Lithuanian

Swahili: New Testament

Romans

9

1Sakau tiesą Kristuje, nemeluoju,­tai liudija ir mano sąžinė Šventojoje Dvasioje,
1Nasema ukweli mtupu; nimeungana na Kristo nami sisemi uongo. Dhamiri yangu ikiongozwa na Roho Mtakatifu inanithibitishia jambo hili pia.
2kad man labai sunku ir nuolat liūdi mano širdis.
2Nataka kusema hivi: nina huzuni kubwa na maumivu yasiyopimika moyoni mwangu
3Man mieliau būtų pačiam būti prakeiktam ir atskirtam nuo Kristaus vietoj savo brolių, tautiečių pagal kūną,
3kwa ajili ya watu wangu, walio damu moja nami! Kama ingekuwa kwa faida yao, ningekuwa radhi kulaaniwa na kutengwa na Kristo.
4kurie yra izraelitai, turintys įsūnystę, šlovę, sandoras, įstatymą, tarnavimą Dievui ir pažadus.
4Hao ndio watu wa Israeli ambao Mungu aliwateua wawe watoto wake, akawashirikisha utukufu wake; aliagana nao, akawapa Sheria yake, imani ya kweli na ahadi zake.
5Iš jų­tėvai, ir iš jų kūno atžvilgiu yra kilęs Kristus­visiems viešpataujantis Dievas, palaimintas per amžius. Amen!
5Wao ni wajukuu wa mababu, naye Kristo, kadiri ya ubinadamu wake, ametoka katika ukoo wao. Mungu atawalaye juu ya yote, na atukuzwe milele! Amina.
6Netiesa, kad gali neišsipildyti Dievo žodis. Ne visi, kilę iš Izraelio, priklauso Izraeliui.
6Sisemi kwamba ahadi ya Mungu imebatilika; maana si watu wote wa Israeli ni wateule wa Mungu.
7Ir ne visi Abraomo palikuonys yra jo vaikai, bet kaip pasakyta: “Iš Izaoko tau bus pašaukti palikuonys”.
7Wala, si wazawa wote wa Abrahamu ni watoto wake wa kweli. Ila, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Wazao wake watatokana na Isaka."
8Tai reiškia, kad ne vaikai pagal kūną yra Dievo vaikai, bet vaikai pagal pažadą laikomi palikuonimis.
8Nido kusema, wale waliozaliwa kimaumbile ndio watoto wa Mungu, bali wale waliozaliwa kutokana na ahadi ya Mungu ndio watakaoitwa watoto wake.
9O pažado žodis toks: “Apie tą laiką Aš ateisiu, ir Sara turės sūnų”.
9Maana ahadi yenyewe ni hii: "Nitakujia wakati maalum, naye Sara atapata mtoto."
10Ir ne tik tai, bet taip pat ir Rebekai, pradėjusiai iš vieno, mūsų tėvo Izaoko
10Tena si hayo tu ila pia Rebeka naye alipata mapacha kwa baba mmoja, yaani Isaka, babu yetu.
11(dar jos dvyniams negimus ir jiems dar nepadarius nei gero, nei blogo,­kad Dievo nutarimas įvyktų pagal pasirinkimą, ne dėl darbų, bet šaukiančiojo valia),
11Lakini, ili Mungu aonekane kwamba anao uhuru wa kuchagua, hata kabla wale ndugu hawajazaliwa na kabla hawajaweza kupambanua jema na baya,
12buvo pasakyta: “Vyresnysis tarnaus jaunesniajam”,
12Rebeka aliambiwa kwamba yule mtoto wa kwanza atamtumikia yule wa nyuma. Hivyo uchaguzi wa Mungu unategemea jinsi anavyoita mwenyewe, na si matendo ya binadamu.
13kaip ir parašyta: “Jokūbą pamilau, o Ezavo nekenčiau”.
13Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Yakobo nilimpenda, lakini Esau nilimchukia."
14Ką gi pasakysime? Gal Dievas neteisingai daro? Jokiu būdu!
14Basi, tuseme nini? Je, Mungu amekosa haki? Hata kidogo!
15Jis Mozei kalba: “Aš pasigailėsiu to, kurio norėsiu pasigailėti, ir būsiu gailestingas tam, kuriam norėsiu gailestingas būti”.
15Maana alimwambia Mose: "Nitamhurumia mtu yeyote ninayetaka kumhurumia; nitamwonea huruma mtu yeyote ninayetaka."
16Taigi viskas priklauso ne nuo to, kuris trokšta ar kuris bėga, bet nuo gailestingojo Dievo.
16Kwa hiyo, yote hutegemea huruma ya Mungu, na si bidii au mapenzi ya mtu.
17Juk Raštas faraonui sako: “Aš iškėliau tave, kad parodyčiau savo jėgą tau ir kad mano vardas būtų skelbiamas visoje žemėje”.
17Maana Maandiko Matakatifu yasema hivi kwa Farao: "Nilikufanya mfalme ili kwa njia yako, uwezo wangu ujulikane, na jina langu litangazwe popote duniani."
18Vadinasi, ko Jis nori, to pasigaili, ir kurį nori, tą užkietina.
18Ni wazi, basi, kwamba Mungu humhurumia yeyote anayetaka kumhurumia, na akipenda kumfanya mtu awe mkaidi, hufanya hivyo.
19Gal man pasakysi: “O už ką tada Jis kaltina? Kas gi galėtų atsispirti Jo valiai?”
19Labda utaniuliza: "Ikiwa mambo yako hivyo, Mungu anawezaje kumlaumu mtu? Nani awezaye kuyapinga mapenzi yake?"
20Ak, žmogau! Kas gi, tiesą sakant, tu toks esi, kad drįsti prieštarauti Dievui? Argi dirbinys klausia meistro: “Kodėl mane tokį padarei?”
20Lakini, ewe binadamu, u nani hata uthubutu kumhoji Mungu? Je, chungu chaweza kumwuliza mfinyanzi wake: "Kwa nini umenitengeneza namna hii?"
21Ar puodžius neturi galios moliui, kad iš to paties minkalo pagamintų vieną indą garbingam panaudojimui, o kitą negarbingam?
21Mfinyanzi anaweza kuutumia udongo apendavyo na kufinyanga vyungu viwili kwa udongo uleule; kimoja kwa matumizi ya heshima, na kingine kwa matumizi ya kawaida.
22O jeigu Dievas, norėdamas parodyti savo rūstybę ir apreikšti savo jėgą, didžiu kantrumu pakentė pražūčiai nužiestus rūstybės indus,
22Hivyo ndivyo ilivyo kwa Mungu. Alitaka kuonyesha ghadhabu yake na kujulisha uwezo wake, Basi, alikuwa na saburi sana, akiwavumilia wale ambao walikuwa lengo la ghadhabu yake, ambao walistahili kuangamizwa.
23kad apreikštų ir savo šlovės turtus gailestingumo indams, kuriuos iš anksto paruošė šlovei,­
23Alitaka pia kudhihirisha wingi wa utukufu wake ambao alitumiminia sisi tulio lengo la huruma yake; sisi ambao alikwisha kututayarisha kuupokea utukufu wake.
24ir mus pašaukė ne tik iš žydų, bet ir iš pagonių?
24Maana sisi ndio hao aliowaita, si tu kutoka miongoni mwa Wayahudi bali pia kutoka kwa watu wa mataifa mengine.
25Jis kalba per Ozėją: “Ne savo tautą pavadinsiu savąja tauta ir nemylimą­mylima.
25Maana ndivyo asemavyo katika kitabu cha Hosea: "Wale waliokuwa Si watu wangu nitawaita: Watu wangu! Naye Sikupendi ataitwa: Mpenzi wangu!
26Ir toje vietoje, kur jiems buvo sakyta: ‘Jūs ne manoji tauta’, ten jie bus vadinami gyvojo Dievo vaikais”.
26Na pale walipoambiwa: Ninyi si wangu hapo wataitwa: Watoto wa Mungu hai."
27O Izaijas šaukia apie Izraelį: “Nors Izraelio vaikų skaičius būtų kaip jūros smiltys, tik likutis bus išgelbėtas.
27Naye nabii Isaya, kuhusu Israeli anapaaza sauti: "Hata kama watoto wa Israeli ni wengi kama mchanga wa pwani, ni wachache tu watakaookolewa;
28Nes Jis pabaigs darbą, greitai įvykdydamas teisumą, skubiai Viešpats atliks darbą žemėje”.
28maana, Bwana ataitekeleza upesi hukumu yake kamili juu ya ulimwengu wote."
29Izaijas nusakė iš anksto: “Jei kareivijų Viešpats nebūtų mums palikuonių palikęs, būtume tapę kaip Sodoma, būtume į Gomorą panašūs”.
29Ni kama Isaya alivyosema hapo awali: "Kama Bwana Mwenye Nguvu asingalituachia baadhi ya watoto wa Israeli, tungalikwisha kuwa kama Sodoma, tungalikwisha kuwa ma Gomora."
30Tai ką gi pasakysime? Kad pagonys, kurie neieškojo teisumo, gavo teisumą, būtent teisumą iš tikėjimo.
30Basi, tuseme nini? Ni hivi: watu wa mataifa ambao hawakutafuta kukubaliwa kuwa waadilifu, wamekubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya imani,
31O Izraelis, ieškojęs teisumo įstatyme, nepasiekė teisumo įstatymo.
31hali watu wa Israeli waliokuwa wakitafuta Sheria iletayo kukubaliwa kuwa waadilifu, hawakuipata.
32Kodėl? Todėl, kad ieškojo jo ne tikėjimu, bet įstatymo darbais. Jie užkliuvo už suklupimo akmens,
32Kwa nini? Kwa sababu walitegemea matendo yao badala ya kutegemea imani. Walijikwaa juu ya jiwe la kujikwaa
33kaip parašyta: “Štai dedu Sione suklupimo akmenį, papiktinimo uolą; bet kas Juo tiki, nebus sugėdintas”.
33kama yesemavyo Maandiko Matakatifu: "Tazama! Naweka huko Sioni jiwe likwazalo, mwamba utakaowafanya watu waanguke. Mtu atakayemwamini yeye aliye hilo jiwe, hataaibishwa!"