1Paikan Ankuanglui kipat main, Jesun, hiai khovel nusiaa Pa kianga a pai hun hongtungta chih a theia; hiai khovel amah-ate na itkhinin a tawp phain a it hi.
1Ilikuwa kabla ya sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua kwamba saa yake ya kuondoka ulimwenguni na kwenda kwa Baba ilikuwa imefika. Alikuwa amewapenda daima watu wake walioko duniani; naam, aliwapenda mpaka mwisho!
2Huan, nitak annek laiin, diabolin Juda Iskariot, Simon tapa lungtanga Jesu juausana-matsak lungsim a koihsak khitnungin,
2Basi, Yesu na wanafunzi wake walikuwa mezani kwa chakula cha jioni. Ibilisi alikwisha mtia Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti, nia ya kumsaliti Yesu.
3Jesun, Pa-in a khut ah thil bangkim a peta chih leh Pathian akipana hongpai ahia, Pathian kianga pai ding ahi chih theigigein,
3Yesu alijua kwamba Baba alikuwa amemkabidhi kila kitu, na kwamba alikuwa ametoka kwa Mungu na anarudi kwa Mungu.
4A nitakan um tuh a dinga, a puante a koiha, kinulna puan a laa, tenga.
4Basi, Yesu aliondoka mezani, akaweka kando vazi lake, akachukua kitambaa na kujifunga kiunoni.
5Huan, maiphiatkuangah tui a sunga, nungjuite khe a silta a, kinulna puan a tenin a nul jel hi.
5Kisha akatia maji katika bakuli, akaanza kuwaosha wanafunzi wake miguu na kuipangusa kwa kile kitambaa alichojifungia.
6Huchiin, Simon Peter kiangah a hong a. Aman, Toupa, nang telin ka khe na sil dia hia? a chi a.
6Basi, akamfikia Simoni Petro; naye Petro akasema, "Bwana, wewe utaniosha miguu mimi?"
7Jesun a kiangah, Ka thilhih tunah na theikei: himahleh tunung chiangin na thei ding, a chi a, a dawnga.
7Yesu akamjibu, "Huelewi sasa ninachofanya lakini utaelewa baadaye."
8Peterin a kiangah, Ka khe na sil kei hial ding, a chi a. Jesun a kiangah, Kon sil kei leh ka kiangah tan na neikei ding, a chi a.
8Petro akamwambia, "Wewe hutaniosha miguu kamwe!" Yesu akamjibu, "Nisipokuosha hutakuwa na uhusiano nami tena."
9Simon Peterin a kiangah, Toupa, ka khe kia hilouin, ka khut leh ka lutang leng aw, a chi a,
9Simoni Petro akamwambia, "Bwana, nioshe, si miguu tu, bali na mikono yangu na kichwa pia."
10Jesun a kiangah, Kisil khinsa a khe lou ngal sil a kiphamoh kei, a pumpiin a siang; nou na siang uh, na vek un jaw ahi kei, a chi a.
10Yesu akamwambia, "Aliyekwisha oga hana lazima ya kunawa isipokuwa miguu, maana amekwisha takata mwili wote. Ninyi mmetakata, lakini si nyote."
11A mansakpa ding a thei ngala; huaijiakin, Na vek un na siang kei uh, a chi ahi.
11(Yesu alimjua yule ambaye atamsaliti, ndiyo maana alisema: "Ninyi mmetakata, lakini si nyote.")
12Huchiin, a khe tuh a sila, a puante a laka, a tut nawn in a kiang uah, Na tung ua ka thil hih bang chhihna ahia?
12Alipokwisha waosha miguu na kuvaa tena vazi lake, aliketi mezani, akawaambia, "Je, mmeelewa hayo niliyowatendeeni?
13Nou Sinsakpa leh Toupa non chi ua; na chi dik uhi, ka hi ngei tak a.
13Ninyi mwaniita Mwalimu na Bwana, nanyi mwasema vyema, kwa kuwa ndimi.
14Kei Toupa leh Sinsakpan, na khe uh ka sil leh, nou leng na khe uh na kisil sak ding uh ahi.
14Basi, ikiwa mimi niliye Bwana na Mwalimu, nimewaosha ninyi miguu, nanyi pia mnapaswa kuoshana miguu.
15Na tung ua ka hih bangin, nou leng na hih samna ding un, hihdingdan honhilh ka hi ngala.
15Nimewapeni mfano, ili nanyi pia mfanye kama nilivyowafanyieni.
16Chihtaktakin, chihtaktakin kon hilh ahi, Sikha a pu sangin a thupizo kei; sawltak leng a sawlpa sangin a thupizo sam kei hi.
16Kweli nawaambieni, mtumishi si mkuu zaidi kuliko bwana wake, wala mtume si mkuu zaidi kuliko yule aliyemtuma.
17Huai thilte na theih ua, na hih uleh hampha nahi uh.
17Basi, ikiwa mwayajua hayo, mtakuwa na heri mkiyatekeleza.
18Na vek ua thu ka gen kei a; ka telte ka thei; himahleh, huai tuh, Ka tanghou nepan ka tungah a khetul a likta, chih, laisiangthou a hongtun theihna ding ahi.
18"Haya nisemayo hayawahusu ninyi nyote. Mimi nawajua wale niliowachagua. Lakini lazima yatimie Maandiko Matakatifu yasemayo: Yule aliyeshiriki chakula changu amegeuka kunishambulia.
19Tuin a hongtun main kon hilh ahi, a hongtun hun chia kei amah ka hi chih na gintak theihna ding un.
19Mimi nimewaambieni mambo haya sasa kabla hayajatokea, ili yatakapotokea mpate kuamini kuwa mimi ndimi.
20Chihtaktakin, chihtaktakin, kon hilh ahi, Kuapeuh ka sawl kipahpih tuh, keimah honkipahpih ahi; kuapeuh kei honkipahpih tuh, honsawlpa kipahpih ahi, a chi a.
20Kweli nawaambieni anayempokea yule ninayemtuma anaponipokea mimi; na anayenipokea mimi, anampokea yule aliyenituma."
21Jesun huchi banga a genkhitin, a lungsim a mangbang a, Chihtaktakin, chihtaktakin kon hilh ahi, na lak ua mi khatin kei honmansak ding, chiin a theisakta a.
21Alipokwisha sema hayo, Yesu alifadhaika sana rohoni, akasema wazi, "Kweli nawaambieni, mmoja wenu atanisaliti!"
22Huan, nungjuiten a chihtuampen a theikei ua, a kien chiat ua.
22Wanafunzi wakatazama wasiweze kabisa kujua anasema nani.
23Huan, a nungjuite laka khat, Jesun a itpa, dohkan sikah Jesu angsung ah kingaiin a om a.
23Mmoja wa wanafunzi, ambaye Yesu alikuwa anampenda sana, alikuwa ameketi karibu na Yesu.
24Huan, Simon Peterin huai mi kiangah, Kua thu pen ahia a gen, honhilh dih, chiin a mitmei a.
24Basi, Simoni Petro akamwashiria na kusema: "Mwulize anasema juu ya nani."
25Huan, Jesu awm ngai mahin a awn pheia, a kiangah, Toupa, kuapen ahia? a chi a.
25Mwanafunzi huyo akasogea karibu zaidi na Yesu, akamwuliza, "Bwana, ni nani?"
26Huan, Jesun, Tanghou them ka diah saka, ka piakpa ahi ding, a chi a, a dawnga. Huchiin, tanghou them a diah nungin, Iskariot, Simon tapa Juda kiangah a pai a.
26Yesu akajibu, "Yule nitakayempa kipande cha mkate nilichochovya katika sahani, ndiye." Basi, akatwaa kipande cha mkate, akakichovya katika sahani, akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti.
27Huan, tanghou them a piak nungin Setan a sungah a lutta a. Huchiin, Jesun a kiangah, Na hih ding hih meng in, a chi a.
27Yuda alipokwisha pokea kipande hicho, Shetani akamwingia. Basi Yesu akamwambia, "Unachotaka kufanya, kifanye haraka!"
28Huan, dohkan sika miten kuamahin bang jiaka chi ahi chih a theikei uh.
28Lakini hakuna hata mmoja wa wale waliokaa pale mezani aliyefahamu kwa nini alikuwa amemwambia hivyo.
29A khenin, Judain dangka ip a vom jiakin, Jesun, Ankuangluinaa dingin i thil kiphamoh peuh lei in, a chi hiam, mi gentheite kiangah banghiam piak ding, a chi hiam a sa uh.
29Kwa kuwa Yuda alikuwa na wajibu wa kuutunza mfuko wa fedha, baadhi yao walidhani kwamba Yesu alikuwa amemwambia anunue vilivyohitajiwa kwa sikukuu, au kwamba alikuwa amemwambia akatoe chochote kwa maskini.
30Huan, aman tanghou them a la a, a pawt khe pah a; huai tuh jan lai ahi.
30Basi, Yuda alipokwisha twaa kile kipande cha mkate, akatoka nje mara. Na ilikuwa usiku.
31Huchiin a pawt nungin, Jesun a gen a, Tuin Mihing Tapa pahtawiin a om, huna, amah ah Pathian leng pahtawiin a om ahi.
31Baada ya Yuda kuondoka, Yesu akasema, "Sasa Mwana wa Mtu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake.
32Amaha Pathian pahtawia a om leh amah leng Pathianin amah ah a pahtwi ding, a pahtawi pah ngal ding hi.
32Na kama utukufu wa Mungu umefunuliwa ndani ya Mwana, basi, naye Mungu ataudhihirisha utukufu wa Mwana ndani yake mwenyewe, na atafanya hivyo mara.
33Naute aw, sawt lou chik na kiang uah ka omlai tadih a. Nou non zong ding uh; huan, Judate kianga, Ka paina dingah nou na hongpai theikei ding uh, chih ka gen bangin, tuin huchi mahbangin na kiang uah ka gen ahi.
33"Watoto wangu, bado niko nanyi kwa muda mfupi tu. Mtanitafuta, lakini sasa nawaambieni yale niliyowaambia viongozi wa Wayahudi: Niendako ninyi hamwezi kwenda!
34Thuchiam thak kon pia ahi, kiit un; ken nou kon it bangin, nou leng kiit un.
34Nawapeni amri mpya: pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda ninyi.
35Na kiit uleh, mi tengtengin ka nungjuite nahi uh chih huai ah a thei ding uh, a chi a.
35Mkipendana, watu wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu."
36Simon Peterin a kiang ah, Toupa, koia hoh ding na hia? a chi a, Jesun, Ka hohna dingah nang tuin non jui theikei ding; tunung chiah jaw nonjui ding, a chi a, a dawng a.
36Simoni Petro akamwuliza, "Bwana, unakwenda wapi?" Yesu akajibu, "Niendako huwezi kunifuata sasa, lakini utanifuata baadaye."
37Peterin a kiangah, Toupa, bangdingin ahia tua leng kon zuih theih louh ding? Nangmah jiakin ka hinna ka pai ding, a chi a.Jesun a dawnga, Keimah jiakin na hinna na pai ding maw? Chihtaktakin, chihtaktakin kon hilh ahi, nang thum vei non kitheihmohbawl main, ak a khuang kei ding.
37Petro akamwambia "Bwana, kwa nini siwezi kukufuata sasa? Niko tayari kufa kwa ajili yako!"
38Jesun a dawnga, Keimah jiakin na hinna na pai ding maw? Chihtaktakin, chihtaktakin kon hilh ahi, nang thum vei non kitheihmohbawl main, ak a khuang kei ding.
38Yesu akajibu, "Je, uko tayari kweli kufa kwa ajili yangu? Kweli nakwambia, kabla jogoo hajawika utanikana mara tatu!"