau iš dangaus kitą balsą, skelbiantį: “Išeikite iš jos, mano žmonės, kad nedalyvautumėte jos nuodėmėse ir nepatirtumėte jos negandų!
4Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni ikisema, "Watu wangu, ondokeni kwake, ili msishirikiane naye katika dhambi zake, msije mkaipata adhabu yake.
5Nes jos nuodėmės pasiekė dangų, ir Dievas prisiminė jos piktadarystes.
5Kwa maana dhambi zake zimekuwa nyingi mno, zimelundikana mpaka mbinguni, na Mungu ameyakumbuka maovu yake.
6Atmokėkite jai, kaip ji jums atlygino, ir atiduokite dvigubai pagal jos darbus. Dvigubai sumaišykite taurę, kurią ji jums maišė.
6Mtendeeni kama alivyowatendea ninyi; mlipeni mara mbili kwa yale aliyoyatenda. Jazeni kikombe chake kwa kinywaji kikali mara mbili zaidi ya kile alichowapeni.
7Kiek ji puikavo ir lėbavo, tiek jai paruoškite kentėjimų ir nuliūdimo, nes ji savo širdyje kalba: ‘Aš sėdžiu kaip karalienė, nesu našlė ir liūdesio nematysiu’.
7Mpeni mateso na uchungu kadiri ya kujigamba kwake, na kuishi kwake kwa anasa. Maana anajisemea moyoni: Ninaketi hapa; mimi ni malkia. Mimi si mjane, wala sitapatwa na uchungu!
8Todėl vieną dieną ją apniks negandos: mirtis, gedulas, badas, ir ji bus sudeginta ugnyje, nes galingas yra Viešpats Dievas, kuris nuteisė ją.
8Kwa sababu hiyo mabaa yake yatampata kwa siku moja: ugonjwa, huzuni na njaa. Atachomwa moto, maana Bwana Mungu mwenye kumhukumu ni Mwenye Uwezo."
9Jos verks ir raudos žemės karaliai, kurie su ja ištvirkavo bei lėbavo, kai pamatys jos gaisro dūmus.
9Wafalme wa Dunia waliofanya uzinzi naye na kuishi naye maisha ya anasa wataomboleza na kulia wakati watakapoona moshi wa mji huo unaoteketea.
10Jie stovės iš tolo ir, jos kankinimų išgąsdinti, sakys: ‘Vargas, vargas, didysis mieste! Babele, galingasis mieste, per vieną valandą įvyko tavo teismas!’
10Wanasimama kwa mbali kwa sababu ya kuogopa mateso yake, na kusema, "Ole! Ole kwako Babuloni, mji maarufu na wenye nguvu! Kwa muda wa saa moja tu adhabu yako imekupata."
11Žemės pirkliai verks ir gedės jos, nes niekas jau nebepirks jų atplukdytų prekių:
11Wafanyabiashara wa dunia watalia na kumfanyia matanga, maana hakuna mtu anayenunua tena bidhaa zao;
12aukso, sidabro, brangakmenių, perlų, švelnios drobės, purpuro, šilko, škarlato, jokios kvapios medienos, jokių dramblio kaulo dirbinių, jokių brangmedžio rakandų, nei vario, geležies, marmuro,
12hakuna tena wa kununua dhahabu yao, fedha, mawe ya thamani na lulu, kitani na nguo za rangi ya zambarau, hariri na nguo nyekundu; vyombo vya kila aina ya miti ya pekee, vyombo vya pembe za ndovu, vya miti ya thamani kubwa, vya shaba, chuma na marmari;
13cinamono, kvapių augalų, miros, smilkalų, vyno, aliejaus, smulkių miltų, kviečių, galvijų, avių, arklių, vežimų, žmonių kūnų ir sielų.
13mdalasini, viungo, ubani, manemane, udi, divai, mafuta, unga na ngano, ng'ombe na kondoo, farasi na magari ya kukokotwa, watumwa wao na hata maisha ya watu.
14Vaisiai, kurių taip geidė tavo siela, nutolo nuo tavęs; visas puošnumas ir spindesys tau pražuvo, ir niekad jų neberasi.
14Wafanyabiashara wanamwambia: "Faida yote uliyotazamia imetoweka, na utajiri na fahari vimekuponyoka; hutaweza kuvipata tena!"
15Tų daiktų pirkliai, iš jos pralobę, stovės iš tolo, išsigandę jos kankinimų, verks, gedės
15Wafanya biashara waliotajirika kutokana na mji huo, watasimama mbali kwa sababu ya hofu ya mateso yake, watalalamika na kuomboleza,
16ir sakys: ‘Vargas, vargas didžiajam miestui, vilkėjusiam ploniausia drobe, purpuru, škarlatu, išsipuošusiam auksu, brangakmeniais ir perlais.
16wakisema, "Ole! Ole kwa mji huu mkuu. Ulizoea kuvalia nguo za kitani, za rangi ya zambarau na nyekundu, na kujipamba kwa dhahabu, mawe ya thamani na lulu!
17Per vieną valandą niekais virto šitokie turtai!’ Visi laivų vairininkai, visi pakrančių laivininkai, visi jūreiviai ir visi, kurie jūroje darbuojasi, iš tolo sustoję
17Kwa saa moja tu utajiri wako umetoweka!" Halafu manahodha wote na wasafiri wao, wanamaji na wote wanaofanya kazi baharini, walisimama kwa mbali,
18ir, stebėdami jos gaisro dūmus, šaukė: ‘Kas galėtų lygintis su didžiuoju miestu?!’
18na walipouona moshi wa moto ule uliouteketeza, wakalia kwa sauti: "Hakujapata kuwako mji kama mji huu mkuu!"
19Jie bėrė žemes ant galvų, šaukė, verkė ir aimanavo: ‘Vargas, vargas didžiajam miestui, iš kurio prabangos pralobo, kurie jūroje turėjo laivų. Per vieną valandą jis virto dykyne!’
19Wakajimwagia vumbi juu ya vichwa vyao wakilia kwa sauti na kuomboleza: "Ole! Ole kwako mji mkuu! Ni mji ambamo wote wenye meli zisafirizo baharini walitajirika kutokana na utajiri wake. Kwa muda wa saa moja tu umepoteza kila kitu!"
20Džiūgauk dėl jo, dangau, ir jūs, šventieji, ir apaštalai, ir pranašai, nes dėl jūsų Dievas nubaudė jį teismu!”
20Furahi ee mbingu, kwa sababu ya uharibifu wake. Furahini watu wa Mungu, mitume na manabii! Kwa maana Mungu ameuhukumu kwa sababu ya mambo uliyowatenda ninyi!
21Tuomet vienas galingas angelas iškėlė akmenį, tarsi didelį girnakmenį, ir sviedė jį į jūrą, sakydamas: “Tokiu smarkumu bus nublokštas didysis Babelės miestas, ir jo nebebus galima rasti.
21Kisha malaika mmoja mwenye nguvu sana akainua jiwe mfano wa jiwe kubwa la kusagia, akalitupa baharini akisema, "Ndivyo, Babuloni atakavyotupwa na kupotea kabisa.
22Nebesigirdės daugiau tavyje arfininkų, giesmininkų, vamzdininkų, trimitininkų balsų. Niekas neberas tavyje nė vieno jokio meno kūrėjo, ir nebesigirdės tavyje malūno dūzgimo.
22Sauti za vinubi za muziki, sauti za wapiga filimbi na tarumbeta hazitasikika tena ndani yako. Hakuna fundi wa namna yoyote ile atakayepatikana tena ndani yako; wala sauti ya jiwe la kusagia haitasikika tena ndani yako.
23Tavyje nebešvies žiburio spindulys, niekas nebegirdės jaunikio ir nuotakos balso. Nes tavo pirkliai buvo tapę žemės didžiūnais, nes tavo burtais buvo suvedžiotos visos tautos
23Mwanga wa taa hautaonekana tena ndani yako; sauti za bwana arusi na bibi arusi hazitasikika tena ndani yako. Wafanyabiashara wako walikuwa wakuu duniani, na kwa uchawi wako mataifa yote yalipotoshwa!"
24ir tavyje buvo rastas pranašų ir šventųjų ir visų žemėje nužudytųjų kraujas”.
24Mji huo uliadhibiwa kwani humo mlipatikana damu ya manabii, damu ya watu wa Mungu na damu ya watu wote waliouawa duniani.