Lithuanian

Swahili: New Testament

Romans

10

1Broliai, mano širdies troškimas ir malda Dievui yra už Izraelį,­kad jie išsigelbėtų.
1Ndugu zangu, ninataka na kutazamia kwa moyo wangu wote hao wananchi wenzangu wakombolewe. Tena nawaombea kwa Mungu daima.
2Aš jiems liudiju, kad jie turi uolumo Dievui, tačiau be pažinimo.
2Maana naweza kuthibitisha kwa niaba yao kwamba wanayo bidii ya kumtafuta Mungu; lakini bidii hiyo haikujengwa juu ya ujuzi wa kweli.
3Nesuprasdami Dievo teisumo ir bandydami įtvirtinti savąjį teisumą, jie nepakluso Dievo teisumui.
3Maana hawakufahamu jinsi Mungu anavyowafanya watu wawe waadilifu, na wamejaribu kuanzisha mtindo wao wenyewe, na hivyo hawakuikubali njia hiyo ya Mungu ya kuwafanya wawe waadilifu.
4Nes įstatymo pabaiga­Kristus, išteisinimui kiekvieno, kuris tiki.
4Maana kwa kuja kwake Kristo, Sheria imefikia kikomo chake, ili kila mtu anayeamini akubaliwe kuwa mwadilifu.
5Mozė rašo apie teisumą iš įstatymo: “Jį vykdydamas žmogus juo gyvens”.
5Kuhusu kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa kuitii Sheria, Mose aliandika hivi: "Mtu yeyote anayetimiza matakwa ya Sheria ataishi."
6Bet teisumas iš tikėjimo kalba taip: “Nesakyk savo širdyje: ‘Kas įžengs į dangų?’­tai yra Kristaus atsivesti;
6Lakini, kuhusu kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa njia ya imani, yasemwa hivi: "Usiseme moyoni mwako: Nani atapanda mpaka mbinguni? (yaani, kumleta Kristo chini);
7arba: ‘Kas nusileis į bedugnę?’­ tai yra Kristaus iš numirusių susigrąžinti”.
7wala usiseme: Nani atashuka mpaka Kuzimu (yaani, kumleta Kristo kutoka kwa wafu)."
8Bet ką jis sako?­“Arti tavęs yra žodis­tavo burnoje ir tavo širdyje”,­tai yra mūsų skelbiamas tikėjimo žodis.
8Maandiko Matakatifu yesema hivi, "Ujumbe huo wa Mungu uko karibu nawe, uko kinywani mwako na moyoni mwako" nao ndio ile imani tunayoihubiri.
9Jeigu lūpomis išpažinsi Viešpatį Jėzų ir širdimi tikėsi, kad Dievas Jį prikėlė iš numirusių, būsi išgelbėtas.
9Kama ukikiri kwa kinywa chako kwamba Yesu ni Bwana na kuamini moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka wafu, utaokoka.
10Nes širdimi tikima, ir taip įgyjamas teisumas, o lūpomis išpažįstama, ir taip įgyjamas išgelbėjimas.
10Maana tunaamini kwa moyo na kukubaliwa kuwa waadilifu; na tunakiri kwa midomo yetu na kuokolewa.
11Raštas juk sako: “Kiekvienas, kuris Jį tiki, nebus sugėdintas”.
11Maandiko Matakatifu yasema: "Kila amwaminiye hatakuwa na sababu ya kuaibika."
12Nėra skirtumo tarp žydo ir graiko, nes tas pats Viešpats visiems, turtingas kiekvienam, kuris Jo šaukiasi,
12Jambo hili ni kwa wote, kwani hakuna tofauti kati ya Wayahudi na wasio Wayahudi; Bwana wa wote ni mmoja, naye ni mkarimu sana kwao wote wamwombao.
13juk “kiekvienas, kuris šaukiasi Viešpaties vardo, bus išgelbėtas”.
13Maana Maandiko Matakatifu yasema: "Kila mtu atakayeomba kwa jina la Bwana, ataokolewa."
14Kaip žmonės šauksis To, kurio neįtikėjo? Ir kaip jie įtikės Tą, apie kurį negirdėjo? Kaip išgirs be skelbėjo?
14Basi, watamwombaje yeye ambaye hawamwamini? Tena, watamwaminije kama hawajapata kusikia habari zake? Na watasikiaje habari zake kama hakuna mhubiri?
15Ir kaip jie skelbs, jei nebus pasiųsti? Kaip parašyta: “Kokios puikios kojos tų, kurie skelbia ramybės Evangeliją, kurie neša geras žinias!”
15Na watu watahubirije kama hawakutumwa? Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Ni jambo la kupendeza mno kuja kwa wale wanaohubiri Habari Njema!"
16Bet ne visi pakluso Evangelijai. Nes Izaijas sako: “Viešpatie, kas patikėjo mūsų skelbimu?”
16Lakini wote hawakuipokea hiyo Habari Njema. Maana Isaya alisema: "Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu?"
17Taigi tikėjimas­iš klausymo, klausymas­iš Dievo žodžio.
17Hivyo basi, imani inatokana na kuusikiliza ujumbe, na huo ujumbe unatokana na neno la Kristo.
18Bet aš klausiu: argi jie negirdėjo? Kaipgi ne! “Po visą žemę pasklido jų garsas, ir jų žodžiai­iki pasaulio pakraščių”.
18Lakini nauliza: je, hawakuusikia huo ujumbe? Naam, waliusikia; kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Sauti yao imeenea duniani kote; maneno yao yamefika mpaka kingo za ulimwengu."
19Klausiu toliau: ar Izraelis nežinojo? Bet Mozė pirmas sako: “Aš sukelsiu jums pavydą per netautą, sukelsiu pyktį per neišmanančią tautą”.
19Tena nauliza: je, yawezekana kwamba watu wa Israeli hawakufahamu? Mose mwenyewe ni kwa kwanza kujibu: "Nitawafanyeni mwaonee wivu watu ambao si taifa; nitawafanyeni muwe na hasira juu ya taifa la watu wapumbavu."
20Izaijas labai drąsiai sako: “Mane atrado tie, kurie manęs neieškojo, apsireiškiau tiems, kurie apie mane neklausinėjo”.
20Tena Isaya anathubutu hata kusema: "Wale ambao hawakunitafuta wamenipata; nimejionyesha kwao wasiouliza habari zangu."
21Bet Izraeliui sako: “Ištisą dieną Aš laikiau ištiesęs savo rankas į neklusnią ir prieštaraujančią tautą”.
21Lakini kuhusu Israeli anasema: "Mchana kutwa niliwanyoshea mikono yangu watu waasi na wasiotii."