Lithuanian

Swahili: New Testament

Romans

12

1gailestingumu aš prašau jus, broliai, aukoti savo kūnus kaip gyvą, šventą, Dievui patinkančią auką,­tai jūsų sąmoningas tarnavimas.
1Kwa hiyo, ndugu zangu, maadam Mungu ni mwenye huruma nyingi, nawasihi kwa moyo wote: jitoleeni nafsi zenu kwa Mungu kama tambiko iliyo hai, takatifu na yenye kupendeza. Hii ndiyo njia yenu halisi ya kumwabudu.
2Ir neprisitaikykite prie šio pasaulio, bet pasikeiskite, atnaujindami savo protą, kad galėtumėte ištirti, kas yra gera, priimtina ir tobula Dievo valia.
2Msiige mitindo ya ulimwengu huu, bali Mungu afanye mabadiliko ndani yenu kwa kuzigeuza fikira zenu. Hapo ndipo mtakapoweza kuyajua mapenzi ya Mungu, kutambua jambo lililo jema, linalompendeza na kamilifu.
3Iš man suteiktos malonės raginu kiekvieną iš jūsų nemanyti apie save geriau negu dera manyti, bet manyti apie save blaiviai, pagal kiekvienam Dievo duotąjį tikėjimo saiką.
3Kutokana na neema aliyonijalia Mungu, nawaambieni ninyi nyote: msijione kuwa ni kitu zaidi kuliko mnavyopaswa kuwa. Fikira zenu na ziwe na kiasi kufuatana na kipimo cha imani Mungu aliyomgawia kila mmoja.
4Juk kaip viename kūne turime daug narių, bet ne visi nariai atlieka tą patį uždavinį,
4Mwili una viungo vingi, kila kimoja na kazi yake.
5taip ir mūsų daugybė yra vienas kūnas Kristuje, o pavieniui­vieni kitų nariai.
5Hali kadhalika ingawa sisi ni wengi, tu mwili mmoja kwa kuungana na Kristo, na kila mmoja ni kiungo cha mwenzake.
6Pagal mums suteiktą malonę turime įvairių dovanų. Jei kas turi pranašavimą, tepranašauja pagal tikėjimo saiką;
6Basi, tunavyo vipaji mbalimbali kufuatana na neema tuliyopewa. Mwenye kipaji cha unabii na akitumie kadiri ya imani yake.
7jei kas turi tarnavimą­tetarnauja; kas mokymą­temoko;
7Mwenye kipaji cha utumishi na atumikie. mwenye kipaji cha kufundisha na afundishe.
8kas skatinimą­teskatina; kas duoda­tedaro tai iš atviros širdies; kas vadovauja­tevadovauja uoliai; kas daro gailestingumo darbus­tedaro tai su džiaugsmu.
8Mwenye kipaji cha kuwafariji wengine na afanye hivyo. Mwenye kumgawia mwenzake alicho nacho na afanye hivyo kwa ukarimu. Msimamizi na asimamie kwa bidii; naye mwenye kutenda jambo la huruma na afanye hivyo kwa furaha.
9Meilė tebūna neveidmainiška. Venkite pikto, laikykitės gero.
9Mapendo yenu na yawe bila unafiki wowote. Chukieni jambo lolote ovu, zingatieni jema.
10Švelniai mylėkite vienas kitą broliška meile; pagarbiai vertinkite kitus aukščiau nei save.
10Pendaneni kidugu; kila mmoja amfikirie mwenzake kwanza kwa heshima.
11Uolumu nebūkite tingūs; būkite liepsnojančios dvasios, tarnaukite Viešpačiui.
11Msilegee katika bidii, muwe wachangamfu rohoni katika kumtumikia Bwana.
12Džiaukitės viltimi, būkite kantrūs išmėginimuose, nepaliaujamai melskitės.
12Tumaini lenu liwaweke daima wenye furaha; muwe na saburi katika shida na kusali daima.
13Dalinkitės šventųjų poreikiais, puoselėkite svetingumą.
13Wasaidieni watu wa Mungu katika mahitaji yao; wapokeeni wageni kwa ukarimu.
14Laiminkite savo persekiotojus, laiminkite, o ne keikite.
14Watakieni baraka wote wanaowadhulumu ninyi; naam, watakieni baraka na wala msiwalaani.
15Džiaukitės su besidžiaugiančiais, verkite su verkiančiais.
15Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
16Būkite vienminčiai tarpusavyje. Negalvokite apie didelius dalykus, bet sekite nuolankiaisiais. Nebūkite išmintingi savo akyse.
16Muwe na wema uleule kwa kila mtu. Msijitakie makuu, bali jishugulisheni na watu wadogo. Msijione kuwa wenye hekima sana.
17Niekam neatmokėkite piktu už pikta, rūpinkitės tuo, kas dora visų žmonių akyse.
17Msilipe ovu kwa ovu. Zingatieni mambo mema mbele ya wote.
18Kiek įmanoma ir kiek nuo jūsų priklauso, gyvenkite taikingai su visais žmonėmis.
18Kadiri inavyowezekana kwa upande wenu, muwe na amani na watu wote.
19Nekeršykite patys, mylimieji, bet palikite tai rūstybei, nes parašyta: “Mano kerštas, Aš atmokėsiu”,­sako Viešpats.
19Wapenzi wangu, msilipize kisasi, bali mwachieni Mungu jambo hilo; maana Maandiko Matakatifu yasema: "Kulipiza kisasi ni shauri langu; mimi nitalipiza asema Bwana."
20Todėl, jei tavo priešininkas alkanas, pavalgydink jį, jei trokšta, pagirdyk jį. Taip darydamas, tu sukrausi žarijas ant jo galvos.
20Tena, Maandiko yasema: "Adui yako akiwa na njaa, mpe chakula; akiwa na kiu, mpe kinywaji. Maana kwa kufanya hivyo utamfanya apate aibu kali kama makaa ya moto juu ya kichwa chake."
21Nesiduok pikto nugalimas, bet nugalėk pikta gerumu.
21Usikubali kushindwa na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.