Paite

Swahili: New Testament

Luke

5

1Huan, hichi ahia, mipiin Pathian thu a ngaihkhiak ua, amah a boh huthut lai un, amah tuh Gennesaret dil gei ah a dinga.
1Siku moja Yesu alikuwa amesimama kando ya ziwa Genesareti, na watu wengi walikuwa wamemzunguka wakisongana wanalisikiliza neno la Mungu.
2Huan, dil geia long nih om a mua, himahleh nga manmite lah a pawt khia ua, a lente uh a sawp ua.
2Akaona mashua mbili ukingoni mwa ziwa; wavuvi wenyewe walikuwa wametoka, wanaosha nyavu zao.
3Huchiin, long khat Simon-a pen ah a tuanga, a kiangah luigei akipan neukha tolh lut sak deuh a ngena. Huan, a tu a, long akipanin mipite thu a hilhta.
3Baada ya Yesu kuingia katika mashua moja, iliyokuwa ya Simoni, alimtaka Simoni aisogeze majini, mbali kidogo na ukingo wa ziwa. Akaketi, akafundisha umati wa watu akiwa ndani ya mashua.
4Huan, thugen a tawpin, Simon kiangah, Li thuk lam naih unla, nga man dingin, na lente uh pai un, a chi a.
4Alipomaliza kufundisha, akamwambia Simoni, "Peleka mashua mpaka kilindini, mkatupe nyavu zenu mpate kuvua samaki."
5Huan, Simonin a kiangah, Heutupa, gimtakin jankhuain ka pang ua, bangmah ka man kei ua, himahleh na thuin lente ka pai nawn ding leh, a chi a, a dawnga.
5Simoni akamjibu, "Bwana, tumejitahidi kuvua samaki usiku kucha bila kupata kitu, lakini kwa kuwa umesema, nitatupa nyavu."
6Huan, a paih uleh nga tampi tak a khuh ua, a lente uh tuh a kek iakkiaka.
6Baada ya kufanya hivyo, wakavua samaki wengi, hata nyavu zao zikaanza kukatika.
7Huan, long danga om a lawmte uh amau honghuh dingin a khutvan ua. Huan, a hongpai ua, long nih tum phialphialin a sung dim tuaktuak uh.
7Wakawaita wenzao waliokuwa katika mashua nyingine waje kuwasaidia. Wakaja, wakazijaza mashua zote mbili samaki, hata karibu zingezama.
8Huan, Simon Peterin huai a muhin, Jesu khuk kiangah khupbohin, Toupa, honpai sanin, mikhial ka hi, a chi a.
8Simoni Petro alipoona hayo, akapiga magoti mbele ya Yesu akisema, "Ondoka mbele yangu, ee Bwana, kwa kuwa mimi ni mwenye dhambi!"
9A nga mat u tuh amah leh a lawmten lamdang a sa mahmah ngal ua;
9Simoni pamoja na wenzake wote walishangaa kwa kupata samaki wengi vile.
10Simon pawlte mah Zebedai Tapa Jakob leh Johanin leng lamdanga sa mahmah sam uh. Huan, Jesun, Simon kiangah, Lau ken, tuban siah mihing na manta ding, a chi a.
10Hali kadhalika Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo, waliokuwa wavuvi wenzake Simoni. Yesu akamwambia Simoni, "Usiogope; tangu sasa utakuwa ukivua watu."
11Huan, a longte uh luigei ah a tolh galkai ua, bangkim pai sanin amah tuh a juita uh.
11Basi, baada ya kuzileta zile mashua ukingoni mwa ziwa, wakaacha yote, wakamfuata.
12Huan, hichi ahia, khua khata a omlaiin ngai dih, mi khat phak bop a oma, aman Jesu a na mu a, khupbohin Toupa, na ut leh non hihsiangthou thei, a chi a, a ngen ngutngut a.
12Ikawa, Yesu alipokuwa katika mmojawapo wa miji ya huko, mtu mmoja mwenye ukoma mwili mzima akamwona. Basi, mtu huyo akaanguka kifudifudi akamwomba Yesu: "Mheshimiwa, ukitaka, waweza kunitakasa."
13Huan, aman a sawka, a khoiha, Ka ut, nanasiangthoutain, a chi a. Huan, thakhatin a phak tuh a hongbei pah hi.
13Yesu akaunyosha mkono wake, akamgusa na kusema, "Nataka, takasika!" Mara ule ukoma ukamwacha.
14Huan, a kiangah, Kuamah hilh ken, a hihhangin siampu kiangah vakiensak inla, na sianhonna ding Mosi seh bangin lan in, mite theihchetna dingin, a chi a.
14Yesu akamwamuru: "Usimwambie mtu yeyote; bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani, ukatoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama inavyotakiwa na Sheria ya Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona."
15Himahleh, a tanchin thu tuh a thang sansan a; mipi thupitak a thu za nuam leh a natnate uh hihdam utin a hongkikhawm kheukhou ua.
15Lakini habari za Yesu zilizidi kuenea kila mahali. Watu makundi mengi wakakusanyika ili kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao.
16Himahleh, amah tuh gamdaiah a tuam pai a, a thum hi.
16Lakini yeye alikwenda zake mahali pasipo na watu, akawa anasali huko.
17Huan, hichi ahia, huai lain, ni khat tuh, thu a hilh a. Huan, akiangah Pharisaite leh dan siam te tuin a om ua, huaite tuh, Galili leh Judia gam kho teng akipana hongpai ahi ua; huan mi hihdamna dingin Toupa thilhihtheihna a kiangah a om.
17Siku moja Yesu alikuwa akifundisha. Mafarisayo na walimu wa Sheria kutoka katika kila kijiji cha Galilaya, Yudea na Yerusalemu, walikuwa wameketi hapo. Nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye kwa ajili ya kuponyea wagonjwa.
18Huan, ngai dih, lupna toh mijaw khat a honjawng ua; a maa koih dingin jawn lut a tum ua.
18Mara watu wakaja wamemchukua mtu mmoja aliyepooza maungo, amelala kitandani; wakajaribu kumwingiza ndani wamweke mbele ya Yesu.
19Huan, mipi jiakin jawn lutna dan a mu theikei ua, in tunga kipan, a lai takah, Jesu ma ah a lupna toh a khai khe suk ua.
19Lakini kwa sababu ya wingi wa watu, hawakuweza kuingia ndani. Basi, wakapanda juu ya dari, wakaondoa vigae, wakamshusha huyo aliyepooza pamoja na kitanda chake, wakamweka mbele ya Yesu.
20Huan, a gindan uh a namuh in, a kiang ah, Mihing, na khelhnate ngaihdam a hita, a chi a.
20Yesu alipoona jinsi walivyokuwa na imani kubwa, akamwambia huyo mtu, "Rafiki, umesamehewa dhambi zako."
21Huan, laigelh mite leh Pharisaiten, Pathian gensia hiai mi kua ahia? Pathian kia louin kuan ahia khelhnate ngaidam thei? chiin a ngaihtuah ua.
21Walimu wa Sheria na Mafarisayo wakaanza kujiuliza: "Nani huyu anayemkufuru Mungu kwa maneno yake? Hakuna mtu awezaye kusamehe dhambi ila Mungu peke yake!"
22Huchiin, Jesun a ngaihtuah uh a theia, a kiang uah, na lungtang uah bang na ngaihtuah ua?
22Yesu alitambua mawazo yao, akawauliza, "Mnawaza nini mioyoni mwenu?
23Na khelhnate ngaihdam a hita, chih leh, Thou inla, khein paita in, chih, a koipen a gen nuam jaw a?
23Ni lipi lililo rahisi zaidi: kusema, Umesamehewa dhambi, au kusema, Simama utembee?
24Abang abang hitaleh, khovelah Mihing Tapain khelhnate ngaihdam theihna a nei chih na theihna ding un a chi a, (Jaw kiangah) Thou inla, na lupna la inla, na in ah paiin, ka honchi, a chi a.
24Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anao uwezo wa kusamehe dhambi duniani." Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza, "Simama, chukua kitanda chako uende zako nyumbani."
25Huchiin, a mit muh un a thou paha, a lupna a la a, Pathian phat kawmkawmin a in ah a paita.
25Mara, huyo mtu aliyepooza akasimama mbele yao wote, akachukua kitanda chake akaenda zake nyumbani huku akimtukuza Mungu.
26Huan, a vek un lamdang a sa mahmah ua, Pathian a phat ua. Tuniin thillamdang pitak i mu hi, a chi ua, a lau mahmah uh.
26Wote wakashangaa na kushikwa na hofu; wakamtukuza Mungu wakisema: "Tumeona maajabu leo."
27Huan, huaite khitin a pawta, siahpiakna muna tu, siahkhonmi khat a min Levi a mu a; huan, a kiangah, Honjui in, a chi a.
27Baada ya hayo, Yesu akatoka nje, akamwona mtoza ushuru mmoja aitwaye Lawi, ameketi ofisini. Yesu akamwambia, "Nifuate!"
28Huchiin, bangkim a paisana, a thou a, a juita.
28Lawi akaacha yote, akamfuata.
29Huan, Leviin a in ah Jesu adingin ankuang thupitak a luia; huchiin, siahkhonmi midangte toh mi tampiin amau a umpih chiat ua.
29Kisha Lawi akamwandalia Yesu karamu kubwa nyumbani mwake; na kundi kubwa la watoza ushuru na watu wengine walikuwa wameketi pamoja nao.
30Huan, Pharisaite, a laigelhmite utoh a nungjuite tungah a phun ua, Bang dia siahkhonmite leh khialte kianga ne-a dawn na hi ua? a chi ua.
30Mafarisayo na walimu wa Sheria wakawanung'unikia wafuasi wake wakisema: "Mbona mnakula na kunywa pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?"
31Huan, Jesun, a kiang uah, Mi damtheiten daktor a kiphamoh kei ua, mi damtheilouten a kiphamoh jaw uh.
31Yesu akawajibu, "Wenye afya hawahitaji daktari, lakini wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa.
32Mi diktatte sam dinga hongpai ka hi keia, mi khialte kisik dinga sam din hongpai ka hijaw, chi in a dawng hi.
32Sikuja kuwaita watu wema, bali wenye dhambi, ili wapate kutubu."
33Huan, amau a kiangah, Johan nungjuiten an a ngawl jel ua, a thum jel uh: Pharisai nungjuiten leng huchibang mahin a hih jel uh: himahleh, na nungjuiten a ne un a dawn gige uh, a chi ua.
33Watu wengine wakamwambia Yesu, "Wafuasi wa Yohane mbatizaji hufunga mara nyingi na kusali; hata wafuasi wa Mafarisayo hufanya vivyo hivyo. Lakini wafuasi wako hula na kunywa."
34Jesun a kiang uah, Mou pimite kianga a pasal ding a om lai siah mou pimite na ngawl sak thei ngei ua hia?
34Yesu akawajibu, "Je, mnaweza kuwataka wale walioalikwa arusini wafunge hali bwana arusi yuko pamoja nao?
35Himahleh apasal ding amau akipana pimang nite a hongtung dinga, huai ni chiangin jaw a ngawl ding uh, a chi a.
35Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kati yao, na wakati huo ndipo watakapofunga."
36Huan, a kiang uah gentehna thu leng a gena: Kuamahin puan thak eu khiain puan lui a thuap ngei kei, thuap him taleh, a thakin a kaikek dia, a thak them leh a lui tuh a kituak tuan kei ding.
36Yesu akawaambia mfano huu: "Hakuna mtu akataye kiraka cha nguo mpya na kukitia katika vazi kuukuu; kama akifanya hivyo, atakuwa amelikata hilo vazi jipya, na hicho kiraka hakitachukuana na hilo vazi kuukuu.
37Huan, kuamahin uain thak savun uain thawl lui ah a thun ngei kei uh, thunta him le uleng, uain thakin savun thawlte a phukek dia, a bo dia, savun thawlte leng a se ding uh.
37Wala hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu; kwani hiyo divai mpya itavipasua hivyo viriba, divai itamwagika, na viriba vitaharibika.
38Uain thak tuh savun uain thawl thakah a thun zo ding uh ahi.Huan, kuamah, uain lui na dawn khinin leng, a thak a duh pah kei hi; a lui a hoihjaw, a chi ngala, a chi hi.
38Divai mpya hutiwa katika viriba vipya!
39Huan, kuamah, uain lui na dawn khinin leng, a thak a duh pah kei hi; a lui a hoihjaw, a chi ngala, a chi hi.
39Wala hakuna mtu ambaye hutamani kunywa divai mpya baada ya kunywa ya zamani, kwani husema: Ile ya zamani ni nzuri zaidi."