1Ir išvydau angelą, nužengiantį iš dangaus, laikantį rankoje bedugnės raktą ir didžiulę grandinę.
1Kisha nikamwona malaika mmoja anashuka kutoka mbinguni akiwa na ufunguo wa kuzimu na mnyororo mkubwa mkononi mwake.
2Jis nutvėrė slibinąsenąją gyvatę, kuri yra Velnias ir Šėtonas, surišo jį tūkstančiui metų
2Akalikamata lile joka--nyoka wa kale, yaani Ibilisi au Shetani--akalifunga kwa muda wa miaka elfu moja.
3ir įmetė į bedungę, užrakino ją ir iš viršaus užantspaudavo, kad nebegalėtų daugiau suvedžioti tautų, kol pasibaigs tūkstantis metų. Po to jis turės būti atrištas trumpam laikui.
3Malaika akalitupa Kuzimu, akaufunga mlango wa kuingilia huko na kuutia mhuri ili lisiweze tena kuyapotosha mataifa mpaka hapo miaka elfu moja itakapotimia. Lakini baada ya miaka hiyo ni lazima lifunguliwe tena, lakini kwa muda mfupi tu.
4Aš pamačiau sostus ir juose sėdinčiuosius, kuriems buvo pavesta teisti. Taip pat regėjau sielas tų, kuriems buvo nukirstos galvos dėl Jėzaus liudijimo ir dėl Dievo žodžio, kurie negarbino žvėries, nei jo atvaizdo, ir neėmė ženklo sau ant kaktos ar rankos. Jie atgijo ir viešpatavo su Kristumi tūkstantį metų.
4Kisha nikaona viti vya enzi na watu walioketi juu yake; watu hao walipewa mamlaka ya hukumu. Niliona pia roho za wale waliokuwa wamenyongwa kwa sababu ya kumtangaza Yesu na kwa sababu ya neno la Mungu. Hawa hawakumwabudu yule mnyama na sanamu yake, wala hawakupigwa alama yake juu ya paji za nyuso zao, au juu ya mikono yao. Walipata tena uhai, wakatawala pamoja na Kristo kwa muda wa miaka elfu moja.
5O visi kiti mirusieji neatgijo, iki pasibaigiant tūkstančiui metų. Šis yra pirmasis prisikėlimas.
5(Wale wengine waliokufa hawakupata uhai mpaka miaka elfu moja itimie.) Huu ndio ufufuo wa kwanza.
6Palaimintas ir šventas, kas turi dalį pirmajame prisikėlime. Šitiems antroji mirtis neturi galios; jie bus Dievo ir Kristaus kunigai ir valdys su Juo tūkstantį metų.
6Wameneemeka sana, tena heri yao wote wanaoshiriki ufufuo huu wa kwanza. Kifo cha pili hakitakuwa na nguvu juu yao; watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, na watatawala pamoja naye kwa miaka elfu moja.
7Kai pasibaigs tūkstantis metų, šėtonas bus išleistas iš savo kalėjimo
7Wakati miaka elfu mia moja itakapotimia, Shetani atafunguliwa kutoka gerezani mwake.
8ir išeis suvedžioti tautų, gyvenančių keturiuose žemės kampuose, Gogo ir Magogo, ir surinkti jų kovai. Jų skaičius kaip pajūrio smiltys.
8Basi, atatoka nje, ataanza kuyapotosha mataifa yote yaliyotawanyika kila mahali duniani, yaani Gogu na Magogu. Shetani atawakusanya pamoja kwa ajili ya vita; nao watakuwa wengi kama mchanga wa pwani.
9Jie išėjo ant žemės platumos ir apsupo šventųjų stovyklą ir mylimąjį miestą. Ir nužengė ugnis iš dangaus nuo Dievo ir juos prarijo,
9Walitawanyika katika nchi yote, wakaizunguka kambi ya watu wa Mungu na mji wa Mungu aupendao. Lakini moto ulishuka kutoka mbinguni, ukawaangamiza.
10o jų suvedžiotojas velnias buvo įmestas į ugnies ir sieros ežerą, kur jau yra žvėris ir netikrasis pranašas. Jie bus kankinami dieną ir naktį per amžių amžius.
10Ibilisi, aliyekuwa anawapotosha, akatupwa ndani ya ziwa linalowaka moto wa kiberiti, walimo yule mnyama na yule nabii wa uongo, nao watateswa mchana na usiku, milele na milele.
11Paskui mačiau didelį baltą sostą ir jame Sėdintįjį, nuo kurio veido pabėgo žemė ir dangus, ir nebeliko jiems vietos.
11Kisha nikaona kiti cha enzi kikubwa cheupe, na yule aketiye juu yake. Dunia na mbingu vikatoweka mbele ya macho yake, na havikuonekana tena.
12Ir mačiau mirusius, didelius ir mažus, stovinčius priešais Dievą. Buvo atskleistos knygos. Ir buvo atversta dar viena, būtent gyvenimo knyga. Mirusieji buvo teisiami iš užrašų knygose pagal jų darbus.
12Kisha nikawaona watu wakubwa na wadogo, wamesimama mbele ya kiti cha enzi, na vitabu vikafunguliwa. Halafu kitabu kingine, yaani kitabu cha uzima, kikafunguliwa pia. Wafu wakahukumiwa kadiri ya matendo yao, kama ilivyoandikwa ndani ya vitabu hivyo.
13Jūra atidavė savo mirusiuosius, o mirtis ir pragaras atidavė savuosius. Ir kiekvienas buvo teisiamas pagal savo darbus.
13Bahari ikawatoa nje wafu waliokuwa ndani yake; kifo na kuzimu vikawatoa nje wafu waliokuwa ndani yao. Kila mmoja akahukumiwa kufuatana na matendo yake.
14Mirtis ir pragaras buvo įmesti į ugnies ežerą. Tai yra antroji mirtis.
14Kisha kifo na kuzimu vikatupwa ndani ya ziwa la moto. Ziwa hili la moto ndicho kifo cha pili.
15Kas tik nebuvo rastas įrašytas gyvenimo knygoje, buvo įmestas į ugnies ežerą.
15Mtu yeyote ambaye jina lake halikupatikana limeandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika ziwa la moto.