1Huchiin, unaute aw, a tawppenin, na om dingdan u leh Pathian na hihkipahdan ding uh, tua na omdan bang uh, koumaua kipana na lak bang un na hauh semna ding un Toupa Jesu ah ka honngen un ka honhasuan uhi.
1Hatimaye, ndugu zangu, mmejifunza kutoka kwetu namna mnavyopaswa kuishi ili kumpendeza Mungu. Na kweli mmekuwa mnaishi hivyo. Sasa tunawaombeni na kuwasihi kwa jina la Bwana Yesu mfanye vema zaidi.
2Toupa Jesu jiakin bangthute khawng ahia ka honpiak uh na thei ngal ua.
2Maana mnayajua yale maagizo tuliyowapeni kwa mamlaka ya Bwana Yesu.
3Pathian deihlam, na siangthouna ding uh hiai ahi: kingaih tawpsan unla;
3Mungu anataka ninyi muwe watakatifu na mjiepushe kabisa na maisha ya zinaa.
4Siangthou leh zahtakhuaia noumau ji kem siam chiata,
4Kila mwanamume anapaswa kujua namna ya kuishi na mkewe kwa utakatifu na heshima,
5Pathian theilou Jentelte banga huk lamsanga ut louin.
5na si kwa tamaa mbaya kama watu wa mataifa mengine wasiomjua Mungu.
6Huai lam thu ajaw kuamah takhial in a unau tungah thil hoihlou hih kei hen; Toupa tuh huhchibang thilhihte tengteng phulapa a hih jiakin-kou leng ka honhilh khol un ka hontheisak khinta uhi.
6Basi, mtu yeyote asimkosee au kumpunja mwenzake kuhusu jambo hili. Tulikwisha waambieni hayo na kuwaonya kwamba Bwana atawaadhibu wanaofanya mambo hayo.
7Pathianin sianglou dingin a honsam keia, siangthou dingin a honsam ahi zo ngala.
7Mungu hakutuita tuishi maisha ya zinaa, bali tuishi katika utakatifu.
8Huaijiakin a nialin tuh mihing nial ahi keia, Pathian, noua Kha Siangthou honpepa nial ahi jaw hi.
8Kwa hiyo basi, anayedharau mafundisho hayo hamdharau mtu, bali amdharau Mungu mwenyewe anayewapeni Roho wake Mtakatifu.
9A hihangin, unaute itdan lam thu gelh sak na kiphamoh kei ua, kiit tuah chiat dingin noumau ngei Pathian hilhin na om ngal ua.
9Hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya kuwapenda ndugu zenu waumini. Ninyi wenyewe mmefundishwa na Mungu namna mnavyopaswa kupendana.
10Masidonia gama unau om tengteng tungah huai tuh na hih ngei uhi. Himahleh, unaute aw, na hauh semsemna ding un ka honhasuan uhi;
10Na mmekuwa mkiwatendea hivyo ndugu zenu wote kila mahali katika Makedonia. Basi, ndugu tunawaombeni mfanye hata zaidi.
11Kamsiam deuha om leh, noumau na chiat limsak leh, thu ka honpiak bang ua na khut ua sep ngei na tupna ding un;
11Muwe na nia ya kuishi maisha ya utulivu, kila mmoja ashughulikie mambo yake mwenyewe na afanye kazi kwa mikono yake mwenyewe kama tulivyowaagiza pale awali.
12Huchiin polama mite tungah kilawm takin na om thei ding ua, bangmah na kitasam theikei ding uhi.
12Kwa namna hiyo mtajipatia sifa nzuri kutoka kwa wale wasio Wakristo, na hamtakuwa na lazima ya kuwategemea wengine kwa mahitaji yenu.
13Himahleh, unaute aw, mi dang lametna himhim neiloute banga na lungkham louhna ding un, ihmute tungtang na theih louh uh ka deih kei uhi.
13Ndugu, twataka mjue ukweli kuhusu wale ambao wamekwisha fariki dunia, ili msipatwe na huzuni kama watu wengine wasio na matumaini.
14Jesu a si a, a thou nawnta chih i gingta ua, huchimahbangin Jesua ihmu khinsate tuh Pathianin amah toh hontonpih ding ahi ngala.
14Sisi tunaamini kwamba Yesu alikufa, akafufuka; na hivyo sisi tunaamini kwamba Mungu atawaleta pamoja na Yesu wale wote waliofariki wakiwa wanamwamini.
15Hiai tuh Toupa thuin na kiang uah ka gen uhi; eite Toupa hongpai phaa hingdama naom laiten, ihmu khinsate tuh i makhelh kei hial ding hi, chih.
15Hili tunalowaambieni ni fundisho la Bwana; sisi tulio hai, ambao tutakuwa tumebaki, wakati Bwana atakapokuja, hakika hatutawatangulia wale waliokwisha fariki dunia.
16Toupa mahmah kikou aw toh, angel tungnungpen aw toh, Pathian pengkul ging toh, van akipana hongpai suk ding ahi ngala, huan, Krisa siasate a thou masa phot ding ua;
16Maana patatolewa amri, sauti ya malaika mkuu, sauti ya tarumbeta ya Mungu, naye Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni. Ndipo wale waliokufa wakiwa wanamwamini Kristo watafufuliwa kwanza.
17Huai khit chiangin eite hingdama naom laite, huihkhua ah Toupa tuak ding in amau toh mei lakah lak touhin i om ding ua; huchiin khantawnin Toupa kiangah i omta ding hi.Huaijiakin hiai thutein kikhamuan tuah chiat un.
17Kisha sisi tulio hai wakati huo tutakusanywa pamoja nao katika mawingu kumlaki Bwana hewani. Na hivyo tutakuwa daima pamoja na Bwana.
18Huaijiakin hiai thutein kikhamuan tuah chiat un.
18Basi, farijianeni kwa maneno haya.