Paite

Swahili: New Testament

Luke

19

1Huan, Jesu Jeriko khua ah a luta, pai suak din a kisa a.
1Yesu aliingia mjini Yeriko, akawa anapita katika njia za mji huo.
2Huan, ngai in, mi khat a min Zakai a om a; huai mi tuh siahkhon heutu ahi a, amah leng a hau ngiala.
2Kulikuwa na mtu mmoja mjini, jina lake Zakayo ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3Huan, Jesu mi bangchi bang hiam chih, muh a tuma; amah lah a niam ngala, mipi jiakin, a mu theikei a.
3Alitaka kuona Yesu alikuwa nani, lakini kwa sababu ya umati wa watu, na kwa vile alikuwa mfupi, hakufaulu.
4Huchiin, a matai a, a en dingin theipi kung ah a kaha; huai lampi tuh a hontot ding ahi ngala.
4Hivyo, alitangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona Yesu, kwa maana alikuwa apitie hapo.
5Huan, Jesu huai mun a tunin a daka, a kiangah, Zakai, hongkum meng in; tuniin na ina tung ding ka hi, a chi a.
5Basi, Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, "Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako."
6Huan kintakin a kuma, kipaktakin amah tuh a zintuntaa.
6Zakayo akashuka haraka, akamkaribisha kwa furaha.
7Huan huai amuh tak un, a vek un, Mi khialte kianga tung dingin a lutta ve, a chi ua, a phun ua.
7Watu wote walipoona hayo, wakaanza kunung'unika wakisema, "Amekwenda kukaa kwa mtu mwenye dhambi."
8Huan, Zakai a dinga, Toupa kiang ah, Ngai in, Toupa, ka sum kimkhat tagahte kiangah kape dinga; huan, kua lakah leng thil bangpeuh na negu taleng, a leh liin ka din ding, a chi a.
8Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, "Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne."
9Huan, Jesun, akiangah, Tuniin hiai in ah hotdamna a hongtungta, amah leng Abraham tapa ahi ngala.
9Yesu akamwambia, "Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa vile huyu pia ni wa ukoo wa Abrahamu.
10Mangthangte zonga hotdam dingin Mihing Tapa a hongpai, ahi him hi, a chi a.
10Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa waliopotea."
11Huan, huai thute a ngaihkhiak lai un, Jerusalem khua a naih tak jiak leh Pathian gam honglang pah ding hia a gin jiak un gentehna thu a gen tela.
11Wakati watu walipokuwa bado wanasikiliza hayo, Yesu akawaambia mfano. (Hapo alikuwa anakaribia Yerusalemu, na watu wale walidhani kwamba muda si muda, Ufalme wa Mungu ungefika.)
12Huchiin hiai thu khawng a gena; Mi Hoih kuahiam gam ukna thu laa hongkik nawn dingin kho gamla takah a hoha.
12Hivyo akawaambia, "Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa kifalme aliyefanya safari kwenda nchi ya mbali ili apokee madaraka ya ufalme, halafu arudi.
13A hoh dingin a sikhate sawm a sama, a kiang uah dangkaeng sawm a pia a, a kianguah, Ka hongtun nawn masiah hiaiin sum na sin un, achia.
13Basi, kabla ya kuondoka aliwaita watumishi wake kumi, akawapa kiasi cha fedha kila mmoja na kumwambia: Fanyeni nazo biashara mpaka nitakaporudi.
14Himahleh, a khuaten a hua ua, Hiai mi katung ua vaihawm dingin ka deih kei uh, chiin a nungah thu akha ua.
14Lakini wananchi wenzake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende wakaseme: Hatumtaki huyu atutawale.
15Huan, hichi ahia, gam ukna thu tuh a laka, a hong kik nawn in, a sikha sum a piakte, a hekpung dan uh theihna din, a sam saka.
15"Huyo mtu mashuhuri alirudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, na mara akaamuru wale watumishi aliowapa zile fedha waitwe ili aweze kujua kila mmoja amepata faida gani.
16Huan, a masapen a hongpaia, Toupa, na dangka sawmin a pung, a chi a.
16Mtumishi wa kwanza akatokea, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara kumi ya zile fedha ulizonipa.
17Huan aman, a kiangah, Sikha hoih, nahih hoih e; tawm chik tunga na ginom jiakin kho sawm tungah heutuin om in, a chi a.
17Naye akamwambia: Vema; wewe ni mtumishi mwema. Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi!
18Huan, a zom a hongpaia, Toupa, na dangka ngain a pung e, a chi a.
18Mtumishi wa pili akaja, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara tano ya zile fedha ulizonipa.
19Huan, aman, amah kiangah leng, Nang leng kho nga tungah heutuin omin, a chi a.
19Naye akamwambia pia: Nawe utakuwa na madaraka juu ya miji mitano.
20Huan, mi dang a hongpaia, Toupa, en in, hiai na dangka: khoulnulna puanin ka kem kinken ahi;
20"Mtumishi mwingine akaja, akasema: Chukua fedha yako; niliificha salama katika kitambaa,
21Mi mawktak na hih jiakin kon kihta ahi; na koih louh leng na la naka, na tuh louh leng na at nak ngala, a chi a.
21kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Wewe ni mtu ambaye huchukua yasiyo yako, na huchuma ambacho hukupanda.
22Huan, aman, a kiangah, sikha gilou, na paukam suak ngeiin kon siam louh ding. Mi mawktat ka hiha, ka koih louh leng ka lak naka, ka tuh louh leng ka at nak na thei maw?
22Naye akamwambia: Nakuhukumu kutokana na msemo wako, ewe mtumishi mbaya! Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, ambaye huchukua yasiyo yangu na kuchuma nisichopanda.
23Huchi a hih leh, bang dia ka sum sumina na koih lou? huchiin ka hongpaiin a pung toh ka lak ding ahi, a chi a.
23Kwa nini basi, hukuiweka fedha yangu benki, nami ningeichukua pamoja na faida baada ya kurudi kwangu?
24Huan, a kianga dingte kiangah, A dangka lak sak unla, dangka sawm neipa kiangah pia un, a chi a.
24Hapo akawaambia wale waliokuwa pale: Mnyang'anyeni hizo fedha, mkampe yule aliyepata faida mara kumi.
25Huan, amau, a kiangah, Toupa, aman jaw dangka sawm a nei a ka, a chi ua.
25Nao wakamwambia: Lakini Mheshimiwa, huyo ana faida ya kiasi hicho mara kumi!
26Ka honchi ahi, a nei peuh piakbehlap ahi ding a, a neilou tuh a neih sun leng lak sak ahi ding hi.
26Naye akawajibu: Kila aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27Himahleh, hiai ka galte a tung ua vaihawm dia hondeih lou, honpi unla, ka maah that un, a chi a, a chi a.
27Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu."
28Huan, huchibang thu agen khitin Jerusalem kho lam naih tou in ma a kaia.
28Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
29Huan hichi ahia, Bethphage leh Bethani kho kiang, Oliv tang kichi a tunin, nungjuite laka mi nih a sawla.
29Alipokaribia kufika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30Na ma jawn khua uah vahohta unla; huaiah na lut tung un sabengtung nou khih, kuamah tuanna ngei nai louh, na vamu ding ua, huai honphel unla, honkai un.
30akawaambia: "Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana punda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungeni, mkamlete hapa.
31Huan, kuapeuhin, Bangdia phel? chia a hondot uleh, hichin na gen ding uh, Toupan a deih ahi, chiin.
31Kama mtu akiwauliza, kwa nini mnamfungua, mwambieni, Bwana ana haja naye."
32Huan, asawlte tuh a paita ua, a kiang ua a gen bang ngeiin a vamu ua.
32Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
33Huan, sabengtung nou tuh a phel lai un, a neiten a kiang uah, Sabengtung nou bangdia phel? a chi ua.
33Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, "Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?"
34Huan, amau, Toupan a deih ahi, a chi ua.
34Nao wakawajibu, "Bwana anamhitaji."
35Huchiin, Jesu kiangah a honkai ua; huan, sabengtung nou tungah a puante uh aphah ua, a tungah Jesu a tuang sak uhi.
35Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
36Huan, a paina ding lampi ah a puante uh a phah jel ua.
36Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37Huan, a tun ding kuan in, Oliv tang kumsukna ding takah, nungjui mipi tengtengin a thilthupi hih tengteng a muh jiak un a kipak ua, aw ngaihtakin Pathian tuh a phat uhi;
37Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
38Toupa mina kumpipa hongpai tuh a hampha e; vanah lem thu leng henla, tungnungpen ah thupina om hen, chiin.
38wakawa wanasema: "Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!"
39Huan, mipi laka Pharisai khenkhatin a kiangah, Sinsakpa, na nungjuite taiin, a chi ua.
39Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, "Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!"
40Aman bel, Ka honhilh ahi, Hiaite a daih uleh suangte bek a kikou ding uh, a chi a, a dawnga.
40Yesu akawajibu, "Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti."
41Huan, a tun kuanin, khua a mu a, a kahkhuma;
41Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia
42Aw nang telin tu sungin khamuanna ding thu honthei leteh aw: Himahleh tun jaw na muh louhna dingin a kisel ta ngala.
42akisema: "Laiti ungelijua leo hii yale yaletayo amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43Na galten na kimin lei kulh a khoh ding ua, a honum ding ua, na kimin pawt theih louhin a honom khum ding ua, huchibang nite tuh na tungah a hong tung ding;
43Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.
44na sunga na ta na naute, nangmah toh leiah hon pai ek ding ua; na sungah suang kichiang himhim a hawi kei ding uh; veha na om ni na theihlouh jiakin, chiin.
44Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa."
45Huan, Pathian biakin ah a va luta, bangpeuh juakte a delhkhia a, a kiang uah,
45Kisha, Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuzia nje wafanyabiashara
46Ka in thumna in ahi ding, chih gelh ahi; nou bel suamhatte khukin na bawl jaw uh, a chi a.
46akisema, "Imeandikwa: Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi."
47Huan, nitengin Pathian biakin ah thu a hilh jela. Huan, siampu liante leh, laigelhmite leh, vantang laka heutu deuhten, amah hihmang atum ua;Himahleh, min phatuam ngai taka a thu a ngaihkhiak jiak un, a hihna dingdan a thei tuan kei uhi.
47Yesu akawa anafundisha kila siku Hekaluni. Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,
48Himahleh, min phatuam ngai taka a thu a ngaihkhiak jiak un, a hihna dingdan a thei tuan kei uhi.
48lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.