Paite

Swahili: New Testament

1 Corinthians

1

1Paula, Pathian deihlama Jesu Kris sawltaka sap leh i unaupa Sostheni,
1Mimi Paulo, niliyeitwa kuwa mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Sosthene,
2Korinth khua a Pathian saptuam omte, Kris Jesu a sehtuam, gam chiha I Toupa, amau leh eite Toupa, Jesu Kris min lou tengteng toh misiangthou hi dinga sapte kiangah:
2tunawaandikia ninyi mlio kanisa la Mungu huko Korintho. Ninyi mmefanywa watakatifu katika kuungana na Kristo Yesu, mkaitwa muwe watu wa Mungu, pamoja na watu wote popote wanaomwomba Bwana wetu Yesu Kristo aliye Bwana wao na wetu pia.
3Pathian I Pa leh Toupa Jesu Kris kianga kipan hehpihna leh lemna na kiang uah om hen.
3Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
4Kris Jesu a Pathian hehpihna na kiang ua hongkipia jiakin na tung thu uah Pathian kiangah kipahthu ka gen gige hi;
4Ninamshukuru Mungu wangu daima kwa ajili yenu kwa sababu amewatunukia ninyi neema yake kwa njia ya Kristo Yesu.
5Bangkimah thugen peuhmah ah leh theihna chi tengah, amaha hihhauhin na om uh.
5Maana, kwa kuungana na Kristo mmetajirishwa katika kila kitu. Mmejaliwa elimu yote na uwezo wote wa kuhubiri,
6Huchibangin Kris thu ka theihsak pen noumau ah hihkipin a om hi;
6kwani, ujumbe juu ya Kristo umethibitishwa ndani yenu,
7Huan, i Toupa Jesu Kris kilakna ngak kawmin, khalam thilpiak himhim na tasam kei uhi;
7hata hampungukiwi kipaji chochote cha kiroho mkiwa mnangojea kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
8Aman, i Toupa Jesu Kris ni chia gensiat beia na omna ding un, a tawp phain a honhihkip behlap ding hi.
8Yeye atawaimarisha ninyi mpaka mwisho mpate kuonekana bila hatia Siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.
9Pathian, a Tapa Jesu Kris i Toupa kithuahpihnaa nou honsam lutpa, a muanhuai hi.
9Mungu ni mwaminifu; yeye aliwaita ninyi muwe na umoja na Mwanae Yesu Kristo Bwana wetu.
10Huan, unaute aw, na vek un thu kibang na gen ua, na lak ua kikhenna himhim a om louhna dingin lungsim munkhat leh ngaihtuah munkhata diktaka na kizop chinten jawkna ding un Toupa Jesu Kris minin kon ngen ahi.
10Ndugu, ninawasihi kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo: pataneni nyote katika kila jambo msemalo; yasiweko mafarakano kati yenu; muwe na fikira moja na nia moja.
11Ka unaute aw, na tungtangthu uh, na lak uah kiselna bang a om chih Kloi inkuanpihten honhilh ua.
11Ndugu zangu, habari nilizopata kutoka kwa watu kadhaa wa jamaa ya Kloe, zaonyesha wazi kwamba kuna kutoelewana kati yenu.
12Hiai ka chihna ahi, mi tengtengin, Kei Paula pawl ka hi, Kei jaw Apolla pawl ka hi, Kei jaw Kifa pawl ka hi, Kei jaw Kris pawl ka hi, na chih vengvung uh.
12Nataka kusema hivi: kila mmoja anasema chake: mmoja husema, "Mimi ni wa Paulo," mwingine: "Mimi ni wa Apolo," mwingine: "Mimi ni wa Kefa," na mwingine: "Mimi ni wa Kristo,".
13Kris khenin a om ahia? Paula na sik un kilhdenin a om ahia? Ahihkeileh Paula mina baptisin na om ua hia?
13Je, Kristo amegawanyika? Je, Paulo ndiye aliyesulubiwa kwa ajili yenu? Au je, mlibatizwa kwa jina la Paulo?
14Krispa leh Gaia loungal na lak uah mi kuamah kon baptis louh jiakin Pathian kiangah kipahthu ka gen jel ahi;
14Namshukuru Mungu kwamba sikumbatiza mtu yeyote miongoni mwenu isipokuwa tu Krispo na Gayo.
15Huchi hikei leh jaw min keimah mina baptis na hi uh a chi kha ding uhi.
15Kwa hiyo hakuna awezaye kusema amebatizwa kwa jina langu.
16Stephan inkuanpihte bel ka baptis ngeia, tuate loujaw mi dang ka baptis hiam ka theikei.
16(Samahani, nilibatiza pia jamaa ya Stefana; lakini zaidi ya hawa, sidhani kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote.)
17Kris in baptis dingin honsawl ngal keia, Tanchin Hoih gen dingin honsawl jaw ahi; thu pila gen louin, huchilou injaw Kris kros thilhihtheihna bangmah lou a suaksak kha ding uhi.
17Kristo hakunituma kubatiza, bali kuhubiri Habari Njema; tena, niihubiri bila kutegemea maarifa ya hotuba za watu kusudi nguvu ya kifo cha Kristo msalabani isibatilishwe.
18Kros thu jaw mangthang lelte adin haina ahi ngala; eite hotdam lelte adin bel Pathian thilhihtheihna ahi jaw hi.
18Maana ujumbe kuhusu kifo cha Kristo msalabani ni jambo la kipumbavu kwa wale walio katika mkumbo wa kupotea, lakini kwetu sisi tulio katika njia ya wokovu ujumbe huo ni nguvu ya Mungu.
19Mi pil pilna ka hihmang dinga, lemthei lemtheihna leng ka paikhe ding, chih gelh ahi ngal a.
19Maana Maandiko Matakatifu yasema: "Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, na elimu ya wataalamu nitaitupilia mbali."
20Mipil koiah ahia? Laigelhmi koiah ahia? Hiai khovela selhatmi koiah ahia? Pathianin khovel pilna haihuai ahi chih a theisak kei ahia?
20Yu wapi basi, mwenye hekima? Yu wapi basi, mwalimu wa Sheria? Naye bingwa wa mabishano wa nyakati hizi yuko wapi? Mungu ameifanya hekima ya ulimwengu kuwa upumbavu.
21Pathian pilna ah bel, khovelin a pilna zanga Pathian a theihtheih louh nungin thugen haihuai zanga a gingtate hotdam tuh a kipahlam ahi.
21Maana, kadiri ya hekima ya Mungu, watu hawawezi kumjua Mungu kwa njia ya hekima yao wenyewe. Badala yake, Mungu amependa kuwaokoa wale wanaoamini kwa njia ya kile ambacho wenye hekima wanakiona kuwa ni upumbavu, yaani ujumbe tunaohubiri.
22Judaten chiamtehnate a phut nak ua, Grikten pilna a zong nak uhi.
22Wayahudi wanataka ishara, na Wagiriki wanatafuta hekima;
23Eiten bel Kris kilhden thu i gen jel ua; huai tuh Judate adin pukna, Jentelte adin haina ahi a;
23lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa. Kwa Wayahudi jambo hili ni kikwazo, na kwa watu wa mataifa ni upumbavu;
24Himahleh Judate leng hi hen aw, Grikte leng hi heh, sapte adin jaw Kris, Pathian thilhihtheihna leh Pathian pilna pen ahi.
24lakini kwa wale walioitwa, Wayahudi kwa Wagiriki, Kristo ni nguvu ya Mungu na hekima ya Mungu.
25Pathian haina mihing sangin a piljaw a, Pathian hatlouhna leng huai mihing sangin a hat jaw nak nak hi.
25Maana kinachoonekana kuwa ni upumbavu wa Mungu, kina busara zaidi kuliko hekima ya binadamu; na kinachoonekana kuwa ni udhaifu wa Mungu, kina nguvu zaidi kuliko nguvu za binadamu.
26Unaute aw, a honsapna ngaihtuah dih ua, salama mi pil tampite, mi hat tampite, mi hoih pipite, sap a hih louhdan uh:
26Ndugu, kumbukeni wakati mlipoitwa: wengi wenu hawakuwa wenye hekima hata kwa fikira za binadamu; wengi hawakuwa wenye nguvu au watu wa tabaka ya juu.
27Himahleh, Pathian in khovel thil haite a tel jaw a, mi pilte a zahlaksak theihna dingin; huan Pathianin khovel thil hatloute a tela, a hatte a zahlak sak theihna dingin;
27Ndiyo kusema, Mungu aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni upumbavu, ili awaaibishe wenye hekima; na aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni dhaifu, ili awaaibishe wenye nguvu.
28Khovel thil niam leh thil siammohhuaite, thil omloute toh tanin Pathian in a tela, thil omte bangmah loua a bawl theihna dingin;
28Mungu ameyachagua yale ambayo kwa fikira za dunia ni mambo yaliyo duni na yanayodharauliwa, mambo ambayo hata hayakuwako, ili kwa hayo ayafutilie mbali yale ambayo kwa fikira za binadamu ni mambo ya maana.
29Huchiin, Pathian maah mi kuamah a kiuangsak theikei ding uh.
29Basi, hakuna mtu awezaye kujivunia chochote mbele ya Mungu.
30Amah tuh Kris-a noute hinna nak ahi; huan Pathianin Kris tuh i pilna bang, I diktatna bang, i sianthouna bang, i tatna bang hi dingin a bawlta;Huaijiakin, gelh ahih bangin, a suang peuhmahin Toupa suang hen.
30Mungu mwenyewe ndiye aliyewaunganisha ninyi na Kristo Yesu. Mungu amemfanya Kristo awe hekima yetu; kwa njia yake sisi tunapatanishwa na Mungu, tunakuwa watu wake Mungu na kukombolewa.
31Huaijiakin, gelh ahih bangin, a suang peuhmahin Toupa suang hen.
31Basi, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Mwenye kutaka kujivuna, basi, na ajivunie kazi ya Bwana."