Lithuanian

Swahili: New Testament

2 Timothy

4

1Aš primygtinai prašau prieš Dievą ir Viešpatį Jėzų Kristų, kuris teis gyvuosius ir mirusiuosius, Jam ir Jo karalystei atėjus:
1Nakuamuru mbele ya Mungu, na mbele ya Kristo Yesu atakayewahukumu watu walio hai na wafu, na kwa sababu anakuja kutawala akiwa Mfalme:
2skelbk žodį, veik laiku ir nelaiku, bark, drausk, ragink su didžia ištverme ir pamokymu.
2hubiri huo ujumbe, sisitiza kuutangaza (iwe ni wakati wa kufaa au wakati usiofaa), karipia, onya na himiza watu ukiwafundisha kwa uvumilivu wote.
3Nes ateis laikas, kai žmonės nebepakęs sveiko mokslo, bet, pasidavę savo įgeidžiams, pasikvies sau mokytojus, kad tie dūzgentų ausyse;
3Utakuja wakati ambapo watu hawatasikiliza mafundisho ya kweli, ila watafuata tamaa zao wenyewe na kujikusanyia walimu tele watakaowaambia mambo yale tu ambayo masikio yao yako tayari kusikia.
4jie nukreips ausis nuo tiesos ir atvers pasakoms.
4Watakataa kuusikia ukweli, watageukia hadithi za uongo.
5Bet tu būk visame kame apdairus, iškęsk sunkumus, dirbk evangelisto darbą, atlik savo tarnavimą.
5Wewe, lakini, uwe macho katika kila hali; vumilia mateso, fanya kazi ya mhubiri wa Habari Njema, timiza kikamilifu utumishi wako.
6Nes aš jau atnašaujamas, ir mano iškeliavimo laikas jau čia pat.
6Kwa upande wangu mimi, niko karibu kabisa kutolewa dhabihu na wakati wa kufariki kwangu umefika.
7Aš kovojau gerą kovą, baigiau bėgimą, išlaikiau tikėjimą.
7Nimefanya bidii katika mashindano, nimemaliza safari yote na imani nimeitunza.
8Nuo šiol manęs laukia teisumo vainikas, kurį aną dieną man duos Viešpats, teisingasis Teisėjas,­ir ne tik man, bet ir visiems, kurie pamilo Jo pasirodymą.
8Na sasa imebakia tu kupewa tuzo la ushindi kwa maisha ya uadilifu, tuzo ambalo Bwana Hakimu wa haki, atanipa mimi Siku ile na wala si mimi tu, ila na wale wote wanaotazamia kwa upendo kutokea kwake.
9Pasistenk greitai atvykti pas mane,
9Fanya bidii kuja kwangu karibuni.
10nes Demas, pamilęs šį pasaulį, paliko mane ir iškeliavo į Tesaloniką, Krescentas­į Galatiją, Titas­į Dalmatiją.
10Dema ameupenda ulimwengu huu akaniacha na kwenda zake Thesalonike. Kreske amekwenda Galatia, na Tito amekwenda Dalmatia.
11Vienas Lukas tėra su manimi. Pasiimk ir atvesk su savimi Morkų, jis man naudingas tarnavimui.
11Luka peke yake ndiye aliye hapa pamoja nami. Mpate Marko uje naye, kwa maana ataweza kunisaidia katika kazi yangu.
12Tichiką pasiunčiau į Efezą.
12Nilimtuma Tukiko kule Efeso.
13Atvykdamas atgabenk apsiaustą, kurį palikau Troadėje pas Karpą, taip pat ir knygas, ypač pergamentus.
13Utakapokuja niletee koti langu nililoacha kwa Karpo kule Troa; niletee pia vile vitabu, na hasa vile vilivyotengenezwa kwa ngozi.
14Kalvis Aleksandras man padarė daug bloga, Viešpats jam teatmoka pagal jo darbus.
14Yule sonara aitwaye Aleksanda amenitendea maovu mengi; Bwana atamlipa kufuatana na hayo matendo yake.
15Ir tu saugokis jo, nes jis labai priešinosi mūsų žodžiams.
15Jihadhari naye kwa sababu aliupinga ujumbe wetu kwa ukali.
16Mano pirmajame apsigynime nė vieno nebuvo su manimi, visi mane paliko. Tenebus jiems tai palaikyta nusikaltimu!
16Wakati nilipojitetea kwa mara ya kwanza hakuna mtu aliyesimama upande wangu; wote waliniacha. Mungu asiwahesabie kosa hilo!
17Bet Viešpats stovėjo su manimi ir sustiprino mane, kad toliau skelbčiau Evangeliją ir išgirstų visi pagonys; aš buvau išgelbėtas iš liūto nasrų.
17Lakini, Bwana alikaa pamoja nami, akanipa nguvu, hata nikaweza kuutangaza ujumbe wote, watu wa mataifa wausikie; tena nikaokolewa katika hukumu ya kifo kama kinywani mwa simba.
18Ir Viešpats išgelbės mane iš visų piktų kėslų ir išsaugos savo dangiškajai karalystei. Jam šlovė per amžių amžius! Amen.
18Bwana ataniokoa na mambo yote maovu, na kunichukua salama mpaka katika Utawala wake wa mbinguni. Kwake uwe utukufu milele na milele! Amina.
19Pasveikink Priską, Akvilą ir Onesiforo namiškius.
19Wasalimu Priska na Akula, pamoja na jamaa ya Onesiforo.
20Erastas pasiliko Korinte, o Trofimą palikau Milete sergantį.
20Erasto alibaki Korintho, naye Trofimo nilimwacha Mileto kwa sababu alikuwa mgonjwa.
21Pasistenk atvykti dar prieš žiemą! Tave sveikina Eubulas, Pudentas, Linas ir Klaudija bei visi broliai.
21Fanya bidii kuja kabla ya majira ya baridi. Ebulo, Pude, Lino na Klaudia wanakusalimu; vilevile ndugu wengine wote.
22Viešpats Jėzus Kristus tebūna su tavo dvasia! Malonė teesie su jumis! Amen.
22Bwana awe nawe rohoni mwako. Nawatakieni nyote neema.