Lithuanian

Swahili: New Testament

Acts

26

1Tada Agripa tarė Pauliui: “Tau leidžiama paaiškinti savo bylą”. Paulius, pamojęs ranka, pradėjo gynimosi kalbą:
1Basi, Agripa akamwambia Paulo, "Unaruhusiwa kujitetea." Hapo Paulo alinyosha mkono wake akajitetea hivi:
2“Karaliau Agripa! Esu laimingas, galėdamas šiandien tavo akivaizdoje gintis nuo viso to, kuo esu žydų kaltinamas,
2"Mfalme Agripa, ninajiona mwenye bahati leo kujitetea mbele yako kuhusu yale mashtaka yote ambayo Wayahudi walikuwa wamesema juu yangu.
3juo labiau, kad tau žinomi visi žydų papročiai ir ginčijami klausimai. Todėl prašau kantriai manęs išklausyti.
3Hasa kwa vile wewe mwenyewe ni mtaalamu wa desturi za Wayahudi na migogoro yao, ninakuomba basi unisikilize kwa uvumilivu.
4Visi žydai žino apie mano gyvenimą nuo jaunystės, kuris nuo pradžių prabėgo mano tautoje, Jeruzalėje.
4"Wayahudi wanajua habari za maisha yangu tangu utoto, jinsi nilivyoishi tangu mwanzo kati ya taifa langu huko Yerusalemu.
5Jie pažįsta mane nuo seno ir, jei norėtų, galėtų paliudyti, kad aš, būdamas fariziejus, gyvenau, laikydamasis griežčiausios mūsų religijos krypties.
5Wananifahamu kwa muda mrefu, na wanaweza kushuhudia, kama wakipenda, kwamba tangu mwanzo niliishi kama mmoja wa kikundi chenye siasa kali zaidi katika dini yetu, yaani kikundi cha Mafarisayo.
6Dabar aš čia stoviu ir esu teisiamas už tai, kad viliuosi pažadu, kurį Dievas yra davęs mūsų tėvams.
6Na sasa niko hapa nihukumiwe kwa sababu ninaitumainia ile ahadi ambayo Mungu aliwaahidia babu zetu.
7Jo išsipildant tikisi sulaukti mūsų dvylika giminių, uoliai tarnaudamos Dievui dieną ir naktį. Dėl šitos vilties, karaliau Agripa, aš ir esu žydų kaltinamas.
7Ahadi hiyo ndiyo ileile inayotumainiwa na makabila kumi na mawili ya taifa letu, wakimtumikia Mungu kwa dhati mchana na usiku. Mheshimiwa mfalme, Wayahudi wananishtaki kwa sababu ya tumaini hilo!
8Kodėl jums atrodo neįtikėtina, kad Dievas prikelia numirusius?
8Kwa nini ninyi mnaona shida sana kuamini kwamba Mungu huwafufua wafu?
9Tiesa, ir aš maniau, kad privalau visais būdais kovoti su Jėzaus Nazariečio vardu.
9Kwa kweli mimi mwenyewe niliamini kwamba ni wajibu wangu kufanya mambo mengi kulipinga jina la Yesu wa Nazareti.
10Aš taip ir dariau Jeruzalėje. Gavęs iš aukštųjų kunigų įgaliojimus, daugybę šventųjų uždariau į kalėjimus, o kai jie buvo žudomi, pritardavau.
10Mambo hayo ndiyo niliyoyafanya huko Yerusalemu. Mimi binafsi, nikiwa nimepewa mamlaka kutoka kwa makuhani wakuu, nilipata kuwatia gerezani wengi wa watu wa Mungu. Nao walipohukumiwa kuuawa, nilipiga kura ya kukubali.
11Visose sinagogose dažnai juos bausdavau, versdavau piktžodžiauti ir, be saiko prieš juos įtūžęs, persekiojau net svetimuose miestuose.
11Mara nyingi niliwafanya waadhibiwe katika masunagogi yote nikiwashurutisha waikane imani yao. Hasira yangu kwao ilikuwa kubwa hata nikawasaka mpaka miji ya mbali.
12Tais pačiais tikslais keliavau į Damaską, turėdamas aukštųjų kunigų įgaliojimus ir leidimą.
12"Kwa mujibu huohuo, nilikwenda Damasko wakati mmoja, nikiwa na mamlaka na maagizo kutoka kwa makuhani wakuu.
13Kelyje vidurdienį, karaliau, aš staiga išvydau, kaip mane ir keliavusius su manimi apšvietė šviesa iš dangaus, skaistesnė už saulę.
13Mheshimiwa, wakati nilipokuwa njiani, saa sita mchana, niliona mwanga mkubwa kuliko wa jua ukiangaza kutoka mbinguni, ukanizunguka mimi na wale wasafiri wenzangu.
14Mes visi parpuolėme žemėn, ir aš išgirdau balsą, kuris man sakė hebrajiškai: ‘Sauliau, Sauliau, kam mane persekioji? Sunku tau spyriotis prieš akstiną!’
14Sisi sote tulianguka chini, nami nikasikia sauti ikiniambia kwa Kiebrania: Saulo, Saulo! Kwa nini unanitesa? Unajiumiza bure kama punda anayepiga teke fimbo ya bwana wake.
15Aš paklausiau: ‘Kas Tu esi, Viešpatie?’ Jis atsakė: ‘Aš esu Jėzus, kurį tu persekioji.
15Mimi nikauliza: Ni nani wewe Bwana? Naye Bwana akajibu: Mimi ni Yesu ambaye wewe unamtesa.
16Kelkis ir stokis ant kojų! Aš tau apsireiškiau, kad paskirčiau tave tarnu bei liudytoju tų dalykų, kuriuos matei ir kuriuos tau dar apreikšiu.
16Haidhuru, inuka sasa; simama wima. Nimekutokea ili nikuweke rasmi kuwa mtumishi wangu. Utawathibitishia watu wengine mambo uliyoyaona leo na yale ambayo bado nitakuonyesha.
17Aš tave gelbėsiu nuo tautiečių ir pagonių, pas kuriuos tave dabar siunčiu,
17Nitakuokoa na watu wa Israeli na watu wa mataifa mengine ambao mimi ninakutuma kwao.
18kad atvertum jų akis ir jie iš tamsybių gręžtųsi į šviesą, nuo šėtono valdžios­į Dievą ir, tikėdami mane, gautų nuodėmių atleidimą bei paveldėjimą su pašventintaisiais’.
18Utayafumbua macho yao na kuwawezesha watoke gizani na kuingia katika mwanga; watoke katika utawala wa Shetani, wamgeukie Mungu; ili kwa kuamini, wapate kusamehewa dhambi na kuchukua nafasi yao kati ya wale ambao wamepata kuwa watu wa Mungu.
19Todėl, karaliau Agripa, nebuvau nepaklusnus dangiškam regėjimui
19"Hivyo, mfalme Agripa, sikuweza kuwa mkaidi kwa maono hilo la mbinguni.
20ir iš pradžių Damaske ir Jeruzalėje, o paskui visame Judėjos krašte ir pagonijoje skelbiau, kad žmonės atgailautų, gręžtųsi į Dievą ir imtųsi atgailos vertų darbų.
20Ila nilianza kuhubiri kwanza kwa watu wa Damasko, halafu kwa wale wa Yerusalemu na nchi yote ya Yudea, na pia kwa watu wa mataifa mengine. Niliwahimiza wamgeukie Mungu na kuonyesha kwa vitendo kwamba wamebadilisha mioyo yao.
21Už tai žydai sugriebė mane šventykloje ir mėgino užmušti.
21Kwa sababu hiyo, Wayahudi walinikamata nikiwa Hekaluni, wakajaribu kuniua.
22Bet, Dievui padedant, iki šios dienos tebeliudiju mažam ir dideliam, neskelbdamas nieko viršaus, o tik tai, ką skelbė įvyksiant pranašai ir Mozė,
22Lakini Mungu alinisaidia; na hivyo mpaka siku ya leo nimesimama imara nikitoa ushuhuda kwa wote, wakubwa na wadogo. Ninayosema ni yale ambayo manabii na Mose walisema yatatukia;
23būtent, kad Kristus kentės, jog pirmutinis prisikels iš numirusių ir paskelbs šviesą tautai ir pagonims”.
23yaani ilimpasa Kristo ateseke na kuwa wa kwanza kufufuka kutoka wafu, ili atangaze kwamba mwanga wa ukombozi unawaangazia sasa watu wote, Wayahudi na pia watu wa mataifa mengine."
24Jam tai kalbant, Festas garsiai sušuko: “Pauliau, tu iš galvos kraustaisi! Iš didelio rašto išėjai iš krašto”.
24Paulo alipofika hapa katika kujitetea kwake, Festo alisema kwa sauti kubwa, "Paulo! Una wazimu! Kusoma kwako kwingi kunakutia wazimu!"
25Paulius atsiliepė: “Ne, nesikraustau iš galvos, prakilnusis Festai, bet skelbiu tiesos ir sveiko proto žodžius.
25Lakini Paulo akasema, "Sina wazimu mheshimiwa Festo: Ninachosema ni ukweli mtupu.
26Šiuos dalykus žino karalius, kuriam taip atvirai kalbu. Esu tikras, kad iš viso to jam nieko nėra nežinomo, nes šitai dėjosi ne kur nors užkampyje.
26Wewe Mfalme unayafahamu mambo haya, kwa hiyo ninaweza kuongea bila uoga mbele yako. Sina mashaka kwamba matukio hayo yanajulikana kwako maana jambo hili halikutendeka mafichoni.
27Karaliau Agripa, ar tiki pranašais? Žinau, kad tiki”.
27Mfalme Agripa, je, una imani na manabii? Najua kwamba unaamini."
28Agripa atsakė: “Ko gero įtikinsi mane krikščionimi tapti...”
28Agripa akamjibu Paulo, "Kidogo tu utanifanya Mkristo!"
29Paulius tarė: “Meldžiu Dievą, kad ar per trumpą, ar per ilgą laiką ne tik tu, bet ir visi, šiandien girdėję mane kalbant, taptų tokie, kaip aš, tik be šitų pančių!”
29Paulo akamjibu, "Namwomba Mungu kwamba, kwa muda mfupi au mrefu, si wewe tu bali wote wanaonisikia leo wapate kuwa kama nilivyo mimi, lakini bila hii minyororo."
30Jam tai pasakius, pakilo karalius, valdytojas, Berenikė ir visi sėdėję su jais.
30Hapo mfalme Agripa, mkuu wa mkoa, Bernike na wale wote waliokuwa pamoja nao, walisimama.
31Išeidami jie tarpusavyje kalbėjosi: “Šitas žmogus nepadarė nieko baustino mirtimi ar kalėjimu”.
31Walipokwisha ondoka, waliambiana, "Mtu huyu hakufanya chochote kinachostahili adhabu ya kifo au kifungo."
32Agripa Festui pareiškė: “Būtų galima paleisti šitą žmogų, jeigu jis nebūtų šaukęsis ciesoriaus”.
32Naye Agripa akamwambia Festo, "Mtu huyu angeweza kufunguliwa kama asingalikuwa amekata rufani kwa Kaisari."