1Huchiin, unau siangthou, van sapna tangsamte aw, I thugina Sawltak leh Siampu Lian, Jesu tuh, ngaihtuah un;
1Ndugu zangu watu wa Mungu ambao mmeitwa na Mungu, fikirini juu ya Yesu ambaye Mungu alimtuma awe Kuhani Mkuu wa imani tunayoiungama.
2Pathian inkuante tengteng lakah Mosi tuh a muanhuai bangmahin, amah tuh a seppa lakah amuanhuai ahi.
2Yeye alikuwa mwaminifu kwa Mungu aliyemteua kufanya kazi yake kama vile Mose alivyokuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu.
3Insunga papen tuh ainkuante sanga apahtawi jawk bang ngei un, amah tuh Mosi sanga thupi jawkna sem mu dia kilawma seh a hita ngala.
3Mjenzi wa nyumba hupata heshima zaidi kuliko hiyo nyumba yenyewe. Hali kadhalika naye Yesu anastahili heshima kubwa zaidi kuliko Mose.
4Inkuan chihin papen kuahiam bek a nei chiat ngal ua; bangkim papen bel Pathian ahi.
4Kila nyumba hujengwa na mjenzi fulani--na Mungu ndiye mjenzi wa vitu vyote.
5Huan, huai nunga thugen nalai dingte theihsakna dingin, Mosi tuh Pathian inkuante tengteng laka nasempa injaw a muanhuai ngei hi;
5Mose alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Bwana kama mtumishi, na alinena juu ya mambo ambayo Mungu atayasema hapo baadaye.
6Kris bel Pathian inkuante tunga Tapa-in a muanhuai ahi. A inkuante tuh eite I hi uhi, atawp tana I hansanna leh I lametna suanna kiptaka I vom hoih photphot leh.
6Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana mwenye mamlaka juu ya nyumba ya Mungu. Sisi ni nyumba yake kama tukizingatia uhodari wetu na uthabiti wetu katika kile tunachotumainia.
7Huchiin, Kha Siangthou gen bangin, Tuni a a aw na jak chiangun,
7Kwa hiyo, basi, kama asemavyo Roho Mtakatifu: "Kama mkisikia sauti ya Mungu leo,
8Gamdaia zeet na nia hel bang un, na lungtang uh khauh sak kei un;
8msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama wazee wenu walivyokuwa wakati walipomwasi Mungu; kama walivyokuwa siku ile kule jangwani,
9Huailai ah tuh na pi leh pute un honjeet in hon khem ua, kum sawmli sunga ka thil hihte a mu ua;
9Huko wazee wenu walinijaribu na kunichunguza, asema Bwana, ingawa walikuwa wameyaona matendo yangu kwa miaka arobaini.
10Huchiin huai suan te tungah ka lung hita keia, a lungtangun a ngaihtuah khial gige ua, Kalampite leng a theikei uhi, ka chi a,
10Kwa sababu hiyo niliwakasirikia watu hao nikasema, Fikira za watu hawa zimepotoka, hawajapata kamwe kuzijua njia zangu.
11Ka thangpaihna aka kichiam bangin ka khawlna ah alut kei ding uh, chiin.
11Basi, nilikasirika, nikaapa: Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko."
12Unaute aw, pilvang un, huchi lou in jaw, Pathian hing tawpsan ding in na lak uah kuapeuh sungah ginlouhna lungtang gilou ahong om kha ding hi.
12Basi ndugu, jihadharini asije akawako yeyote miongoni mwenu aliye na moyo mbaya hivyo na asiyeamini hata kujitenga na Mungu aliye hai.
13Tuniin achih lai un niteng in ki hasuan tuah jaw un, huchia nalak ua mi kuamah khelhna khemhat jiaka hihkhawla na om louhna ding un,
13Maadamu hiyo "Leo" inayosemwa katika Maandiko bado inatuhusu sisi, mnapaswa kusaidiana daima, ili mtu yeyote miongoni mwenu asidanganywe na dhambi na kuwa mkaidi.
14Kris neite ina hita ngal ua, i ginna pen kipat na tuh a tawptan a kiptaka I vom hoih phot leh,
14Maana sisi tunashirikiana na Kristo ikiwa tutazingatia kwa uthabiti tumaini tulilokuwa nalo mwanzoni.
15Tuniin a aw nazak chiangun a hel lai bang un, na lungtang uh khauhsak kei un. a kichih laiteng.
15Maandiko yasema hivi: "Kama mkisikia sauti ya Mungu leo, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama wazee wenu walivyokuwa wakati walipomwasi Mungu."
16Ahihleh, kuate ahi ua theinapi a helte? Aigupta akipana Mosi pi pawt tengteng hi lou uhia?
16Ni akina nani basi, waliosikia sauti ya Mungu wakamwasi? Ni wale wote walioongozwa na Mose kutoka Misri.
17Huan, kuate tungah ahia, kum sawmli sung a alunghihlouh? Hihkhialte a luang uh gamdaia puk tate tungah hilou hia?
17Mungu aliwakasirikia akina nani kwa miaka arobaini? Aliwakasirikia wale waliotenda dhambi, maiti zao zikatapakaa kule jangwani.
18Huan, thu mangloute kiangah kia loungal kua kiangah ahia a khawlna a lut lou dinga a kichiam?Huchiin, ginlahna jiakin a lut theita kei uh chih I thei uhi.
18Mungu alipoapa: "Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko," alikuwa anawasema akina nani? Alikuwa anasema juu ya hao walioasi.
19Huchiin, ginlahna jiakin a lut theita kei uh chih I thei uhi.
19Basi, twaona kwamba hawakuingia huko kwa sababu hawakuamini.