1Esi nepateisinamas, kas bebūtum, žmogau, kuris teisi kitą. Juk teisdamas kitą, pasmerki save, nes ir pats tai darai, už ką teisi.
1Basi, rafiki, kama unawahukumu wengine, huwezi kamwe kujitetea haidhuru wewe ni nani. Kwa maana, kwa kuwahukumu wengine, unajilaani wewe mwenyewe kwa vile nawe unayafanya mambo yaleyale unayohukumu.
2Mes žinome, kad Dievas teisingai teis tuos, kurie tokius nusikaltimus daro.
2Tunajua kwamba hukumu ya Mungu kwa wale wanaofanya mambo kama hayo ni hukumu ya haki.
3Nejaugi manai, žmogau, pats taip darydamas ir teisdamas taip darančius, išvengsiąs Dievo teismo?!
3Lakini wewe, rafiki, unayewahukumu wale wanaofanya mambo kama hayo bali wewe pia unayafanya, je unadhani utaiepa hukumu ya Mungu?
4Kaip drįsti niekinti Jo gerumo, pakantumo ir kantrumo turtus? Ar nesupranti, kad Dievo gerumas skatina tave atgailauti?
4Au labda unaudharau wema wake mkuu, uvumilivu wake na saburi yake, bila kutambua kwamba wema wake huo una shabaha ya kukuongoza upate kutubu?
5Deja, savo užkietėjimu bei neatgailaujančia širdimi tu pats sau kaupi rūstybę Dievo rūstybės ir Jo teisingo teismo apsireiškimo dienai.
5Lakini unao ugumu na ukaidi wa moyo, na hivyo unajilundikia adhabu kwa Siku ile ambayo ghadhabu ya Mungu na hukumu zake za haki vitadhihirishwa.
6Jis kiekvienam atmokės pagal jo darbus:
6Siku hiyo Mungu atamlipa kila mmoja kufuatana na matendo yake.
7tiems, kurie, ištvermingai darydami gera, ieško šlovės, garbingumo ir nemirtingumo,amžinuoju gyvenimu,
7Wale wanaozingatia kutenda mema, kutafuta utukufu na heshima ya Mungu na kutokufa, watapata uzima wa milele.
8o išpuikėliams, kurie nepaklūsta tiesai, bet yra pasidavę neteisumui,pykčiu ir rūstybe.
8Lakini wale wengine wenye ubinafsi, wenye kukataa mambo ya haki na kufuata uovu, wataangukiwa na ghadhabu na hasira ya Mungu.
9Sielvartas ir suspaudimas sielai kiekvieno žmogaus, kuris daro bloga, pirma žydo, paskui graiko.
9Mateso na maumivu yatampata binadamu yeyote atendaye uovu. Yatawapata Wayahudi kwanza, na watu wa mataifa mengine pia.
10Ir šlovė, pagarba bei ramybė kiekvienam, kuris daro gera, pirma žydui, paskui graikui.
10Lakini Mungu atawapa utukufu, heshima na amani wale wanaotenda mema; Wayahudi kwanza, na watu wa mataifa mengine pia.
11Juk Dievas nėra šališkas.
11Maana Mungu hambagui mtu yeyote.
12Visi, kurie nusidėjo, neturėdami įstatymo, pražus be įstatymo, o visi, kurie nusidėjo, turėdami įstatymą, bus nuteisti pagal įstatymą.
12Wale wanaotenda dhambi bila kuijua Sheria ya Mose wataangamia ingawaje hawajui Sheria. Na wale wanaotenda dhambi wakiwa wanaijua Sheria watahukumiwa kisheria.
13Ne įstatymo klausytojai teisūs Dievo akyse, bet įstatymo vykdytojai bus išteisinti.
13Mtu hafanywi kuwa mwadilifu mbele yake Mungu kwa kuisikia Sheria, bali kwa kuitii Sheria.
14Kai jokio įstatymo neturintys pagonys iš prigimties vykdo įstatymo reikalavimus, tada jieneturintys įstatymopatys sau yra įstatymas.
14Mathalan: watu wa mataifa mengine hawana Sheria ya Mose; lakini kila wanapotimiza matakwa ya Sheria wakiongozwa na dhamiri zao, wao wenyewe wanakuwa kipimo cha Sheria ingawa hawaijui Sheria.
15Jie parodo, kad įstatymo reikalavimai įrašyti jų širdyse, ir tai liudija jų sąžinė bei mintys, kurios tai kaltina, tai teisina viena kitą.
15Mwenendo wao unaonyesha kwamba matakwa ya Sheria yameandikwa mioyoni mwao. Dhamiri zao zinashuhudia pia jambo hilo, maana fikira zao mara nyingine huwashtaki, na mara nyingine huwatetea.
16Aną dieną Dievas per Jėzų Kristų teis žmonių slėpinius, kaip sako mano skelbiama Evangelija.
16Hivyo, kufuatana na hii Habari Njema ninayohubiri, ndivyo itakavyokuwa wakati Mungu atakapohukumu mambo ya siri ya binadamu kwa njia ya Yesu Kristo.
17Štai tu vadiniesi žydas, pasikliauji įstatymu ir giriesi Dievu.
17Na wewe, je? Wewe mwenyewe unajiita Myahudi; unaitumainia Sheria na kujivunia kuwa wa Mungu;
18Tu žinai Jo valią ir, įstatymo pamokytas, išmanai, kas geriau.
18kwa njia ya Sheria unajua matakwa ya Mungu na unaweza kuchagua jambo jema;
19Įsitikinęs, kad esi aklųjų vadovas, šviesa tamsoje esantiems,
19wewe unajiona kuwa kiongozi wa vipofu na mwanga kwa wale walio gizani;
20neišmanančių mokytojas, kūdikių auklėtojas, turįs įstatyme išreikštą pažinimą ir tiesą.
20unajiona kuwa mkufunzi wa wajinga na mwalimu wa wale wasiokomaa bado. Unayo katika Sheria picha kamili ya elimu na ukweli.
21Tai kodėl tu, mokydamas kitus, nepamokai pats savęs? Kodėl, liepdamas nevogti, pats vagi?
21Basi, wewe unawafundisha wengine; kwa nini hujifundishi wewe mwenyewe? Unawahubiria wengine wasiibe, lakini kumbe wewe mwenyewe unaiba.
22Sakydamas nesvetimauti, pats svetimauji? Bjaurėdamasis stabais, pats apiplėši šventyklas?
22Unasema: "Msizini," na huku wewe unazini; unachukia sanamu za miungu hali wewe unajitajirisha kwa kuiba katika nyumba za miungu.
23Giriesi įstatymu, o paniekini Dievą, laužydamas įstatymą?
23Kwa kujigamba ati unayo Sheria ya Mungu, je huoni kwamba kwa kuivunja Sheria unamdharau Mungu?
24Juk parašyta: “Dėl jūsų piktžodžiauja Dievo vardui pagonys”.
24Kama vile Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Watu wa mataifa mengine wamelikufuru jina la Mungu kwa sababu yenu ninyi Wayahudi!"
25Apipjaustymas, tiesa, naudingas, jei vykdai įstatymą. O jeigu esi įstatymo laužytojas, tavo apipjaustymas tampa neapipjaustymu.
25Kutahiriwa kwako kutakuwa na maana kama ukiitii Sheria. Lakini kama unaivunja Sheria, basi, ni afadhali ungalibaki bila kutahiriwa.
26Taigi, kai neapipjaustytas žmogus laikosi įstatymo reikalavimų, ar jo neapipjaustymas nebus įskaitytas apipjaustymu?
26Kama mtu wa mataifa mengine ambaye hakutahiriwa akitimiza matakwa ya Sheria, hakika atafikiriwa kana kwamba ametahiriwa.
27Ar nuo gimimo neapipjaustytas kūne, bet vykdantis įstatymą nepasmerks tavęs, kuris laužai įstatymą, turėdamas jo raidę ir apipjaustymą?
27Watu wa mataifa mengine watakuhukumu wewe Myahudi kama ukiivunja Sheria, ingawaje unayo maandishi ya Sheria na umetahiriwa, hali wao wanaitii Sheria ingawa hawakutahiriwa.
28Ne tas yra žydas, kuris išoriškai laikomas žydu, ir ne tas apipjaustymas, kuris išoriškai atliktas kūne.
28Ndiyo kusema, si kila anayeonekana kwa nje kuwa Myahudi ni Myahudi wa kweli, wala mtu hawi Myahudi wa kweli ati kwa kuwa ametahiriwa kimwili.
29Bet tas yra žydas, kuris toks viduje, ir tada yra apipjaustymas, kai širdis apipjaustyta dvasioje, o ne pagal raidę. Tokiam ir šlovė ne iš žmonių, bet iš Dievo.
29Myahudi wa kweli ni yule aliye Myahudi kwa ndani, yaani yule ambaye ametahiriwa moyoni. Hili ni jambo la Roho, na si jambo la maandishi ya Sheria. Mtu wa namna hiyo anapata sifa, si kutoka kwa watu, bali kutoka kwa Mungu.