1Paulius, Dievo tarnas ir Jėzaus Kristaus apaštalas, pagal Dievo išrinktųjų tikėjimą bei dievotumą atitinkantį tiesos pažinimą
1Mimi Paulo, mtumishi wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo naandika. Mimi nimechaguliwa kuijenga imani ya wateule wa Mungu na kuwaongoza waufahamu ukweli wa dini yetu,
2su viltimi amžinojo gyvenimo, kurį nemeluojantis Dievas pažadėjo prieš amžinuosius laikus,
2ambayo msingi wake ni tumaini la kupata uzima wa milele. Mungu ambaye hasemi uongo, alituahidia uzima huo kabla ya mwanzo wa nyakati,
3o nustatytam metui atėjus, apreiškė savo žodį skelbimu, kuris man patikėtas Dievo, mūsų Gelbėtojo, įsakymu,
3na wakati ufaao ulipowadia, akaudhihirisha katika ujumbe wake. Mimi nilikabidhiwa ujumbe huo nuutangaze kufuatana na amri ya Mungu, Mwokozi wetu.
4Titui, tikram sūnui bendrame tikėjime: malonė, gailestingumas ir ramybė nuo Dievo Tėvo ir mūsų Gelbėtojo Viešpaties Jėzaus Kristaus!
4Ninakuandikia wewe Tito, mwanangu wa kweli katika imani tunayoshiriki. Nakutakia neema na amani kutoka kwa Mungu Baba, na kutoka kwa Kristo Yesu, Mkombozi wetu.
5Aš tam palikau tave Kretoje, kad sutvarkytum, kas buvo likę nesutvarkyta, ir paskirtum kiekviename mieste vyresniuosius, kaip esu įsakęs:
5Nilikuacha Krete ili urekebishe yale mambo ambayo hayakuwa yamekamilika bado, na kuwateua wazee wa kanisa katika kila mji. Kumbuka maagizo yangu:
6jei kas yra be priekaištų, vienos žmonos vyras, turįs ištikimus vaikus, kurie nekaltinami palaidu gyvenimu ar neklusnumu.
6mzee wa kanisa anapaswa kuwa mtu asiye na hatia; aliye na mke mmoja tu, na watoto wake wanapaswa kuwa waumini, wasiojulikana kuwa wakorofi au wakaidi.
7Nes vyskupas, kaip Dievo ūkvedys, turi būti be priekaištų: ne savavaliautojas, ne karštakošis, ne girtuoklis, ne kivirčius, ne geidžiantis nešvaraus pelno,
7Maana kwa vile kiongozi wa kanisa ni mkurugenzi wa kazi ya Mungu, anapaswa kuwa mtu asiye na hatia. Asiwe mwenye majivuno, mwepesi wa hasira, mlevi, mkorofi au mchoyo.
8bet svetingas, trokštantis gero, blaiviai mąstantis, teisingas, šventas, susivaldantis,
8Anapaswa kuwa mkarimu na anayependa mambo mema. Anapaswa kuwa mtu mtaratibu, mwadilifu, mtakatifu na mwenye nidhamu.
9tvirtai besilaikantis patikimo žodžio kaip buvo išmokytas, kad sveiku mokymu sugebėtų ir paraginti, ir įtikinti prieštaraujančius.
9Ni lazima ashike kikamilifu ujumbe ule wa kuaminika kama unavyofundishwa. Ndivyo atakavyoweza kuwatia wengine moyo kwa mafundisho ya kweli na kuyafichua makosa ya wale wanaoyapinga mafundisho hayo.
10Nes daug yra neklusnių, tuščiakalbių ir apgavikų, ypač iš apipjaustytųjų.
10Maana, wako watu wengi, hasa wale walioongoka kutoka dini ya Kiyahudi, ambao ni wakaidi, wanaowapotosha wengine kwa upumbavu wao.
11Juos reikia užčiaupti, nes jie apverčia aukštyn kojomis ištisas šeimynas, mokydami, kas nedera, dėl nesąžiningo pelno.
11Lazima kukomesha maneno yao, kwani wanavuruga jumuiya nzima kwa kufundisha mambo ambayo hawapaswi kufundisha; wanafanya hivyo kwa nia mbaya ya kupata faida ya fedha.
12Vienas iš jų, jų pačių pranašas, yra pasakęs: “Kretiečiai visada melagiai, pikti žvėrys, tingūs pilvai”.
12Hata mmoja wa manabii wao, ambaye naye pia ni Mkrete, alisema: "Wakrete, husema uongo daima; ni kama wanyama wabaya, walafi na wavivu!"
13Šis liudijimas teisingas. Todėl sudrausk juos griežtai, kad būtų sveiki tikėjimu,
13Naye alitoboa ukweli kwa sababu hiyo, unapaswa kuwakaripia vikali, ili wawe na imani kamilifu.
14nekreipdami dėmesio į žydų pasakas ir į žmonių priesakus, nukreipiančius nuo tiesos.
14Wasiendelee kushikilia hadithi tupu za Kiyahudi na maagizo ya kibinadamu yanayozuka kwa watu walioukataa ukweli.
15Tyriems viskas tyra, o susitepusiems ir netikintiems nieko nėra tyro, net ir jų protas bei sąžinė suteršti.
15Kila kitu ni safi kwa watu walio safi; lakini hakuna chochote kilicho safi kwa wale waliochafuliwa na wasioamini, maana dhamiri na akili zao zimechafuliwa.
16Jie skelbiasi pažįstą Dievą, o darbais Jį neigia; jie pasibjaurėtini, nepaklusnūs, netikę jokiam geram darbui.
16Watu kama hao hujidai kwamba wanamjua Mungu, lakini kwa matendo yao humkana. Ni watu wa kuchukiza mno na wakaidi, hawafai kwa jambo lolote jema.