Lithuanian

Swahili: New Testament

Romans

3

1Koks tada pranašumas būti žydu arba kokia nauda iš apipjaustymo?
1Basi, Myahudi ana nini zaidi kuliko watu wengine? Au kutahiriwa kuna faida gani?
2Visokeriopas! Pirmiausia tas, kad jiems buvo patikėtas Dievo žodis.
2Naam, iko faida kwa kila upande. Kwanza, Mungu aliwakabidhi Wayahudi ujumbe wake.
3Jei kai kurie tapo netikintys,­negi jų netikėjimas panaikins Dievo ištikimybę?
3Lakini itakuwaje iwapo baadhi yao hawakuwa waaminifu? Je, jambo hilo litaondoa uaminifu wa Mungu?
4Jokiu būdu! Dievas išlieka teisingas, o kiekvienas žmogus­melagis, kaip parašyta: “Kad Tu būtum pripažintas teisus savo žodžiuose ir laimėtum, kai esi teisiamas”.
4Hata kidogo! Mungu hubaki mwaminifu daima, ingawaje kila binadamu ni mwongo. Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Kila usemapo, maneno yako ni ya haki; na katika hukumu, wewe hushinda."
5Jei mūsų neteisumas iškelia Dievo teisumą,­ką gi sakysime? Gal Dievas neteisus, rūsčiai bausdamas? Kalbu, kaip žmonėms įprasta.
5Lakini, ikiwa uovu wetu unathibitisha kwamba Mungu anatenda kwa haki, tutasema nini? Je, tutasema kwamba anakosa haki akituadhibu? (Hapa naongea kibinadamu).
6Jokiu būdu! Kaip tada Dievas galėtų teisti pasaulį?
6Hata kidogo! Ingekuwa hivyo, Mungu angewezaje kuuhukumu ulimwengu?
7Bet jeigu Dievo tiesa per mano melagystę tik dar labiau iškilo Jo šlovei, tai kam dar teisti mane kaip nusidėjėlį?
7Labda utasema: "Ikiwa ukosefu wa uaminifu kwa upande wangu unamdhihirisha Mungu kuwa mwaminifu zaidi na hivyo kumpatia utukufu, basi singepaswa kuhukumiwa kuwa mwenye dhambi!"
8Tai gal “darykime bloga, kad išeitų gera”,­kaip esame šmeižiami ir kaip kai kurie sako mus skelbiant? Tokie pasmerkti vertai.
8Ni sawa na kusema: tufanye maovu ili tupate mema! Ndivyo wengine walivyotukashifu kwa kutushtaki kwamba tumefundisha hivyo. Watahukumiwa wanavyostahili!
9Tai ką gi? Ar mes turime pirmenybę? Visai ne! Juk jau įrodėme, kad žydai ir pagonys­visi yra nuodėmės valdžioje,
9Tuseme nini, basi? Je, sisi Wayahudi ni bora zaidi kuliko wengine? Hata kidogo! Kwa maana nimekwisha bainisha hapo mwanzoni kwamba Wayahudi na watu wa mataifa mengine wote wako chini ya utawala wa dhambi.
10kaip parašyta: “Nėra teisaus, nėra nė vieno.
10Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Hakuna hata mmoja aliye mwadilifu!
11Nėra išmanančio, nėra kas Dievo ieškotų.
11Hakuna mtu anayeelewa, wala anayemtafuta Mungu.
12Visi paklydo ir tapo netikusiais; nėra kas darytų gera, nėra nė vieno!
12Wote wamepotoka wote wamekosa; hakuna atendaye mema, hakuna hata mmoja.
13Jų gerklė­atviras kapas; savo liežuviais klastas jie raizgė, gyvačių nuodai jų lūpose.
13Makoo yao ni kama kaburi wazi, ndimi zao zimejaa udanganyifu, midomoni mwao mwatoka maneno yenye sumu kama ya nyoka.
14Jų burna pilna keiksmų ir kartumo,
14Vinywa vyao vimejaa laana chungu.
15jų kojos eiklios kraujo pralieti,
15Miguu yao iko mbioni kumwaga damu,
16jų keliuose griuvimas ir vargas.
16popote waendapo husababisha maafa na mateso;
17Jie nepažino taikos kelio,
17njia ya amani hawaijui.
18ir prieš jų akis nestovi Dievo baimė”.
18Hawajali kabisa kumcha Mungu."
19Mes gi žinome, kad, ką besakytų įstatymas, jis kalba tiems, kurie yra įstatymo valdžioje, kad visos burnos užsičiauptų ir visas pasaulis pasirodytų kaltas prieš Dievą,
19Tunajua kwamba Sheria huwahusu walio chini ya Sheria hiyo, hata hawawezi kuwa na kisingizio chochote, na ulimwengu wote uko chini ya hukumu ya Mungu.
20nes įstatymo darbais Jo akivaizdoje nebus išteisintas nė vienas žmogus. Per įstatymą tik pažįstame nuodėmę.
20Maana hakuna binadamu yeyote anayekubaliwa kuwa mwadilifu mbele yake Mungu kwa kuishika Sheria; kazi ya Sheria ni kumwonyesha tu mtu kwamba ametenda dhambi.
21Bet dabar, nepriklausomai nuo įstatymo, yra apreikštas Dievo teisumas, kurį paliudijo Įstatymas ir Pranašai,­
21Lakini sasa, njia ya Mungu ya kuwakubali watu kuwa waadilifu imekwisha dhihirishwa, tena bila kutegemea Sheria. Sheria na manabii hushuhudia jambo hili.
22Dievo teisumas, tikėjimu į Jėzų Kristų duodamas visiems, kurie tiki. Nėra jokio skirtumo,
22Mungu huwakubali watu kuwa waadilifu kwa njia ya imani yao kwa Yesu Kristo; Mungu hufanya hivyo kwa wote wanaoamini; hakuna ubaguzi wowote.
23nes visi nusidėjo ir stokoja Dievo šlovės,
23Watu wote wametenda dhambi na wametindikiwa utukufu wa Mungu.
24o išteisinami dovanai Jo malone dėl atpirkimo, kuris yra Jėzuje Kristuje.
24Lakini kwa zawadi ya neema ya Mungu, watu wote hukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya Yesu Kristo anayewakomboa.
25Dievas Jį paskyrė permaldavimo auka, veikiančia per tikėjimą Jo kraujo galia. Jis parodė savo teisumą tuo, kad, būdamas kantrus, nenubaudė už nuodėmes, padarytas anksčiau,
25Mungu alimtoa Yesu kusudi, kwa damu yake, awe njia ya kuwaondolea watu dhambi zao kwa imani yao kwake. Alifanya hivyo ili apate kuonyesha kwamba yeye ni mwadilifu. Hapo zamani Mungu alikuwa mvumilivu bila kuzijali dhambi za watu;
26ir parodė savo teisumą dabartiniu metu, pasirodydamas esąs teisus ir išteisinantis tą, kuris tiki Jėzų.
26lakini sasa, wakati huu, anazikabili dhambi za watu apate kuonyesha uadilifu wake. Kwa namna hiyo Mungu mwenyewe huonyesha kwamba yeye ni mwadilifu na kwamba humkubali kuwa mwadilifu mtu yeyote anayemwamini Yesu.
27Kur tada pagrindas girtis? Jis atmestas. Kokiu įstatymu? Darbų? Ne, tik tikėjimo įstatymu.
27Basi, tunaweza kujivunia nini? Hakuna! Kwa nini? Je, kwa sababu ya kutimiza Sheria? La! Bali kwa sababu tunaamini.
28Mes įsitikinę, kad žmogus išteisinamas tikėjimu, be įstatymo darbų.
28Maana mtu hukubaliwa kuwa mwadilifu kwa imani, wala si kwa kutimiza matakwa ya Sheria.
29Argi Dievas­tiktai žydų Dievas? Ar Jis nėra ir pagonių? Taip, ir pagonių,
29Au je, Mungu nu Mungu wa Wayahudi tu, ama pia wa watu wa mataifa mengine? Naam, wa mataifa mengine pia.
30nes tėra vienas Dievas, kuris per tikėjimą išteisins apipjaustytus ir per tikėjimą išteisins neapipjaustytus.
30Mungu ni mmoja, naye atawakubali Wayahudi kuwa waadilifu kwa imani yao, na watu wa mataifa mengine pia kwa imani yao.
31O gal tikėjimu panaikiname įstatymą? Jokiu būdu! Priešingai, mes įstatymą įtvirtiname.
31Je, tunaitumia imani kuibatilisha Sheria? Hata kidogo; bali tunaipa Sheria thamani yake kamili.