1Kai buvo nuspręsta, kad mes turime išplaukti į Italiją, Paulių ir kelis kitus kalinius perdavė Augusto kohortos šimtininkui Julijui.
1Walipokwisha amua tusafiri mpaka Italia, walimweka Paulo pamoja na wafungwa wengine chini ya ulinzi wa Yulio aliyekuwa ofisa wa jeshi katika kikosi kiitwacho "Kikosi cha Augusto."
2Mes įlipome į Adramitijos laivą, kuris turėjo plaukti Azijos pakrantėmis, ir leidomės į kelionę. Su mumis buvo makedonietis Aristarchas iš Tesalonikos.
2Tulipanda meli ya Adiramito iliyokuwa inasafiri na kupitia bandari kadhaa za mkoa wa Asia, tukaanza safari. Aristarko, mwenyeji wa Makedonia kutoka Thesalonika, alikuwa pamoja nasi.
3Kitą dieną atplaukėme į Sidoną. Julijus kilniai elgėsi su Pauliumi ir leido jam aplankyti bičiulius, kad galėtų pasidžiaugti jų globa.
3Kesho yake tulitia nanga katika bandari ya Sidoni. Yulio alimtendea Paulo vizuri kwa kumruhusu awaone rafiki zake na kupata mahitaji yake.
4Išvykę iš ten, plaukėme Kipro užuovėja, nes pūtė priešingi vėjai.
4Kutoka huko tuliendelea na safari, lakini kwa kuwa upepo ulikuwa unavuma kwa kasi kutujia kwa mbele, tulipitia upande wa kisiwa cha Kupro ambapo upepo haukuwa mwingi.
5Perplaukę jūrą ties Kilikija ir Pamfilija, atvykome į Lykijos miestą Myrą.
5Halafu tulivuka bahari ya Kilikia na Pamfulia, tukatia nanga Mura, mji wa Lukia.
6Tenai šimtininkas surado Aleksandrijos laivą, kuris plaukė į Italiją, ir persodino mus į jį.
6Hapo yule ofisa alikuta meli moja ya Aleksandria iliyokuwa inakwenda Italia, na hivyo akatupandisha ndani.
7Daug dienų plaukėme palengva ir vargais negalais atsiradome ties Knidu. Kadangi vėjas kliudė, plaukėme Kretos priedangoje, link Salmonės.
7Kwa muda wa siku nyingi tulisafiri polepole, na kwa shida tulifika karibu na Nido. Kwa sababu upepo ulikuwa bado unatupinga, tuliendelea mbele moja kwa moja tukapitia upande wa Krete karibu na rasi Salmone ambapo upepo haukuwa mwingi.
8Šiaip ne taip ją aplenkę, atvykome į vietovę, kuri vadinosi Dailioji Prieplauka, netoli Lasėjos miesto.
8Tulipita kando yake polepole tukafika mahali paitwapo "Bandari Nzuri", karibu na mji wa Lasea.
9Prabėgo daug laiko, ir laivyba tapo pavojinga, nes jau buvo pasibaigęs rudens pasninko metas. Paulius juos įspėjo,
9Muda mrefu ulikuwa umepita, na hata siku ya kufunga ilikuwa imekwisha pita. Sasa ilikuwa hatari sana kusafiri kwa meli. Basi, Paulo aliwapa onyo:
10sakydamas: “Vyrai, numatau, jog šis plaukimas bus grėsmingas ir pražūtingas ne tik kroviniams bei laivui, bet ir mūsų gyvybėms”.
10"Waheshimiwa, nahisi kwamba safari hii itakuwa ya shida na hasara nyingi si kwa shehena na meli tu, bali pia kwa maisha yetu."
11Tačiau šimtininkas labiau tikėjo vairininku ir laivo savininku negu tuo, ką kalbėjo Paulius.
11Lakini yule ofisa alivutiwa zaidi na maoni ya nahodha na ya mwenye meli kuliko yale aliyosema Paulo.
12Kadangi uostas buvo netinkamas žiemoti, dauguma nusprendė iš ten plaukti toliau, kaip nors pasiekti Feniksą, Kretos uostą, atvirą į pietvakarius ir šiaurės vakarus, ir ten žiemoti.
12Kwa kuwa bandari hiyo haikuwa mahali pazuri pa kukaa wakati wa baridi, wengi walipendelea kuendelea na safari, ikiwezekana mpaka Foinike. Foinike ni bandari ya Krete inayoelekea kusini-magharibi na kaskazini-magharibi; na huko wangeweza kukaa wakati wa baridi.
13Kai ėmė pūsti lengvas pietų vėjas, jie tikėjosi įvykdyti savo sumanymą ir, pakėlę inkarą, leidosi pirmyn palei Kretos krantus.
13Basi, upepo mzuri wa kusi ulianza kuvuma, nao wakadhani wamefanikiwa lengo lao; hivyo wakang'oa nanga, wakaiendesha meli karibu sana na pwani ya Krete.
14Bet netrukus nuo salos pusės pakilo viesulas, vadinamas Šiauriaryčiu.
14Lakini haukupita muda, upepo mkali uitwao "Upepo wa Kaskazi" ulianza kuvuma kutoka kisiwani.
15Jis pagavo laivą, nepajėgusį jam priešintis, ir mes turėjome jį leisti pavėjui.
15Upepo uliipiga ile meli, na kwa kuwa hatukuweza kuukabili, tukaiacha ikokotwe na huo upepo.
16Kai mus nešė pro salelę, vardu Klaudą, mes tik vargais negalais išsaugojome gelbėjimo valtį.
16Kisiwa kimoja kiitwacho Kanda kilitukinga kidogo na ule upepo; na tulipopita kusini mwake tulifaulu, ingawa kwa shida, kuusalimisha ule mtumbwi wa meli.
17Kai ji buvo užkelta, jūreiviai ėmė stiprinti laivąapjuosė jį virvėmis. Bijodami pakliūti ant Sirtės seklumų, jie nuleido bures ir taip plaukė toliau.
17Wale wanamaji waliuvuta mtumbwi ndani, kisha wakaizungushia meli kamba na kuifunga kwa nguvu. Waliogopa kwamba wangeweza kukwama kwenye ufuko wa bahari, pwani ya Libya. Kwa hiyo walishusha matanga na kuiacha meli ikokotwe na upepo.
18Mus baisiai vargino audra. Todėl rytojaus dieną teko išmesti į jūrą dalį krovinio.
18Dhoruba iliendelea kuvuma na kesho yake wakaanza kutupa nje shehena ya meli.
19Trečią dieną savo rankomis išmetėme kai kuriuos laivo įrengimus.
19Siku ya tatu, wakaanza pia kutupa majini vifaa vya meli kwa mikono yao wenyewe.
20Ilgą laiką nematydami nei saulės, nei žvaigždžių, smarkios audros blaškomi, galiausiai praradome bet kokią viltį išsigelbėti.
20Kwa muda wa siku nyingi hatukuweza kuona jua wala nyota; dhoruba iliendelea kuvuma sana, hata matumaini yote ya kuokoka yakatuishia.
21Žmonės jau ilgą laiką nieko nevalgė. Paulius, atsistojęs tarp jų, tarė: “Vyrai! Reikėjo paklausyti manęs ir neplaukti nuo Kretos į jūrą. Būtų išvengta šių pavojų ir nuostolių.
21Baada ya kukaa muda mrefu bila kula chakula, Paulo alisimama kati yao, akasema, "Waheshimiwa, ingalikuwa afadhali kama mngalinisikiliza na kuacha kusafiri kutoka Krete. Kama mngalifanya hivyo tungaliiepuka shida hii na hasara hizi zote.
22Tačiau ir dabar raginu laikytis drąsiai. Niekas iš jūsų nežus, vien tik laivas.
22Lakini sasa ninawaombeni muwe na moyo; hakuna hata mmoja wenu atakayepoteza maisha yake; meli tu ndiyo itakayopotea.
23Šią naktį mane aplankė angelas Dievo, kuriam aš priklausau ir tarnauju,
23Kwa maana jana usiku malaika wa yule Mungu ambaye mimi ni wake na ambaye mimi ninamwabudu alinitokea,
24ir pasakė: ‘Nebijok, Pauliau! Tu privalai stoti prieš ciesorių. Ir štai Dievas tau dovanoja visus, plaukiančius su tavimi’.
24akaniambia: Paulo usiogope! Ni lazima utasimama mbele ya Kaisari; naye Mungu, kwa wema wake, amekufadhili kwa kuwaokoa wote wanaosafiri nawe wasiangamie.
25Tad, vyrai, drąsiau! Aš tikiu Dievu, kad taip ir įvyks, kaip man pasakyta.
25Hivyo, waheshimiwa, jipeni moyo! Maana ninamwamini Mungu kwamba itakuwa sawa kama nilivyoambiwa.
26Mus išmes į kokią nors salą”.
26Lakini ni lazima tutatupwa ufukoni mwa kisiwa fulani."
27Kai buvome svaidomi Adrijos jūroje keturioliktą naktį, apie vidurnaktį jūreiviams pasirodė, kad artėjame prie kažkokios sausumos.
27Usiku wa siku ya kumi na nne, tulikuwa tunakokotwa huku na huku katika bahari ya Adria. Karibu na usiku wa manane wanamaji walijihisi kuwa karibu na nchi kavu.
28Jie išmetė grimzlę ir nustatė dvidešimties sieksnių gylį; po kiek laiko išmatavo dar kartą ir berado penkiolika.
28Hivyo walitafuta kina cha bahari kwa kuteremsha kamba iliyokuwa imefungiwa kitu kizito, wakapata kina cha mita arobaini. Baadaye wakapima tena wakapata mita thelathini.
29Bijodami užšokti ant povandeninių uolų, jie išmetė iš paskuigalio keturis inkarus ir laukė aušros.
29Kwa sababu ya kuogopa kukwama kwenye miamba, waliteremsha nanga nne nyuma ya meli; wakaomba kuche upesi.
30Jūreiviai mėgino pabėgti iš laivo. Jie nuleido į jūrą gelbėjimo valtį, neva norėdami išmesti inkarus laivo priešakyje.
30Wanamaji walitaka kutoroka, na walikwisha kuteremsha ule mtumbwi majini, wakijisingizia kwamba wanakwenda kuteremsha nanga upande wa mbele wa meli.
31Paulius tarė šimtininkui ir kareiviams: “Jeigu šitie nepasiliks laive, jūs neišsigelbėsite”.
31Lakini Paulo alimwambia yule ofisa wa jeshi na askari wake, "Kama wanamaji hawa hawabaki ndani ya meli, hamtaokoka."
32Tada kareiviai nukapojo valties virves ir leido jai nukristi į jūrą.
32Hapo wale askari walizikata kamba zilizokuwa zimeshikilia ule mtumbwi, wakauacha uchukuliwe na maji.
33Prieš rytą Paulius paragino visus valgyti, sakydamas: “Šiandien jau keturiolikta diena, kai jūs laukiate nevalgę, nieko burnoje neturėję.
33Karibu na alfajiri, Paulo aliwahimiza wote wale chakula: "Kwa siku kumi na nne sasa mmekuwa katika mashaka na bila kula; hamjala kitu chochote.
34Todėl aš jus prašau valgyti. To reikia jūsų išsigelbėjimui. Nė vienam iš jūsų nenukris nė plaukas nuo galvos!”
34Basi, ninawasihi mle chakula kwa maana mnakihitaji ili mweze kuendelea kuishi. Maana hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea."
35Tai pasakęs, jis paėmė duonos, visų akivaizdoje padėkojo Dievui, sulaužė ir pradėjo valgyti.
35Baada ya kusema hivyo, Paulo alichukua mkate, akamshukuru Mungu mbele yao wote, akaumega, akaanza kula.
36Tada visi pralinksmėjo ir ėmėsi valgio.
36Hapo wote wakapata moyo, nao pia wakala chakula.
37Laive iš viso buvome du šimtai septyniasdešimt šeši žmonės.
37Jumla tulikuwa watu mia mbili na sabini na sita katika meli.
38Pavalgę jie palengvino laivą, išmesdami jūron javus.
38Baada ya kila mmoja kula chakula cha kutosha, walipunguza uzito wa meli kwa kutupa nafaka baharini.
39Rytui išaušus, jūreiviai negalėjo pažinti žemės, tiktai pastebėjo nedidelę įlanką lėkštais krantais, į kurią, jei bus įmanoma, jie nutarė pasukti laivą.
39Kulipokucha, wanamaji hawakuweza kuitambua nchi ile, ila waliona ghuba moja yenye ufuko; wakaamua kutia nanga huko kama ikiwezekana.
40Nupjovė inkarus, paliko juos jūroje, atleido vairo diržus ir, iškėlę prieš vėją priekinę burę, leidosi į krantą.
40Hivyo walikata nanga na kuziacha baharini, na wakati huohuo wakazifungua kamba zilizokuwa zimeufunga usukani, kisha wakatweka tanga moja mbele kushika upepo, wakaelekea ufukoni.
41Atsidūrę prie seklumos, jie užšokdino ant jos laivą. Priekis liko tvirtai įsmigęs, o paskuigalis ėmė irti nuo smarkios bangų mūšos.
41Lakini walifika mahali ambapo mikondo miwili ya bahari hukutana, na meli ikakwama. Sehemu ya mbele ilikuwa imezama mchangani bila kutikisika. Sehemu ya nyuma ya meli ilianza kuvunjika vipandevipande kwa mapigo ya nguvu ya mawimbi.
42Kareiviai sumanė išžudyti kalinius, kad kuris išplaukęs nepaspruktų.
42Askari walitaka kuwaua wafungwa wote kwa kuogopa kwamba wangeogelea hadi pwani na kutoroka.
43Bet šimtininkas, gelbėdamas Paulių, sutrukdė jų sumanymą. Jis įsakė, kad mokantys plaukti pirmi šoktų į jūrą ir plauktų į krantą,
43Lakini kwa vile yule ofisajeshi alitaka kumwokoa Paulo, aliwazuia wasifanye hivyo. Aliamuru wale waliojua kuogelea waruke kutoka melini na kuogelea hadi pwani,
44o kiti tai padarytų kas ant lentų, kas ant laivo nuolaužų. Šitaip visi išsigelbėjo ir pasiekė žemę.
44na wengine wafuate wakijishikilia kwenye mbao au kwenye vipande vya meli iliyovunjika. Ndivyo sisi sote tulivyofika salama pwani.