Paite

Swahili: New Testament

Matthew

25

1Huaihun chiang in vangam tuh nungak siangthou sawm, a khawnvak uh tawi a mouneipa dawn ding a pawtte toh teh a hita ding.
1"Wakati huo, Ufalme wa mbinguni utafanana na wasichana kumi waliochukua taa zao, wakaenda kumlaki bwana arusi.
2Huchi in a lak ua mi nga a hai ua, nga a pil uh.
2Watano miongoni mwao walikuwa wapumbavu na watano walikuwa wenye busara.
3A haite'n a khawnvakte uh a tawi un, a tui leng a tawi ngalkei ua;
3Wale wapumbavu walichukua taa zao, lakini hawakuchukua akiba ya mafuta.
4a pilte'n bel a khawnvakte uh a tawi un, a um ah a tui leng a tawi uh.
4Lakini wale wenye busara walichukua mafuta katika chupa pamoja na taa zao.
5Huan, mou neipa tuh a hong zekai jiak in a vek un a lusu ua, a na ihmuta ua.
5Kwa kuwa bwana arusi alikawia kuja, wale wanawali wote wote walisinzia, wakalala.
6Huan, janlai tak in, Ngai dih uh mouneipa a hong e: a dawn ding in hong pawt un: chi in, kikou ging a hong omta a.
6Usiku wa manane kukawa na kelele: Haya, haya! Bwana arusi anakuja; nendeni kumlaki.
7Huaitak in nungak siangthoute tuh a thou vek ua, a khawnvakte uh tuh a kem ua.
7Hapo wale wanawali wote wakaamka, wakazitayarisha taa zao.
8Huan, a haite'n, a pilte kiang ah, Na khawnvaktui uh hon pe sam un; ka khawnvak uh mit din a kisa, a chi ua.
8Wale wapumbavu wakawaambia wale wenye busara: Tupeni mafuta yenu kidogo maana taa zetu zinazimika.
9Himahleh, a pilte'n, Kou leh nou a ding in a kiching kei ding; a juakte kiang ah pai unla, lei jaw un, chi in, a dawng ua,
9Lakini wale wenye busara wakawaambia, Hayatatutosha sisi na ninyi! Afadhali mwende dukani mkajinunulie wenyewe!
10Huan, lei ding a a paimang kal un mouneipa tuh a hong tungta a; huchi in, a mansate tuh amah toh kitenna ankuang um ding in a lut ua; huan, kongkhak a khakta uh.
10Basi, wale wanawali wapumbavu walipokwenda kununua mafuta, bwana arusi akafika, na wale wanawali waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye katika jumba la arusi, kisha mlango ukafungwa.
11Huai nung in nungak siangthou dangte leng a hongtung ua, Toupa, Toupa, hon hon in, a chi uh:
11Baadaye wale wanawali wengine wakaja, wakaita: Bwana, bwana, tufungulie!
12Himahleh aman tuh, Chihtaktakin ka hon hilh ahi, ka hon thei ngeikei, a chi a, a dawng a.
12Lakini yeye akawajibu, Nawaambieni kweli, siwajui ninyi."
13Huchi in, ki ging un, a ni leh a hun na theihlouh jiak un.
13Kisha Yesu akasema, "Kesheni basi, kwa maana hamjui siku wala saa.
14Mi, gam dang a pai dia kisa, a sikhate sam a, a sumte a kiang ua kemsak bang ahi ngal a:
14"Itakuwa kama mtu mmoja aliyetaka kusafiri ng'ambo: aliwaita watumishi wake, akawakabidhi mali yake.
15Sikha khat kiang ah talent nga a pia a, sikha dang kiang ah talent nih a pia a, sikha dang kiang ah talent khat a pia a; a hih theih hun dingdan chiat un a pia a; huan, a paita a.
15Alimpa kila mmoja kadiri ya uwezo wake: mmoja sarafu tano za fedha ziitwazo talanta, mwingine talanta mbili na mwingine talanta moja, kisha akasafiri.
16Huan, talent nga mupa tuh huai in a vasumsin pah a, talent nga dang a mu kheta a,
16Mara yule aliyekabidhiwa talanta tano akafanya kazi nazo akapata faida talanta tano.
17Huchimah bang in talent nih mupa'n leng talent nih dang a mu kheta a.
17Hali kadhalika na yule aliyekabidhiwa talanta mbili akapata faida talanta mbili.
18Talent khat mupa bel a va kuan a, lei a tou a, a pu dangka a selgu zota.
18Lakini yule aliyekabidhiwa talanta moja akaenda akachimba shimo ardhini, akaificha fedha ya bwana wake.
19Huan, sawtpi nung in huai sikhate pu tuh a hongpai a, a mau toh a sum tanchin a hihfelta hi.
19"Baada ya muda mrefu, yule bwana alirudi, akaanza kukagua hesabu ya matumizi na mapato ya fedha yake.
20Huan, talent nga mupa a hongpai a, talent nga dang a hon tawi a, Pu, nang talent nga non kemsak a; en dih; talent nga dang ka mukhia e, a chi a.
20Mtumishi aliyekabidhiwa talanta tano akaja amechukua zile talanta tano faida, akamwambia, Bwana, ulinikabidhi talanta tano, hapa pana talanta tano zaidi faida niliyopata.
21A pu'n a kiang ah, Sikha hoih leh muanhuai, na hih hoih hi, tawmchik tungah na muanhuai a, tampi tungah ka hon omsak ding; na pu kipahna ah lut in, a chi a.
21Bwana wake akamwambia, Vema, mtumishi mwema na mwaminifu. Umekuwa mwaminifu katika mambo madogo nitakukabidhi makubwa. Njoo ufurahi pamoja na bwana wako.
22Huan, talent nih mupa leng a hongpai a, Pu, nang talent nih non kemsak a; en dih, talent nih dang ka mukhia e, a chi a.
22"Mtumishi aliyekabidhiwa talanta mbili akaja, akatoa talanta mbili faida, akisema, Bwana, ulinikabidhi talanta mbili. Chukua talanta mbili zaidi faida niliyopata.
23A pu'n a kiang ah, Sikha hoih leh muanhuai, na hihhoih e, tawmchik tungah na muanhuai a, tampi tungah ka hon omsak ding; na pu kipahna ah lut in, a chi a.
23Bwana wake akamwambia, Vema, mtumishi mwema na mwaminifu. Umekuwa mwaminifu katika mambo madogo, nitakukabidhi makubwa. Njoo ufurahi pamoja na bwana wako.
24Huan, talent khat mupa leng a hongpai a, Pu, mi chihhakpi na hi chih ka hon thei a; na tuhlouhna ah leng na at nak, na thehlouhna ah leng na khawm nak ahi;
24"Lakini yule aliyekabidhiwa talanta moja akaja, akasema, Bwana, najua wewe ni mtu mgumu; wewe huvuna pale ambapo hukupanda, na kukusanya pale ambapo hukutawanya.
25huaiziak in ka lau a, ka vapai a, na talent lei ah ka selgu a; en in, nang a ngei na mu nawn hi, a chi a.
25Niliogopa, nikaificha fedha yako katika ardhi. Chukua basi mali yako.
26A pu'n a kiang ah, Sikha gilou leh zongjaw, ka tuh louhna ah leng ka at a, ka thehlouhna ah leng ka khawm nak chih na thei maw?
26"Bwana wake akamwambia, Wewe ni mtumishi mwovu na mvivu! Unajua kuwa mimi huvuna mahali ambapo sikupanda, na hukusanya pale ambapo sikutawanya.
27Huchi ahih ngal leh ka dangka sumsinte kiang a na koihtak ding hi a, huchia, ka hongpai a kei a tuh a pung toh ka muh nawn ding ahi veleh.
27Ilikupasa basi, kuiweka fedha yangu katika benki, nami ningelichukua mtaji wangu na faida yake!
28Huaiziak in a talent khat laksak unla, talent sawm neipa kiang ah pia un.
28Basi, mnyang'anyeni hiyo fedha mkampe yule mwenye talanta kumi.
29Kuapeuh a nei tuh piak behlap ahi ding a, a hong hau ding; kuapeuh a neilou tuh a neih sun nangawn laksak ahi ding.
29Maana, aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
30Huan, sikha phatuamlou tuh polam mial ah paikhia un, huai ah kah leh hagawi a om ding, a chi a, a dawng a.
30Na kuhusu huyu mtumishi asiye na faida, mtupeni nje gizani! Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.
31Ahihhang in, Mihing Tapa, a angelte tengteng toh, a thupina a kivan a a hongpai hun chiang in, a thupina tutphah ah a tu dia;
31"Wakati Mwana wa Mtu atakapokuja katika utukufu wake na malaika wote wakiwa pamoja naye, hapo ataketi juu ya kiti chake cha enzi kitukufu,
32a ma ah nam chih a kikhawm ding ua; belam chingpa'n kel lak a a belamte a khenkhia bang in amau tuh a khenkhe ding:
32na mataifa yote yatakusanyika mbele yake, naye atawatenganisha watu kama mchungaji anavyotenganisha kondoo na mbuzi.
33belamte tuh a taklam ah a koih ding a, kelte tuh a veilam ah a koih ding.
33Atawaweka kondoo upande wake wa kulia na mbuzi upande wake wa kushoto.
34Huai hun chiang in Kumpipa'n a taklam a mite kiang ah, Ka Pa deihsakte aw, hongpai unla, khovel siam chil a pata nou a dia gam bawlsa luah un;
34"Kisha Mfalme atawaambia wale walio upande wake wa kulia, Njoni enyi mliobarikiwa na Baba yangu; pokeeni Ufalme mliotayarishiwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
35ka gil a kial in, nou nek ding non pia ua; ka dang a tak in, dawn ding non pia uh; mikhual ka hih in non zintun ua;
35Maana nilikuwa na njaa nanyi mkanipa chakula; nilikuwa na kiu nanyi mkanipa maji; nilikuwa mgeni nanyi mkanikaribisha;
36vuaktang ka hih in, puan non silhsak uh; ka chi a nat in, ka kiang a na hong jiak un, a chi ding.
36nilikuwa uchi, mkanivika; nilikuwa mgonjwa nanyi mkaja kunitazama; nilikuwa gerezani nanyi mkaja kunitembelea.
37Huai hun chiang in, mi diktatte'n, Toupa, Chik in ahia gilkial a kon muh ua nek ding kon piak uh? dangtak a kon muh ua, dawn ding kon piak uh?
37Hapo, hao watu wema watamjibu mfalme Bwana, ni lini tulikuona mwenye njaa nasi tukakupa chakula, au ukiwa na kiu nasi tukakunywesha maji?
38Chik in ahia mikhual a kon muh ua, kon zintun uh? vuaktang a kon muh ua, puan kon silhsak uh?
38Ni lini tulikuona ukiwa mgeni nasi tukakukaribisha, au bila nguo nasi tukakuvika?
39Chik in ahia china in hiam suangkulh ah hiam kon muh ua, na kiang a ka hong uh? chi in, a dong ding uh.
39Ni lini tulikuona ukiwa mgonjwa au mfungwa nasi tukaja kukutazama?
40Huan, Kumpipa'n a kiang uah, Chihtaktakin ka hon holh ahi, Hiai ka unau neupente lak a mi khat tung a na hih uh tuh, ka tung a hih na hi uh, chi in, a dawng ding.
40Mfalme atawajibu, Kweli nawaambieni, kila kitu mlichomtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu wadogo, mlinitendea mimi.
41Huaikhit in, a veilam a mite kiang ah leng, Hamsiat thuakte aw, khantawn mei diabol leh a sawltakte dia a bawl uah hon paimangsan un;
41"Kisha atawaambia wale walio upande wake wa kushoto, Ondokeni mbele yangu enyi mliolaaniwa! Nendeni katika moto wa milele aliotayarishiwa Ibilisi na malaika wake.
42ka gil a kial in, nou nek ding non pekei ua; ka dang a tak in, dawn ding non pekei ua;
42Maana nilikuwa na njaa nanyi hamkunipa chakula; nilikuwa na kiu nanyi hamkunipa maji.
43mikhual ka hih in, non zintunkei uh; vuaktang ka hih in, puan non silhsakkei ua; china leh suangkulh a ka om in, non vehlouh jiak un, a chi ding.
43Nilikuwa mgeni nanyi hamkunikaribisha; nilikuwa mgonjwa na mfungwa nanyi hamkuja kunitazama.
44Huai hun chiang in amau leng, Toupa, chik in ahia gilkial ahiam, vuaktang in hiam, china in hiam, suangkulh ah hiam kon muh ua, na kon sepsaklouh uh? chi in a dong ding uh,
44"Hapo nao watajibu, Bwana, ni lini tulikuona ukiwa na njaa au kiu, ukiwa mgeni au bila nguo, ukiwa mgonjwa au mfungwa, nasi hatukuja kukuhudumia?
45Huan, aman a kiang uah, Chihtaktakin ka hon hilh ahi, Hiai mi neupente lak a mi khat tung a na hihlouh utuh ka tung a hihlou na hi uh, chi in, a dawng ding.Huan, huaite khantawn gawtna ah a pai ding ua; mi diktatte tuh khantawn hinna ah a pai ding uh, a chi a.
45Naye atawajibu, Nawaambieni kweli, kila mlipokataa kumtendea mambo haya mmojawapo wa hawa wadogo, mlikataa kunitendea mimi.
46Huan, huaite khantawn gawtna ah a pai ding ua; mi diktatte tuh khantawn hinna ah a pai ding uh, a chi a.
46Basi, hawa watakwenda kwenye adhabu ya milele, lakini wale waadilifu watakwenda kwenye uzima wa milele."