1Tad aš klausiu: ar Dievas atstūmė savo tautą? Jokiu būdu! Juk ir aš izraelitas, iš Abraomo palikuonių, iš Benjamino giminės.
1Basi, nauliza: je, Mungu amewakataa watu wake? Hata kidogo! Mini binafsi ni Mwisraeli mzawa wa Abrahamu, wa kabila la Benyamini.
2Dievas neatstūmė savosios tautos, kurią iš anksto numatė. Ar nežinote, ką sako Raštas apie Eliją, kai šis skundžiasi Izraeliu:
2Mungu hakuwakataa watu wake aliowateua tangu mwanzo. Mnakumbuka yasemavyo Maandiko Matakatifu juu ya Eliya wakati alipomnung'unikia Mungu kuhusu Israeli:
3“Viešpatie, jie išžudė Tavo pranašus, išgriovė Tavo aukurus; aš vienas belikau, ir jie tyko mano gyvybės”.
3"Bwana, wamewaua manabii wako na kubomoa madhabahu yako. Ni mimi tu peke yangu niliyebaki, nao wanataka kuniua?"
4O kaip skamba Dievo atsakymas? “Aš pasilaikiau septynis tūkstančius vyrų, kurie nesulenkė kelių prieš Baalį”.
4Je, Mungu alimjibu nini? Alimwambia: "Nimejiwekea elfu saba ambao hawakumwabudu Baali."
5Ir dabartiniu metu yra malonės išrinktas likutis.
5Basi, ndivyo ilivyo pia wakati huu wa sasa: ipo idadi ya waliobaki ambao Mungu aliwateua kwa sababu ya neema yake.
6Ir jei malone, tai ne dėl darbų, nes tada malonė nebūtų malonė. Bet jeigu darbais, tai jau nebus malonė; kitaip darbas nebūtų darbas.
6Uteuzi wake unatokana na neema yake, na si kwa sababu ya matendo yao. Maana, kama uteuzi wake ungetegemea matendo ya watu, neema yake haingekuwa neema tena.
7Tai ką gi? Izraelis nepasiekė to, ko ieškojo. Pasiekė tiktai išrinktoji dalis. Kiti buvo apakinti,
7Sasa, je? Watu wa Israeli hawakukipata kile walichokuwa wanakitafuta; lakini wote walioteuliwa walikipata. Wengine walipumbazwa,
8kaip parašyta: “Dievas jiems siuntė snaudulio dvasią, kad akys neregėtų ir ausys negirdėtų iki šios dienos”.
8kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Mungu ameifanya mioyo yao kuwa mizito, na mpaka leo hii hawawezi kuona kwa macho yao wala kusikia kwa masikio yao."
9Ir Dovydas sako: “Jų stalas tepavirsta jiems spąstais, žabangais, suklupimo akmeniu ir atpildu.
9Naye Daudi anasema: "Karamu zao na ziwe mtego wa kuwanasa, waanguke na kuadhibiwa.
10Tegul aptemsta jų akys, kad neregėtų, ir jų nugarą laikyk nuolat sulenktą”.
10Macho yao yatiwe giza wasiweze kuona. Migongo yao ipindike kwa taabu daima!"
11Tad aš klausiu: negi izraelitai taip suklupo, kad pargriūtų? Jokiu būdu! Tik per jų suklupimą pagonims atėjo išgelbėjimas, kad juos paimtų pavydas.
11Basi, nauliza: je, Wayahudi wamejikwaa hata wakaangamia kabisa? Hata kidogo! Kutokana na kosa lao ukombozi umewajia watu wa mataifa mengine, ili Wayahudi wapate kuwaonea wivu.
12Bet jeigu jų suklupimas yra pasauliui praturtinimas ir jų sumažėjimaspagonims praturtinimas, tai ką duos jų visuma?
12Kosa la Wayahudi limesababisha baraka nyingi kwa ulimwengu, na utovu wao kwa kiroho umeleta baraka nyingi kwa watu wa mataifa mengine. Basi, ni dhahiri zaidi kwamba utimilifu wao utasababisha baraka nyingi zaidi.
13Jums, pagonims, sakau: būdamas pagonių apaštalas, aš gerbiu savo tarnavimą:
13Basi, sasa nawaambieni ninyi watu wa mataifa mengine: Maadamu mimi nimekuwa mtume kwa watu wa mataifa mengine, ninajivunia huduma yangu,
14gal kaip nors man pavyks sukelti savo tautiečių pavydą ir bent kai kuriuos išgelbėti.
14nipate kuwafanya wananchi wenzangu wawaonee ninyi wivu, na hivyo nipate kuwaokoa baadhi yao.
15Jeigu jų atmetimas reiškia pasauliui sutaikinimą, tai ką gi reikštų jų priėmimas, jei ne gyvenimą iš numirusių?
15Maana ikiwa kukataliwa kwao kulisababisha ulimwengu upatanishwe na Mungu, itakuwaje wakati watakapokubaliwa na Mungu? Wafu watafufuka!
16Jei pirmieji vaisiai šventi, tai šventa ir visuma. Jei šaknis šventa, tai ir šakos.
16Ikiwa kipande cha kwanza cha mkate kimewekwa wakfu, mkate wote umewekwa wakfu; mizizi ya mti ikiwa mizuri, na matawi yake huwa mazuri pia.
17Jeigu kai kurios šakos buvo nulaužtos, o tulaukinis alyvmedisesi tarp jų įskiepytas ir tapęs šaknies bei alyvmedžio syvų dalininku,
17Naam, baadhi ya matawi ya mzeituni bustanini yalikatwa, na mahali pake tawi la mzeituni mwitu likapandikizwa. Ninyi watu wa mataifa mengine ndio hilo tawi la mzeituni mwitu; na sasa mnashiriki nguvu na utomvu wa mzeituni bustanini.
18tai nesididžiuok prieš anas šakas! O jeigu didžiuojiesi, tai žinok, kad ne tu išlaikai šaknį, bet šaknis tave.
18Basi, msiwadharau wale waliokatwa kama matawi! Na, hata kama kuna la kujivunia, kumbukeni kwamba si ninyi mnaoitegemeza mizizi, bali mizizi ndiyo inayowategemeza ninyi.
19Gal pasakysi: “Šakos nulaužtos tam, kad aš būčiau įskiepytas?”
19Lakini utasema: "Matawi yalikatwa kusudi mimi nipandikizwe mahali pake."
20Gerai! Jos nulaužtos dėl netikėjimo, o tu stovi tikėjimu. Nesididžiuok, bet bijok!
20Sawa! Yalikatwa kwa sababu ya kukosa imani, bali wewe unasimama kwa imani yako. Lakini usijivune; ila uwe na tahadhari.
21Jei Dievas nepagailėjo prigimtinių šakų, gali nepagailėti ir tavęs.
21Kwa maana, ikiwa Mungu hakuwahurumia Wayahudi ambao ni kama matawi ya asili, je, unadhani atakuhurumia wewe?
22Taigi matai Dievo gerumą ir griežtumą: nupuolusiemsgriežtumas, o taugerumas, jei pasiliksi Jo gerume, kitaipir tu būsi iškirstas!
22Kumbuka, basi, jinsi Mungu alivyo mwema na mkali. Yeye ni mkali kwa wale walioanguka, na ni mwema kwako wewe ikiwa utaendelea katika wema wake; la sivyo, nawe pia utakatwa.
23Bet ir anie, jei nepasiliks netikėjime, bus priskiepyti, nes Dievas turi galią ir vėl juos priskiepyti.
23Nao Wayahudi, hali kadhalika; wakiacha utovu wao wa imani, watapandikizwa tena. Maana Mungu anao uwezo wa kuwapandikiza tena.
24Tad jeigu buvai iškirstas iš prigimtojo laukinio alyvmedžio ir prieš prigimtį įskiepytas tauriajame alyvmedyje, tai juo labiau jie tikrosios šakosbus priskiepyti savajame alyvmedyje.
24Ninyi watu wa mataifa mengine, kwa asili ni kama tawi la mzeituni mwitu, lakini mmeondolewa huko, mkapandikizwa katika mzeituni bustanini mahali ambapo kwa asili si penu. Lakini, Wayahudi kwa asili ni kama mzeituni bustanini, na itakuwa jambo rahisi zaidi kwao kupandikizwa tena katika mti huohuo wao.
25Aš nenoriu, broliai, palikti jus nežinioje dėl šios paslapties,kad jūs per aukštai apie save nemanytumėte: dalis Izraelio užkietėjo, kol įeis pagonių visuma,
25Ndugu zangu, napenda mjue ukweli huu uliofichika msije mkajiona wenye akili sana. Ukaidi wa Wayahudi ulikuwa ni wa muda tu, mpaka watu wa mataifa mengine watakapokuwa wamemfikia Mungu.
26o tada bus išgelbėtas visas Izraelis, kaip parašyta: “Iš Siono ateis Gelbėtojas ir nukreips bedievystes nuo Jokūbo.
26Hapo ndipo taifa lote la Israeli litakapookolewa, kama yesemavyo Maandiko Matakatifu: "Mkombozi atakuja kutoka Sioni, atauondoa uovu wa Yakobo.
27Tokia bus jiems mano sandora, kai nuimsiu jų nuodėmes”.
27Hili ndilo agano nitakalofanya nao wakati nitakapoziondoa dhambi zao."
28Žiūrint Evangelijos, jie yra Dievo priešai jūsų naudai; bet pagal išrinkimą jie numylėtiniai dėl savųjų tėvų.
28Kwa sababu wanaikataa Habari Njema, Wayahudi wamekuwa adui wa Mungu, lakini kwa faida yenu nyinyi watu wa mataifa. Lakini, kwa kuwa waliteuliwa, bado ni rafiki wa Mungu kwa sababu ya baba zao.
29Juk Dievo dovanos ir pašaukimasneatšaukiami.
29Maana Mungu akisha wapa watu zawadi zake na kuwateua, hajuti kwamba amefanya hivyo.
30Kaip jūs kadaise netikėjote Dievu, o dabar per jų netikėjimą patyrėte gailestingumą,
30Hapo awali ninyi mlikuwa mmemwasi Mungu, lakini sasa mmepata huruma yake kutokana na kuasi kwao.
31taip ir jie dabar netiki, kad dėl jums suteikto pasigailėjimo ir jie susilauktų gailestingumo.
31Hali kadhalika, kutokana na huruma mliyojaliwa ninyi, Wayahudi wanamwasi Mungu sasa ili nao pia wapokee sasa huruma ya Mungu.
32Dievas juos visus uždarė netikėjime, kad visų pasigailėtų.
32Maana Mungu amewafunga watu wote katika uasi wao ili wapate kuwahurumia wote.
33O Dievo turtų, išminties ir pažinimo gelme! Kokie neištiriami Jo teismai ir nesusekami Jo keliai!
33Utajiri, hekima na elimu ya Mungu ni kuu mno! Huruma zake hazichunguziki, na njia zake hazieleweki! Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu:
34“Ir kas gi pažino Viešpaties mintį? Ir kas buvo Jo patarėju?”
34"Nani aliyepata kuyajua mawazo ya Bwana? Nani awezaye kuwa mshauri wake?
35“Arba kas Jam yra davęs pirmas, kad jam būtų atmokėta?”
35Au, nani aliyempa yeye kitu kwanza hata aweze kulipwa tena kitu hicho?"
36Iš Jo, per Jį ir Jam yra visa. Jam šlovė per amžius! Amen.
36Kwa maana vitu vyote vyatoka kwake, vyote vipo kwa uwezo wake na kwa ajili yake. Utukufu na uwe kwake hata milele! Amina.