1Jis parodė man tyrą gyvenimo vandens upę, tvaskančią tarsi krištolas, ištekančią nuo Dievo ir Avinėlio sosto.
1Kisha malaika akanionyesha mto wa maji ya uzima maangavu kama kioo yakitoka kwenye kiti cha enzi cha Mungu na Mwanakondoo.
2Viduryje miesto gatvės, abejose upės pusėse, augo gyvenimo medis, duodantis dvylika derlių, kiekvieną mėnesį vedantis vaisių, o to medžio lapaitautoms gydyti.
2Mto huo ulitiririka kupitia katikati ya barabara kuu ya mji. Kandokando ya mto huo kulikuwa na mti wa uzima unaozaa matunda mara kumi na mbili kwa mwaka, yaani kila mwezi; na majani yake ni dawa ya kuwaponya watu wa mataifa.
3Ir nebus daugiau jokio prakeikimo. Mieste stovės Dievo ir Avinėlio sostas, ir Jo tarnai tarnaus Jam.
3Hapana kitu chochote kilicholaaniwa kitakachokuwa katika mji huo. Kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwanakondoo kitakuwa katika mji huo, na watumishi wake watamwabudu.
4Jie regės Jo veidą, ir jų kaktose bus Jo vardas.
4Watauona uso wake, na jina lake litaandikwa juu ya paji za nyuso zao.
5Ten nebebus nakties, jiems nereikės nei žiburio, nei saulės šviesos, nes Viešpats Dievas jiems švies, ir jie viešpataus per amžių amžius.
5Usiku hautakuwako tena, wala hawatahitaji mwanga wa taa au wa jua, maana Bwana Mungu atawaangazia, nao watatawala milele na milele.
6Tuomet jis man pasakė: “Šie žodžiai patikimi ir tikri. Viešpats, šventų pranašų Dievas, atsiuntė savo angelą parodyti savo tarnams, kas turi įvykti netrukus”.
6Kisha malaika akaniambia, "Maneno haya ni ya kweli na ya kuaminika. Bwana Mungu ambaye huwapa manabii Roho wake, alimtuma malaika wake awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo lazima yatukie punde.
7“Štai Aš veikiai ateinu! Palaimintas, kas laikosi šios knygos pranašystės žodžių!”
7"Sikiliza! Naja upesi. Heri yake anayeyazingatia maneno ya unabii yaliyo katika kitabu hiki."
8Aš, Jonas, visa tai mačiau ir girdėjau. Išgirdęs ir pamatęs, puoliau po kojų angelui, kuris man visa tai parodė, norėdamas jį pagarbinti.
8Mimi Yohane, niliyaona na kusikia mambo haya. Nilipokwisha sikia na kuona nikajitupa chini mbele ya miguu ya huyo malaika aliyenionyesha mambo hayo, nikataka kumwabudu.
9Bet jis man pasakė: “Žiūrėk, kad to nedarytum! Juk ir aš esu tarnas, kaip tu ir tavo broliai pranašai, ir visi, kurie laikosi šios knygos žodžių. Dievą garbink!”
9Lakini yeye akaniambia, "Acha! Mimi ni mtumishi tu kama wewe na ndugu zako manabii na wote wanaoyatii maagizo yaliyomo katika kitabu hiki. Mwabudu Mungu!"
10Jis sako man: “Neužantspauduok pranašiškų šios knygos žodžių, nes laikas trumpas.
10Tena akaniambia, "Usiyafiche kama siri maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki, maana wakati wa kutimizwa kwake umekaribia.
11Neteisusis toliau tesielgia neteisiai, kas susitepęs, ir toliau tebūna susitepęs, teisusis toliau tevykdo teisumą, ir šventasis dar tepašventėja”.
11Kwa sasa anayetenda mabaya na aendelee kutenda mabaya, na aliye mchafu aendelee kuwa mchafu. Mwenye kutenda mema na azidi kutenda mema, na aliye mtakatifu na azidi kuwa mtakatifu."
12“Štai Aš veikiai ateinu, ir mano atlygis su manimi, kad kiekvienam atlyginčiau pagal jo darbus.
12"Sikiliza!" Asema Yesu, "Naja upesi, pamoja na tuzo nitakalompa kila mmoja kufuatana na matendo yake.
13Aš esu Alfa ir Omega, Pradžia ir Pabaiga, Pirmasis ir Paskutinysis”.
13Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho, wa kwanza na wa mwisho."
14“Palaiminti, kurie vykdo Jo įsakymus, kad įgytų teisę į gyvenimo medį ir galėtų įžengti pro vartus į miestą.
14Heri yao wale wanaoosha mavazi yao, kwani watakuwa na haki ya kula tunda la mti wa uzima, na haki ya kuingia mjini kwa kupitia milango yake.
15O lauke lieka šunys, burtininkai, ištvirkėliai, žudikai, stabmeldžiai ir visi, kurie mėgsta melą ir jį daro”.
15Lakini mbwa, wachawi, wazinzi, wauaji, waabudu sanamu na wote wanaopenda kusema uongo, watakaa nje ya mji.
16“Aš, Jėzus, pasiunčiau savo angelą jums tai paliudyti apie bažnyčias. Aš esu Dovydo šaknis ir palikuonis, žėrinti aušrinė žvaigždė!”
16"Mimi, Yesu, nimemtuma malaika wangu awathibitishieni mambo haya katika makanisa. Mimi ni mzawa wa ukoo wa Daudi. Mimi ni nyota angavu ya asubuhi!"
17Ir Dvasia, ir sužadėtinė kviečia: “Ateik!” Ir kas girdi, teatsiliepia: “Ateik!” Ir kas trokšta, teateina, ir kas nori, tesisemia dovanai gyvenimo vandens.
17Roho na Bibiarusi waseme, "Njoo!" Kila mtu asikiaye hili, na aseme, "Njoo!" Kisha, yeyote aliye na kiu na aje; anayetaka maji ya uzima na apokee bila malipo yoyote.
18Aš sakau kiekvienam, kuris girdi šios knygos pranašystės žodžius: “Jeigu kas prie jų ką pridėsDievas jam pridės aprašytų šioje knygoje negandų.
18Mimi Yohane nawapa onyo wote wanaosikia maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki: mtu yeyote akiongeza chochote katika mambo haya, Mungu atamwongezea mabaa yaliyoandikwa katika kitabu hiki.
19Ir jeigu kas atims ką nors nuo šios pranašystės knygos žodžių Dievas atims jo dalį iš gyvenimo knygos ir šventojo miesto, kurie aprašyti šitoje knygoje”.
19Na mtu yeyote akipunguza chochote katika maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki, Mungu atamnyang'anya sehemu yake katika ule mti wa uzima, na sehemu yake katika mji mtakatifu, ambavyo vimeelezwa katika kitabu hiki.
20Tas, kuris šitai liudija, sako: “Taip, Aš veikiai ateinu!” Amen. Taip, ateik, Viešpatie Jėzau!
20Naye anayetoa ushahidi wake juu ya mambo haya asema: "Naam! Naja upesi." Amina. Na iwe hivyo! Njoo Bwana Yesu!
21Mūsų Viešpaties Jėzaus Kristaus malonė su jumis visais! Amen!
21Nawatakieni nyote neema ya Bwana Yesu. Amen.