1Paulus, Guds tjener og Jesu Kristi apostel til å føre Guds utvalgte til tro og til å kjenne den sannhet som hører til gudsfrykt,
1Mimi Paulo, mtumishi wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo naandika. Mimi nimechaguliwa kuijenga imani ya wateule wa Mungu na kuwaongoza waufahamu ukweli wa dini yetu,
2i håp om evig liv, som Gud, han som ikke lyver, har lovt fra evige tider,
2ambayo msingi wake ni tumaini la kupata uzima wa milele. Mungu ambaye hasemi uongo, alituahidia uzima huo kabla ya mwanzo wa nyakati,
3men nu i sin tid har han åpenbaret sitt ord i den forkynnelse som blev mig betrodd efter Guds, vår frelsers befaling
3na wakati ufaao ulipowadia, akaudhihirisha katika ujumbe wake. Mimi nilikabidhiwa ujumbe huo nuutangaze kufuatana na amri ya Mungu, Mwokozi wetu.
4- til Titus, min ekte sønn i den felles tro; Nåde og fred fra Gud Fader og Kristus Jesus, vår frelser!
4Ninakuandikia wewe Tito, mwanangu wa kweli katika imani tunayoshiriki. Nakutakia neema na amani kutoka kwa Mungu Baba, na kutoka kwa Kristo Yesu, Mkombozi wetu.
5Derfor lot jeg dig bli efter på Kreta at du skulde sette det i rette skikk som ennu stod tilbake, og innsette eldste i hver by, således som jeg foreskrev dig,
5Nilikuacha Krete ili urekebishe yale mambo ambayo hayakuwa yamekamilika bado, na kuwateua wazee wa kanisa katika kila mji. Kumbuka maagizo yangu:
6om nogen er ulastelig, én kvinnes mann, og har troende barn som ikke har ondt ord på sig for ryggesløshet eller er gjenstridige.
6mzee wa kanisa anapaswa kuwa mtu asiye na hatia; aliye na mke mmoja tu, na watoto wake wanapaswa kuwa waumini, wasiojulikana kuwa wakorofi au wakaidi.
7For en tilsynsmann skal være ulastelig som en Guds husholder, ikke selvgod, ikke vredladen, ikke drikkfeldig, ikke voldsom, ikke lysten efter ussel vinning,
7Maana kwa vile kiongozi wa kanisa ni mkurugenzi wa kazi ya Mungu, anapaswa kuwa mtu asiye na hatia. Asiwe mwenye majivuno, mwepesi wa hasira, mlevi, mkorofi au mchoyo.
8men gjestfri, glad i det gode, sindig, rettferdig, hellig, avholdende,
8Anapaswa kuwa mkarimu na anayependa mambo mema. Anapaswa kuwa mtu mtaratibu, mwadilifu, mtakatifu na mwenye nidhamu.
9en som holder fast ved det troverdige ord efter læren, forat han kan være i stand til både å formane ved den sunde lære og å tale til rette dem som sier imot.
9Ni lazima ashike kikamilifu ujumbe ule wa kuaminika kama unavyofundishwa. Ndivyo atakavyoweza kuwatia wengine moyo kwa mafundisho ya kweli na kuyafichua makosa ya wale wanaoyapinga mafundisho hayo.
10For der er mange gjenstridige, som farer med tomt snakk og dårer folks hu, helst de av omskjærelsen.
10Maana, wako watu wengi, hasa wale walioongoka kutoka dini ya Kiyahudi, ambao ni wakaidi, wanaowapotosha wengine kwa upumbavu wao.
11Disse skal en målbinde; for de nedriver hele hus ved å føre utilbørlig lære for ussel vinnings skyld.
11Lazima kukomesha maneno yao, kwani wanavuruga jumuiya nzima kwa kufundisha mambo ambayo hawapaswi kufundisha; wanafanya hivyo kwa nia mbaya ya kupata faida ya fedha.
12En av dem, deres egen profet, har sagt: Kreterne er alltid løgnere, onde dyr, late buker.
12Hata mmoja wa manabii wao, ambaye naye pia ni Mkrete, alisema: "Wakrete, husema uongo daima; ni kama wanyama wabaya, walafi na wavivu!"
13Dette vidnesbyrd er sant. Derfor skal du tale dem strengt til rette, forat de må bli sunde i troen,
13Naye alitoboa ukweli kwa sababu hiyo, unapaswa kuwakaripia vikali, ili wawe na imani kamilifu.
14så de ikke gir sig av med jødiske eventyr og bud av mennesker som vender sig bort fra sannheten.
14Wasiendelee kushikilia hadithi tupu za Kiyahudi na maagizo ya kibinadamu yanayozuka kwa watu walioukataa ukweli.
15Alt er rent for de rene; men for de urene og vantro er intet rent; både deres sinn og deres samvittighet er urene.
15Kila kitu ni safi kwa watu walio safi; lakini hakuna chochote kilicho safi kwa wale waliochafuliwa na wasioamini, maana dhamiri na akili zao zimechafuliwa.
16De sier at de kjenner Gud; men de fornekter ham med sine gjerninger, for de er vederstyggelige og ulydige og uduelige til all god gjerning.
16Watu kama hao hujidai kwamba wanamjua Mungu, lakini kwa matendo yao humkana. Ni watu wa kuchukiza mno na wakaidi, hawafai kwa jambo lolote jema.