1Paulius, Jėzaus Kristaus tarnas, pašauktas apaštalu, išrinktas skelbti Dievo Evangeliją,
1Kutoka kwangu mimi Paulo, mtumishi wa Kristo Yesu, na mtume niliyeteuliwa na kuitwa kwa ajili ya kuhubiri Habari Njema ya Mungu.
2kurią Jis iš anksto pažadėjo per savo pranašus Šventuosiuose Raštuose,
2Hapo kale, Mungu aliwaahidia watu hii Habari Njema kwa njia ya manabii wake katika Maandiko Matakatifu.
3apie Jo Sūnų, kūnu kilusį iš Dovydo palikuonių,
3Hii Habari Njema inamhusu Mwana wa Mungu, Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye mintarafu ubinadamu wake, alikuwa mzawa wa Daudi;
4šventumo Dvasia per prisikėlimą iš numirusių pristatytą galingu Dievo Sūnumi,Jėzų Kristų, mūsų Viešpatį.
4mintarafu utakatifu wake wa kimungu, alithibitishwa kwa uwezo mkuu kwamba ni Mwana wa Mungu kwa kufufuliwa kutoka wafu.
5Per Jį gavome malonę ir apaštalystę, kad Jo vardu padarytume klusnias tikėjimui visas tautas,
5Kwa njia yake, mimi nimepewa neema ya kuwa mtume, ili kwa ajili yake niwaongoze watu wa mataifa yote wapate kuamini na kutii.
6iš kurių ir jūs esate Jėzaus Kristaus pašaukti.
6Ninyi ni miongoni mwa watu hao; mmeitwa muwe watu wake Yesu Kristo.
7Visiems Dievo numylėtiesiems, esantiems Romoje, pašauktiesiems šventiesiems: tebūna jums malonė bei ramybė nuo mūsų Dievo Tėvo ir Viešpaties Jėzaus Kristaus!
7Basi, ninawaandikia ninyi nyote mlioko Roma ambao Mungu anawapenda, akawateua muwe watu wake. Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.
8Pirmiausia dėkoju savo Dievui per Jėzų Kristų už jus visus, nes visame pasaulyje kalbama apie jūsų tikėjimą.
8Awali ya yote, namshukuru Mungu wangu kwa njia ya Yesu Kristo kwa ajili yenu nyote, kwa sababu imani yenu inasikika duniani kote.
9Man liudytojas Dievas, kuriam tarnauju dvasia, skelbdamas Jo Sūnaus Evangeliją, jog be paliovos jus prisimenu savo maldose,
9Mungu, ambaye ninamtumikia kwa moyo wangu wote katika kuhubiri Habari Njema ya Mwanae, ni shahidi wangu kwamba ninawakumbukeni
10prašydamas, kad Dievo valia man pavyktų kaip nors atvykti pas jus.
10daima katika sala zangu. Namwomba Mungu akipenda, anipatie nafasi nzuri ya kuja kwenu sasa.
11Trokštu jus pamatyti, kad galėčiau perduoti šiek tiek dvasinių dovanų jums sustiprinti,
11Kwa maana ninatamani sana kuwaoneni ili nipate kuwagawieni zawadi ya kiroho na kuwaimarisha.
12tai yra drauge pasiguosti bendru jūsų ir mano tikėjimu.
12Ndiyo kusema, tutaimarishana: imani yenu itaniimarisha mimi, na yangu itawaimarisha ninyi.
13Noriu, broliai, kad žinotumėte, jog ne kartą ketinau atvykti pas jus,bet iki šiol vis pasitaikydavo kliūčių,kad ir tarp jūsų turėčiau šiek tiek vaisių kaip ir tarp kitų pagonių.
13Ndugu zangu, nataka mjue kwamba mara nyingi nilikusudia kuwatembeleeni, lakini mpaka sasa nimezuiwa. Ningependa kupata mafanikio mema kati yenu kama nilivyopata kati ya watu wa mataifa mengine.
14Juk aš skolingas graikams ir barbarams, mokytiems ir nemokytiems.
14Ninalo jukumu kwa watu wote, waliostaarabika na wasiostaarabika, wenye elimu na wasio na elimu.
15Štai kodėl mano širdį traukia ir jums Romoje skelbti Evangeliją.
15Ndiyo maana ninatamani pia kuihubiri Habari Njema kwenu ninyi mlioko huko Roma.
16Aš nesigėdiju Evangelijos, nes ji yra Dievo jėga išgelbėti kiekvienam, kuris tiki, pirma žydui, paskui graikui.
16Sioni aibu kutangaza Habari Njema; yenyewe ni nguvu ya Mungu inayowaokoa wote wanaoamini: Wayahudi kwanza, na wasio Wayahudi pia.
17Joje apsireiškia Dievo teisumas iš tikėjimo į tikėjimą, kaip parašyta: “Teisusis gyvens tikėjimu”.
17Kwa maana Habari Njema inaonyesha wazi jinsi Mungu anavyowakubali watu kuwa waadilifu; jambo hili hufanyika kwa imani, tangu mwanzo mpaka mwisho. Kama ilivyoandikwa: "Mwadilifu kwa imani ataishi."
18Dievo rūstybė apsireiškia iš dangaus už visokią žmonių bedievystę ir neteisybę, kai teisybę jie užgniaužia neteisumu.
18Ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni dhidi ya uasi na uovu wote wa binadamu ambao kwa njia zao mbaya wanaupinga ukweli usijulikane.
19Juk tai, kas gali būti žinoma apie Dievą, jiems aišku, nes Dievas jiems tai apreiškė.
19Kwa maana, yote yanayoweza kujulikana juu ya Mungu ni wazi kwao; maana Mungu mwenyewe ameyadhirisha.
20Jo neregimosios ypatybėsJo amžinoji galybė ir dievystėnuo pat pasaulio sukūrimo aiškiai suvokiamos iš Jo kūrinių, todėl jie nepateisinami.
20Tangu Mungu alipoumba ulimwengu, uwezo wake wa milele na uungu wake, ingawa havionekani kwa macho, vinafahamika wazi. Watu wanaweza kuyajua mambo hayo kutokana na vitu hivyo alivyoumba Mungu. Kwa hiyo hawana njia yoyote ya kujitetea!
21Pažinę Dievą, jie negarbino Jo kaip Dievo ir Jam nedėkojo, bet tuščiai mąstydami paklydo, ir neišmani jų širdis aptemo.
21Ingawa wanajua kuna Mungu, lakini hawampi heshima anayostahili, wala hawamshukuru. Badala yake, fikira zao zimekuwa batili na akili zao tupu zimejaa giza.
22Vadindami save išmintingais, tapo kvaili.
22Wanajidai kuwa wenye hekima, kumbe ni wapumbavu.
23Jie išmainė nenykstančiojo Dievo šlovę į nykstančius žmogaus, paukščių, keturkojų bei šliužų atvaizdus.
23Wanaacha kumwabudu Mungu aishiye milele, na badala yake, wanaabudu sanamu zilizo mfano wa binadamu ambaye hufa, mfano wa wanyama, ndege, au wanyama watambaao.
24Todėl Dievas per jų širdies geidulius atidavė juos neskaistumui, kad jie patys terštų savo kūnus.
24Kwa sababu hiyo, Mungu amewaacha wafuate tamaa mbaya za mioyo yao na kufanyiana mambo ya aibu kwa miili yao.
25Jie Dievo tiesą iškeitė į melą ir garbino kūrinius bei tarnavo jiems, o ne Kūrėjui, kuris palaimintas per amžius. Amen!
25Wanaubadili ukweli juu ya Mungu kwa uongo; wanaheshimu na kuabudu kiumbe badala ya Muumba mwenyewe, ambaye ndiye astahiliye sifa milele! Amina.
26Todėl Dievas paliko juos gėdingų aistrų valiai. Jų moterys prigimtinius santykius pakeitė priešingais prigimčiai.
26Kwa hiyo, Mungu amewaacha wafuate tamaa mbaya. Hata wanawake wanabadili matumizi yanayopatana na maumbile.
27Panašiai ir vyrai, pametę prigimtinius santykius su moterimis, užsigeidė vienas kito, ištvirkavo vyrai su vyrais, ir gaudavo už savo paklydimą vertą atpildą.
27Nao wanaume hali kadhalika, wanaacha kufuata matumizi ya maumbile ya mume na mke wakawakiana tamaa wao kwa wao. Wanaume wanafanyiana mambo ya aibu, na hivyo wanajiletea wenyewe adhabu wanayostahili kwa vitendo vyao viovu.
28Kadangi jie nesirūpino pažinti Dievą, tai Dievas leido jiems vadovautis netikusiu išmanymu ir daryti, kas nepridera.
28Kwa vile watu walikataa kumtambua Mungu, Mungu amewaacha katika fikira zao potovu, wakafanya yale ambayo hawangestahili kufanya.
29Todėl jie pilni visokio neteisumo, netyrumo, piktybių, godulystės ir piktumo, pilni pavydo, žudynių, nesantaikos, klastingumo, paniekos, apkalbų.
29Wamejaa kila aina ya uovu, dhuluma, ulafi na ufisadi. Wamejaa wivu, uuaji, ugomvi, udanganyifu na nia mbaya; husengenya,
30Tai šmeižikai, nekenčiantys Dievo, akiplėšos, išpuikėliai, pagyrūnai, išradingi piktadariai, neklausantys tėvų,
30na kusingiziana; ni watu wa kuchukiza kwa Mungu, wafidhuli, wenye kiburi na majivuno; hodari sana katika kutenda mabaya, na hawawatii wazazi wao;
31neprotingi, nepatikimi, nemylintys, neatlaidūs, negailestingi.
31hawana dhamiri, hawatimizi ahadi zao, hawana wema wala huruma kwa wengine.
32Nors jie žino teisingą Dievo nuosprendį, kad visa tai darantys verti mirties, jie ne tik patys taip daro, bet ir palaiko taip darančius.
32Wanajua kwamba Sheria ya Mungu yasema kwamba watu wanaoishi mithili hiyo, wanastahili kifo. Zaidi ya hayo, siyo tu kwamba wanafanya mambo hayo wao wenyewe, bali hata huwapongeza wale wanaofanya mambo hayohayo.