1Išsigelbėję jie sužinojo, kad sala vadinasi Melitė.
1Tulipokwisha fika salama kwenye nchi kavu, tuligundua kwamba kile kisiwa kinaitwa Malta.
2Barbarai su mumis elgėsi labai draugiškai. Užkūrė ugnį ir pakvietė mus visus prie jos, nes lijo ir buvo šalta.
2Wenyeji wa hapo walikuwa wema sana kwetu. Mvua ilikuwa inaanza kunyesha na kulikuwa na baridi, hivyo waliwasha moto, wakatukaribisha.
3Paulius pririnko glėbį sausų šakų ir metė į ugnį. Čia nuo kaitros iš laužo iššoko gyvatė ir įsikirto jam į ranką.
3Paulo aliokota mzigo mdogo wa kuni akawa anazitia motoni. Hapo, kwa sababu ya lile joto la moto, nyoka akatoka katika kuni akamnasa Paulo mkononi na kujishikilia hapo.
4Pamatę prie rankos prikibusią gyvatę, barbarai ėmė vienas kitam kalbėti: “Tas žmogus tikriausiai žmogžudys: išsigelbėjo iš jūros, o keršto deivė vis tiek neduoda jam gyventi”.
4Wenyeji wa pale walipokiona kile kiumbe kinaning'inia kwenye mkono wake waliambiana, "Bila shaka mtu huyu amekwisha ua mtu, na ingawa ameokoka kuangamia baharini, Haki haitamwacha aendelee kuishi!"
5Tačiau jis nupurtė šliužą į ugnį, nepatirdamas nieko blogo.
5Lakini Paulo alikikung'utia kile kiumbe motoni na hakuumizwa hata kidogo.
6Barbarai laukė, kada jis ištins ar staiga kris negyvas. Laukę nesulaukę ir pamatę, kad jam nesidaro nieko blogo, jie pakeitė nuomonę ir ėmė kalbėti, jog jis esąs dievas.
6Wale watu walikuwa wakitazamia kwamba angevimba au hapohapo angeanguka chini na kufa. Baada ya kungojea kwa muda mrefu bila kuona kwamba Paulo amepatwa na jambo lolote lisilo la kawaida, walibadilisha fikira zao juu yake, wakasema kuwa ni mungu.
7Netoli tos vietos buvo vyriausiojo salos valdininko, vardu Publijus, valdos. Jis mus priėmė ir tris dienas bičiuliškai globojo.
7Karibu na mahali pale palikuwa na mashamba ya Publio, mkuu wa kile kisiwa. Publio alitukaribisha kirafiki, tukawa wageni wake kwa siku tatu.
8Tuo metu Publijaus tėvas susirgo karštine ir viduriavimu. Paulius užėjo pas jį, pasimeldė, uždėjęs ant jo rankas, ir išgydė.
8Basi, ikawa kwamba baba yake Publio alikuwa amelala kitandani, mgonjwa, ana homa na kuhara. Paulo alikwenda kumwona na baada ya kusali, akaweka mikono yake juu ya mgonjwa, akamponya.
9Po šito įvykio ir kiti salos gyventojai, turėję ligų, ėjo pas Paulių ir buvo pagydomi.
9Kutokana na tukio hilo, wagonjwa wote katika kile kisiwa walikuja wakaponywa.
10Už tai jie mus didžiai gerbė, o išvykstant aprūpino viskuo, ko mums reikėjo.
10Watu walitupatia zawadi mbalimbali na wakati tulipoanza tena safari, walitia ndani ya meli masurufu tuliyohitaji.
11Po trijų mėnesių mes išplaukėme žiemojusiu saloje Aleksandrijos laivu, kuris turėjo Dvynių ženklą.
11Baada ya miezi mitatu tulianza tena safari yetu kwa meli moja ya Aleksandria iitwayo "Miungu Pacha". Meli hiyo ilikuwa imetia nanga kisiwani wakati wote wa baridi.
12Atplaukę į Sirakūzus, prastovėjome tris dienas.
12Tulifika katika mji wa Sirakusa, tukakaa hapo kwa siku tatu.
13Iš ten plaukdami, esant nepalankiam vėjui, pasiekėme Regijų ir dar po dienos, ėmus pūsti pietų vėjui, kitą dieną atvykome į Puteolus.
13Toka huko tuling'oa nanga, tukazunguka na kufika Regio. Baada ya siku moja, upepo ulianza kuvuma kutoka kusini, na baada ya siku mbili tulifika bandari ya Potioli.
14Ten susitikome su broliais; jie pakvietė mus septynioms dienoms paviešėti. Taip mes atvykome į Romą.
14Huko tuliwakuta ndugu kadhaa ambao walituomba tukae nao kwa juma moja. Hivi ndivyo tulivyopata kufika Roma.
15Tenykščiai broliai, išgirdę apie mus, atėjo pasitikti iki Apijaus aikštės ir Trijų tavernų. Juos išvydęs, Paulius dėkojo Dievui ir įgavo naujo pasitikėjimo.
15Ndugu wa kule Roma walipopata habari zetu, wakaja kutulaki kwenye soko la Apio na Mikahawa Mitatu. Paulo alipowaona alimshukuru Mungu, akapata moyo.
16Kai atvykome į Romą, šimtininkas perdavė kalinius sargybos viršininkui, o Pauliui buvo leista apsigyventi vienam su saugojančiu jį kareiviu.
16Tulipofika Roma, Paulo aliruhusiwa kukaa peke yake pamoja na askari mmoja wa kumlinda.
17Po trijų dienų Paulius pakvietė pas save žydų vadovus. Jiems susirinkus, jis prabilo: “Vyrai broliai! Nors aš nieku nesu nusikaltęs nei tautai, nei mūsų tėvų papročiams, buvau Jeruzalėje suimtas ir atiduotas į romėnų rankas.
17Baada ya siku tatu, Paulo aliwaita pamoja viongozi wa Kiyahudi wa mahali hapo. Walipokusanyika, Paulo aliwaambia, "Wananchi wenzangu, mimi, ingawa sikufanya chochote kibaya wala kupinga desturi za wazee wetu, nilitiwa nguvuni kule Yerusalemu na kutiwa mikononi mwa Waroma.
18Tie ištardę, norėjo mane paleisti, nes nerado jokio mirties verto nusižengimo.
18Waliponihoji na kuona kwamba sikuwa na hatia yeyote, walitaka kuniacha.
19Kadangi žydai prieštaravo, turėjau šauktis ciesoriaus, tiktai ne tam, kad apkaltinčiau savo tautą.
19Lakini Wayahudi wengine walipinga jambo hilo, nami nikalazimika kukata rufani kwa Kaisari, ingawa sikuwa na chochote cha kuwashtaki wananchi wenzangu.
20Dėl šios priežasties ir pakviečiau jus, kad su jumis pasimatyčiau ir pasikalbėčiau; nes dėl Izraelio vilties esu surakintas šita grandine!”
20Ni kwa sababu hiyo nimeomba kuonana na kuongea nanyi, maana nimefungwa minyororo hii kwa sababu ya tumaini lile la Israeli."
21Jie atsakė jam: “Mes nesame gavę apie tave iš Judėjos laiškų, ir nė vienas iš atvykusių brolių nepranešė ir nekalbėjo nieko blogo apie tave.
21Wao wakamwambia, "Sisi hatujapokea barua yoyote kutoka Yudea, wala hakuna ndugu yeyote aliyefika hapa na kutoa habari rasmi au kusema chochote kibaya juu yako.
22Vis dėlto norėtume išgirsti tavo pažiūras. Mat apie šitą sektą tiek težinome, jog jai visur prieštaraujama”.
22Lakini tunafikiri inafaa tusikie kutoka kwako mwenyewe mambo yaliyo kichwani mwako. Kwa maana tujualo sisi kuhusu hicho kikundi ni kwamba kinapingwa kila mahali."
23Paskyrę jam dieną, jie gausiai susirinko pas jį svečių kambaryje. Nuo ryto iki vakaro jis aiškino jiems ir liudijo apie Dievo karalystę, įrodinėdamas jiems Jėzų iš Mozės Įstatymo ir Pranašų.
23Basi, walipanga naye siku kamili ya kukutana, na wengi wakafika huko alikokuwa anakaa. Tangu asubuhi mpaka jioni Paulo aliwaeleza na kuwafafanulia juu ya Ufalme wa Mungu akijaribu kuwafanya wakubali habari juu ya Yesu kwa kutumia Sheria ya Mose na maandiko ya manabii.
24Vieni jo žodžiais patikėjo, kiti ne.
24Baadhi yao walikubali maneno yake, lakini wengine hawakuamini.
25Nesutardami tarpusavyje, jie ėmė skirstytis, o Paulius tepasakė jiems viena: “Teisingai Šventoji Dvasia yra mūsų tėvams pasakiusi per pranašą Izaiją:
25Basi, kukawa na mtengano wa fikira kati yao. Walipokuwa wanakwenda zao, Paulo alisema jambo hili, "Kweli ni sawa yale aliyoyanena Roho Mtakatifu kwa wazee wenu kwa njia ya nabii Isaya
26‘Eik pas šitą tautą ir sakyk: girdėti girdėsite, bet nesuprasite, žiūrėti žiūrėsite, bet nematysite.
26akisema: Nenda kwa watu hawa ukawaambie: kusikia mtasikia, lakini hamtaelewa; kutazama mtatazama, lakini hamtaona.
27Šitų žmonių širdis aptuko, jie prastai girdėjo ausimis ir užmerkė akis, kad kartais nepamatytų akimis, neišgirstų ausimis, nesuprastų širdimi ir neatsiverstų, ir Aš jų nepagydyčiau’.
27Maana akili za watu hawa zimepumbaa, wameziba masikio yao, wamefumba macho yao. La sivyo, wangeona kwa macho yao, wangesikia kwa masikio yao. Wangeelewa kwa akili zao, na kunigeukia, asema Bwana, nami ningewaponya."
28Tebūnie tad jums žinoma: šis Dievo išgelbėjimas yra pasiųstas pagonims, ir jie išgirs”.
28Halafu Paulo akamaliza na kusema, "Jueni basi, kwamba ujumbe wa Mungu juu ya wokovu umepelekwa kwa watu wa mataifa. Wao watasikiliza!"
29Jam tai pasakius, žydai išėjo, smarkiai ginčydamiesi tarpusavyje.
29Paulo alipokwisha sema hayo, Wayahudi walijiondokea huku wakiwa wanabishana vikali wao kwa wao.
30Paulius gyveno savo išsinuomotame name ištisus dvejus metus ir priiminėdavo visus, kurie pas jį ateidavo.
30Kwa muda wa miaka miwili mizima Paulo aliishi katika nyumba aliyoipanga yeye mwenyewe; akawa anawakaribisha wote waliofika kumsalimu.
31Jis skelbė Dievo karalystę ir labai drąsiai, netrukdomas mokė apie Viešpatį Jėzų Kristų.
31Alikuwa akihubiri Ufalme wa Mungu na kufundisha juu ya Bwana Yesu Kristo kwa uhodari, bila kizuizi.