1Huan, unaute aw, kha mite kianga gen bangin na kiang uah thu ka gen theikei hi; sa mite kianga gen bangin ka gen jaw, Kris a naungekte kianga gen bang lel in.
1Ndugu, mimi sikuweza kusema nanyi kama watu mlio na huyo Roho. Nilipaswa kusema nanyi kama watu wa kidunia, kama watoto wachanga katika maisha ya Kikristo.
2Ann gum hilouin, nawituiin kon vaka, a ann gum na nek theih nailouh jiak un; ahi, tuin leng na nethei naikei lailai uh, sa mi na hih lailai jiak un.
2Ilinibidi kuwalisheni kwa maziwa, na si kwa chakula kigumu, kwani hamkuwa tayari kukipokea. Hata sasa hamko tayari.
3Na lak uah kihajatna leh kiselna a om nak jiakin sa mi hi laiin mihing banga omlai hilou na hi u hiam?
3Maana bado mu watu wa kidunia. Je, si kweli kwamba bado uko wivu na magombano kati yenu? Mambo hayo yanaonyesha wazi kwamba ninyi bado ni watu wa kidunia, mnaishi mtindo wa kidunia.
4Mi khatin Paula pawl ka hi, mi dangin, Kei jaw Apollo pawl ka hi, na chih laiteng uh mihing lel hilai hilou na hi uhiam?
4Mmoja wenu anaposema, "Mimi ni wa Paulo", na mwingine, "Mimi ni wa Apolo", je, hiyo haionyeshi kwamba mnaishi bado kama watu wa dunia hii tu?
5Apollo kua ahia leh? Paula leng kua ahia? Nasemmi, noumau hon gingta sakmi lel ei ve ua, huai leng Toupan a piak bang jelin ahi.
5Apolo ni nani? na Paulo ni nani? Sisi ni watumishi tu ambao tuliwaleteeni ninyi imani. Kila mmoja wetu anafanya kazi aliyopewa na Bwana.
6Ken ka suana, Apolloin tuiin a vaka, himahleh Pathianin a khang sak ahi.
6Mimi nilipanda mbegu, Apolo akamwagilia maji; lakini aliyeiotesha mbegu ni Mungu.
7Huchiin, a khangsakpa Pathian kia loungal, a suanpa lah bangmah ahi kei, tuia vakpa leng bangmah ahi tuan kei.
7Wa maana si yule aliyepanda mbegu, au yule aliyemwagilia maji; wa maana ni Mungu aliyeiwezesha mbegu kuota.
8Huan, a suanpa leh tuia vakpa pumkhat ahi ua, himahleh, amau sep gim bang jelin, amau kipahman a mu tuaktuak ding uh.
8Yule aliyepanda na yule aliyemwagilia maji wote ni sawa, ingawa kila mmoja atapokea tuzo lake kufuatana na jitihada yake mwenyewe.
9Koute jaw Pathian na seppihte ka hi ngal ua, nou bel Pathian louma na hi uhi, Pathian inlam leng na hi uhi.
9Maana sisi ni ndugu, wafanyakazi pamoja na Mungu; na ninyi ni shamba lake; ninyi ni jengo lake.
10Pathianin hehpihna honpiak bang jelin innlam heutupen piltak bangin ken suangphum ka lema, mi dangin a tungah inn a lam uhi. Himahleh mi chih a tunga a lamdan ding uah pilvang chiat uhen.
10Kwa msaada wa neema aliyonipa Mungu, nimefaulu, kama mwashi stadi mwenye busara, kuweka msingi ambao juu yake mtu mwingine anajenga. Basi, kila mmoja awe mwangalifu jinsi anavyojenga juu yake.
11Suangphum lepkhitsa loungal suangphum dang kuamahin a lem theita kei ua, huai suangphum tuh Jesu Kris ahi.
11Hakuna mtu awezaye kuweka msingi mwingine badala ya ule uliokwisha wekwa, yaani Yesu Kristo.
12Huan, suangphum tuangah kuapeuhin dangkaeng in hiam, dangkain hiam, suang mantamin hiam, singin hiam, loupain hiam, buhpawl hiamin lam leh,
12Juu ya msingi huo mtu anaweza kujenga kwa dhahabu, fedha au mawe ya thamani; anaweza kutumia miti, majani au nyasi.
13Mi chih nasep tuh a honglang ding hi; Niin a hihlang ding ahi ngala, meia a kilak dingjiakin; mei ngeingeiin mi chih nasep bangchibang ahia chih a hihchian ding hi.
13Iwe iwavyo, ubora wa kazi ya kila mmoja utaonekana wakati Siku ile ya Kristo itakapoifichua. Maana, Siku hiyo itatokea na moto, na huo moto utaipima na kuonyesha ubora wake.
14Kua nasep leng a tunga a lampen a omgige leh, huai miin kipahman a mu ding.
14Ikiwa alichojenga mtu juu ya huo msingi kitaustahimili huo moto, atapokea tuzo;
15Kua nasep leng a kat leh, huai miin a tan ding hi; amah taktak jaw hotdamin a om ding, himahleh, meia pai suak bangin.
15lakini kama alichojenga kitaunguzwa, basi, atapoteza tuzo lake; lakini yeye mwenyewe ataokolewa kana kwamba ameponyoka kutoka motoni.
16Pathian temple na hih uh leh Pathian Kha noumau ah a om gige chih na theikei ua hia?
16Je, hamjui kwamba ninyi ni hekalu la Mungu, na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
17Kuapeuhmahin Pathian temple a hihsiat leh huai mi tuh Pathianin a hihse ding; Pathian temple tuh a siangthou ngala, huai temple tuh noumau na hi uhi.
17Basi, mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu; maana hekalu la Mungu ni takatifu, na hekalu hilo ni ninyi wenyewe.
18Kuamah amah leh amah kikhem kei hen. Na lak ua kuapeuh hiai khovela pil a kisak leh, a hongpil theihna dingin mi hai hongsuak hen.
18Msijidanganye! Mtu yeyote miongoni mwenu akijidhania mwenye hekima mtindo wa kidunia, heri awe mjinga kusudi apate kuwa na hekima ya kweli.
19Hiai khovel pilna tuh Pathian ngaihdanin haina ahi. Aman tuh amaute a pillepchiahna uah a man hi, chih gelh ahi ngala:
19Maana, hekima ya kidunia ni upumbavu mbele ya Mungu. Kwani Maandiko Matakatifu yasema: "Mungu huwanasa wenye hekima katika ujanja wao."
20Toupan mi pilte ngaihtuahna a thawn ahi chih, a thei chi-a gelh ahi nawn laia.
20Na tena: "Bwana ajua kwamba mawazo ya wenye hekima hayafai."
21Huaijiakin kuamahin mihingte suang kei uhen; bangkim noua ahi vekta ngala;
21Basi, mtu asijivunie watu. Maana kila kitu ni chenu.
22Paula hiam, Apollo hiam, Kifa hiam, khovel hiam, hinna hiam, sihna hiam, thil omsa hiam, thil hongom ding hiam;A vekin noua ahi vek hi; noumau leng Krisa na hi ua; Kris leng Pathiana ahi.
22Paulo, Apolo na Kefa, ulimwengu, maisha na kifo; mambo ya sasa na ya baadaye, yote ni yenu.
23A vekin noua ahi vek hi; noumau leng Krisa na hi ua; Kris leng Pathiana ahi.
23Lakini ninyi ni wa Kristo naye Kristo ni wa Mungu.