Lithuanian

Swahili: New Testament

Revelation

19

1Paskui aš girdėjau danguje galingą didžiulės minios balsą, skelbiantį: “Aleliuja! Išgelbėjimas, galybė, šlovė ir garbė priklauso Viešpačiui, mūsų Dievui,
1Baada ya hayo nikasikia kitu kama sauti kubwa ya umati wa watu wengi mbinguni ikisema, "Haleluya! Ukombozi, utukufu na nguvu ni mali yake Mungu wetu!
2nes tikri ir teisingi Jo teismai! Jis nuteisė didžiąją paleistuvę, kuri suteršė žemę savo ištvirkavimu; Jis atkeršijo už savo tarnų kraują, pralietą jos rankomis”.
2Maana hukumu yake ni ya kweli na ya haki. Amemhukumu yule mzinzi mkuu ambaye alikuwa ameipotosha dunia kwa uzinzi wake. Amemwadhibu kwa sababu ya kumwaga damu ya watumishi wake!"
3Ir dar kartą jie skelbė: “Aleliuja! Jos dūmai rūks per amžių amžius!”
3Wakasema, "Asifiwe Mungu! Moshi wa moto unaoteketeza mji huo utapanda juu milele na milele!"
4Dvidešimt keturi vyresnieji ir keturios būtybės parpuolė ir pagarbino Dievą, sėdintį soste, sakydami: “Amen! Aleliuja!”
4Na wale wazee ishirini na wanne, na vile viumbe hai vinne, wakajitupa chini, wakamwabudu Mungu aliyeketi juu ya kiti cha enzi wakisema, "Amina! Asifiwe Mungu!"
5O nuo sosto nuskambėjo balsas: “Šlovinkite mūsų Dievą visi Jo tarnai ir tie, kurie bijote Jo: maži ir dideli!”
5Kisha kukatokea sauti kwenye kiti cha enzi: "Msifuni Mungu enyi watumishi wake wote, nyote mnaomcha, wadogo kwa wakubwa."
6Ir išgirdau gausios minios balsą, lyg daugybės vandenų šniokštimą ar galingų griaustinių dundėjimą, sakantį: “Aleliuja! Užviešpatavo Viešpats Dievas, Visagalis.
6Kisha nikasikia kitu kama sauti ya umati mkubwa wa watu na sauti ya maji mengi na ya ngurumo kubwa, ikisema, "Haleluya! Maana Bwana Mungu wetu Mwenye Uwezo ni Mfalme!
7Džiūgaukime ir linksminkimės, ir duokime Jam šlovę! Nes atėjo Avinėlio vestuvės ir Jo nuotaka pasiruošė”.
7Tufurahi na kushangilia; tumtukuze, kwani wakati wa arusi ya Mwanakondoo umefika, na bibi arusi yuko tayari.
8Jai buvo duota apsirengti spindinčia, tyra drobe, o ta drobė­tai šventųjų teisūs darbai.
8Amepewa uwezo wa kujivalia nguo ya kitani safi, iliyotakata na yenye kung'aa!" (Nguo hiyo ya kitani safi ni matendo mema ya watu wa Mungu.)
9Ir angelas sako man: “Rašyk: ‘Palaiminti, kurie pakviesti į Avinėlio vestuvių pokylį’ ”. Jis pridūrė: “Šie žodžiai yra tikri Dievo žodžiai!”
9Kisha malaika akaniambia, "Andika haya: Heri wale walioalikwa kwenye karamu ya arusi ya Mwanakondoo!" Tena akaniambia, "Hayo ni maneno ya kweli ya Mungu."
10Aš puoliau jam po kojų, norėdamas jį pagarbinti, bet jis pasakė: “Žiūrėk, kad to nedarytum! Aš esu tarnas, kaip tu ir broliai, kurie turi Jėzaus liudijimą. Dievą garbink! Nes Jėzaus liudijimas yra pranašystės dvasia”.
10Basi, mimi nikaanguka kifudifudi mbele ya miguu yake nikataka kumwabudu. Lakini yeye akaniambia, "Acha! Mimi ni mtumishi tu kama wewe na ndugu zako; sote tunauzingatia ukweli ule alioufunua Yesu. Mwabudu Mungu! Maana ukweli alioufunua Yesu ndio unaowaangazia manabii."
11Ir aš išvydau atvirą dangų, ir štai pasirodė baltas žirgas. Ant jo sėdėjo raitelis, vardu Ištikimasis ir Teisusis; Jis teisingai teisia ir kovoja.
11Kisha nikaona mbingu zimefunguliwa; na huko alikuwako farasi mmoja mweupe, na mpanda farasi wake aliitwa "Mwaminifu" na "Kweli". Huyo huhukumu na kupigana kwa ajili ya haki.
12Jo akys švietė kaip ugnies liepsna, o ant Jo galvos daug diademų ir įrašytas vardas, kurio niekas nežino, tik Jis pats.
12Macho yake ni kama mwali wa moto, na alikuwa amevaa taji nyingi kichwani. Alikuwa ameandikwa jina ambalo hakuna mtu alijuaye isipokuwa tu yeye mwenyewe.
13Jis apsirengęs kraujyje pamirkytu drabužiu ir Jo vardas­Dievo žodis.
13Alikuwa amevaa vazi lililokuwa limelowekwa katika damu. Na jina lake huyo ni "Neno la Mungu."
14Paskui Jį sekė dangaus kariaunos pulkai ant baltų žirgų, apsivilkę tyros baltos drobės drabužiais.
14Majeshi ya mbinguni yalimfuata yakiwa yamepanda farasi weupe na walikuwa wamevaa mavazi ya kitani, meupe na safi.
15Iš Jo burnos ėjo aštrus dviašmenis kalavijas, kuriuo Jis ištiks tautas. Jis valdys jas geležine lazda. Jis mina visagalio Dievo įniršio ir rūstybės vyno spaustuvą.
15Upanga mkali hutoka kinywani mwake, na kwa upanga huo atawashinda mataifa. Yeye ndiye atakayetawala kwa fimbo ya chuma na kuikamua divai katika chombo cha kukamulia zabibu za ghadhabu kuu ya Mungu Mwenye Uwezo.
16Ant Jo drabužio ir ant strėnų užrašytas vardas: “Karalių Karalius ir viešpačių Viešpats”.
16Juu ya vazi lake, na juu ya mguu wake, alikuwa ameandikwa jina: "Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana."
17Aš regėjau angelą, stovintį saulėje. Jis garsiai šaukė, kviesdamas visus paukščius, skrendančius dangaus viduriu: “Skriskite šen, į didžiojo Dievo pokylį,
17Kisha nikamwona malaika mmoja amesimama katika jua. Akapaaza sauti na kuwaambia ndege wote waliokuwa wanaruka juu angani, "Njoni! Kusanyikeni pamoja kwa karamu kuu ya Mungu.
18ir leskite kūnus karalių, karo vadų, galiūnų, žirgų, raitelių, visų laisvųjų ir vergų, mažų ir didelių!”
18Njoni mkaitafune miili ya wafalme, ya majemadari, ya watu wenye nguvu, ya farasi na wapanda farasi wao; njoni mkaitafune miili ya watu wote: walio huru na watumwa, wadogo na wakubwa."
19Ir išvydau žvėrį ir žemės karalius bei jų kariuomenes, susirinkusias kovoti su sėdinčiuoju ant žirgo ir Jo kariuomene.
19Kisha nikaona yule mnyama pamoja na mfalme wa dunia na askari wao wamekusanyika pamoja kusudi wapigane na yule aliyekuwa ameketi juu ya farasi, pamoja na jeshi lake.
20Žvėris buvo sugautas, o kartu su juo netikrasis pranašas, jo akyse daręs ženklus ir jais klaidinęs žmones, kurie buvo priėmę žvėries ženklą ir garbino jo atvaizdą. Jiedu gyvi buvo įmesti į ugnies ežerą, degantį siera.
20Lakini huyo mnyama akachukuliwa mateka, pamoja na nabii wa uongo aliyekuwa akifanya miujiza mbele yake. (Kwa miujiza hiyo, alikuwa amewapotosha wale waliokuwa na chapa ya huyo mnyama, na ambao walikuwa wameiabudu sanamu yake.) Huyo mnyama pamoja na huyo nabii walitupwa wote wawili, wakiwa wazimawazima, ndani ya ziwa linalowaka moto wa kiberiti.
21O visi kiti buvo užmušti kalaviju, einančiu iš raitelio burnos. Ir visi paukščiai prisilesė jų lavonų.
21Majeshi yao yaliuawa kwa upanga uliotoka kinywani mwa yule anayepanda farasi. Ndege wote wakajishibisha kwa nyama zao.