Paite

Swahili: New Testament

Acts

17

1Huan, Amphikoli khua leh Appolonia khua a kheng ua, Thessalonika khua a tungta uh, huaiah Judate kikhop in a om hi;
1Kwa kupitia Amfipoli na Apolonia, walisafiri mpaka Thesalonika ambako kulikuwa na sunagogi la Wayahudi.
2Huan, Paula, a dan ngeinain, a kiang uah a luta, Khawlni thumvei Laisiangthou akipanin teltaka sutpihin,
2Paulo alijiunga nao kama ilivyokuwa desturi yake akajadiliana nao Sabato tatu mfululizo, akatumia Maandiko Matakatifu.
3Kris tuh gimthuak ding him a hihdan khawng, misi lak akipana leng thou nawn ding him a hihdan khawng a hilhchiana, a hihlang jel hi. Hiai Jesu, a thu ka honhilh, amah Kris tuh ahi, chiin a gen behlap hi.
3Aliyaeleza na kuonyesha kwamba ilimbidi Kristo kuteswa na kufufuka kutoka wafu. Akawaambia, "Yesu ambaye mimi namhubiri kwenu ndiye Kristo."
4Huchiin, a lak ua khenkhatin a ging ua, Paula leh Sila a kithuahpihta uhi; Pathian limsak Grik mipi thupi tak leh numei makai tampi toh.
4Baadhi yao walikubali wakajiunga na Paulo na Sila. Kadhalika, idadi kubwa ya Wagiriki waliomcha Mungu pamoja na wanawake wengi wa tabaka la juu, walijiunga nao.
5Himahleh ginglou Judaten a mullit ua; dawl mun a mi gilou thadah kuate hiam a kiang uah a tonpih ua, mipi a sam khawm ua, khua pumpi a tokbuai ua, Jason in a luh ua, vantang kianga pikhiak a tum uhi.
5Lakini Wayahudi wakaona wivu; wakawakodi wafidhuli sokoni, wakafanya kikundi na kuzusha fujo mjini kote. Wakaivamia nyumba ya Yasoni wakitumaini kuwapata humo Paulo na Sila ili wawalete hadharani.
6Huan, amau a mu kei ua, Jason leh unau ding kuate hiam kho heutute kiangah a kailut ua, a kikou ua, Khovel tokbuaite hiaiah leng a hong ua,
6Lakini hawakuwapata na hivyo walimburuta Yasoni pamoja na ndugu wengine mpaka kwa wakuu wa mji, wakapiga kelele: "Watu hawa wamekuwa wakivuruga dunia yote na sasa wako hapa mjini.
7Jasonin a nazintun viala; hiaite tengteng tuh, A min Jesu, kumpipa dang a om chiin, Kaisar thu kalhin a om uhi, a chi ua.
7Yasoni amewakaribisha nyumbani kwake. Wote wanafanya kinyume cha amri ya Kaisari wakisema eti Kuna mfalme mwingine aitwaye Yesu."
8Huan, mipi leh kho heututen huai thu a jak un a buaita ua.
8Kwa maneno hayo waliwatia wasiwasi wakuu wa mji na kundi la watu.
9Huan, Jason leh midangte kiang akipanin, a sik ua hen dingin bang hiam a la ua, amau tuh a khahta uhi.
9Wakawafanya Yasoni na wenzake watoe dhamana, kisha wakawaacha waende zao.
10Huan, unauten ajan ajanin Beria khua ah Paula leh Sila a hohsak pah uh; huailai a vatun un Judate kikhopna in ah a lut ua.
10Usiku, wale ndugu waliwahimiza Paulo na Sila waende Berea. Mara tu walipofika huko, walikwenda katika sunagogi la Wayahudi.
11Huai mite tuh Thessalonika khuate sangin a na hoihjaw ua, huchiin lungsim kipaktakin thu a pom ua, a thugen uh a dik leh diklouh theihna dingin nitengin laisiangthou a zong jel uhi.
11Watu wa huko walikuwa wasikivu zaidi kuliko wale wa Thesalonika. Waliupokea ule ujumbe kwa hamu kubwa, wakawa wanayachunguza Maandiko Matakatifu kila siku, ili kuona kama yale waliyosema Paulo na Sila yalikuwa kweli.
12Huchiin, huaite mi tampiin a gingtata uhi; Grik numei zahtakhuai leh pasalte leng duaisanin a gingtata kei uhi.
12Wengi wao waliamini na pia wanawake wa Kigiriki wa tabaka la juu na wanaume pia.
13Himahleh, Thessalonika khuaa Judanten, Paulain Beria khua ah Pathian thu a gen chih a jak tak un, huaiah leng a vahoh ua, mipite a hasuan gawp ua, a hihbuai nawnta uhi.
13Lakini, Wayahudi wa Thesalonika walipogundua kwamba Paulo alikuwa anahubiri neno la Mungu huko Berea, walikwenda huko, wakaanza kufanya fujo na kuchochea makundi ya watu.
14Huchiin, unauten tuipi tana hoh dingin Paula a sawlkhe pah ua, Sila leh Timothi bel huaiah a om tadih uhi.
14Wale ndugu wakamsindikiza haraka aende pwani lakini Sila na Timotheo walibaki Berea.
15Huan, Paula piten Anthen kha tannin a pi ua; huan, Sila leh Timothi tuh theihtawpa a kianga hongpai mengna ding thukhah puain a paita uhi.
15Wale ndugu waliomsindikiza Paulo walikwenda pamoja naye mpaka Athene. Kisha, wakarudi pamoja na maagizo kutoka kwa Paulo kwamba Sila na Timotheo wamfuate upesi iwezekanavyo.
16Huan, Paulain Athen khua a amau a nangak lain, huai khua pathian lima dimin a mu a, a lungsimin a hehta a.
16Paulo alipokuwa anawasubiri Sila na Timotheo huko Athene, moyo wake ulighadhibika sana alipoona jinsi mji huo ulivyokuwa umejaa sanamu za miungu.
17Huchiin, kikhopna in ah Judate leh Pathian limsakte a sel jela, dawl mun ah leng huaia naom peuhmahte tuh nitengin a sel jel hi.
17Alijadiliana na Wayahudi na watu wengine waliomcha Mungu katika sunagogi; na kila siku alikuwa na majadiliano sokoni pamoja na wowote wale waliojitokeza.
18Huan, Epikuria mi leh Stok mi laka mi pil kuate hiam in leng amah a hongkiselpih ua. Hiai mi tamtamin bang ahia gen a tup? a chi ua. Akhenin, Jesu thu leh Thohnawnna thu a gen jiakin gam dang pathiante thugenpa a hih tuak e, a chi ua.
18Wengine waliofuata falsafa ya Epikuro na Stoiki walibishana naye. Wengine walisema, "Anataka kusema nini huyu bwanamaneno?" Kwa kuwa Paulo alikuwa anahubiri juu ya Yesu na juu ya ufufuo, wengine walisema, "Inaonekana kama anahubiri juu ya miungu ya kigeni."
19Huan, amah a len ua, Areopaga ah a honpi ua, a kiangah, hiai thuhilhna thak na gengen non theisak thei diam?
19Hivyo walimchukua Paulo, wakampeleka Areopago, wakasema, "Tunataka kujua jambo hili jipya ulilokuwa unazungumzia.
20Thil lamdang banghiam ka bil uah na hontun ahi; huchiin, hiai thil omdan theih ka ut uh, a chi ua.
20Vitu vingine tulivyosikia kwa masikio yetu vinaonekana kuwa viroja kwetu. Tungependa kujua mambo haya yana maana gani."
21Athente tengteng, a khua ua mikhual omte leng, a man chiang peuh un thu thak photphot genin hiam, a ngaikhe bekin hiamin a om uhi.
21Wananchi wa Athene na wakazi wengine wa huko walikuwa wanatumia wakati wao wote kuhadithiana na kusikiliza habari mpyampya.
22Huan, Areopaga laitak ah Paula a dinga, a gena, nou Athen khua a mite aw, bangkim ah sabiak limsaktak mi na hi uh chih ka thei hi.
22Basi, Paulo alisimama mbele ya baraza la Areopago, akasema, "Wananchi wa Athene! Ninaona kwamba ninyi, kwa vyovyote, ni watu wa dini sana.
23Ka vak kawma, na chibai bukte uh ka et lain, maitam khat, a tunga, Theihlouh Pathian Ading, chia gelh, ka mu ahi. Huchiin, theiloua chibai na buk uh, huai thu tuh ka honhilh ahi.
23Sababu yenyewe ni kwamba katika pitapita yangu niliangalia sanamu zenu za ibada nikakuta madhabahu moja ambayo imeandikwa: Kwa ajili ya Mungu yule Asiyejulikana. Basi, huyo mnayemwabudu bila kujua, ndiye ninayemhubiri kwenu.
24Pathian khovel leh a sunga thil tengteng siampa, lei leh van Toupa a hihjiakin khuta lam in ah khawngpeuh a om kei hi;
24Mungu, aliyeumba ulimwengu na vyote vilivyomo, ni Bwana wa mbingu na nchi; yeye hakai katika hekalu zilizojengwa na watu.
25thil tasam bangin mihing khuta nasep sakin leng om kei, amah mah tuh bangkim kianga hinna, hatna leh thil tengteng pepa ahi jaw hi.
25Wala hatumikiwi kwa mikono ya watu kana kwamba anahitaji chochote kile, kwa maana yeye mwenyewe ndiye anayewapa watu uhai, anawawezesha kupumua na anawapa kila kitu.
26Huan, leitung maikaih tengtenga om dingin bul mun khat vekin nam chih mi a siama, amau adingin hun bisehte a sehsaka, a omna gi uh leng a khunsak.
26Kutokana na mtu mmoja aliumba mataifa yote na kuyawezesha kuishi duniani kote. Aliamua na kupanga kabla kabisa lini na wapi mataifa hayo yangeishi.
27Pathian a zon ua, a mai a mai ua, a muh teiteina ding un; himahleh aman lah hongamlat kei chiat ngala.
27Alifanya hivyo, ili mataifa hayo yapate kumfuata, na kama vile kwa kupapasapapasa, yapate kumfikia. Hata hivyo lakini, Mungu hayuko mbali na kila mmoja wetu.
28Amah vangin i hingin i tangin, i om uh ahi ngala; Noumau laphuahsiam kuate hiamin leng, ei leng a suante i hi ngal ua, chia a gen bang un.
28Kama alivyosema mtu mmoja: Ndani yake yeye sisi tunaishi, tunajimudu, na tuko! Ni kama washairi wenu wengine walivyosema: Sisi ni watoto wake.
29Huchiin, Pathian Suante i hih nung, Pathian tuh dangkaeng peuh, dangka peuh, suang peuh, mihing khutsiam leh suktuaha sekte bang hiam ahi, chih, i gingta ding ahi kei.
29Ikiwa basi, sisi ni watoto wa Mungu, haifai kumfikiria Mungu kuwa kama dhahabu, fedha au hata jiwe lililochongwa na kutiwa nakshi na binadamu.
30Huchiin, Pathianin i theihlouh laikhawng bang a kitheihmohbawla; himahleh, tunah jaw gam chiha mi tengteng kisik ding thu a peta hi, ni achiam jiakin;
30Mungu alifanya kama kwamba haoni nyakati zile watu walipokuwa wajinga. Lakini sasa, anaamuru watu wote kila mahali watubu.
31huai ni chiangin Pathianin a mi seh zangin diktatnain khovel a vaihawm ding; huan a miseh tung thu tuh amah misi laka kipana kaithouin, mitengteng kiangah a theisakta hi, chiin.
31Kwa maana amekwisha weka siku ambayo atauhukumu ulimwengu kwa haki kwa njia ya mtu mmoja aliyemteua. Mungu amewathibitishia wote jambo hili kwa kumfufua mtu huyo kutoka wafu!"
32Huan, misi laka kipana thohnawnna thu a jak tak un, a khenin a nuihsan ua; a khenin, hiai thu na kiangah ka ngaikhe nawn ding uh, a chi ua.
32Walipomsikia Paulo anasema juu ya jambo la kufufuka kwa wafu, wengine wao waliangua kicheko; lakini wengine walisema, "Tunataka kukusikia tena juu ya jambo hili!"
33Huchiin, Paula tuh a lak ua kipan a pawtta hi.Himahleh, mi kuate hiam amah lamah a pang chinten ua, a gingtata ua, huai laka khenkhat tuh Areopaga mi Dionisia leh, numei khat a min Damari leh, a kiang ua midangte toh ahi uh.
33Hivyo, Paulo aliwaacha, akatoka barazani.
34Himahleh, mi kuate hiam amah lamah a pang chinten ua, a gingtata ua, huai laka khenkhat tuh Areopaga mi Dionisia leh, numei khat a min Damari leh, a kiang ua midangte toh ahi uh.
34Lakini watu kadhaa waliandamana naye, wakawa waumini. Miongoni mwao walikuwa Dionisio wa Areopago, mwanamke mmoja aitwaye Damari na wengineo.