Lithuanian

Swahili: New Testament

Romans

6

1Ką gi sakysime? Gal mums pasilikti nuodėmėje, kad gausėtų malonė?
1Tuseme nini basi? Je, twendelee kubaki katika dhambi ili neema ya Mungu iongezeke?
2Jokiu būdu! Mirę nuodėmei, kaipgi gyvensime joje?
2Hata kidogo! Kuhusu dhambi sisi tumekufa--tutaendeleaje kuishi tena katika dhambi?
3Argi nežinote, jog mes, pakrikštyti Jėzuje Kristuje, buvome pakrikštyti Jo mirtyje?
3Maana, mnajua kwamba sisi tuliobatizwa tukaungana na Kristo Yesu, tulibatizwa na kuungana na kifo chake.
4Taigi krikštu mes esame kartu su Juo palaidoti mirtyje, kad kaip Kristus buvo prikeltas iš numirusių Tėvo šlove, taip ir mes gyventume naują gyvenimą.
4Tulipobatizwa tuliungana na kifo chake, tukazikwa pamoja naye, ili kama vile Kristo alivyofufuliwa kutoka wafu kwa kitendo kitukufu cha Baba, sisi pia tuweze kuishi maisha mapya.
5Jei esame suaugę su Jo mirties paveikslu, būsime suaugę ir su prisikėlimo,
5Maana, kama sisi tumeungana naye katika kufa kama yeye, vivyo hivyo tutaungana naye kwa kufufuliwa kutoka wafu kama yeye.
6žinodami, jog mūsų senasis žmogus buvo nukryžiuotas kartu su Juo, kad būtų sunaikintas nuodėmės kūnas ir kad mes daugiau nebevergautume nuodėmei.
6Tunajua kwamba utu wetu wa kale ulisulubiwa pamoja na Kristo, ili hali ya dhambi iharibiwe, tusiwe tena watumwa wa dhambi.
7Juk kas miręs, tas išlaisvintas iš nuodėmės.
7Kwa maana, mtu aliyekufa, amenasuliwa kutoka katika nguvu ya dhambi.
8Jeigu esame mirę su Kristumi, tikime, kad ir gyvensime su Juo.
8Basi, ikiwa tumekufa pamoja na Kristo, tunaamini kwamba tutaishi pia pamoja naye.
9Žinome, kad, prisikėlęs iš numirusių, Kristus daugiau nebemiršta; mirtis jau nebeturi Jam galios.
9Maana, tunajua kwamba Kristo amekwisha fufuliwa kutoka wafu na hafi tena; kifo hakimtawali tena.
10Kad Jis mirė, tai mirė nuodėmei kartą visiems laikams, o kad gyvena­gyvena Dievui.
10Hivyo, kwa kuwa alikufa--mara moja tu--dhambi haina nguvu tena juu yake; na sasa anaishi maisha yake katika umoja na Mungu.
11Taip ir jūs laikykite save mirusiais nuodėmei, o gyvais Dievui Kristuje Jėzuje, mūsų Viešpatyje.
11Hali kadhalika nanyi lazima mjione kuwa mmekufa kuhusu dhambi, lakini kama mnaoishi katika umoja na Mungu kwa njia ya Kristo Yesu.
12Todėl neleiskite nuodėmei viešpatauti jūsų mirtingame kūne, kad nepasiduotumėte jo geiduliams.
12Kwa hiyo, dhambi isiitawale tena miili yenu ambayo hufa, na hivyo kuzitii tamaa zake.
13Neduokite nuodėmei savo kūno narių kaip neteisumo ginklų, bet paveskite save Dievui, kaip iš numirusiųjų atgijusius, ir savo narius Jam­kaip teisumo ginklus.
13Wala msitoe hata sehemu moja ya miili yenu iwe chombo cha kutenda uovu na dhambi. Badala yake, jitoleeni ninyi wenyewe kwa Mungu kama watu waliofufuliwa kutoka wafu; toeni nafsi zenu zote kwa Mungu kwa ajili ya uadilifu.
14Nuodėmė neturi jums viešpatauti: jūs ne įstatymo, bet malonės valdžioje.
14Maana, dhambi haitawatawala ninyi tena, kwani hamko chini ya Sheria, bali chini ya neema.
15Tai ką? Gal darysime nuodėmes, jei esame ne įstatymo, bet malonės valdžioje? Jokiu būdu!
15Basi, tuseme nini? Je, tutende dhambi ati kwa sababu hatuko chini ya Sheria bali chini ya neema? Hata kidogo!
16Argi nežinote, kad pasiduodami kam nors vergauti, jūs iš tiesų tampate vergais to, kuriam paklūstate: ar tai būtų nuodėmė, vedanti į mirtį, ar paklusnumas, vedantis į teisumą.
16Mnajua kwamba mkijitolea ninyi wenyewe kama watumwa na kumtii fulani, mnakuwa kweli watumwa wake mtu huyo--au watumwa wa dhambi, na matokeo yake ni kifo, au wa utii, na matokeo yake ni kukubaliwa kuwa waadilifu.
17Bet ačiū Dievui, kad, nors buvote nuodėmės vergais, jūs iš širdies paklusote tam mokymo pavyzdžiui, kuriam buvote pavesti;
17Ingawa mlikuwa watumwa wa dhambi zamani, sasa lakini--namshukuru Mungu--mmetii kwa moyo wote yale maazimio na mafundisho mliyopokea.
18ir, išlaisvinti iš nuodėmės, tapote teisumo tarnais.
18Mlikombolewa kutoka utumwa wa dhambi, mkawa watumwa wa uadilifu.
19Kalbu grynai žmogiškai dėl jūsų kūniško silpnumo. Kaip buvote atidavę savo kūno narius vergauti netyrumui ir nedorybei, kad elgtumėtės nedorai, taip pat atiduokite savo narius vergauti teisumui, kad taptumėte šventi.
19(Hapa natumia lugha ya kawaida ya watu kwa sababu ya udhaifu wenu wenyewe.) Kama vile wakati fulani mlivyojitolea ninyi wenyewe kutumikia uchafu na uhalifu kwa ajili ya uovu, vivyo hivyo sasa jitoleeni nafsi zenu wenyewe kutumikia uadilifu kwa ajili ya utakatifu.
20Būdami nuodėmės vergai, jūs buvote nepriklausomi nuo teisumo.
20Mlipokuwa watumwa wa dhambi, mlikuwa huru mbali na uadilifu.
21Bet kokį vaisių turėjote tuomet iš to, ko dabar gėdijatės? Juk tų dalykų galas­mirtis.
21Sasa, mlipata faida gani siku zile kutokana na mambo yale ambayo mnayaonea aibu sasa? Maana, matokeo ya mambo haya ni kifo!
22O dabar, išlaisvinti iš nuodėmės ir tapę Dievo tarnais, turite kaip vaisių­šventumą, ir kaip baigtį­amžinąjį gyvenimą.
22Lakini sasa, mmekwisha kombolewa kutoka utumwa wa dhambi na mmekuwa watumishi wa Mungu; faida mliyo nayo sasa ni utakatifu, na matokeo yake ni uzima wa milele.
23Atpildas už nuodėmę­mirtis, o Dievo dovana­amžinasis gyvenimas per Jėzų Kristų, mūsų Viešpatį.
23Kwa maana mshahara wa dhambi ni kifo; lakini zawadi anayotoa Mungu ni uzima wa milele katika kuungana na Kristo Yesu, Bwana wetu.