1Taigi dabar nebėra pasmerkimo tiems, kurie yra Kristuje Jėzuje, kurie gyvena ne pagal kūną, bet pagal Dvasią.
1Kwa hiyo, sasa hakuna hukumu kwa wale ambao katika maisha yao wameungana na Kristo.
2Nes gyvenimo Kristuje Jėzuje Dvasios įstatymas išlaisvino mane iš nuodėmės ir mirties įstatymo.
2Maana, sheria ya Roho iletayo uzima kwa kuungana na Kristo Yesu imenikomboa kutoka katika sheria ya dhambi na kifo.
3Ko įstatymas nepajėgė, būdamas silpnas dėl kūno, tai įvykdė Dievas. Jis atsiuntė savo Sūnų nuodėmingo kūno pavidalu kaip auką už nuodėmę ir pasmerkė nuodėmę kūne,
3Mungu ametekeleza jambo lile ambalo Sheria haikuweza kutekeleza kwa sababu ya udhaifu w binadamu. Mungu alimtuma Mwanae akiwa mwenye mwili sawa na miili yetu sisi wenye dhambi, ili aikabili dhambi, na kwa mwili huo akaiangamiza dhambi.
4kad įstatymo teisumas išsipildytų mumyse, gyvenančiuose ne pagal kūną, bet pagal Dvasią.
4Mungu alifanya hivyo kusudi matakwa ya haki ya Sheria yatekelezwe kikamilifu ndani yetu sisi ambao tunaishi, si kwa nguvu za kibinadamu, bali kwa nguvu ya Roho.
5Kurie gyvena pagal kūną, tie mąsto kūniškai, o kurie gyvena pagal Dvasiądvasiškai.
5Maana, wale wanaoishi kufuatana na matakwa ya mwili, hutawaliwa na fikira za mwili. Lakini wale wanaoishi kufuatana na matakwa ya Roho Mtakatifu, hutawaliwa na fikira za Roho.
6Kūniškas mąstymastai mirtis, o dvasiškasgyvenimas ir ramybė.
6Fikira za mwili huleta kifo; fikira za Roho huleta uzima na amani.
7Kūniškas mąstymas priešiškas Dievui; jis nepaklūsta Dievo įstatymui ir net negali paklusti.
7Maana, mwenye kutawaliwa na fikira za mwili ni adui wa Mungu; haitii sheria ya Mungu, wala hawezi kuitii.
8Ir todėl gyvenantys pagal kūną negali patikti Dievui.
8Watu wanaotii matakwa ya mwili hawawezi kumpendeza Mungu.
9Tačiau jūs negyvenate pagal kūną, bet pagal Dvasią, jei tik Dievo Dvasia gyvena jumyse. O kas neturi Kristaus Dvasios, tas nėra Jo.
9Lakini ninyi hamuishi kufuatana na matakwa ya mwili, bali kufuatana na matakwa ya Roho, ikiwa Roho wa Mungu anaishi ndani yenu. Yeyote asiye na Roho wa Kristo, huyo si wake Kristo.
10Jeigu Kristus yra jumyse, tai kūnas yra miręs dėl nuodėmės, bet dvasiagyva dėl teisumo.
10Lakini kama Kristo yumo ndani yenu, ingawa miili yenu itakufa kwa sababu ya dhambi, kwenu Roho ndiye uhai kwa sababu mmekubaliwa kuwa waadilifu.
11Jei jumyse gyvena Dvasia To, kuris Jėzų prikėlė iš numirusių, tai Jisprikėlęs iš numirusių Kristųatgaivins ir jūsų mirtingus kūnus savo Dvasia, gyvenančia jumyse.
11Ikiwa Roho wa Mungu aliyemfufua Kristo kutoka wafu anaishi ndani yenu, basi huyo aliyemfufua Kristo kutoka wafu ataipa uzima miili yenu yenye hali ya kufa; atafanya hivyo kwa njia ya Roho wake akaaye ndani yenu.
12Taigi, broliai, mes nesame skolingi kūnui, kad gyventume pagal kūną.
12Hivyo basi, ndugu zangu, tunalo jukumu, lakini si la kuishi kufuatana na maumbile ya kibinadamu.
13Jei jūs gyvenate pagal kūną mirsite. Bet jei dvasia marinate kūniškus darbusgyvensite.
13Kwa maana, kama mkiishi kufuatana na matakwa ya maumbile ya kibinadamu, hakika mtakufa. Lakini, kama kwa njia ya Roho mnayaua matendo yenu maovu, basi, mtaishi.
14Visi, vedami Dievo Dvasios, yra Dievo vaikai.
14Wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu ni watoto wa Mungu.
15Jūs gi gavote ne vergystės dvasią, kad vėl bijotumėte, bet gavote įsūnystės Dvasią, kuria šaukiame: “Aba, Tėve!”
15Kwa maana, Roho mliyempokea si Roho mwenye kuwafanya ninyi watumwa na kuwatia tena hofu; sivyo, bali mmempokea Roho mwenye kuwafanya ninyi watoto wa Mungu, na kwa nguvu ya huyo Roho, sisi tunaweza kumwita Mungu, "Aba," yaani "Baba!"
16Pati Dvasia liudija mūsų dvasiai, kad esame Dievo vaikai.
16Naye Roho mwenyewe anajiunga na roho zetu na kuthibitisha kwamba sisi ni watoto wa Mungu.
17O jei esame vaikai, tai ir paveldėtojai. Dievo paveldėtojai ir Kristaus bendrapaveldėtojai, jeigu tik su Juo kenčiame, kad su Juo būtume pašlovinti.
17Basi, kwa vile sisi ni watoto wa Mungu, tutapokea baraka zote Mungu alizowawekea watu wake, na tutashiriki urithi huo pamoja na Kristo; maana, tukiyashiriki mateso yake Kristo, tutaushiriki pia utukufu wake.
18Aš manau, jog šio laiko kentėjimai nieko nereiškia, lyginant juos su būsimąja šlove, kuri mumyse bus apreikšta.
18Naona kuwa mateso ya wakati huu wa sasa si kitu kamwe kama tukiyafananisha na ule utukufu utakaodhihirishwa kwetu.
19Kūrinija su ilgesiu laukia, kada bus apreikšti Dievo sūnūs.
19Viumbe vyote vinatazamia kwa hamu Mungu awadhihirishe watoto wake.
20Mat kūrinija buvo pajungta tuštybei,ne savo noru, bet pavergėjo valia,su viltimi,
20Kwa maana, viumbe viliwekwa katika hali ya kutojiweza kabisa, si kwa hiari yao, ila vilifanywa hivyo kwa mapenzi ya Mungu. Hata hivyo yapo matumaini,
21kad ir pati kūrinija bus išlaisvinta iš suirimo vergijos ir įgis šlovingą Dievo vaikų laisvę.
21maana hivyo viumbe navyo vitaokolewa kutoka katika utumwa wa uharibifu, vishiriki uhuru mtukufu wa watoto wa Mungu.
22Juk mes žinome, kad visa kūrinija iki šiol dejuoja ir tebėra gimdymo skausmuose.
22Kwa maana tunajua kwamba mpaka hivi sasa, viumbe vyote vinalia kwa maumivu kama ya kujifungua mtoto.
23Ir ne tik ji, bet ir mes patys, turintys pirmuosius Dvasios vaisius,ir mes dejuojame, kantriai laukdami įsūnijimo, mūsų kūno atpirkimo.
23Wala si hivyo viumbe peke yake, bali hata sisi tulio na huyo Roho, aliye wa kwanza wa zawadi za Mungu; sisi pia tunalalamika ndani yetu, tukitazamia kufanywa watoto wa Mungu, nazo nafsi zenu zikombolewe.
24Šia viltimi mes esame išgelbėti, bet regima viltis nėra viltis. Jeigu kas mato, tai kam jam viltis?
24Maana kwa matumaini hayo sisi tumekombolewa; lakini tumaini halina maana ikiwa tunakiona kile tunachotumainia. Maana ni nani anayetumaini kile ambacho tayari anakiona?
25Bet jei viliamės to, ko nematome, tada laukiame ištvermingai.
25Kama tunakitumaini kile ambacho hatujakiona bado, basi, tunakingojea kwa uvumilivu.
26Taip pat ir Dvasia padeda mūsų silpnumui. Nes mes nežinome, ko turėtume melsti, bet pati Dvasia užtaria mus neišsakomom dejonėm.
26Hali kadhalika, naye Roho anatusaidia katika udhaifu wetu. Maana hatujui inavyotupasa kuomba; lakini Roho mwenyewe anatuombea kwa Mungu kwa mlio wa huzuni usioelezeka.
27Širdžių Tyrėjas žino Dvasios mintis, nes Ji užtaria šventuosius pagal Dievo valią.
27Naye Mungu aonaye mpaka ndani ya mioyo ya watu, anajua fikira ya huyo Roho; kwani huyo Roho huwaombea watu wa Mungu kufuatana na mapenzi ya Mungu.
28Be to, mes žinome, kad mylintiems Dievą viskas išeina į gera, būtent Jo tikslu pašauktiesiems.
28Tunajua kwamba, katika mambo yote, Mungu hufanya kazi na kuifanikisha pamoja na wote wampendao, yaani wale aliowaita kufuatana na kusudi lake.
29O kuriuos Jis iš anksto numatė, tuos iš anksto ir paskyrė tapti panašius į Jo Sūnaus atvaizdą, kad šis būtų pirmagimis tarp daugelio brolių.
29Maana hao aliowachagua tangu mwanzo, ndio aliowateua wapate kufanana na Mwanae, ili Mwana awe wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi.
30O kuriuos Jis iš anksto paskyrė, tuos ir pašaukė; kuriuos pašaukė, tuos ir išteisino; kuriuos išteisino, tuos ir pašlovino.
30Basi, Mungu aliwaita wale aliokuwa amewateua; na hao aliowaita aliwakubali kuwa waadilifu; na hao aliowakubali kuwa waadilifu aliwashirikisha pia utukufu wake.
31Tai ką dėl viso šito pasakysime? Jei Dievas už mus, tai kas gi prieš mus?!
31Kutokana na hayo, tuseme nini zaidi? Ikiwa Mungu yuko upande wetu, nani awezaye kutupinga?
32Tas, kuris nepagailėjo savo Sūnaus, bet atidavė Jį už mus visus,kaipgi Jis ir visko nedovanotų kartu su Juo?
32Mungu hakumhurumia hata mwanae wa pekee, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote. Ikiwa amefanya hivyo, je, hatatujalia pia mema yote?
33Kas kaltins Dievo išrinktuosius? Juk Dievas išteisina!
33Ni nani atakayewashtaki wateule wa Mungu? Mungu mwenyewe huwaondolea hatia!
34Kas pasmerks? Kristus mirė, bet buvo prikeltas ir yra Dievo dešinėje, ir užtaria mus.
34Ni nani atakayewahukumu? Hakuna! Maana Kristo ndiye aliyekufa, tena alifufuka kutoka wafu na anakaa upande wa kulia wa Mungu. Yeye anatuombea!
35Kas gi mus atskirs nuo Kristaus meilės? Ar sielvartas? ar nelaimė? ar persekiojimas? ar badas? ar nuogumas? ar pavojus? ar kalavijas?
35Ni nani awezaye kututenga na mapendo ya Kristo? Je, ni taabu, au dhiki, au mateso, au njaa, au ukosefu wa nguo, au hatari, au kuuawa?
36Parašyta: “Dėl Tavęs mes žudomi ištisą dieną, laikomi avimis skerdimui”.
36Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Kwa ajili yako, twakikabili kifo kutwa kucha: tunatendewa kama kondoo wa kuchinjwa."
37Tačiau visuose šiuose dalykuose mes esame daugiau negu nugalėtojai per Tą, kuris mus pamilo.
37Lakini, katika mambo haya yote, tumepata ushindi mkubwa kwa msaada wake yeye aliyetupenda.
38Ir aš įsitikinęs, kad nei mirtis, nei gyvenimas, nei angelai, nei kunigaikštystės, nei galybės, nei dabartis, nei ateitis,
38Maana ninajua hakika kwamba hakuna kitu kiwezacho kututenganisha na upendo wake: wala kifo, wala uhai; wala malaika, au nguvu nyingine za mbinguni; wala yanayotokea sasa, wala yatakayotokea baadaye; wala mamlaka;
39nei aukštumos, nei gelmės, nei jokie kiti kūriniai negalės mūsų atskirti nuo Dievo meilės, kuri yra Kristuje Jėzuje, mūsų Viešpatyje.
39Wala ulimwengu wa juu, wala wa chini kabisa. Hakuna kiumbe chochote kitakachoweza kututenga na upendo wa Mungu kwetu kwa njia ya Kristo Yesu Bwana wetu.