1Huan, hichi ahi a, Khawlni khatin buh lei khawngah a pai suaka, a nungjuiten buh vuite a khiak ua, a khutpek un a nuai siang ua, a ne ua.
1Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano, na wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakaondoa punje zake kwa mikono, wakala.
2Huan, Pharisai kuate hiamin, Bangdia Khawlnia hih sianglou hih na hi ua? a chi ua.
2Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, "Mbona mnafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato?"
3Huan, Jesun a dawnga, David a gilkial laia a lawmte toh a thil hih uh huai bangte leng na sim kei ua hia?
3Yesu akawajibu, "Je, hamjasoma jinsi alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
4Huchia Pathian ina a luta, siampute loungalin a nek siang louh tanghou koih a laka, a lawmte kianga a piak sam thu, a chi a.
4Yeye aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akachukua ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu, akala na kuwapa wenzake. Kisheria, ni makuhani tu peke yao ndio walioruhusiwa kula mikate hiyo."
5Huan, amahmahin, a kiang uah, Mihing Tapa jaw Khawlni Toupa ahi, a chi hi.
5Hivyo akawaambia, "Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato."
6Huan, hichi ahi a, Khawlni dangin kikhopna in ah a luta, thu a hilha; huan, huai ah mi khat khut taklam jaw a na oma.
6Siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia katika sunagogi, akafundisha. Mle ndani mlikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
7Huan, laigelhmite leh Pharisaiten a hekna ding a muh theihna ding un, Khawlniin hihdam dingin a kisa hia kisa lou a simet ua.
7Walimu wa Sheria na Mafarisayo walitaka kupata kisingizio cha kumshtaki Yesu na hivyo wakawa wanangojea waone kama angemponya mtu siku ya Sabato.
8Himahleh, aman, a lungsim uh a theia, khutjaw kiang ah, Thou inla, a laiah ding khia in, a chi a. Huan a thou a, a ding khetaa.
8Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, "Inuka, simama katikati." Yule mtu akaenda akasimama katikati.
9Huan, Jesun a kiang uah, Khawlniin hihhoih a sianga, hih siat? hotdam a sianga, hihlup? ka hondong ahi, a chi a.
9Kisha Yesu akawaambia, "Nawaulizeni, je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuyaangamiza?"
10Huan, a vek un a en velvela, a kiangah, Na khut zan khia in, a chi a. Huan, a zan khiaa, a khut tuh a damta.
10Baada ya kuwatazama wote waliokuwa pale, akamwambia yule mtu, "Nyosha mkono wako." Naye akafanya hivyo, na mkono wake ukawa mzima tena.
11Huchiin a heh lo mahmah ua, Jesu tunga hihdingdan a kihouta uh.
11Lakini wao wakakasirika sana, wakajadiliana jinsi ya kumtendea Yesu maovu.
12Huan, hichi ahi a, huailaiin, a pawta, thum dingin tang ah a kuana, Pathian kiangah jan khuain a thum a.
12Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akimwomba Mungu.
13Huan, khovak takin a nungjuite a sama; a lak uah nih a tela, a min uh leng sawltak a sa hi:
13Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akachagua kumi na wawili ambao aliwaita mitume:
14Huaite tuh Simon Peter a chih leh a unaupa Andru, Jakob leh Johan, Philip leh Bartholomai,
14Simoni (ambaye Yesu alimpa jina Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo na Yohane, Filipo na Bartholomayo,
15Matthai leh Thoma, Alphai tapa Jakob,
15Mathayo na Thoma, Yakobo wa Alfayo na Simoni (aliyeitwa Zelote),
16Simon, Zelot kichi leh Jakob tapa Juda leh a mansakpa Juda Iskariot ahi uh.
16Yuda wa Yakobo na Yuda Iskarioti ambaye baadaye alikuwa msaliti.
17Huan, amau toh a pai khia a, mun jangah a dinga, a nungjuite mipite toh, Judia gam tengteng akipan leh, Jerusalem khua akipan leh, Tura leh Sidon kho lama tuipi gei akipan mipi tampitak a thu ngai nuam leh a damlouhnate uh hihdam utin a hongpai ua;
17Baada ya kushuka mlimani pamoja na mitume, Yesu alisimama mahali palipokuwa tambarare. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati wa watu waliotoka pande zote za Yudea na Yerusalemu na pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walifika kumsikiliza Yesu na kuponywa magonjwa yao.
18Huchiin, dawi nin bawlgawpte leng damsakin omta uh.
18Aliwaponya pia wote waliokuwa wanasumbuliwa na pepo wachafu.
19Huan, a kianga kipan thilhihtheihna pawtkhiaa, mi chih a hidam jel jiakin mipi tengtengin amah khoih a tum ua.
19Watu wote walitaka kumgusa, kwa maana nguvu ilikuwa inatoka ndani yake na kuwaponya wote.
20Huan, a dak khia a, a nungjuite enin a gena: Nou gentheite aw, na hampha uhi; Pathian gam noua ahi ngala.
20Yesu akawageukia wanafunzi wake, akasema: "Heri ninyi mlio maskini, maana Ufalme wa Mungu ni wenu.
21Nou tua gilkialte aw, na hampha uhi, tai ding na hi ngal ua. Nou tua kapte aw, na hampha uhi, nui ding na hi ngal ua.
21Heri ninyi mnaosikia njaa sasa, maana baadaye mtashiba. Heri ninyi mnaolia sasa, maana baadaye mtacheka kwa furaha.
22Mihing Tapa jiaka miten a honhuat ua, honpampaih ua, hontai ua, na min uh a hoih kei chia a honpaih mang chiang un, na hampha ding uh.
22"Heri yenu ninyi iwapo watu watawachukia, watawatenga, watawatukana na kuwaharibieni jina kwa ajili ya Mwana wa Mtu!
23Huai niin kipak unla, nuamin tawm un, ngai un, van ah na kipahman uh a om kikeih ngal a; huchi bangmahin a pipute un jawlneite tungah a hih uhi.
23Wakati hayo yatakapotokea, furahini na kucheza, maana hakika tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Kwa maana wazee wao waliwatendea manabii vivyo hivyo.
24A hihhangin, nou mi haute aw, na tung uh a gik e; na khamuanna uh na mu khinta ngal ua:
24Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, maana mmekwisha pata faraja yenu.
25Nou tua vahte aw, na tung uh a gik e; na gil uh hongkial ding ahi ngal a. Nou tua nuite aw; na tung uh a gik e; lungkhama kap ding na hi ngal ua;
25Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa, maana baadaye mtasikia njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka kwa furaha sasa, maana baadaye mtaomboleza na kulia.
26Mi tengtengin a honphat chiang un na tung uh a gik ding hi; huchimahbangin a pipute un jawlnei takloute tungah a hih uhi.
26Ole wenu ninyi iwapo watu wote wanawasifu, maana wazee wao waliwafanyia manabii wa uongo vivyo hivyo.
27Ka thu ngaikhete aw, konhilh ahi, Na melmate uh it unla, a honhote a hoihna ding uh hih un,
27"Lakini nawaambieni ninyi mnaonisikiliza: wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukieni.
28Hamsia honlohte vualjawl unla, a honsimmohte thum sak un.
28Watakieni baraka wale wanaowalaani, na waombeeni wale wanaowatendea vibaya.
29Biang langkhata honbengpa tuh a lehlam leng dohin; huan, na puan honlaksakpa kiangah na puannak leng it ken.
29Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie na la pili. Mtu akikunyang'anya koti lako mwachie pia shati lako.
30A honngen peuh kiangah pia un; huan, na van honlaksakpa kiangah ngen nawn ken.
30Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyang'anya mali yako usimtake akurudishie.
31Huan, min na tung ua a hih uh na deih ding bang jel un mi tungah leng hih sam un.
31Watendeeni wengine kama mnavyotaka wawatendee ninyi.
32Huan, a honitte kia na it un, pahtak bang na loh ding ua? mikhialten leng amau itte a it sam ve ua oi.
32"Na ikiwa mnawapenda tu wale wanaowapenda ninyi, je, mtapata tuzo gani? Hakuna! Kwa maana hata wenye dhambi huwapenda wale wanaowapenda wao.
33Huan, na tung ua hoihte tung kiaa na hoih un, pahtak bang na loh ding ua? mikhialten leng huchibangmahin a hih jel ve ua oi.
33Tena, kama mkiwatendea mema wale tu wanaowatendeeni mema, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo!
34Huan, muh nawn lametnate kiang kiaa thil na leitawi sak un, pahtak bang na loh ding ua? mikhialten leng a ngeingei mu nawn dingin mikhialte kiangah a leitawisak sam ngal ua.
34Na kama mnawakopesha wale tu mnaotumaini watawalipeni, je, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi wenzao ili warudishiwe kima kilekile!
35A hihhangin na melmate uh it unla, a hoihna ding un hih unla, leitawi sak un, lunglel het lou in; huchiin na kipah man uh a tam dia, Tungnungpen tate na hi ding uh; aman mi kipahnadantheiloute leh migiloute a hehpih naknak hi.
35Ila nyinyi wapendeni adui zenu, na kuwatendea mema; kopesheni bila kutazamia malipo, na tuzo lenu litakuwa kubwa, nanyi mtakuwa watoto wa Mungu aliye juu. Kwa maana yeye ni mwema kwa wale wasio na shukrani na walio wabaya.
36Na Pa un mi a hehpih bangin mi hehpih sam un.
36Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.
37Hawmsak kei un, huchiin hawmsakin na om kei ding uh; kuamah siamlouin sep dah un, huchiin siamlouhin na om kei ding uh; ngaidam un, huchiin ngaihdamin na om ding uh;
37"Msiwahukumu wengine, nanyi hamtahukumiwa; msiwalaumu wengine, nanyi hamtalaumiwa; wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
38Pia un, huchiin, piakin na om ding uh, hoihtaka teha, hen gaka, sin gaka, let nawinawiin na angsung uah piakin na om ding uh. Noumau tehna ngei maha tehsaka piak hi ding na hi ngal ua, a chi a.
38Wapeni wengine wanavyohitaji, nanyi mtapewa. Naam, mtapokea mikononi mwenu kipimo kilichojaa, kikashindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika. Kwa maana kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho ambacho Mungu atatumia kwenu."
39Huan, a kiang uah, gentehnain a gen a, Mittawin mittaw mah a pi thei diam? a nih un kokhuk ah a ke khawm kei ding ua hia?
39Akawaambia mfano huu: "Je, kipofu anaweza kumwongoza kipofu mwenzake? La! Wote wataanguka shimoni.
40Nungjui tuh a heutupa tungah a om kei; himahleh mi chih a siamkim chiang un a heutupa bangin a om ding uh.
40Mwanafunzi hamshindi mwalimu wake, lakini kila mwanafunzi akisha hitimu huwa kama mwalimu wake.
41Huan, bangdia, na mita singtum om limsak loua, na unau mita ninneng neuchik om mu na hia?
41Unawezaje kukiona kibanzi kilicho katika jicho la mwenzio, usione boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe?
42Nangmah mita singtum om mu lou piin, na unau kianga, Unau, na mita ninneng neuchik om honla khesak ve, bangchia chi thei na hia? Mi lepchiah: na mit apat singtum la khe masa in, huchiin na unau mita ninneng neuchik lak khiak ding tuh chiantakin na mu thei ding.
42Au, unawezaje kumwambia mwenzako, Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi katika jicho lako, na huku huioni boriti iliyoko katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Toa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako, na hivyo utaona sawasawa kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilicho katika jicho la ndugu yako.
43Sing hoih himhim gah siaa gah a om ngei kei; sing sia lah gah hoiha gah a om ngei sam kei.
43"Mti mwema hauzai matunda mabaya, wala mti mbaya hauzai matunda mazuri.
44Sing chih amau gah chiatah a kithei hi. Min khau lingnei kungah theipi a lou ngei kei uh, lingnok lakah grep gah a loungei sam kei uh.
44Watu huutambua mti kutokana na matunda yake. Ni wazi kwamba watu hawachumi tini katika michongoma, wala hawachumi zabibu katika mbigili.
45Mi hoihin a lungtang gou bawm hoih akipan thil hoihte a honla khe jela; mi gilouin a lungtang gou bawm sia akipan thil hoihloute a honla khe jel hi; a lungtanga dim val tuh a kamin a gen jel ngala.
45Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka katika hazina bora iliyo moyoni mwake; na mtu mbaya hutoa yaliyo mabaya katika hazina mbaya iliyo moyoni mwake, kwa maana mtu huongea kutokana na yale yaliyojaa moyoni mwake.
46Huan, nou bang dinga, ka gente hih loupi a, Toupa, Toupa, honchi nahi ua?
46"Mbona mwaniita Bwana, Bwana, na huku hamtimizi yale ninayosema?
47Mi chih ka kianga honga, ka thu jaa mang peuhmah kua bang ahi ua, ka honen sak ding:
47Nitawapeni mfano unaofaa kuonyesha alivyo yeyote yule anayekuja kwangu, akasikia maneno yangu na kuyatimiza:
48In lammi, thukpia tou a, suangpi tou a, suangpi tunga suangphum lemmi bang ahi uh; huan, tui a hongkhanin, tui khauhin huai in tuha khoh a, a hihling theikeia, hoihtaka lam a hih jiakin.A hihhangin, jaa mang lou tuh, suangphum lou a, leitung maimaha in lammi ahi; huan, tui khauhin huai tuh a khoh a, a chim paha; huai in siatna tuh thupi tak ahi, a chi a.
48Huyo anafanana na mtu ajengaye nyumba, ambaye amechimba chini na kuweka msingi wake juu ya mwamba; kukatokea mafuriko ya mto, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, lakini haukuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa imara.
49A hihhangin, jaa mang lou tuh, suangphum lou a, leitung maimaha in lammi ahi; huan, tui khauhin huai tuh a khoh a, a chim paha; huai in siatna tuh thupi tak ahi, a chi a.
49Lakini yeyote anayesikia maneno yangu lakini asifanye chochote, huyo anafanana na mtu aliyejenga nyumba juu ya udongo, bila msingi. Mafuriko ya mto yakatokea, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, ikaanguka na kuharibika kabisa!"