1Jeg vidner for Gud og Kristus Jesus, som skal dømme levende og døde, og ved hans åpenbarelse og hans rike;
1Nakuamuru mbele ya Mungu, na mbele ya Kristo Yesu atakayewahukumu watu walio hai na wafu, na kwa sababu anakuja kutawala akiwa Mfalme:
2Forkynn ordet, vær rede i tide og utide, overbevis, irettesett, forman med all langmodighet og lære!
2hubiri huo ujumbe, sisitiza kuutangaza (iwe ni wakati wa kufaa au wakati usiofaa), karipia, onya na himiza watu ukiwafundisha kwa uvumilivu wote.
3For det skal komme en tid da de ikke skal tåle den sunde lære, men efter sine egne lyster ta sig selv lærere i hopetall, fordi det klør dem i øret,
3Utakuja wakati ambapo watu hawatasikiliza mafundisho ya kweli, ila watafuata tamaa zao wenyewe na kujikusanyia walimu tele watakaowaambia mambo yale tu ambayo masikio yao yako tayari kusikia.
4og de skal vende øret bort fra sannheten og vende sig til eventyr.
4Watakataa kuusikia ukweli, watageukia hadithi za uongo.
5Men vær du edru i alle ting, lid ondt, gjør en evangelists gjerning, fullfør din tjeneste!
5Wewe, lakini, uwe macho katika kila hali; vumilia mateso, fanya kazi ya mhubiri wa Habari Njema, timiza kikamilifu utumishi wako.
6For jeg ofres allerede, og tiden for min bortgang er forhånden.
6Kwa upande wangu mimi, niko karibu kabisa kutolewa dhabihu na wakati wa kufariki kwangu umefika.
7Jeg har stridt den gode strid, fullendt løpet, bevart troen.
7Nimefanya bidii katika mashindano, nimemaliza safari yote na imani nimeitunza.
8Så ligger da rettferdighetens krans rede for mig, den som Herren, den rettferdige dommer, skal gi mig på hin dag, dog ikke mig alene, men alle som har elsket hans åpenbarelse.
8Na sasa imebakia tu kupewa tuzo la ushindi kwa maisha ya uadilifu, tuzo ambalo Bwana Hakimu wa haki, atanipa mimi Siku ile na wala si mimi tu, ila na wale wote wanaotazamia kwa upendo kutokea kwake.
9Gjør dig umak for å komme snart til mig!
9Fanya bidii kuja kwangu karibuni.
10For Demas forlot mig, fordi han fikk kjærlighet til den nuværende verden, og drog til Tessalonika, Kreskens til Galatia, Titus til Dalmatia;
10Dema ameupenda ulimwengu huu akaniacha na kwenda zake Thesalonike. Kreske amekwenda Galatia, na Tito amekwenda Dalmatia.
11Lukas er alene hos mig. Ta Markus og ha ham med dig! for han er mig nyttig til tjeneste.
11Luka peke yake ndiye aliye hapa pamoja nami. Mpate Marko uje naye, kwa maana ataweza kunisaidia katika kazi yangu.
12Tykikus har jeg sendt til Efesus.
12Nilimtuma Tukiko kule Efeso.
13Når du kommer, da ha med dig den kappe som jeg lot bli i Troas hos Karpus, og bøkene, især skinnbøkene!
13Utakapokuja niletee koti langu nililoacha kwa Karpo kule Troa; niletee pia vile vitabu, na hasa vile vilivyotengenezwa kwa ngozi.
14Kobbersmeden Aleksander gjorde mig meget ondt; Herren vil lønne ham efter hans gjerninger.
14Yule sonara aitwaye Aleksanda amenitendea maovu mengi; Bwana atamlipa kufuatana na hayo matendo yake.
15Vokt dig for ham du også! for han stod hårdt imot våre ord.
15Jihadhari naye kwa sababu aliupinga ujumbe wetu kwa ukali.
16Ved mitt første forsvar møtte ingen med mig, men alle forlot mig; gid det ikke må bli dem tilregnet!
16Wakati nilipojitetea kwa mara ya kwanza hakuna mtu aliyesimama upande wangu; wote waliniacha. Mungu asiwahesabie kosa hilo!
17Men Herren stod hos mig og styrket mig, forat forkynnelsen skulde fullbyrdes ved mig og alle folk få høre den, og jeg blev fridd ut av løvens gap.
17Lakini, Bwana alikaa pamoja nami, akanipa nguvu, hata nikaweza kuutangaza ujumbe wote, watu wa mataifa wausikie; tena nikaokolewa katika hukumu ya kifo kama kinywani mwa simba.
18Herren skal fri mig fra all ond gjerning og frelse mig inn i sitt himmelske rike; ham være æren i all evighet! Amen.
18Bwana ataniokoa na mambo yote maovu, na kunichukua salama mpaka katika Utawala wake wa mbinguni. Kwake uwe utukufu milele na milele! Amina.
19Hils Priska og Akvilas og Onesiforus' hus!
19Wasalimu Priska na Akula, pamoja na jamaa ya Onesiforo.
20Erastus blev i Korint; Trofimus lot jeg syk efter mig i Milet.
20Erasto alibaki Korintho, naye Trofimo nilimwacha Mileto kwa sababu alikuwa mgonjwa.
21Gjør dig umak for å komme før vinteren! Eubulus og Pudens og Linus og Klaudia og alle brødrene hilser dig.
21Fanya bidii kuja kabla ya majira ya baridi. Ebulo, Pude, Lino na Klaudia wanakusalimu; vilevile ndugu wengine wote.
22Den Herre Jesus være med din ånd! Nåden være med eder!
22Bwana awe nawe rohoni mwako. Nawatakieni nyote neema.