Lithuanian

Swahili: New Testament

2 Timothy

3

1Žinok, kad paskutinėmis dienomis užeis sunkūs laikai,
1Kumbuka kwamba, katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za taabu.
2nes žmonės bus savimylos, pinigų mylėtojai, pagyrūnai, išdidūs, piktžodžiautojai, neklusnūs tėvams, nedėkingi, nešventi,
2watu watakuwa na ubinafsi, wenye tamaa ya fedha, wenye majivuno, wenye kujiona, wenye kumtukana Mungu, wasiowatii wazazi wao, wasio na shukrani na waovu;
3nemylintys, nesutaikomi, šmeižikai, nesusivaldantys, šiurkštūs, nekenčiantys to, kas gera,
3watatokea watu wasio na upendo moyoni, wasio na huruma, wachongezi, walafi na wakali; watachukia chochote kilicho chema;
4išdavikai, užsispyrę, pasipūtėliai, labiau mylintys malonumus negu Dievą,
4watakuwa wahaini, wakaidi na waliojaa kiburi; watapenda anasa kuliko kumpenda Mungu.
5turintys dievotumo išvaizdą, bet atsižadėję jo jėgos. Šalinkis tokių žmonių!
5Kwa nje wataonekana kama watu wenye kumcha Mungu, lakini wataikana nguvu yake. Jiepushe kabisa na watu wa namna hiyo.
6Iš jų yra tie, kurie įsiskverbia į namus ir pavergia silpnas moterėles, pilnas nuodėmių, geidulių vedžiojamas,
6Baadhi yao huenda katika nyumba za watu na huwateka wanawake dhaifu waliolemewa mizigo ya dhambi na ambao wanaongozwa na tamaa za kila aina;
7nuolat besimokančias ir vis nesugebančias pasiekti tiesos pažinimo.
7wanawake ambao wanajaribu daima kujifunza lakini hawawezi kuufikia ujuzi wa huo ukweli.
8Kaip Janas ir Jambras priešinosi Mozei, taip ir jie priešinasi tiesai. Tai žmonės sugedusio proto, netikusio tikėjimo.
8Watu hao huupinga ukweli kama vile Yane na Yambre walivyompinga Mose.
9Bet jie toli nenužengs, nes jų kvailumas, kaip ir anų, bus visiems regimas.
9Lakini hawataweza kuendelea zaidi kwa maana upumbavu wao utaonekana wazi kwa wote. Ndivyo ilivyokuwa kwa akina Yane na Yambre.
10Bet tu stropiai pasekei mano mokymu, gyvenimo būdu, tikslu, tikėjimu, ištverme, meile, kantrybe,
10Wewe lakini, umeyafuata mafundisho yangu, mwenendo wangu, makusudi yangu katika maisha, imani yangu, uvumilivu wangu, upendo wangu, subira yangu,
11persekiojimais, sunkumais, kurie mane ištiko Antiochijoje, Ikonijuje, Listroje. O kokių tik persekiojimų man neteko iškęsti! Bet iš visų išgelbėjo mane Viešpats.
11udhalimu na mateso yangu. Unayajua mambo yaliyonipata huko Antiokia, Ikonio na Lustra. Nilivumilia udhalimu mkubwa mno! Lakini Bwana aliniokoa katika mambo hayo yote.
12Taip ir visi, kurie trokšta dievotai gyventi Kristuje Jėzuje, bus persekiojami.
12Kila mtu anayetaka kuishi maisha ya kumcha Mungu katika kuungana na Kristo Yesu lazima adhulumiwe.
13Pikti žmonės ir suvedžiotojai eis blogyn, klaidindami ir klysdami.
13Watu waovu na wadanyanyifu watazidi kuwa waovu zaidi na zaidi kwa kuwadanganya wengine na kudanganyika wao wenyewe.
14O tu pasilik prie to, ką išmokai ir įtikėjai, žinodamas, iš ko išmokai.
14Lakini wewe dumu katika ukweli ule uliofundishwa, ukaukubali kabisa. Unawajua wale waliokuwa walimu wako.
15Tu nuo vaikystės žinai šventuosius Raštus, galinčius tave pamokyti išgelbėjimui per tikėjimą, kuris yra Kristuje Jėzuje.
15Unakumbuka kwamba tangu utoto wako umeyajua Maandiko Matakatifu ambayo yaweza kukupatia hekima iletayo wokovu kwa njia ya imani kwa Kristo Yesu.
16Visas Raštas yra Dievo įkvėptas ir naudingas mokyti, barti, taisyti, auklėti teisumui,
16Maandiko yote Matakatifu yameandikwa kwa uongozi wa Mungu, na yanafaa katika kufundishia ukweli, kuonya, kusahihisha makosa, na kuwaongoza watu waishi maisha adili,
17kad Dievo žmogus taptų tobulas, pasiruošęs kiekvienam geram darbui.
17ili mtu anayemtumikia Mungu awe mkamilifu, na tayari kabisa kufanya kila tendo jema.