1Huan, huai lai khawngin Kumpipa Herodin saptuamte laka kuate hiam hihgim tumin a khut a likta a.
1Karibu wakati huohuo, mfalme Herode alianza kuwatesa baadhi ya Wakristo.
2Huan, Jakob, Johan unau, temsauin a sat lum hi.
2Alimwua kwa upanga Yakobo ndugu yake Yohane.
3Huaiin Judate a kipaksak chih a theihin, Peter leng mat a tum jel a. (Huai nite tuh tanghou silngou sohlouh ni ahi).
3Alipoona kuwa kitendo hiki kiliwapendeza Wayahudi, aliendelea, akamkamata Petro. (Hiyo ilifanyika wakati wa sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu.)
4Huan, a mat nungin suangkulh ah a khuma, sepaih pawl li, li chiat jelin, a ven khel saka; Paikan Ankuanglui nungin mi tengteng kiangah pi khiak a tum a.
4Baada ya kutiwa nguvuni, Petro alifungwa gerezani, akawekwa chini ya ulinzi wa vikundi vinne vya askari wannewanne. Herode alikusudia kumtoa hadharani baada ya sikukuu ya Pasaka.
5Huaijiakin Peter tuh suangkulh ah a omsak tadih hi; himahleh, saptuamten amah a dingin phatuamngaitakin Pathian kiangah a thumsak sak uh.
5Basi, Petro alipokuwa gerezani, kanisa lilikuwa linamwombea kwa Mungu kwa moyo.
6Huan, Herodin a pi khiak dingin, huai jan takin Peter tuh sepaih nih kikalah khainiang nih bunin a ihmu a; a vengte leng kongkhak bul ah a om uhi, suangkulh a veng uh.
6Usiku, kabla ya siku ile ambayo Herode angemtoa Petro hadharani, Petro alikuwa amelala kati ya askari wawili. Alikuwa amefungwa minyororo miwili, na walinzi walikuwa wanalinda lango la gereza.
7Huan, ngai in, Toupa angel khat a kiangah a hong dinga, suangkulh sungah vak a hongtangta a; huan, Peter nak ah a beng halha, Thou meng in, a chi a. Huan, a khainiangte a khut akipan a ke suk a.
7Ghafla, malaika wa Bwana akasimama karibu naye na mwanga ukaangaza kile chumba cha gereza. Malaika akamgusa akisema, "Amka upesi!" Mara ile minyororo ikaanguka kutoka katika mikono yake.
8Huan angelin a kiangah, na puan silh inla, na khetuam bun in, a chi a. Huan aman huchibangin a hih a. Huan, angelin, a kiangah, na puan silh hoih inla, honjui in, a chi a.
8Malaika akamwambia, "Jifunge mshipi wako, vaa viatu vyako." Akafanya hivyo. Kisha huyo malaika akamwambia, "Vaa koti lako, unifuate."
9Huan, Peter a pawta, a juita a, a ngel tatdan a tak a hih a theikeia, mengmu banga a muh ahia eita a chi a.
9Petro akamfuata nje lakini hakujua kama hayo yaliyofanywa na huyo malaika yalikuwa ya kweli; alidhani alikuwa anaota ndoto.
10Huan, chingmi masa leh a zom a khen nung un khopi lutna sik kongpi a vatung ua, huai tuh amau adingin a kihong tawmta a; huan, a pawt ua, kongzing khat a kheng ua; huah, angelin a paisan pahta hi.
10Walipita kituo cha kwanza cha ulinzi na cha pili, halafu wakafika kwenye mlango wa chuma wa kuingilia mjini. Huo mlango ukawafungukia wenyewe, nao wakatoka nje. Wakawa wanatembea katika barabara moja na mara yule malaika akamwacha Petro peke yake.
11Huan, Peter a halh takin, Toupan a angel a sawlkhia a, Herod khut leh Juda mite lametna teng teng akipanin a honhumhingta chih tuin diktakin ka theita, a chi a.
11Hapo ndipo Petro alipotambua yaliyotukia, akasema, "Sasa najua kwa hakika kwamba Bwana amemtuma malaika wake akaniokoa kutoka katika mkono wa Herode na kutoka katika mambo yale yote watu wa Israeli waliyotazamia."
12Huan, a kingaihtuah khitin, Johan, Marka a chih uh, huai nu Mari in ah a vahoh a; huaiah tuh thumin mi tampi a naom khawm ua.
12Alipotambua hivyo alikwenda moja kwa moja mpaka nyumbani kwa Maria mama yake Yohane aitwaye Marko. Humo watu wengi walikuwa wamekusanyika wakisali.
13Huan, kongpi kongkhak a kiuh takin, a min, Roda, nungak khat a dawng dingin a va hoha.
13Petro alibisha mlango wa nje na mtumishi mmoja msichana aitwaye Roda, akaenda mlangoni kuitikia.
14Huan, Peter aw a jak takin, a kipah jiakin kong hong louin a tailut nawn zosopta a, kongkhak bul ah Peter a ding chih a vagen a.
14Huyo msichana aliitambua sauti ya Petro akafurahi mno, hata badala ya kuufungua ule mlango, akakimbilia ndani na kuwaambia kwamba Petro alikuwa amesimama nje mlangoni.
15Himahleh, amau, a kiangah, hai neita ve, a nachi ua. Aman bel, hi petmah ahi, chiin, a pang teitei a. Huan, amau a angel hiin teh, a chi ua.
15Wakamwambia yule msichana, "Una wazimu!" Lakini yeye akasisitiza kwamba ilikuwa kweli. Nao wakamwambia, "Huyo ni malaika wake."
16Himahleh, Peterin a kiukiu a; huan, a hon uleh, amah a mu ua, lamdang a sa mahmah uh.
16Wakati huo Petro alikuwa anaendelea kupiga hodi. Mwishowe walifungua mlango, wakamwona, wakashangaa.
17Huchiin, aman a daihna ding un, khutin a japa, Pathianin suangkulh akipan amah a pikhiak dan khawng a hilhta a. Huan, hiai thute Jakob leh unaute kiangah vahilh un, a chi a. Huan, a pawta, mun dangah a vapai a.
17Petro aliwaashiria kwa mkono wakae kimya, akawaeleza jinsi Bwana alivyomtoa gerezani. Kisha akawaambia watoe taarifa ya jambo hilo kwa Yakobo na wale ndugu wengine, halafu akatoka akaenda mahali pengine.
18Huan, ni a suah takin, sepaihte tuh Peter koia om ahia, chiin buai chihtakin a buai uhi.
18Kulipokucha, ulitokea wasiwasi mkubwa kati ya wale askari kuhusu yaliyokuwa yamempata Petro.
19Huan, Herodin a zonga, a mu keia, a chingte a enchiana, thah dingin thu a peta ahi. Huan, Judi agama kipan Kaisari khua ah a hoh suka, huaiah a om nilouh hi.
19Herode aliamuru ufanywe msako lakini hawakuweza kumpata. Hivyo aliamuru wale askari wahojiwe, akatoa amri wauawe. Halafu akatoka huko Yudea akaenda Kaisarea ambako alikaa.
20Huan, Tura leh Sidon khuaa mite tungah a lunghikei mahmaha, huan, amau, Blasta, kumpipa lupna ngakpa, a jawlin a bawl ua, thu khat satin a kiangah a hongpai ua, a kho lamte uh kumpipa kholama pukto jel ahih jiak un kituahna a ngen ua.
20Herode alikasirishwa sana na watu wa Tiro na Sidoni. Lakini wao walimpelekea wajumbe. Nao wakafaulu kwanza kumpata Blasto awe upande wao. Blasto alikuwa msimamizi mkuu wa ikulu ya mfalme. Kisha, wakamwendea Herode wakamwomba kuwe na amani, kwa maana nchi yao ilitegemea nchi ya mfalme kwa chakula.
21Huan, a ni chiam niin kumpipa Herodin kumpipa puan a silha, a kiang uah thu a gena.
21Siku moja iliyochaguliwa, Herode akiwa amevaa mavazi rasmi na kuketi katika kiti cha kifalme aliwahutubia watu.
22Huan, mi tengtengin, Pathian ahi, mihing aw ahi kei, a chi ua, a kikou ua.
22Wale watu walimpigia kelele za shangwe wakisema, "Hii ni sauti ya mungu, si ya mtu."
23Huan, aman Pathian kianga pahtawina a piak louh jiakin Toupa angelin amah a man pah ngala, hutin ane a, a sita hi.
23Papo hapo malaika wa Bwana akamwangusha Herode chini kwa sababu hakumpa Mungu hizo sifa. Akaliwa na wadudu, akafa.
24Pathian thu bel a dalha, a pung jela.Huan, Barnaba leh Sualain na a sep khit un, Jerusalem khua akipan a kik nawnta ua, Johan, Marka a chih uh, a tonpih uh.
24Neno la Mungu likazidi kuenea na kukua.
25Huan, Barnaba leh Sualain na a sep khit un, Jerusalem khua akipan a kik nawnta ua, Johan, Marka a chih uh, a tonpih uh.
25Baada ya Barnaba na Saulo kutekeleza shughuli zao, walitoka tena Yerusalemu wakamchukua Yohane aitwaye pia Marko.