Lithuanian

Swahili: New Testament

Romans

4

1O ką pasakysime gavus Abraomą­mūsų protėvį pagal kūną?
1Tuseme nini basi, juu ya Abrahamu baba yetu?
2Jei Abraomas būtų buvęs išteisintas darbais, jis turėtų kuo pasigirti, tik ne prieš Dievą.
2Kama Abrahamu alikubaliwa kuwa mwadilifu kutokana na matendo yake, basi, anacho kitu cha kujivunia mbele ya Mungu.
3Bet ką sako Raštas? “Abraomas patikėjo Dievu, ir tai jam buvo įskaityta teisumu”.
3Kwa maana, Maandiko Matakatifu yasema: "Abrahamu alimwamini Mungu, naye Mungu akamkubali kuwa mwadilifu."
4Tam, kuris dirba, atlyginimas nelaikomas malone, bet skola.
4Mfanyakazi hulipwa mshahara; mshahara wake si zawadi bali ni haki yake.
5O tam, kuris nedirba, bet tiki Tuo, kuris išteisina bedievį, jo tikėjimas įskaitomas jam teisumu.
5Lakini mtu asiyetegemea matendo yake mwenyewe, bali anamwamini Mungu ambaye huwasamehe waovu, basi, Mungu huijali imani ya mtu huyo, na hivi humkubali kuwa mwadilifu.
6Taip ir Dovydas skelbia palaiminimą žmogui, kuriam Dievas be darbų įskaito teisumą:
6Naye Daudi asema hivi juu ya furaha ya mtu ambaye Mungu amemkubali kuwa mwadilifu bila kuyajali matendo yake:
7“Palaiminti, kurių nusikaltimai atleisti, kurių nuodėmės uždengtos;
7"Heri wale waliosamehewa makosa yao ambao makosa yao yamefutwa.
8palaimintas žmogus, kuriam Viešpats nuodėmės neįskaito!”
8Heri mtu yule ambaye Bwana hataziweka dhambi zake katika kumbukumbu."
9Ar šis palaiminimas taikomas tik apipjaustytiesiems, ar taip pat ir neapipjaustytiesiems? Mes sakėme, kad Abraomui tikėjimas buvo įskaitytas teisumu.
9Je, hiyo ni kwa wale waliotahiriwa tu, ama pia kwa wale wasiotahiriwa? Ni kwa wale wasiotahiriwa pia. Kwa maana tumekwisha sema: "Abrahamu aliamini, naye Mungu akamkubali kuwa mwadilifu."
10Kokiu būdu? Jam esant apipjaustytam ar neapipjaustytam? Ne po apipjaustymo, bet prieš apipjaustymą.
10Je, Abrahamu alikubaliwa kabla ya kutahiriwa ama baada ya kutahiriwa? Kabla ya kutahiriwa, na si baada ya kutahiriwa.
11Jis gavo apipjaustymo žymę kaip antspaudą tikėjimo teisumo, kurį turėjo, būdamas dar neapipjaustytas. Taip jis tapo tėvu visiems tikintiesiems iš neapipjaustytųjų, kad ir jiems būtų įskaitytas teisumas,
11Abrahamu alitahiriwa baadaye, na kutahiriwa huko kulikuwa alama iliyothibitisha kwamba Mungu alimkubali kuwa mwadilifu kwa sababu ya imani yake aliyokuwa nayo kabla ya kutahiriwa. Kwa hiyo, Abrahamu amekuwa baba wa wale wote ambao, ingawa hawakutahiriwa, wamemwamini Mungu, wakafanywa waadilifu.
12ir apipjaustymo tėvu tiems, kurie ne tik apipjaustyti, bet ir vaikšto mūsų tėvo Abraomo tikėjimo pėdomis, kurį jis turėjo, būdamas dar neapipjaustytas.
12Vilevile yeye ni baba wa wale waliotahiriwa; lakini si kwa kuwa wametahiriwa, bali kwa sababu wanafuata njia ileile ya imani baba yetu Abrahamu aliyofuata kabla ya kutahiriwa.
13Ne įstatymu rėmėsi Abraomui arba jo palikuonims duotas pažadas, kad paveldės pasaulį, bet tikėjimo teisumu.
13Mungu alimwahidi Abrahamu na wazawa wake kwamba ulimwengu ungekuwa mali yao. Ahadi hiyo haikufanywa kwa sababu Abrahamu aliitii Sheria, bali kwa kuwa aliamini, akakubaliwa kuwa mwadilifu.
14Jei paveldėtojai būtų tie, kurie remiasi įstatymu, tai tikėjimas būtų tuščias, o pažadas netektų vertės.
14Maana kama watakaopewa hayo aliyoahidi Mungu ni wale tu wanaoitii Sheria, basi, imani haina maana yoyote, nayo ahadi ya Mungu si kitu.
15Juk įstatymą lydi baudžianti rūstybė, o kur nėra įstatymo, ten nėra ir nusižengimo.
15Sheria husababisha ghadhabu; lakini kama hakuna Sheria, haiwezekani kuivunja.
16Taigi paveldėjimas priklauso nuo tikėjimo, kad būtų iš malonės ir pažadas būtų tikras visiems palikuonims, ne tik tiems, kurie remiasi įstatymu, bet ir tiems, kurie turi tikėjimą Abraomo, kuris yra mūsų visų tėvas,
16Kwa sababu hiyo, jambo hili lategemea imani, hivyo kwamba ahadi hiyo yatokana na neema ya Mungu, na kwamba ni hakika kuwa ahadi hiyo ni kwa ajili ya wote: si kwa wale tu wanaoishika Sheria, bali pia kwa wale waishio kwa imani kama Abrahamu. Yeye ni baba yetu sisi sote.
17kaip parašyta: “Aš padariau tave daugelio tautų tėvu”;­tėvas prieš Dievą, kuriuo jis tikėjo, kuris atgaivina mirusius, ir tai, ko nėra, vadina taip, lyg būtų.
17Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Nimekuweka uwe baba wa mataifa mengi." Ahadi hiyo ni kweli mbele ya Mungu ambaye Abrahamu alimwamini--Mungu ambaye huwapa wafu uzima, na kwa amri yake, vitu ambavyo havikuwapo huwa.
18Nesant jokios vilties, Abraomas patikėjo viltimi ir taip tapo daugelio tautų tėvu, kaip jam buvo pasakyta: “Tokie bus tavo palikuonys”.
18Abrahamu aliamini na kutumaini ingawa hali yenyewe ilikuwa bila matumaini, na hivyo amekuwa baba wa mataifa mengi kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Wazao wako watakuwa wengi kama nyota!"
19Jis nepavargo tikėti ir nelaikė savo kūno apmirusiu (nors jam buvo apie šimtą metų) ir Saros įsčių apmirusiomis.
19Alikuwa mzee wa karibu miaka mia moja, lakini imani yake haikufifia ingawa alijua kwamba mwili wake ulikuwa kama umekufa, na pia mkewe, Sara, alikuwa tasa.
20Jis nepasidavė netikėjimui Dievo pažadu, bet buvo tvirtas tikėjime, teikdamas Dievui šlovę
20Abrahamu hakuionea mashaka ile ahadi ya Mungu; alipata nguvu kutokana na imani, akamtukuza Mungu.
21ir būdamas visiškai įsitikinęs, jog, ką Jis pažadėjo, įstengs ir įvykdyti.
21Alijua kwamba Mungu anaweza kuyatekeleza yale aliyoahidi.
22Todėl jam tai buvo įskaityta teisumu.
22Ndiyo maana Mungu alimkubali kuwa mwadilifu.
23Tačiau ne vien apie jį parašyta, kad “buvo įskaityta”,
23Inaposemwa, "Alimkubali," haisemwi kwa ajili yake mwenyewe tu.
24bet ir apie mus,­nes turės būti įskaityta ir mums, jei tikime Tą, kuris prikėlė iš numirusių Jėzų, mūsų Viešpatį,
24Jambo hili linatuhusu sisi pia ambao tunamwamini Mungu aliyemfufua Yesu, Bwana wetu, kutoka wafu.
25paaukotą dėl mūsų nusikaltimų ir prikeltą mums išteisinti.
25Yeye alitolewa auawe kwa ajili ya dhambi zetu, akafufuka ili tupate kukubaliwa kuwa waadilifu na Mungu.