1Huai nungin, Tiberia dilah Jesu a nungjuite kiangah a kilak nawna; hichi bangin a kilaka;
1Baada ya hayo Yesu aliwatokea tena wanafunzi wake kando ya ziwa Tiberia. Aliwatokea hivi:
2Simon Peter te, Thoma Didum a chih te uh, Galili gama Kana khuaa Nathanael te, Zebedai tapa nihte, a nungjui dang nihte toh a om khawm ua.
2Simoni Petro, Thoma (aitwaye Pacha), na Nathanieli mwenyeji wa Kana Galilaya, wana wawili wa Zebedayo na wanafunzi wake wengine wawili, walikuwa wote pamoja.
3Simon Peterin a kiang uah, Ngasa beng dingin ka kuan dek, a chi a. Amau a kiangah, Kou leng na kiangah ka hong sam ding uh, a chi ua. Huan, a pawt khia ua, longah a tuang ua, huai janin bangmah a man kei uhi.
3Simoni Petro aliwaambia, "Nakwenda kuvua samaki." Nao wakamwambia, "Nasi tutafuatana nawe." Basi, wakaenda, wakapanda mashua, lakini usiku huo hawakupata chochote.
4Huan, phalvakin Jesu piautak ah a dinga; himahleh a nungjuiten Jesu ahi chih a theikei uh.
4Kulipoanza kupambazuka, Yesu alisimama kando ya ziwa, lakini wanafunzi hawakujua kwamba alikuwa yeye.
5Huan, Jesun a kiang uah, Naute aw, nekding banghiam na nei uh hia? a chi a. Amau a kiangah, Nei lou, a chi ua, a dawng ua.
5Basi, Yesu akawauliza, "Vijana, hamjapata samaki wowote sio?" Wao wakamjibu, "La! Hatujapata kitu."
6Huan, aman a kiang uah, Long sik taklamah len pai le uchin khenkhat na man ding uh, a chi a. Huan, a pai ua, ngasa tam jiakin a kai khe zouta kei ua.
6Yesu akawaambia, "Tupeni wavu upande wa kulia wa mashua nanyi mtapata samaki." Basi, wakatupa wavu lakini sasa hawakuweza kuuvuta tena kwa wingi wa samaki.
7Huchiin, nungjui Jesun a itpan, Peter kiangah, Toupa ei ve, a chi a. Huchiin, Toupa ahi chih Simon Peterin a theih takin, a puannak a tenga, (vuaktanga om ahi ngala), dilah a tawm kheta hi.
7Hapo yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akamwambia Petro, "Ni Bwana!" Simoni Petro aliposikia ya kuwa ni Bwana, akajifunga vazi lake (maana hakuwa amelivaa), akarukia majini.
8Himahleh, nungjuiten long neu chikin, len ngasa a dim toh kai kawmin a honjuan ua, gama kipanin a gamla ngal kei ua, tong zanih hiam phet ahi a.
8Lakini wale wanafunzi wengine walikuja pwani kwa mashua huku wanauvuta wavu uliojaa samaki; hawakuwa mbali na nchi kavu, ila walikuwa yapata mita mia moja kutoka ukingoni.
9Huan, gama a suah tak-un, huai ah meihola mei tohsa a mu ua, a tunga ngasa leh tanghou em toh.
9Walipofika nchi kavu waliona moto wa makaa umewashwa na juu yake pamewekwa samaki na mkate.
10Huan, Jesun a kiang uah, Tuin na ngasa mat uh a khen honla tou un, a chi a.
10Yesu akawaambia, "Leteni hapa baadhi ya samaki mliovua."
11Huchiin Simon Peter a va tuanga, len ngasa lian pipia dim tui geiah a kai khiaa, ja leh sawmnga leh thum ahi; huchi lawmlawm om mahleh len a kek tuan kei a.
11Basi, Simoni Petro akapanda mashuani, akavuta hadi nchi kavu ule wavu uliokuwa umejaa samaki wakubwa mia moja na hamsini na watatu. Na ingawa walikuwa wengi hivyo wavu haukukatika.
12Huan, Jesun a kiang uah, Jingan na ne un, a chi a. Huan, nungjuite lakah kuamahin a kiangah, Kua na hia? chiin a dong ngam kei uh, Toupa ahi chih a thei ngal ua.
12Yesu akawaambia, "Njoni mkafungue kinywa." Hakuna hata mmoja wao aliyethubutu kumwuliza: "Wewe ni nani?" Maana walijua alikuwa Bwana.
13Huan, Jesu a hongpaia, tanghou a la a, a kiang uah a pia a, ngasate leng huchi bangmahin a pe sam a.
13Yesu akaja, akatwaa mkate akawapa; akafanya vivyo hivyo na wale samaki.
14Huai tuh Jesu misi laka kipana a thohnawn nunga, a nungjuite kianga a kilak a thum veina ahi.
14Hii ilikuwa mara ya tatu Yesu kuwatokea wanafunzi wake baada ya kufufuka kutoka wafu.
15Huan, jingan a nek khit un, Jesun, Simon Peter kiangah, Simon, Johan tapa, nang hiaite sangin kei non it jaw hia? a chi a. Aman a kiangah, He, Toupa, kon it chih na thei hi, a chi a. Aman a kiangah, He, Toupa, kon it chih na thei hi, a chi a, Aman a kiangah, Ka belamnoute vak in, a chi a.
15Walipokwisha kula, Yesu alimwuliza Simoni Petro, "Simoni, mwana wa Yohane! Je, wanipenda mimi zaidi kuliko hawa?" Naye akajibu, "Naam, Bwana; wajua kwamba mimi nakupenda." Yesu akamwambia, "Tunza wana kondoo wangu."
16Huan, a nihveina din, a kiangah, Simon, Johan tapa, nang kei non it hia? a chi nawna. Aman a kiangah, He, Toupa, kon it chih na thei hi, a chi nawna. Aman a kiang ah, Ka belamte chingin, a chi a.
16Kisha akamwambia mara ya pili, "Simoni mwana wa Yohane! Je, wanipenda?" Petro akamjibu, "Naam, Bwana; wajua kwamba nakupenda." Yesu akamwambia, "Tunza kondoo wangu."
17Huan, a thumveina din a kiangah, Simon, Johan tapa, nang kei non it hia? a chi a. Huan, thumveina a, Nang kei non it hia? a kianga a chih jiakin Peter a lungkhama, a kiangah, Toupa, bangkim na theia, kon it ahi, chih na thei hi, a chi a, Jesun a kiangah, Ka belamte vak in.
17Akamwuliza mara ya tatu, "Simoni mwana wa Yohane! Je, wanipenda?" Hapo Petro akahuzunika kwa sababu alimwuliza mara ya tatu: "Wanipenda?" akamwambia, "Bwana, wewe wajua yote; wewe wajua kwamba mimi nakupenda." Yesu akamwambia, "Tunza kondoo wangu!
18Chihtaktakin, chihtaktakin kon hilh ahi, na naupan laiin na taiah na kigaka, na utna peuhah na hoh a; himahleh, na upat hun chiangin na khut na jak dinga, mi dangin a hon gak sak ding uh, na ut louhna lam ah a honkai ding uh, a chi a.
18Kweli nakwambia, ulipokuwa kijana ulizoea kujifunga mshipi na kwenda kokote ulikotaka. Lakini utakapokuwa mzee utanyosha mikono yako, na mtu mwingine atakufunga na kukupeleka usikopenda kwenda."
19Huai thu tuh bangchidana siin ahia Pathian a pahtawi ding chih theihsakna dinga a gen ahi. Huan, huai a gen khitin, a kiangah, Honjui in, a chi a.
19(Kwa kusema hivyo, alionyesha jinsi Petro atakavyokufa na kumtukuza Mungu.) Kisha akamwambia, "Nifuate."
20Huan, Peter a kiheia, Jesun nungjui a itpa, nitakan nek laia a awm ngaia hongawn phei a, a mansakpa ding kua pen ahia? chipan, a honjui a mu a.
20Hapo Petro akageuka, akamwona yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda, anafuata (Huyu mwanafunzi ndiye yule ambaye wakati wa chakula cha jioni, alikaa karibu sana na Yesu na kumwuliza: "Bwana ni nani atakayekusaliti?")
21Huan, Peterin amah a muh takin, Jesu kiangah, Toupa, hiai min bang a hih dia? a chi a.
21Basi, Petro alipomwona huyo akamwuliza Yesu, "Bwana, na huyu je?"
22Jesun a kiangah, Ka hongnawn tana om nilouh din houh deih leng, huai nang bang lunghimoh zenzen? Nang honjui mai in, a chi a.
22Yesu akamjibu, "Kama nataka abaki mpaka nitakapokuja, yakuhusu nini? Wewe nifuate mimi."
23Huchiin, huai nungjuipa tuh si lou dingin a thu unaute lakah a thangta a; himahleh, Jesun a si kei ding chih a kiangah a gen ngal keia, Ka hong nawn tana om nilouh din houh deih leng huai nang bang lunghimoh zenzen? a chi lel ahi ngala.
23Basi, habari hiyo ikaenea miongoni mwa wale ndugu kwamba mwanafunzi huyo hafi. Lakini Yesu hakumwambia kwamba mwanafunzi huyo hafi, ila, "Kama nataka abaki mpaka nitakapokuja, yakuhusu nini?"
24Huai nungjui tuh hiai thu theisakpa leh gelhpa ahi; huan a thu theihsak a dik chih I thei uhi.Huan, hiaite lou Jesu thilhih a dang tampi a om lai; huaite gelh siang vek ding hi leh, laibu gelh ding tengteng khovel ah leng tain ka gingta kei hi.
24Huyo ndiye yule aliyeshuhudia mambo haya na kuyaandika. Nasi twajua kwamba aliyoyasema ni kweli.
25Huan, hiaite lou Jesu thilhih a dang tampi a om lai; huaite gelh siang vek ding hi leh, laibu gelh ding tengteng khovel ah leng tain ka gingta kei hi.
25Kuna mambo mengine mengi aliyofanya Yesu, ambayo kama yangeandikwa yote, moja baada ya lingine, nadhani hata ulimwengu wenyewe usingetosha kuviweka vitabu ambavyo vingeandikwa.