Lithuanian

Swahili: New Testament

Revelation

8

1Kai Avinėlis atplėšė septintąjį antspaudą, danguje pusvalandžiui pasidarė tylu.
1Na Mwanakondoo alipouvunja mhuri wa saba, kukawa kimya mbinguni kwa muda wa nusu saa.
2Ir aš išvydau septynis angelus, stovinčius Dievo akivaizdoje, ir jiems buvo įteikti septyni trimitai.
2Kisha nikawaona wale malaika saba wanaosimama mbele ya Mungu wamepewa tarumbeta saba.
3Atėjo dar vienas angelas ir atsistojo prie aukuro, laikydamas aukso smilkytuvą. Jam buvo duota daug smilkalų, kad jis aukotų juos su visų šventųjų maldomis ant auksinio aukuro priešais sostą.
3Malaika mwingine akafika, akiwa anachukua chetezo cha dhahabu, akasimama mbele ya madhabahu ya kufukizia ubani. Naye akapewa ubani mwingi autoe sadaka pamoja na sala za watu wote wa Mungu, juu ya madhabahu ya dhahabu iliyo mbele ya kiti cha enzi.
4Ir pakilo smilkalų dūmai su šventųjų maldomis iš angelo rankų Dievo akivaizdon.
4Moshi wa ubani ukapanda juu, pamoja na sala za watu wa Mungu, kutoka mikononi mwake huyo malaika aliyekuwa mbele ya Mungu.
5Po to angelas paėmė smilkytuvą, pripildė jį aukuro ugnies ir sviedė į žemę. Sugriaudė griausmai, pakilo šauksmai, sublyksėjo žaibai, sudrebėjo žemė.
5Kisha malaika akakichukua hicho chetezo, akakijaza moto wa madhabahuni akakitupa duniani. Kukawa na ngurumo, sauti, umeme na tetemeko la ardhi.
6Septyni angelai, turintys septynis trimitus, pasiruošė trimituoti.
6Kisha wale malaika saba wenye tarumbeta saba wakajiweka tayari kupiga mbiu ya mgambo.
7Sutrimitavo pirmasis angelas. Ir radosi kruša ir ugnis, sumišę su krauju, ir tai buvo numesta žemėn. Ir išdegė trečdalis medžių ir visa žaliuojanti žolė.
7Malaika wa kwanza akapiga tarumbeta yake. Mchanganyiko wa mvua ya mawe na moto, pamoja na damu, ukamwagwa juu ya nchi. Theluthi moja ya nchi ikaungua, theluthi moja ya miti ikaungua, na majani yote mabichi yakaungua.
8Sutrimitavo antrasis angelas. Ir tarytum didžiulis kalnas, liepsnojantis ugnimi, buvo sviestas į jūrą, ir trečdalis jūros pavirto krauju.
8Malaika wa pili akapiga tarumbeta yake. Na kitu kama mlima mkubwa unaowaka moto ukatupwa baharini. Theluthi moja ya bahari ikawa damu,
9Trečdalis jūros padarų, turinčių gyvybę, išdvėsė, ir trečdalis laivų buvo sunaikinti.
9theluthi moja ya viumbe vya baharini vikafa na theluthi moja ya meli zikaharibiwa.
10Ir sutrimitavo trečiasis angelas. Tada iš dangaus nukrito didelė žvaigždė, liepsnodama tarsi deglas, ir nukrito ant trečdalio upių ir ant vandens šaltinių.
10Kisha malaika wa tatu akapiga tarumbeta yake. Na nyota kubwa ikiwaka kama bonge la moto, ikaanguka kutoka mbinguni, na kutua juu ya theluthi moja ya mito na chemchemi za maji.
11Žvaigždės vardas yra Metėlė. Ir pavirto trečdalis vandenų į metėlę, ir daugybė žmonių mirė nuo vandens, nes jis pasidarė kartus.
11(Nyota hiyo inaitwa "Uchungu.") Basi, theluthi moja ya maji yakawa machungu; watu wengi wakafa kutokana na maji hayo, kwa sababu yaligeuka kuwa machungu.
12Ir sutrimitavo ketvirtasis angelas. Tuomet buvo užgautas trečdalis saulės, trečdalis mėnulio ir trečdalis žvaigždžių taip, kad jų trečdalis užtemo. Diena bei naktis prarado trečdalį šviesumo.
12Kisha malaika wa nne akapiga tarumbeta yake. Ndipo theluthi moja ya jua, ya mwezi na ya nyota ikapata pigo; hata mwangaza ukapoteza theluthi moja ya mng'ao wake. Theluthi moja ya mchana ikakosa mwanga, hali kadhalika na theluthi moja ya usiku.
13Aš regėjau ir girdėjau dangaus viduriu lekiantį angelą, kuris garsiu balsu skelbė: “Vargas, vargas, vargas žemės gyventojams nuo besirengiančių užtrimituoti kitų trijų angelų trimitų garsų!”
13Kisha nikatazama, nikasikia tai akiruka juu kabisa angani anasema kwa sauti kubwa, "Ole, ole, ole kwa wanaoishi duniani wakati malaika watatu waliobaki watakapopiga tarumbeta zao!"