1Huaijiakin, noute sapa na omna utoh kikhoma om dingin kei Toupaa hentain ka honngen hi,
1Basi, mimi niliye mfungwa kwa kuwa namtumikia Bwana, nawasihi muishi maisha yanayostahili wito mlioitiwa.
2Kingaihniamna leh migitna tengteng, thuaktheihna toh, itnaa kithuakzou zo chiata,
2Muwe daima wanyenyekevu, wapole na wenye saburi; vumilianeni ninyi kwa ninyi kwa mapendo.
3Lemnaa Khaa kipumkhatna vom chinten dingin.
3Fanyeni bidii ya kuhifadhi umoja uletwao na Roho kwa kuzingatia amani iliyo kati yenu.
4A Honsapna pen lametna mun khata sap na hih mahbang un pumpi khat leh Kha khat kia a om;
4Kuna mwili mmoja na Roho mmoja, kama vile tumaini mliloitiwa na Mungu ni moja.
5Toupa khat, ginna khat, baptisma khat,
5Kuna Bwana mmoja, imani moja na ubatizo mmoja;
6Bangkim Pathian leh Pa khat kia a oma; amah tuh bangkim tungah a oma, bangkim a mu suaka, bangkim sungah a om hi.
6kuna Mungu mmoja na Baba wa wote, ambaye yuko juu ya wote, afanya kazi katika yote na yuko katika yote.
7Himahleh, Kris thilpiak tehna bang jelin hehpihna tuh i kiang chiat ah piak a om hi.
7Kila mmoja wetu amepewa neema kadiri ya kipimo alichojaliwa na Kristo.
8Huaijiakin ahi, Tung lama a kahtouh laiin matte tampi a pia, mihingte kiangah leng thilpiakte a pia, a chihna.
8Kama yasemavyo Maandiko: "Alipopaa mbinguni juu kabisa, alichukua mateka; aliwapa watu zawadi."
9Huchiin, A kah tou, chih tuh, lei mun nuainung pente banga a hongsuk masak phot keileh, bangchi a hita ding leh?
9Basi, inaposemwa: "alipaa juu," ina maana gani? Maana yake ni kwamba, kwanza alishuka mpaka chini kabisa duniani.
10Hongsukpen tuh, thil tengteng a hihdim theihna dingin, van tengteng tung peka kah toupa mah ahi.
10Basi, huyo aliyeshuka hapa duniani, ndiye aliyepaa juu ya mbingu zote apate kuujaza ulimwengu.
11Huan, khenkhatte sawltak hi dingin, khenkhatte jawlnei hi dingin, khhenkhatte Tanchin Hoih gen dingin, khenkhatte pastor hi dingin, khenkhatte thuhilh dingin a pia hi:
11Ndiye aliyewapa watu zawadi: wengine aliwajalia wawe mitume, wengine manabii, wengine wawe waeneza Habari Njema, wengine wachungaji na walimu.
12Huai tuh misiangthoute thopna ding, nasepna sepna ding, Kris pumpi lam touhna dingin:
12Alifanya hivyo apate kuwatayarisha watu wote wa Mungu kwa ajili ya kazi ya huduma ya Kikristo ili kuujenga mwili wa Kristo,
13Huai tuh ginna leh Pathian Ta theihna lama thukituaka, pichinga, Kris tangchinna latdan banga i vek ua i hongom masiaha ding ahi.
13na hivyo sote tuufikie umoja wa imani na kumjua Mwana wa Mungu; tuwe watu waliokomaa na kuufikia utimilifu wake Kristo mwenyewe.
14Huchi-a mihingte diklouhna zekhemna banga lepchiah pila khem tawmtawma oma thuhilhna huih chitenga langkhat langkhata sep leh mut lengleng, naupang i hih nawn louhna dingun.
14Basi, hatutakuwa tena kama watoto, tukitupwa na kupeperushwa huko na huko kwa kila upepo wa mafundisho wanayozua watu wadanganyifu, ili wawapotoshe wengine kwa hila.
15Itnaa thutak gena, bangkima Amah, lupen, Kris ngeia i khanlet jawk ding uh ahi.
15Ila, sisi tukisema ukweli kwa moyo wa mapendo tutakua zidi katika kila jambo kulingana na Kristo ambaye ndiye kichwa;
16Amah akipan pumpi tengteng, kizopna chiteng sep jiaka, lemtaka suktuah leh kizomkhawma, hiang chihin sep dingdan bangtaka a sep chiangin pumpi a khanga itna ah amah leh amah akilam tou hi.
16chini ya uongozi wake, viungo vyote vya mwili hushikamana pamoja, na mwili wote hutegemezwa kwa msaada wa viungo vyake. Basi, kila kiungo kikitekeleza kazi yake ipasavyo, mwili wote hukua na kujijenga katika upendo.
17Tuin hiai ka genin Toupa ah kontheisak ahi, Jentelte a lungsim ginatlouhna uh pu-a a om bangun, na om nawn mahmah ding uh ahi kei;
17Basi, kwa jina la Bwana, nawaonyeni: msiishi tena kama watu wasiomjua Mungu, ambao fikira zao zimekuwa upuuzi mtupu,
18Amau tuh a lungtang uh tak jiaka theihtheihlouhna jiakin Pathian hinna theihtheihna a pan posiahin a om uhi;
18na akili zao zimo gizani. Wako mbali na uzima wa Mungu, kwa sababu ya upumbavu ulio ndani yao na ukaidi wao.
19A khenggawpta ua, sianglou chiteng hihna lama huaihamin jautatna ah a kipumpiak uhi.
19Wamepotoka na hawana aibu, wamejitosa katika ufisadi; hufanya kwa pupa kila aina ya mambo ya aibu.
20Nou jaw huchibangin kris thu na zil kei uhi!
20Lakini ninyi hamkujifunza hivyo juu ya Kristo.
21A thu jaa amaha thuhilhna om khin na hih peuhmah uleh, jesua thutak a om bangin.
21Ni dhahiri kwamba mlisikia barabara habari zake, na mkiwa wafuasi wake mkafundishwa ukweli ulivyo katika Yesu.
22Na pianken lui uh, na nidanglai hindan uh segawpsa suahkhia unla,
22Basi, acheni mwenendo wenu wa awali, yaani ule utu wenu wa kale uliokuwa unaangamizwa kwa tamaa zake danganyifu.
23Na lungsim Kha uah a thakin hongom unla,
23Jirekebisheni upya rohoni na katika fikira zenu.
24Pianken thak, diktatna leh sianthounaa Pathian batpiha siampen silh un.
24Vaeni hali mpya ya utu ambayo imeumbwa kwa mfano wa Mungu na ambayo hujionyesha katika maisha ya kweli ya uadilifu na utakatifu.
25Huchiin, juaugen tawpsanin, noumau inveng kiangah thudiktak gen chiat un; kihiang tuah chiat na hi ngal ua.
25Kwa hiyo, acheni uongo. Kila mmoja anapaswa kumwambia mwenzake ukweli, maana kila mmoja wetu ni kiungo cha mwili wa Kristo.
26Heh unla, khelh jaw khial kei un; na hehna uh niin tum pih kei hen.
26Kama mkikasirika, msikubali hasira yenu iwafanye mtende dhambi, na wala msikae na hasira kutwa nzima.
27Diabol leng mun awn sam kei un.
27Msimpe Ibilisi nafasi.
28Gutain gu nawnta kei hen; tasam kianga piak ding a neih theihna dingin, a khuta thil hoih semin gim jaw hen.
28Aliyekuwa akiiba, asiibe tena, bali na aanze kufanya kazi njema kwa mikono yake, apate kuwa na kitu cha kumsaidia mtu aliye maskini.
29Thu sia peuhmah na kam ua kipanin pawt kei hen; a khawk dan bang jela bawl hoih dingin thu hoih peuhmah pawt jaw hen, a ngaikhete adinga hehpihna a hohnghih theihna dingin.
29Maneno mabaya hata yasisikike kamwe miongoni mwenu; kila mara maneno yenu yawe ya kufaa na ambayo hujenga na kuwasaidia wengine, ili yawaneemeshe wasikilizaji wenu.
30Huan, Pathian Kha Siangthou tuh hihlungkham kei un, tatna nia dingin amahah chiamteh na hi uhi.
30Msimhuzunishe Roho Mtakatifu wa Mungu maana Roho huyo ni alama ya Mungu kwenu kwamba ninyi ni watu wake, na thibitisho kwamba siku itakuja ambapo Mungu atawakomboeni.
31Khatna bang, thangpaihna bang, hehna bang, hanna bang, gensiatna tengteng tawpsanin omta hen, gitlouhna tengteng toh.Huan, kihehpih chiata lainatna neiin om unla, Pathianin Krisa a honngaihdam bangin, noumau leng kingaidam tuah chiat un.
31Basi, achaneni na uhasama, chuki, hasira, kelele, matusi! Achaneni na kila uovu!
32Huan, kihehpih chiata lainatna neiin om unla, Pathianin Krisa a honngaihdam bangin, noumau leng kingaidam tuah chiat un.
32Muwe na moyo mwema na wenye kuhurumiana; kila mmoja na amsamehe mwenzake kama naye Mungu alivyowasamehe ninyi kwa njia ya Kristo.