1Huan, Antiok khuaa saptuam omte lakah jawlnei kuate hiam leh, thuhilhmi kuate hiam a om ua; huaite tuh Barnaba bang, Sumeon Niger a chih bang uh, Kurini khuaa mi Lusia bang, kumpipa Herod unau ding Manaen bang, Saula bang ahi uh.
1Katika kanisa la Antiokia kulikuwa na watu wengine waliokuwa manabii na walimu; miongoni mwao akiwa Barnaba, Simoni aitwaye pia Mweusi, Lukio wa Kurene, Manaeni ambaye alikuwa amelelewa pamoja na mfalme Herode, na Saulo.
2Huan, Toupa na a sem ua, an a ngawl lai un, Kha Siangthouin, Barnaba leh Saula amaute ka sehna hih dingin honhih khensak un, a chi a.
2Walipokuwa wanafanya ibada yao kwa Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu alisema: "Niteulieni Barnaba na Saulo kwa ajili ya kazi niliyowaitia."
3Huchiin, an a ngawl ua, a thum khit un a tunguah a khut uh a koih ua, a paisakta uh.
3Basi, baada ya kusali na kufunga zaidi, wakawawekea mikono, wakawaacha waende zao.
4Huchiin, Kha Siangthou sawlkhiak in a pai ua, Seliusia khua ah a hoh suk ua, huai akipanin Kupra tuikulh ah longin a pai uh.
4Basi, Barnaba na Saulo walipokwisha tumwa na Roho Mtakatifu, walishuka hadi Seleukia, na kutoka huko walipanda meli hadi kisiwa cha Kupro.
5Huan, Salami khuaa a om lai un Judate kikhopna in ah Pathian thu a gen ua; Johan leng a nek uh bawl dingin a pi ua.
5Walipofika Salami walihubiri neno la Mungu katika masunagogi ya Kiyahudi. Yohane (Marko) alikuwa msaidizi wao.
6Huan, tuikulh tuh Papho khua phain a nawk suak ua, bumsiam, jawlnei taklou, Juda mi khat a mu ua, a min tuh Bar-Jesu ahi.
6Walitembea toka upande mmoja wa kisiwa mpaka Pafo upande wa pili, na huko walimkuta mchawi mmoja Myahudi aitwaye Baryesu ambaye alijisingizia kuwa nabii.
7Huai mi tuh gamukpa Serjia Paulus -mi piltak kianga om ahi. Huai gamukpa Barnaba leh Saula a sama, Pathian thu jak a tum a.
7Huyu alikuwa pamoja na Sergio Paulo, mkuu wa kile kisiwa, ambaye alikuwa mtu mwelewa sana. Sergio Paulo aliwaita Barnaba na Saulo ili asikie neno la Mungu.
8Himahleha, bumsiam Elima, (Bar-Jesu min omdan ahi a); huaiin gamukpa ginlouhsak tumin, amau tuh a na khak hi.
8Lakini huyo mchawi Elima (kama alivyokuwa anaitwa kwa Kigiriki), alijaribu kuwapinga ili kumzuia huyo mkuu wa kisiwa asije akaigeukia imani ya Kikristo.
9Huchiin, Saula, Paula a chih mah uh; Kha Siangthouin a dima, amah tuh a ensala.
9Basi, Saulo ambaye aliitwa pia Paulo, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alimkodolea macho huyo mchawi,
10Nang mi khem leh huathuai chitenga dimpa, diabol tapa aw, nang diktatna teng teng melmapa aw, Toupa lam diktakte hihsiat na tawp kei ding maw?
10akasema, "Mdanganyifu wa kupindukia na mlaghai wewe! Wewe ni mtoto wa Ibilisi! Wewe ni adui wa chochote kile kilicho cha kweli; hukomi hata mara moja kujaribu kuzipotosha njia za Bwana zilizonyoka.
11Theiin, tuin Toupa khut na tungah a tu ahi, na mita hongto dinga, khovak na mu tadih kei ding, a chi a. Huchiin mei leh mialin amah a boh pah ngala, khuta kai ding zongin a vak a vakta hi.
11Sasa, mkono wa Bwana utakuadhibu: utakuwa kipofu na hutaweza kuuona mwanga wa jua kwa kitambo." Mara kila kitu kikawa kama ukungu na giza kwake, akaanza kwenda huku na huku akitafuta mtu wa kumshika mkono amwongoze.
12Huan, gamukpan huai thilhih tuh a mu a, Toupa thuhilh tuh lamdang a sa mahmah hi, a gingtata hi.
12Yule mkuu wa kisiwa alipoona hayo, aliongoka akawa muumini; akastaajabia sana mafundisho aliyosikia juu ya Bwana.
13Huan, Paula tuh a tonpihte toh Papho khua akipanin longin a pai ua, Pamphilia gama Perga khua a tung ua; huan, Johanin amau a paisana, Jerusalem khua ah a kik nawnta hi.
13Kutoka Pafo, Paulo na wenzake walipanda meli wakaenda hadi Perga katika Pamfulia; lakini Yohane (Marko) aliwaacha, akarudi Yerusalemu.
14Himahleh, amau Perga khua akipan a pai jel ua, Pisidia gama Antiok khua a tung ua; huan, Khawlniin kikhopna in ah a lut ua, a tu ua.
14Lakini wao waliendelea na safari toka Pisga hadi mjini Antiokia Pisidia. Siku ya Sabato waliingia ndani ya Sunagogi, wakakaa.
15Huan, Dan laibu leh jawlneite laibu a sim khit un, kikhopna in upaten a kiang uah mi a sawl ua, Unaute aw, mite hasotna thu banghiam na neih uh leh gen un, a chi ua.
15Baada ya masomo katika kitabu cha Sheria ya Mose na katika maandiko ya manabii, wakuu wa lile sunagogi waliwapelekea ujumbe huu: "Ndugu, kama mnalo jambo la kuwaambia watu ili kuwapa moyo, semeni."
16Huan, Paula a dinga, khutin a japa, a gen a; Israel mite leh Pathian laudansiamte aw, ngai un.
16Basi, Paulo alisimama, akatoa ishara kwa mkono, akaanza kuongea: "Wananchi wa Israeli na wengine wote mnaomcha Mungu, sikilizeni!
17Hiai Israel chite Pathianin I pipute a tela, Aigupta gama a tam lai un a hihthupi a, tungnung khutin huaia kipanin a pikheta.
17Mungu wa taifa hili la Israeli aliwateua babu zetu na kuwafanya wawe taifa kubwa walipokuwa ugenini kule Misri. Mungu aliwatoa huko kwa uwezo wake mkuu.
18Huan, kum sawmli khawng gamdai ah a thilhihte uh a thuak theitheia.
18Aliwavumilia kwa muda wa miaka arobaini kule jangwani.
19Huan, Kanan gama nam sagih a hihsiat khitin, a gam uh luah dingin a pe jela, kum za li leh kum sawmnga sung teng.
19Aliyaangamiza mataifa ya nchi ya Kanaani akawapa hao watu wake ile nchi kuwa mali yao.
20Huai nungin vaihawmmite a pe jela, jawlnei Samuel tannin.
20Miaka mia nne na hamsini ilipita, halafu akawapatia waamuzi wawaongoze mpaka wakati wa nabii Samweli.
21Huan, huai nungin kumpipa a ngen ua; huchiin Pathianin, Saula, Kish tapa, Benjamin chia, amau a pia a, kum sawmli sung dingin.
21Hapo wakapendelea kuwa na mfalme, na Mungu akawapa Saulo, mtoto wa Kishi wa kabila la Benyamini, awe mfalme wao kwa muda wa miaka arobaini.
22Huan, amah a suan mang nungin a kumpipa ding ua om dingin David a bawlta a; Pathianin huai thu theihsakin, David, Jesai tapa, ka lungtang bang pu mi ka mukheta, aman ka deihlam peuh a hih ding, a chi a.
22Baada ya kumwondoa Saulo, Mungu alimteua Daudi kuwa mfalme wao. Mungu alionyesha kibali chake kwake akisema: Nimemwona Daudi mtoto wa Yese; ni mtu anayepatana na moyo wangu; mtu ambaye atatimiza yale yote ninayotaka kuyatenda.
23Huai suante lakah Pathianin, thuchiam bang jelin, Israelte kiangah Hondampa Jesu a hontuna;
23Kutokana na ukoo wake mtu huyu, Mungu, kama alivyoahidi, amewapelekea watu wa Israeli Mwokozi, ndiye Yesu.
24A hongpai main Johanin kisikna baptisma thu Israel mi tengteng kiang ah a na hilh msask hi.
24Kabla ya kuja kwake Yesu, Yohane alimtangulia akiwahubiria watu wote wa Israeli kwamba ni lazima watubu na kubatizwa.
25Huan, Johanin a lam a tot khit kuan lain, Nouten kua dingin non sep ua? Amah jaw ka hi kei. Himahleh, ngai un, ka nungah mi kuahiam khat hongpai dek ahi, kei jaw a khepeka khetuam phel tham leng ka hi kei, a chi a.
25Yohane alipokuwa anamaliza ujumbe wake aliwaambia watu: Mnadhani mimi ni nani? Mimi si yule mnayemtazamia. Huyo anakuja baada yangu na mimi sistahili hata kuzifungua kamba za viatu vyake.
26Unaute aw, Abraham suana tate aw, na lak ua Pathian laudansiamte tengteng aw, eimahte kiangah hiai hotdamna thu a honkhakkhia uhi.
26"Ndugu, ninyi mlio watoto wa ukoo wa Abrahamu, na wengine wote mnaomcha Mungu! Ujumbe huu wa wokovu umeletwa kwetu.
27Jerusalem khuaa omten a makaite utoh, amah tuh a theih louh jiak uleh, jawlneite thu, Khawlni peuhmahai a sim jel uh, a theih louh jiak un, amah tuh siamlouh tangsakin, huai thu ana hihtangtungta uh ahi.
27Kwa maana wenyeji wa Yerusalemu na wakuu wao hawakumtambua yeye kuwa Mwokozi. Wala hawakuelewa maneno ya manabii yanayosomwa kila Sabato. Hata hivyo, waliyafanya maneno ya manabii yatimie kwa kumhukumu Yesu adhabu ya kifo.
28A sihna ding khop a tungah bangmah a muh louh un leng, Pilat kiangah hihlup dingin a ngen ua.
28Ingawa hawakumpata na hatia inayostahili auawe, walimwomba Pilato amhukumu auawe.
29Huan, a thu jawlneiten a gelh kholh tengteng uh a hihtangtun khit un, singa kipanin a lakhia ua, han ah a sialta uhi.
29Na baada ya kutekeleza yote yaliyokuwa yameandikwa kumhusu yeye, walimshusha kutoka msalabani, wakamweka kaburini.
30Himahleh, Pathianin misi lak akipan a kaithou nawnta a;
30Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu.
31huan, Galili gam akipan Jerusalem khuaa amah toh hohtoute kiangah ni sawtpi tak a kilak ngitngeta; huai mite tun ah mi kianga a thu theihpihte ahi uh.
31Naye, kwa siku nyingi aliwatokea wale waliofuatana naye kutoka Galilaya mpaka Yerusalemu. Hao ndio walio sasa mashahidi wake kwa watu wa Israeli.
32Kou leng pipute kianga chiamsa huai thuchiam a tanchin kipahhuai ka honhilh uhi;
32Sisi tumekuja hapa kuwaleteeni Habari Njema: jambo lile Mungu alilowaahidia babu zetu amelitimiza sasa kwa ajili yetu sisi tulio wajukuu wao kwa kumfufua Yesu kutoka wafu.
33huchia Pathianin Jesu a kaihthoh, I tate kiangah huai tuh a hihtangtung ahi; Sam nihna ah, Ka tapa na knahi a, tuniin kon suang, chih gelh bangin.
33Kama ilivyoandikwa katika zaburi ya pili: Wewe ni Mwanangu, mimi leo nimekuwa baba yako.
34Muatna muna pai nawn lou dingin Pathianin amah misi akipan a kaihthoh dingdan thu sehsa bangin a gen, David kianga hehpihna ka chiamte nangmah ka honpe ding, chiin.
34Na juu ya kumfufua kutoka wafu, asipate tena kurudi huko na kuoza, Mungu alisema hivi: Nitakupa baraka takatifu na za kweli nilizomwahidia Daudi.
35Huaijiakin Sam dangah, Na Mi Siangthou muatmang na phal kei ding, a chi behlap hi.
35Naam, na katika sehemu nyingine za zaburi asema: Hutamwacha Mtakatifu wako aoze.
36David jaw, Pathian vaihawm sak bangin a hinpihte na a sep khitin, a ihmu a, a pipute kiangah a sial ua, a muat mangta ahi;
36Sasa, Daudi mwenyewe alitimiza mapenzi ya Mungu wakati wake; kisha akafa na kuzikwa karibu na wazee wake, na mwili wake ukaoza.
37himahleh Pathian kaihthohin jaw muatna a mu kei hi.
37Lakini yule ambaye Mungu alimfufua kutoka wafu hakupata kuoza.
38Huchiin, unaute aw, thei un; amah jiakin khelhna ngaihdamna thu na kiang ua gen ahi;
38Jueni wazi, ndugu zangu, kwamba ujumbe kuhusu kusamehewa dhambi unahubiriwa kwenu kwa njia ya Yesu Kristo;
39kuapeuh a gingta tuh bangkim ah amah siamtan sakin a om, huaiah tuh Mosi danin siamtansakin na om theikei uh.
39na ya kwamba kila mmoja anayemwamini Yesu anasamehewa dhambi zote, jambo ambalo halingewezekana kwa njia ya Sheria ya Mose.
40Huaijiakin pilvang un, huchilou in jaw jawlneite laibu a a gen uh na tunguah a hongtung ding hi,
40Jihadharini basi, msije mkapatwa na yale yaliyosemwa na manabii:
41Musitte aw, en un, lamdang sa unla, mangthang un; na damsung un na khat ka sem hi, huai na tuh, min nou honhilh mahle uh, na gingta kei hial ding uhi, chih, a chi a.
41Sikilizeni enyi wenye madharau, shangaeni mpotee! Kwa maana kitu ninachofanya sasa, nyakati zenu, ni kitu ambacho hamtakiamini hata kama mtu akiwaelezeni."
42Huan, a pawtun, Khawlni nawn chianga huai thute gen nawn dingin a ngen uh.
42Paulo na Barnaba walipokuwa wanatoka katika ile sunagogi, wale watu waliwaalika waje tena siku ya Sabato iliyofuata, waongee zaidi juu ya mambo hayo.
43Huan, kikhawmte tuh a kikhen tak un, Judate leh phungkaite Pathian limsak laka mi tampiin Paula leh Barnaba a jui jel ua; amau a na houpih ua, Pathian hehpihna ah om gige dingin a hasuan uh.
43Mkutano huo ulipomalizika, Wayahudi wengi na watu wa mataifa mengine waliokuwa wameongokea dini ya Kiyahudi waliwafuata Paulo na Barnaba. Hao mitume waliongea nao, wakawatia moyo waendelee kuishi wakitegemea neema ya Mungu.
44Huan, Khawlni nawnin, a khojang phialin Pathian thu ngaikhe dingin a hongkikhawm ua.
44Siku ya Sabato iliyofuata, karibu kila mtu katika ule mji alikuja kusikiliza neno la Bwana.
45Himahleh, Judaten mipite a muh tak un a haza mahmah ua; Paula thugen a kalh ua, a gensia uhi.
45Lakini Wayahudi walipoliona hilo kundi la watu walijaa wivu, wakapinga alichokuwa anasema Paulo na kumtukana.
46Huan, Paula leh Barnabain hangtakin a genkhia ua, Pathian thu jaw noumaute kiangah gen masak ding him ahi; himahleh, na nial ua, khantawna hing tak loua na kisehkhit nung un, thei un, Jentelte lam ka ngata uh.
46Hata hivyo, Paulo na Barnaba waliongea kwa uhodari zaidi, wakasema, "Ilikuwa ni lazima neno la Mungu liwafikieni ninyi kwanza; lakini kwa kuwa mmelikataa na kujiona hamstahili uzima wa milele, basi, tunawaacheni na kuwaendea watu wa mataifa mengine.
47Huchibangin Toupan thu a honpia hi, Jentelte hihvakpa din ka honsep a, kawlmong pha a Hondampa dia na om theihna dingin, chih gelh bangin, a chi a.
47Maana Bwana alituagiza hivi: Nimekuteua wewe uwe mwanga kwa mataifa, uwe njia ya wokovu kwa ulimwengu wote."
48Huan, Jentelten huai thu a jak un, a kipak ua, Pathian thu a pahtawi ua, huan, khantawna hing dinga seh peuhmahin a gingta uhi.
48Watu wa mataifa mengine waliposikia jambo hilo walifurahi, wakausifu ujumbe wa Mungu; na wale waliokuwa wamechaguliwa kupata uzima wa milele, wakawa waumini.
49Huan, Toupa thu tuh, huai gam khokim khovel ah a dalhta a.
49Neno la Bwana likaenea kila mahali katika sehemu ile.
50Himahleh, Judaten numei zahtakhuai Pathian limsakte leh khua upahonte a hasuan ua, Paula leh Barnaba a sawisak ua, a gam ua kipan a delhkhia uh.
50Lakini Wayahudi waliwachochea wanawake wa tabaka ya juu wa mataifa mengine ambao walikuwa wacha Mungu, na wanaume maarufu wa mji huo. Wakaanza kuwatesa Paulo na Barnaba, wakawafukuza kutoka katika eneo lao.
51Huan, amau a tunguah a khepek ua leivui a singkhia ua, Ikoniam khua a tung uh.Huan, nungjuite kipahna leh Kha Siangthouin a dim chiat uh.
51Basi, mitume wakayakung'uta mavumbi yaliyokuwa katika miguu yao kama onyo, kisha wakaenda Ikonio.
52Huan, nungjuite kipahna leh Kha Siangthouin a dim chiat uh.
52Lakini hao wafuasi walikuwa wamejaa furaha na Roho Mtakatifu.