1Huan, Ikoniam khua ah Judate kikhopna in ah a lut tuak ua, thu a gen jel uh, huchiin Juda leh Grik tampiin leng a gingta hialta uh.
1Kule Ikonio, mambo yalikuwa kama yalivyokuwa kule Antiokia; Paulo na Barnaba walikwenda katika sunagogi la Wayahudi wakaongea kwa uhodari hata Wayahudi wengi na Wagiriki wakawa waumini.
2Himahleh, gingta nuamlou Judaten Jentelte lungsim a hihthou ua, unaute a hosak uh.
2Lakini Wayahudi wengine waliokataa kuwa waumini walichochea na kutia chuki katika mioyo ya watu wa mataifa mengine ili wawapinge hao ndugu.
3Huaijiakin, Toupa ah hangtaka thu genin huaiah sawt sim a om ua, aman tuh chiamtehna leh thillamdangte a khut ua hihsakin, a hehpih thu a theihsak jel hi.
3Paulo na Barnaba waliendelea kukaa huko kwa muda mrefu. Waliongea kwa uhodari juu ya Bwana, naye Bwana akathibitisha ukweli wa ujumbe walioutoa juu ya neema yake, kwa kuwawezesha kutenda miujiza na maajabu.
4Himahleh, khua a mipite a kilangta ua, a khenin Judate a gum ua, a khenin sawltakte a gum uh.
4Watu wa mji huo waligawanyika: wengine waliwaunga mkono Wayahudi, na wengine walikuwa upande wa mitume.
5Huan, Jentelte, Judate a heutute uh toh sawltakte zahhuaitaka bawl leh suanga den tuma a hih dek laiun,
5Mwishowe, baadhi ya watu wa mataifa mengine na Wayahudi, wakishirikiana na wakuu wao, waliazimu kuwatendea vibaya hao mitume na kuwapiga mawe.
6amau a na thei ua, Likaonia gam mah ah Listra leh Darbi khua ah leh, a kim gamah a tai mang ua;
6Mitume walipogundua jambo hilo, walikimbilia Lustra na Derbe, miji ya Lukaonia, na katika sehemu za jirani,
7huaiah Tanchin Hoih a gen jel uh.
7wakawa wanahubiri Habari Njema huko.
8Huan, Listra khua ah khe jaw kuahiam a tu a, a pian tung apat khebai him ahi a, khein a pai ngeikei hi.
8Kulikuwa na mtu mmoja huko Lustra ambaye alikuwa amelemaa miguu tangu kuzaliwa, na alikuwa hajapata kutembea kamwe.
9Huai min Paula thugen a ngaikhia a; huan, Paulain a en gige a, damna dingin ginna a nei chih a theia, aw ngaihtakin, Na khein ding tang in, a chi a.
9Mtu huyo alikuwa anamsikiliza Paulo alipokuwa anahubiri. Paulo alimtazama kwa makini, na alipoona kuwa alikuwa na imani ya kuweza kuponywa,
10Huan, amah a tawma, khein a paita.
10akasema kwa sauti kubwa, "Simama wima kwa miguu yako!" Huyo mtu aliyelemaa akainuka ghafla, akaanza kutembea.
11Huan, mipiten Paula thilhih a muh tak un, Likaonia Pauin, ngaihtakin, Pathiante mihing banga i kiang ua hongsukta uh hi e! a chi ua.
11Umati wa watu walipoona alichofanya Paulo, ulianza kupiga kelele kwa lugha ya Kilukaonia: "Miungu imetujia katika sura za binadamu!"
12Huan, Barnaba, Jupiter, a chi ua, Paula bel, thugenpen a hihjiakin Merkuri, a chi uh.
12Barnaba akaitwa Zeu, na Paulo, kwa vile yeye ndiye aliyekuwa anaongea, akaitwa Herme.
13Huan, Jupiter, siampu a biakin polama om tuh, bawngpate leh pak khigui limte tuh kongkhak kiang khawnga hontawiin, mipite toh biakna dingin oh a tumta a.
13Naye kuhani wa hekalu la Zeu lililokuwa nje ya mji akaleta fahali na shada za maua mbele ya mlango mkuu wa mji, na pamoja na ule umati wa watu akataka kuwatambikia mitume.
14Himahleh sawltak Barnaba leh Paulain huai a jak un, a puan uh a botkek ua, mipi lakah a dianglut ua, a kikou ua.
14Barnaba na Paulo walipopata habari hiyo waliyararua mavazi yao na kukimbilia katika lile kundi la watu wakisema kwa sauti kubwa:
15Pute aw, hiai thilte bangdia hih na hi ua? Kou leng, noumau nuntakdan bang pu mihing ka hive ua le: hiai thil ginaloute khawng na kiheisan ua, van khawng, lei khawng, tuipi khawng, a sung ua om tengteng toh bawlpa Pathian hing kianga nong kaina ding un Tanchin Hoih kon tun uh ahi.
15"Ndugu, kwa nini mnafanya mambo hayo? Sisi pia ni binadamu kama ninyi. Na, tuko hapa kuwahubirieni Habari Njema, mpate kuziacha hizi sanamu tupu, mkamgeukie Mungu aliye hai, Mungu aliyeumba mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo.
16Huai Pathianin nidang laiin nam chih amau lam chiat zuih a phal a,
16Zamani Mungu aliruhusu kila taifa lifanye lilivyopenda.
17Himahleh, amah theihsakna om louin a kibawl kei hi, huchiin thil a hih hoih jela, van akipanin vuahtui khawng a honpia a, na lungtang uh nekding leh kipahnain a hihdim gige a kei hiam, a chi a.
17Hata hivyo, Mungu hakuacha kujidhihirisha kwa mambo mema anayowatendea: huwanyeshea mvua toka angani, huwapa mavuno kwa wakati wake, huwapa chakula na kuijaza mioyo yenu furaha."
18Huan, huai thuin mipiten amaute biakna dia gan a goh ding uh a kham zou teitei hi.
18Ingawa walisema hivyo haikuwa rahisi kuwazuia wale watu wasiwatambikie.
19Himahleh, Antiok leh Ikoniam khua a mi Juda kuate hiam huaiah a hong ua, mipite a khempukta uh; huchiin suangin Paula a deng ua, sia a gintak jiak un khua akipan a kaikheta ua.
19Lakini Wayahudi kadhaa walikuja kutoka Antiokia na Ikonio, wakawafanya watu wajiunge nao, wakampiga mawe Paulo na kumburuta hadi nje ya mji wakidhani amekwisha kufa.
20Himahleh, nungjuite a kima a din lai un, a hongthou a, khua ah a lut nawnta hi. Huan, a jingin Barnaba toh Darbi khua ah a hohta ua.
20Lakini waumini walipokusanyika na kumzunguka, aliamka akarudi mjini. Kesho yake, yeye pamoja na Barnaba walikwenda Derbe.
21Huan, huai khuate kiangah Tanchin Hoih a hilh ua, nungjui tampi a bawl nung un, Listra khua ah, Ikoniam khua ah, Antiok khua ah, a kiknawn jel uhi.
21Baada ya Paulo na Barnabas kuhubiri Habari Njema huko Derbe na kupata wafuasi wengi, walifunga safari kwenda Antiokia kwa kupitia Lustra na Ikonio.
22Gim tampi thuakin Pathian gamah i lut ding ahi him ahi, chiin, nungjuite lungsim a hihkip ua, ginna ah om gige dingin a hasuan jel uh.
22Waliwaimarisha waumini wa miji hiyo na kuwatia moyo wabaki imara katika imani. Wakawaambia, "Ni lazima sisi sote tupitie katika taabu nyingi ili tuingie katika ufalme wa Mungu."
23Huan, saptuam pawl tengah upate a sehsak ua, anngawl kawma a thum khit un, a gin uh Toupa kiangah a kemsak jeljel uhi.
23Waliteua wazee katika kila kanisa kwa ajili ya waumini, na baada ya kusali na kufunga, wakawaweka chini ya ulinzi wa Bwana ambaye walikuwa wanamwamini.
24Huan, Pisidia gam a tawnsuak ua, Pamphilia gam a tung uh.
24Baada ya kupitia katika nchi ya Pisidia, walifika Pamfulia.
25Huan, Perga khua a a thu a genkhit un Attalia khua ah a hoh suk ua;
25Baada ya kuhubiri ule ujumbe huko Perga, walikwenda Atalia.
26huai akipanin longin a pawt ua, Antiok khua a hongtung nawnta ua, huai tuh a thilhih khitsa uh hih dinga unauten Pathian hehpihna kemsaka a pawtna uh ahi.
26Kutoka huko walisafiri kwa meli wakarudi Antiokia ambako hapo awali walikuwa wamewekwa chini ya ulinzi wa neema ya Mungu kwa ajili ya kazi ambayo sasa walikuwa wameitimiza.
27Huan, a tun nung un a saptuamte a sam khawm ua, Pathianin, amau zang a thil a hih tengteng leh, Jentelte dia ginna kongkhak a honsakdan khawng a hilh uh.Huan, nungjuite kiangah sawt sima omte uhi.
27Walipofika huko Antiokia walifanya mkutano wa kanisa la mahali hapo, wakawapa taarifa juu ya mambo Mungu aliyofanya pamoja nao, na jinsi alivyowafungulia mlango watu wa mataifa mengine mlango wa kuingia katika imani.
28Huan, nungjuite kiangah sawt sima omte uhi.
28Wakakaa pamoja na wale waumini kwa muda mrefu.