Paite

Swahili: New Testament

Acts

27

1Huan, Itali gama longa pai ding thu a hihpuk tak un, Paula leh henta dang kuate hiam Awgasta pawla mi sepaih zaheutu a min Julia a kemsak ua.
1Walipokwisha amua tusafiri mpaka Italia, walimweka Paulo pamoja na wafungwa wengine chini ya ulinzi wa Yulio aliyekuwa ofisa wa jeshi katika kikosi kiitwacho "Kikosi cha Augusto."
2Huan, Adramitiam kho long, Asia gam tuipi piau a kho omte tawn ding ah, ka tuang ua, tuipi ah ka paita uhi; Masidonia gama mi Aristarkha, Thessalonika khua mi, ka kiang uah a oma.
2Tulipanda meli ya Adiramito iliyokuwa inasafiri na kupitia bandari kadhaa za mkoa wa Asia, tukaanza safari. Aristarko, mwenyeji wa Makedonia kutoka Thesalonika, alikuwa pamoja nasi.
3Huan, a jingin Sidon khua ka tawn ua. Huan, Juliain Paula a limbawl ngiala, kihihhalh dingin a lawmte kiangah a pawtsaka.
3Kesho yake tulitia nanga katika bandari ya Sidoni. Yulio alimtendea Paulo vizuri kwa kumruhusu awaone rafiki zake na kupata mahitaji yake.
4Huan, huai akipanin tuipi ah ka pai nawn ua, huihin a hilou lama honsawn hiakin Kupra tuikulh jul huih hatlouhna lam ah ka tai ua.
4Kutoka huko tuliendelea na safari, lakini kwa kuwa upepo ulikuwa unavuma kwa kasi kutujia kwa mbele, tulipitia upande wa kisiwa cha Kupro ambapo upepo haukuwa mwingi.
5Huan, Silisia gam leh Pamphilia gam jul tuipi ka khen nung un, Lidia gama Mira khua ka tung ua.
5Halafu tulivuka bahari ya Kilikia na Pamfulia, tukatia nanga Mura, mji wa Lukia.
6Huaiah sepaih zaheutupan Aleksandria kho long Itali gam tawn ding a mu a; huaiah a hontuangsak a.
6Hapo yule ofisa alikuta meli moja ya Aleksandria iliyokuwa inakwenda Italia, na hivyo akatupandisha ndani.
7Huan, ni tampi tak awlawlin ka pai ua, Knida kho jawn haksapiin ka tung teitei ua, huihin hon sawnkik jiakin Salmoni juanin Krit tuikulh jul huih hatlouhna lamah ka tai ua.
7Kwa muda wa siku nyingi tulisafiri polepole, na kwa shida tulifika karibu na Nido. Kwa sababu upepo ulikuwa bado unatupinga, tuliendelea mbele moja kwa moja tukapitia upande wa Krete karibu na rasi Salmone ambapo upepo haukuwa mwingi.
8Huan, haksatakin tui geigei ah ka pai ua, long khawlna kilawm a chih mun uh ka tungta ua; huai kiangah Lasia khua a om hi.
8Tulipita kando yake polepole tukafika mahali paitwapo "Bandari Nzuri", karibu na mji wa Lasea.
9Huan, ni tampi a beitak jiakin leh, longa pai a lauhuai jiakin, (An Ngawl Ni a khengta ngala), Paulain amau a thuhilha, a kiang uah,
9Muda mrefu ulikuwa umepita, na hata siku ya kufunga ilikuwa imekwisha pita. Sasa ilikuwa hatari sana kusafiri kwa meli. Basi, Paulo aliwapa onyo:
10Pute aw, longa tua pai siatna leh manthatna thupitak tung ding ahi chih ka theia, a sum leh long tungah kia ka chi kei, eimah tungah kia ka chi ahi, a chi a.
10"Waheshimiwa, nahisi kwamba safari hii itakuwa ya shida na hasara nyingi si kwa shehena na meli tu, bali pia kwa maisha yetu."
11Himahleh, sepaih zaheutuin Paula thugen sangin longpu leh long neipa thu a ging jawa.
11Lakini yule ofisa alivutiwa zaidi na maoni ya nahodha na ya mwenye meli kuliko yale aliyosema Paulo.
12Huan, phalbi douna dingin longkhawlna a ginat louh jiakin a tamjawin, huai akipana tuipi a pai khiaka, Phinisi khua tun teiteia, huailaia phalbi dou a sawmpih ua; Phinisi tuh Krit tuikulha longkhawlna khat ahi, mal sak leh sim sak lam ahi a.
12Kwa kuwa bandari hiyo haikuwa mahali pazuri pa kukaa wakati wa baridi, wengi walipendelea kuendelea na safari, ikiwezekana mpaka Foinike. Foinike ni bandari ya Krete inayoelekea kusini-magharibi na kaskazini-magharibi; na huko wangeweza kukaa wakati wa baridi.
13Huan, sim huih awlawla a hongnun takin, a deihlam uh mu a kisa ua, sikkip a khai khia ua, Krit tuikulh gei juljul ah ka pai uhi.
13Basi, upepo mzuri wa kusi ulianza kuvuma, nao wakadhani wamefanikiwa lengo lao; hivyo wakang'oa nanga, wakaiendesha meli karibu sana na pwani ya Krete.
14Himahleh, sawtlou chik nungin gam lam akipanin huih hattak a hongnung sukta a, huai huih tuh Euroklidon a chi jel uhi.
14Lakini haukupita muda, upepo mkali uitwao "Upepo wa Kaskazi" ulianza kuvuma kutoka kisiwani.
15Huan, long a honsawnkhata a, huihlam a ngat theihlouhtakin ka khahta ua, honmut leng honmut lengta a.
15Upepo uliipiga ile meli, na kwa kuwa hatukuweza kuukabili, tukaiacha ikokotwe na huo upepo.
16Huan, a min Klauda tuikulh neuchik petmah pansanin huih hatlouhna lamah ka tai ua, haksatakin long neu tuh ka bitsak thei geigei ua;
16Kisiwa kimoja kiitwacho Kanda kilitukinga kidogo na ule upepo; na tulipopita kusini mwake tulifaulu, ingawa kwa shida, kuusalimisha ule mtumbwi wa meli.
17Huan, a kaihkhiak nung un panpihna khaute khawng a zang ua, long nuailam ah a vial ua, a khih ua, huan, puanjakna bangkim a puksak ua, huchilouin jaw Sirti a lenlut a lau ua, huchiin a honmut leng a honmut lengta hi.
17Wale wanamaji waliuvuta mtumbwi ndani, kisha wakaizungushia meli kamba na kuifunga kwa nguvu. Waliogopa kwamba wangeweza kukwama kwenye ufuko wa bahari, pwani ya Libya. Kwa hiyo walishusha matanga na kuiacha meli ikokotwe na upepo.
18Huan, a jingin, tuikihawtin honsep ek jiakin, longa van khawng tui lakah a paikhe panta ua.
18Dhoruba iliendelea kuvuma na kesho yake wakaanza kutupa nje shehena ya meli.
19Huan, a jing nawnin amau khut ngeiin long van a paikhe nawnta uhi.
19Siku ya tatu, wakaanza pia kutupa majini vifaa vya meli kwa mikono yao wenyewe.
20Huan, ni tampi, nil eng, aksi leng a kimu keia, huihpi petmahin honnuaia, hin himhim ka lamen nawnta kei uhi.
20Kwa muda wa siku nyingi hatukuweza kuona jua wala nyota; dhoruba iliendelea kuvuma sana, hata matumaini yote ya kuokoka yakatuishia.
21Huan, an ne loua sawttak a om nung un, Paula a lak uah a dinga, Pute aw, Krit tuikulha phel loua, ka thu man a, hiai siat leh manthatna tun louh ding hina jena.
21Baada ya kukaa muda mrefu bila kula chakula, Paulo alisimama kati yao, akasema, "Waheshimiwa, ingalikuwa afadhali kama mngalinisikiliza na kuacha kusafiri kutoka Krete. Kama mngalifanya hivyo tungaliiepuka shida hii na hasara hizi zote.
22Himahleh, tunah leng khamuangtaka om dingin kon hasuan ahi; na lak uah kuamahin henna na mangsak kei ding uh, long jaw a mangthang ding.
22Lakini sasa ninawaombeni muwe na moyo; hakuna hata mmoja wenu atakayepoteza maisha yake; meli tu ndiyo itakayopotea.
23Amah Pathiana ka hih, a na leng ka sep, amah angel tuh tujanin ka kiangah a hongdinga, ka kiangah,
23Kwa maana jana usiku malaika wa yule Mungu ambaye mimi ni wake na ambaye mimi ninamwabudu alinitokea,
24Paula, lau ken, Kaisar maah na ding ding; huan, ngai in, longa na kianga pai tengteng leng Pathianin a honpia hi, honchi ahi.
24akaniambia: Paulo usiogope! Ni lazima utasimama mbele ya Kaisari; naye Mungu, kwa wema wake, amekufadhili kwa kuwaokoa wote wanaosafiri nawe wasiangamie.
25Huaijiakin, Pute aw, khamuangtakin om un, Pathian ka gingta hi, honhilh bangbangin a om ding.
25Hivyo, waheshimiwa, jipeni moyo! Maana ninamwamini Mungu kwamba itakuwa sawa kama nilivyoambiwa.
26Himahleh, bang tuikulh hiam ah honlenkhe ding ahi, a chi a.
26Lakini ni lazima tutatupwa ufukoni mwa kisiwa fulani."
27Huan, Adria tuipi ah huihin lehlam lehlam ag a honmutleng a honmut lenga, jan sawm leh jan li a chin janin, janlai hiamin, long miten koi gam hiam tung dekin a kithei ua;
27Usiku wa siku ya kumi na nne, tulikuwa tunakokotwa huku na huku katika bahari ya Adria. Karibu na usiku wa manane wanamaji walijihisi kuwa karibu na nchi kavu.
28Huchiin, tui thukdan a the ua, lam sawmnihin a thei ua, huan, sawtlou chikin a teh nawn ua, lam sawm lem lam ngain a thei ua.
28Hivyo walitafuta kina cha bahari kwa kuteremsha kamba iliyokuwa imefungiwa kitu kizito, wakapata kina cha mita arobaini. Baadaye wakapima tena wakapata mita thelathini.
29Huan, longmeilam ah sikkip li a khia ua, huchilouin jaw suang se munah honlenkhe zenzen kha ding, chih, a lau ua; huan khovak kal a ngaklahta uhi.
29Kwa sababu ya kuogopa kukwama kwenye miamba, waliteremsha nanga nne nyuma ya meli; wakaomba kuche upesi.
30Huan, longmiten long malama sikkipte kikhiak ding bawl khempeuhin, long neu tuh tuipi ah a khia ua, long taisan a tum ua.
30Wanamaji walitaka kutoroka, na walikwisha kuteremsha ule mtumbwi majini, wakijisingizia kwamba wanakwenda kuteremsha nanga upande wa mbele wa meli.
31Hiai lain Paulain, sepaih zaheutu leh sepaihte kiangah, hiaite longa om gige kei uleh bit kei nuteh, a chi a.
31Lakini Paulo alimwambia yule ofisa wa jeshi na askari wake, "Kama wanamaji hawa hawabaki ndani ya meli, hamtaokoka."
32Huchiin, sepaihten longneu khaute a attat ua, a khahta uhi.
32Hapo wale askari walizikata kamba zilizokuwa zimeshikilia ule mtumbwi, wakauacha uchukuliwe na maji.
33Huan, khovak kuanin, Paulain an ne dingin mi tengteng a sawla, tuni ni sawm leh li a hita, bangmah ne louin na ngak ua, na ngawl nilouh uhi.
33Karibu na alfajiri, Paulo aliwahimiza wote wale chakula: "Kwa siku kumi na nne sasa mmekuwa katika mashaka na bila kula; hamjala kitu chochote.
34Huaijiakin, an ne dingin ka honsawl chiat ahi; na damna ding uhi; na lak uah kuamah a samzang khat leng a mangthang kei ding, a chi a.
34Basi, ninawasihi mle chakula kwa maana mnakihitaji ili mweze kuendelea kuishi. Maana hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea."
35Huan, huai thu a gen khitin tanghou a la a, mi tengteng maah Pathian kiangah kipahthu a genta a; huan, a balkhama, a ne panta hi.
35Baada ya kusema hivyo, Paulo alichukua mkate, akamshukuru Mungu mbele yao wote, akaumega, akaanza kula.
36Huan, amau leng khamuang takin a om ua, an a ne samta uh.
36Hapo wote wakapata moyo, nao pia wakala chakula.
37Huan, long a mi tuh ka vek un za nih leh sawmsagih leh guk ka hi ua.
37Jumla tulikuwa watu mia mbili na sabini na sita katika meli.
38Huan, an a nek kham khit un, buh tuh tuipi ah a pai ua, long a hihjang deuh uhi.
38Baada ya kila mmoja kula chakula cha kutosha, walipunguza uzito wa meli kwa kutupa nafaka baharini.
39Huan, ni a suahin, koilai gamahia chih a theikei ua; himahleh, koilai longkhawlna hiam piautak nei khat a mu ua, huai tungah, a hih theih uleh, long taikhiak sak a tum uhi.
39Kulipokucha, wanamaji hawakuweza kuitambua nchi ile, ila waliona ghuba moja yenye ufuko; wakaamua kutia nanga huko kama ikiwezekana.
40Huan, sikkip khihnate a attat ua, tuipi ah a nusia ua; tua lai mahin kaihheina khihnate a phel ua, malam puanjak tuh huih mut ding danin a kaitou ua; piautak a juanta uhi.
40Hivyo walikata nanga na kuziacha baharini, na wakati huohuo wakazifungua kamba zilizokuwa zimeufunga usukani, kisha wakatweka tanga moja mbele kushika upepo, wakaelekea ufukoni.
41Himahleh, tuikihawt khauh nih kituahna munah ka lutkha zenzen ua, long tuh lei a susakta ua; huchiin, long malam a tang bikbekta a, hihtat zoh louhin a oma, a meilam bel tuikihawt a hat jiakin a kek gawp panta hi. 4
41Lakini walifika mahali ambapo mikondo miwili ya bahari hukutana, na meli ikakwama. Sehemu ya mbele ilikuwa imezama mchangani bila kutikisika. Sehemu ya nyuma ya meli ilianza kuvunjika vipandevipande kwa mapigo ya nguvu ya mawimbi.
42Huan, sepaihten hentate hihlup a sawm ua, huchilouin jaw tui liau galkai khattou a om kha ding ua, a taimang kha ding uh chih a lau ua.
42Askari walitaka kuwaua wafungwa wote kwa kuogopa kwamba wangeogelea hadi pwani na kutoroka.
43Himahleh, sepaih zaheutuin Paula humhing a uta, a thiltup uh a kham a; tuiliau siam peuhmah tuipi ah tawm khiaka gam nakaimasak ding leh,mi dang, a khen singpek tung khawnga, a khen long van tung khawnga galkai dingin thu a pia hi. Huchiin, a vek un gamah bittakin a galkai vekta uhi.
43Lakini kwa vile yule ofisajeshi alitaka kumwokoa Paulo, aliwazuia wasifanye hivyo. Aliamuru wale waliojua kuogelea waruke kutoka melini na kuogelea hadi pwani,
44mi dang, a khen singpek tung khawnga, a khen long van tung khawnga galkai dingin thu a pia hi. Huchiin, a vek un gamah bittakin a galkai vekta uhi.
44na wengine wafuate wakijishikilia kwenye mbao au kwenye vipande vya meli iliyovunjika. Ndivyo sisi sote tulivyofika salama pwani.