1Primink jiems, kad būtų paklusnūs valdytojams ir valdžioms, kad būtų pasiruošę kiekvienam geram darbui,
1Wakumbushe watu kuwastahi watawala na wenye mamlaka, kuwatii na kuwa tayari kwa kila namna kutenda mambo yote mema.
2niekam nepiktžodžiautų, nesikivirčytų, būtų nuosaikūs, visiems žmonėms rodytų visokeriopą romumą.
2Waambie wasimtukane mtu yeyote; bali waishi kwa amani na masikizano, wawe daima wapole kwa kila mtu.
3Juk ir mes kitados buvome neprotingi, neklusnūs, apgauti, vergaujantys įvairiems geiduliams ir malonumams, gyvenome pilni pykčio ir pavydo, neapkenčiami ir nekenčiantys vieni kitų.
3Maana, wakati mmoja sisi tulikuwa wapumbavu, wakaidi na wapotovu. Tulikuwa watumwa wa tamaa na anasa za kila aina. Tuliishi maisha ya uovu na wivu; watu walituchukia nasi tukawachukia.
4Bet kai pasirodė Dievo, mūsų Gelbėtojo, gerumas ir meilė žmonėms,
4Lakini wakati wema na upendo wa Mungu, Mwokozi wetu, ulipofunuliwa,
5Jis išgelbėjo mus ne dėl mūsų atliktų teisumo darbų, bet iš savo gailestingumo, Šventosios Dvasios atgimdančiu ir atnaujinančiu nuplovimu.
5alituokoa. alituokoa si kwa sababu ya jambo lolote jema tulilotenda sisi, bali alituokoa kwa sababu ya huruma yake, kwa njia ya Roho Mtakatifu anayetujalia tuzaliwe upya na kuwa na maisha mapya kwa kutuosha kwa maji.
6Jis mums dosniai išliejo tos Dvasios per mūsų Gelbėtoją Jėzų Kristų,
6Mungu alitumiminia Roho Mtakatifu bila kipimo kwa njia ya Yesu Kristo, Mwokozi wetu,
7kad, išteisinti Jo malone, viltimi taptume amžinojo gyvenimo paveldėtojais.
7ili kwa neema yake tupate kukubaliwa kuwa waadilifu na kuupokea uzima wa milele tunaoutumainia.
8Tai patikimas žodis. Ir aš noriu, kad tu nuolatos pabrėžtum šiuos dalykus, kad patikėjusieji Dievu rūpintųsi paremti gerus darbus. Tai gera ir naudinga žmonėms.
8Jambo hili ni kweli. Ninakutaka uyatilie mkazo mambo haya, ili wale wanaomwamini Mungu, wawe na hamu ya kuutumia wakati wao katika kutenda mema, ambayo ni mambo mazuri na ya manufaa kwa watu.
9Venk kvailų ginčų, kilmės sąrašų, nesutarimų ir vaidų dėl įstatymo,visa tai nenaudinga ir tuščia.
9Lakini jiepushe na ubishi wa kipumbavu, ugomvi na mabishano juu ya Sheria. Mambo hayo hayana faida yoyote na ni ya bure tu.
10Atskalūno, vieną kitą kartą įspėjęs, šalinkis,
10Mtu anayesababisha mafarakano mpe onyo la kwanza na la pili, kisha achana naye.
11žinodamas, jog jis iškrypęs ir nuodėmiauja, savo paties nuosprendžiu pasmerktas.
11Wajua kwamba mtu wa namna hiyo amepotoka kabisa, na dhambi zake zathibitisha kwamba amekosea.
12Kai nusiųsiu pas tave Artemą ar Tichiką, paskubėk atvykti pas mane į Nikopolį; mat nutariau ten žiemoti.
12Baada ya kumtuma kwako Artema au Tukiko, fanya bidii kuja Nikopoli unione, maana nimeamua kukaa huko wakati wa majira ya baridi.
13Teisininką Zeną ir Apolą išleisk į kelionę gerai aprūpintus, kad jiems nieko netrūktų.
13Jitahidi kumsaidia mwana sheria Zena na Apolo ili waweze kuanza ziara zao na uhakikishe kwamba wana kila kitu wanachohitaji.
14Tesimoko ir mūsiškiai remti gerus darbus būtiniems reikalams patenkinti, kad neliktų bevaisiai.
14Ni lazima watu wetu wajifunze kuutumia wakati wao katika kutenda mema ili wasaidie katika mahitaji ya kweli, na maisha yao yawe ya kufaa.
15Tave sveikina visi esantys su manimi. Pasveikink tuos, kurie myli mus tikėjime. Malonė su jumis visais! Amen.
15Watu wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu rafiki zetu katika imani. Nawatakieni nyote neema ya Mungu.