Lithuanian

Swahili: New Testament

Romans

5

1Taigi, išteisinti tikėjimu, turime ramybę su Dievu per mūsų Viešpatį Jėzų Kristų,
1Sasa, kwa vile tumekubaliwa kuwa wadilifu kwa imani, basi, tunayo amani na Mungu kwa ajili ya Bwana wetu Yesu Kristo.
2per kurį tikėjimu pasiekiame tą malonę, kurioje stovime ir džiaugiamės Dievo šlovės viltimi.
2Kwa imani yetu, yeye ametuleta katika hali hii ya neema ya Mungu ambamo sasa tunaishi. Basi, tunajivunia tumaini tulilo nalo la kushiriki utukufu wa Mungu.
3Ir ne vien tuo. Mes taip pat džiaugiamės sielvartais, žinodami, kad sielvartas ugdo ištvermę,
3Naam, si hayo tu, bali tunafurahi pia katika taabu tukijua kwamba taabu huleta saburi,
4ištvermė­patirtį, patirtis­viltį.
4nayo saburi huleta uthabiti, na uthabiti huleta tumaini.
5O viltis neapvilia, nes Dievo meilė yra išlieta mūsų širdyse per Šventąją Dvasią, kuri mums duota.
5Tumaini hilo haliwezi kutuhadaa, maana Mungu amekwisha miminia mioyoni mwetu upendo wake kwa njia ya Roho Mtakatifu aliyetujalia.
6Mums dar esant silpniems, Kristus savo metu numirė už bedievius.
6Tulipokuwa bado wanyonge, Kristo, wakati ulipotimia, alikufa kwa ajili yetu sisi waovu.
7Vargu ar kas sutiktų mirti už teisųjį; nebent kas ryžtųsi mirti už geradarį.
7Si rahisi mtu kufa kwa ajili ya mtu mwadilifu; labda mtu anaweza kuthubutu kufa kwa ajili ya mtu mwema.
8O Dievas mums parodė savo meilę tuo, kad Kristus mirė už mus, kai tebebuvome nusidėjėliai.
8Lakini Mungu amethibitisha kwamba anatupenda, maana wakati tulipokuwa bado wenye dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.
9Tad dar tikriau dabar, kai esame išteisinti Jo krauju, mes būsime per Jį išgelbėti nuo rūstybės.
9Kwa kuwa sasa tumekubaliwa kuwa waadilifu kwa damu ya Kristo, ni dhahiri zaidi kwamba atatuokoa katika ghadhabu ya Mungu.
10Jeigu, kai dar buvome priešai, mus sutaikė su Dievu Jo Sūnaus mirtis, tai tuo labiau mus išgelbės Jo gyvybė, kai jau esame sutaikinti.
10Maana, tulipokuwa bado adui zake, Mungu alitupatanisha naye kwa kifo cha Mwanae. Na kwa vile sasa tumepatanishwa naye, ni dhahiri zaidi kwamba tutaokolewa kwa uzima wa Kristo.
11Negana to,­mes džiaugiamės Dieve per mūsų Viešpatį Jėzų Kristų, kuriuo esame sutaikyti.
11Wala si hayo tu, ila tunafurahi pia katika Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo ambaye ametupatanisha na Mungu.
12Todėl, kaip per vieną žmogų nuodėmė įėjo į pasaulį, o per nuodėmę mirtis, taip ir mirtis pasiekė visus žmones, nes visi nusidėjo.
12Kwa njia ya mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, nayo ikasababisha kifo. Hivyo kifo kimeenea katika jumuiya yote ya binadamu, kwa maana wote wametenda dhambi.
13Nuodėmė buvo pasaulyje ir iki įstatymo, bet, nesant įstatymo, nuodėmė neįskaitoma.
13Kabla ya Sheria kuwako, dhambi ilikuwako ulimwenguni; lakini dhambi haiwekwi katika kumbukumbu bila sheria.
14Vis dėlto nuo Adomo iki Mozės viešpatavo mirtis net tiems, kurie nebuvo padarę nuodėmių, panašių į nusikaltimą Adomo, kuris buvo Būsimojo provaizdis.
14Lakini tangu wakati wa Adamu mpaka wakati wa Mose, kifo kiliwatawala hata wale ambao hawakutenda dhambi kama ile ya Adamu, ya kumwasi Mungu. Adamu alikuwa kielelezo cha yule ambaye atakuja baadaye.
15Bet su dovana yra ne taip kaip su kalte. Jei dėl vieno žmogaus nusikaltimo mirė daugelis, tai tuo labiau Dievo malonė ir malonės dovana per vieną Žmogų, Jėzų Kristų, gausiai atiteko daugybei.
15Lakini ipo tofauti: neema ya Mungu si kama dhambi ya Adamu. Maana, ingawa dhambi ya mtu mmoja ilisababisha kifo kwa wote, kwa fadhili ya mtu mmoja, yaani Yesu Kristo, Mungu amewazidishia wote neema na zawadi zake.
16Ne taip yra su dovana kaip su vieno žmogaus nusikaltimu. Juk teismas vieno nusikaltimą pasmerkė, bet laisva dovana iš daugybės nusikaltimų atvedė į išteisinimą.
16Kuna tofauti baina ya zawadi ya Mungu, na dhambi ya mtu yule mmoja. Maana, baada ya kosa la mtu mmoja, Mungu alitoa hukumu; lakini baada ya makosa ya watu wengi, Mungu aliwapa zawadi yake kwa kuwasamehe.
17Jei dėl vieno žmogaus nusikaltimo mirtis įsiviešpatavo per tą vieną, tai nepalyginti labiau tie, kurie su perteklium gauna malonės bei teisumo dovaną, viešpataus gyvenime per vieną Jėzų Kristų.
17Kweli, kwa dhambi ya mtu mmoja kifo kilianza kutawala kwa sababu ya huyo mtu mmoja; lakini, ni dhahiri zaidi kwamba alichokifanya yule mtu mmoja, yaani Yesu Kristo, ni bora zaidi. Wote wanaopokea neema na zawadi hiyo ya kukubaliwa kuwa waadilifu, watatawala katika uzima kwa njia ya huyo mmoja, yaani Yesu Kristo.
18Todėl kaip vieno žmogaus nusikaltimas visiems žmonėms užtraukė teismą ir pasmerkimą, taip vieno Žmogaus teisumas visiems pelnė išteisinimą, kad gyventų.
18Basi, kama vile kosa la mtu mmoja lilivyoleta hukumu kwa binadamu wote, kadhalika kitendo kimoja kiadilifu kinawapa uhuru na uzima.
19Kaip vieno žmogaus neklusnumu daugelis tapo nusidėjėliais, taip ir vieno klusnumu daugelis taps teisūs.
19Na kama kwa kutotii kwa mtu mmoja watu wengi walifanywa wenye dhambi, kadhalika kutii kwa mtu mmoja kutawafanya wengi wakubaliwe kuwa waadilifu.
20Be to, įstatymas įsiterpė, kad nusikaltimas dar labiau padidėtų. Bet kur buvo apstu nuodėmės, ten dar apstesnė tapo malonė,
20Sheria ilitokea, ikasababisha kuongezeka kwa uhalifu; lakini pale dhambi ilipoongezeka, neema iliongezeka zaidi.
21kad kaip nuodėmė viešpatavo mirtimi, taip malonė viešpatautų teisumu amžinajam gyvenimui per Jėzų Kristų, mūsų Viešpatį.
21Kama vile dhambi ilivyotawala kwa kifo, kadhalika neema inatawala kwa njia ya uadilifu, na kuleta uzima wa milele kwa njia ya Yesu Kristo Bwana wetu.