Paite

Swahili: New Testament

Acts

16

1Huan, Darbi, khua leh Listra khua ah leng a hoh a; huaiah nungjui khat a min Timothi a oma; amah tuh gingta sam Juda numei tapa ahi, a pa bel Grik ahi a;
1Paulo alifika Derbe na Lustra, ambako aliishi mfuasi mmoja aitwaye Timotheo. Mama yake ambaye pia alikuwa mfuasi, alikuwa Myahudi; lakini baba yake alikuwa Mgiriki.
2Listra leh Ikoniam khua a unau omten amah a phat mahmah uhi.
2Timotheo alikuwa na sifa kubwa kati ya wale ndugu wa Lustra na Ikonio.
3Paula in amah tuh a kianga hoh sam dingin a deiha; huchiin huailama Juda omte jiak in a zek a sumsaka, a pa Grik ahi chih a thei vek ngal ua.
3Paulo alitaka Timotheo aandamane naye safarini, kwa hiyo alimtahiri. Alifanya hivyo kwa sababu Wayahudi wote walioishi sehemu hizo walijua kwamba baba yake Timotheo alikuwa Mgiriki.
4Huan, kho tenga a paikawm un Jerusalem khua a sawltak leh upa omte vaihawm jui dingin unaute kiangah a pe jel uhi.
4Walipokuwa wanapita katika ile miji waliwapa watu yale maagizo yaliyotolewa na mitume na wazee kule Yerusalemu, wakawaambia wayazingatie.
5Huchiin, ginna ah saptuam pawlte a kipta ua, nitengin a khang deuhdeuh uhi.
5Hivyo, yale makanisa yalizidi kuwa imara katika imani, na idadi ya waumini ikaongezeka kila siku.
6Huan, Kha Siangthouin Asia gama thugen a kham jiakin Phrigia leh Galatia gam a tawn suakta ua.
6Walipitia sehemu za Frugia na Galatia kwani Roho Mtakatifu hakuwaruhusu kuhubiri huo ujumbe mkoani Asia.
7Huan, Missia gam kiang a tun un Bithinia gama lut a tum ua; himahleh Jesu Khain a phal kei hi.
7Walipofika kwenye mipaka ya Musia, walijaribu kuingia mkoani Bithunia, lakini Roho wa Yesu hakuwaruhusu.
8Huchiin, Missia gam a kheng ua, Troasi khua ah a hoh sukta uhi.
8Basi, walipitia Musia, wakaenda moja kwa moja mpaka Troa.
9Huan, janin Paulain mengmu bangin Masidonia gama mi khat dinga, Masidonia gamah hongkai inla, honghuh in, chia thumthumin a mu a.
9Usiku huo, Paulo aliona ono ambalo alimwona mtu mmoja wa Makedonia amesimama pale na kumwomba: "Vuka, uje Makedonia ukatusaidie."
10Huan, huai mengmuhna a neih khit takin Masidonia gamah hoh ka tum pah ua, a kiang ua Tanchin Hoih gen dingin Pathianin a honsam ahi chih kichian taka theiin.
10Mara baada ya Paulo kuona ono hilo, tulijitayarisha kwenda Makedonia bila kukawia, tukiwa na hakika kwamba Mungu ametuita tuwapelekee Habari Njema.
11Huan, Troasi khua akipan longin ka pawt ua, tang takin Samothrasi khua ah ka pai ua, a jingin Neapoli khua ah ka pai nawn ua;
11Kutoka Troa, tulisafiri kwa meli moja kwa moja mpaka Samothrake, na kesho yake tukatia nanga Neapoli.
12huan, huai akipanin Phillippi khua ah ka pai ua, huai khua tuh Masidonia gam a khua khat Rome khua a mi pemte khua ahia, huai uk a kho poimoh pen ahi. Huai khua ni tam sim ka tamta ua.
12Kutoka huko, tulikwenda mpaka Filipi, mji wa wilaya ya kwanza ya Makedonia, na ambao pia ni koloni la Waroma. Tulikaa katika mji huo siku kadhaa.
13Huan, Khawlniin kulh kongkhak polam ah luigei ah, thumna mun hia ka gintak uah ka hoh ua; huan, ka tu ua, numei hongpai khawmte kiangah thu ka gen uhi.
13Siku ya Sabato tulitoka nje ya mji, tukaenda kando ya mto ambapo tulidhani ya kuwa ni mahali pa kusali. Tuliketi, tukaongea na wanawake waliokusanyika mahali hapo.
14Huan, a min Lidia, puansan dup juak, Thiatira khua te, Pathian bia numei khatin ka thu a ja a; huan, Paula thugen jui dingin Toupan a lungtang a hihvaksakta hi.
14Miongoni mwa wale waliotusikiliza alikuwa mwanamke mmoja mcha Mungu aitwaye Ludia mwenyeji wa Thuatira, ambaye alikuwa mfanyabiashara ya nguo za kitani za rangi ya zambarau. Bwana aliufungua moyo wake hata akayapokea yale maneno Paulo aliyokuwa anasema.
15Huan, amah leh a inkuanpihten baptisma a tan khit un, Toupa a ginoma non seh uleh, ka in ah hongtung un, chiin, a honngen ngen a, a honkhouta a.
15Baada ya huyo mama pamoja na jamaa yake kubatizwa, alitualika akisema, "Kama kweli mmeona kwamba mimi namwamini Bwana, karibuni nyumbani kwangu mkakae." Akatuhimiza twende.
16Huan, thumna muna ka hoh lai un, nungak kuahiam dawi aisansiam jawlin a honkituahpih a, aman tuh a aisan jiakin a pute sum tampi a muhsak jela.
16Siku moja, tulipokuwa tunakwenda mahali pa kusali, msichana mmoja aliyekuwa na pepo mwenye uwezo wa kuagua alikutana nasi. Msichana huyo alikuwa anawapatia matajiri wake fedha nyingi kwa uaguzi wake.
17Huai miin Paula leh kou a honjuia, hiai mite, hotdamna lampi nou honhilhte, Tungnungpen Pathian sikha ahi uh, chiin, a kikou a.
17Basi, huyo msichana alimfuata Paulo na sisi, akipiga kelele na kusema, "Hawa watu ni watumishi wa Mungu Mkuu. Wanawatangazieni njia ya wokovu."
18Huchi bangin ni tampi a hih a. Huchiin, Paula a lungkimta keia, a kiheia, dawi kiangah, Jesu Kris minin a sunga kipan pawt thu ka honpia, a chi a. Huan, huchih laitakin, a pawt pah a.
18Akawa anafanya hivyo kwa siku nyingi hata siku moja Paulo alikasirika, akamgeukia na kumwambia huyo pepo, "Nakuamuru kwa jina la Yesu Kristo, mtoke huyu!" Mara huyo pepo akamtoka.
19Huan, a puten a summuhna uh a mang chih a theih tak un, Paula leh Sila a man ua, heutute maah dawl munah a kailut uhi.
19Matajiri wa yule msichana walipoona kwamba tumaini lao la kupata mali limekwisha, waliwakamata Paulo na Sila, wakawaburuta mpaka hadharani, mbele ya wakuu.
20Huchin, vaihawmte kiangah a pi ua, hiai mite Judate ahi uh, ka khua uh a hihbuai mahmah ua;
20Wakawashtaki kwa mahakimu wakisema, "Watu hawa ni Wayahudi na wanafanya fujo katika mji wetu.
21Dan bang hiam ka kipahpih louh uh leh zuih siangloute a gengen uh, Rome khote ka hi ngal ua, a chi ua.
21Wanafundisha desturi ambazo sisi raia wa Roma haturuhusiwi kuzikubali wala kuzifuata."
22Huchiin, mipite leng sawltakte sual dingin a hongkisa sam ua, vaihawmten a puan khawng uh a sahkeksak ua, chianga sat dingin thu a pia uhi.
22Kundi la watu likajiunga nao, likawashambulia. Wale mahakimu wakawatatulia Paulo na Sila mavazi yao, wakaamuru wapigwe viboko.
23Huan, tamvei pi a sat khit un suangkulh ah a khum ua, a vengpa kiangah bittaka ven ding a chi bikbek uhi.
23Baada ya kupigwa sana wakatiwa ndani, na askari wa gereza akaamriwa kuwaweka chini ya ulinzi mkali.
24Huchitela thu a piak jiak un aman tuh tanna sungnungjaw ah a khuma, a khe uh singkol a bunsak hi.
24Kutokana na maagizo hayo, huyo askari aliwaweka katika chumba cha ndani kabisa cha gereza na kuifunga miguu yao kwenye nguzo.
25Himahleh, jan lain, Pathian kiangah Paula leh Sila a thum ua, la a sa ua, hentaten a ngaikhia ua;
25Karibu na usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakisali na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu, huku wafungwa wengine wakiwa wanasikiliza.
26huan, thakhat in jin nakpitakin a honglinga, huchiin, suangkulh suangphumte tannin a ling hi; huan, kongkhak tengteng a kihong pah a, mi chih kolbutte a hongkiphel vekta hi.
26Ghafla, kulitokea mtetemeko mkuu wa ardhi ambao uliitikisa misingi ya gereza. Mara, milango yote ikafunguka na minyororo iliyowafunga hao wafungwa ikaachana.
27Huan, a vengpa ihmu a honghalha, suangkulh kongkhakte tuh kihongin a mu a, hentate tuh taimang uh a sa a, a temsau a doka, a kihihlum dek tak hi.
27Askari wa gereza alipoamka na kuiona milango ya gereza imefunguliwa, alidhani kwamba wafungwa wote walikuwa wametoroka na hivyo akauchomoa upanga wake, akataka kujiua.
28Himahleh Paula aw ngaihtakin a kikou a, bangmah kichih ken, ka vek un hiaiah ka om lai ve ua oi, a chi a.
28Lakini Paulo akaita kwa sauti kubwa: "Usijidhuru mwenyewe kwa maana sisi sote tuko hapa."
29Huan, a vengpan a khawnvakte a kana, a tawmluta, laua ling kawmin Paula leh Sila maah a khupboh a;
29Baada ya kumwita mtu alete taa, huyo askari wa gereza alikimbilia ndani, akajitupa mbele ya miguu ya Paulo na Sila huku akitetemeka kwa hofu.
30huan, amau a pi khia a, Pute aw, hotdama om dingin bang ahia ka hih ding? a chi a.
30Halafu aliwaongoza nje, akawauliza, "Waheshimiwa, nifanye nini nipate kuokoka?"
31Huan amau, Toupa Jesu ging inla, huchiin hotdamin na om ding, nang leh na inkuanpihte toh, a chi ua.
31Wao wakamjibu, "Mwamini Bwana Yesu nawe utaokolewa pamoja na jamaa yako yote."
32Huan, a kiangah leh a ina om tengtengte kiangah Toupa thu a gen uhi.
32Basi, wakamhubiria neno la Bwana yeye pamoja na jamaa yake.
33Huan, huai janin, huailai tak mahmahin a pia, a satna golhte uh a sil sianga; huan, amah leh a inkuanpihte tengtengin baptisma a tang pah ngal uhi.
33Yule askari aliwachukua saa ileile ya usiku akawasafisha majeraha yao, kisha yeye na jamaa yake wakabatizwa papo hapo.
34Huan, a in ah a pitou a nekding a luia, huan, Pathian a gintak jiak un, amah, a inkuanpihte tengteng toh, a kipak mahmah uhi.
34Halafu akawachukua Paulo na Sila nyumbani kwake, akawapa chakula. Yeye na jamaa yake yote wakafanya sherehe kwa vile sasa walikuwa wanamwamini Mungu.
35Huan, ni a suahin, vaihawmten, huai mite khahin, chiin, mi manmite a sawl ua.
35Kesho yake asubuhi, mahakimu waliwatuma maofisa wao wakisema, "Wafungueni wale watu."
36Huan, suangkulh vengpan, Paula kiangah a thu uh a hilha, Vaihawmten, nou khah dingin, mi a honsawl uhi; huaijiakin tunah hongpawt unla, khamuangtakin pai un, a chi a.
36Yule askari wa gereza alimpasha habari Paulo: "Mahakimu wametuma ujumbe ili mfunguliwe. Sasa mnaweza kutoka na kwenda zenu kwa amani."
37Himahleh, Paulain, a kiang uah, Rome khote ka hi ngal ua, ka siamna uleh siamlouhna uh theilouin vantang mitmuhin non sat ua, suangkulh ah na honkhum ua; tunah aguka hondelhkhe dek na hi vial u maw? ahi kei hial ding; amau mahmah hong uhenla hongpikhia uheh, a chi a.
37Lakini Paulo alimjibu, "Ati nini? Ingawa hatukuwa na kosa, walitupiga viboko hadharani hali sisi ni raia wa Roma. Tena, walitutia ndani na sasa wanataka kutufungulia kwa siri! Hata kidogo! Ni lazima wao wenyewe waje hapa watufungulie."
38Huchiin mi manmiten huai thute tuh vaihawmte kiangah a hilh ua. Huan, Rome khua a mi ahi uh chih a jak un a lauta uhi;
38Hao maofisa waliwapasha habari mahakimu juu ya jambo hilo, nao waliposikia kwamba Paulo na Sila walikuwa raia wa Roma, waliogopa.
39huan, a vahoh ua, a khemkhem ua, a pi khia ua, khua akipan paimang dingin a ngen uhi.Huan, suangkulh akipan a pawt ua, Lidia in ah a lut ua, a khamuan ua, a pawtta uhi.
39Hivyo, walikwenda kuwataka radhi na baada ya kuwatoa ndani waliwaomba watoke katika mji ule.
40Huan, suangkulh akipan a pawt ua, Lidia in ah a lut ua, a khamuan ua, a pawtta uhi.
40Paulo na Sila walitoka gerezani, wakaenda nyumbani kwa Ludia. Huko walionana na ndugu waumini na baada ya kuwatia moyo wakaondoka.